Foleni ya Tabata - Tazara imeanza kuwa tishio kwa uchumi wa nchi, nini kifanyike?

Foleni ya Tabata - Tazara imeanza kuwa tishio kwa uchumi wa nchi, nini kifanyike?

Kwa uchunguzi wangu, foleni ya kipande hicho cha barabara (Tabata Dampo hadi Buguruni Chama) inasababishwa na junction ya hapo zinapokutana barabara ya kutoka Buguruni kwenda Vingunguti na ile ya Mandela Rd. TAZARA hapasababishi foleni kabisa, kwani kama unatoka Tabata utapata shida kuikamata Buguruni, ila ukishavuka Chama, kule mbele kwenda TAZARA unateleza tu, wala hakuna shida. Kwa mtazamo wangu tatizo lipo hapo Chama/Sheli
80% ya jiji ni squatter barabara kubwa ziko chache sana
 
tunajenga haya mastructure bila kufanya research ya kutosha, jiji linahitaji nini kwanza...

Jiji la Dar es salaam linahitaji mipango miji anayoendana na population iliyopo + ukuaji wa mji...Ni wakati wa kupiga marufuku ujenzi majumba wa watu binafsi baadala yake miji ijengwe na agencies maalum au serikali watu wakopeshwe nyumba...

Baadhi ya huduma zitolewe katikati ya mji zipelekwe nje kama kibaha au bagamoyo....mfano Soko la Kariakoo linaweza kumegwa likaenda Mlandizi au Vigwaza huko...Biashara ya used pale Ilala na gerezani inapaswa kutoka iende mbali huko hata Msata... Soko la samaki feri linaweza kutolewa likaenda Bagamoyo...Kufanyike mgawanyo wa mahospitali makubwa baadhi yatoke katikati ya mji yahamie nje hata Chanika au kisarawe huko.... Serikali ifikirie kujenga miji ya kisasa kigamboni huko kuelekea Mbutu, Miji mingine ijengwe bunju, madale, Goba, Bagamoyo, Chalinze, Msata nk.. Kile chuo cha Ifm na vyuo vingine vitoke katikati ya mji viende hata msata huko... jijengwe express way kutoka mjini kati kuelekea Msata kupitia chalinze mpaka Morogoro na nyingine zipite Bagamoyo to msata...
Kwa hiyo mzee kila huduma muhimu ya kijamii ipelekwe nje ya mji mbali na makazi ya watu walipo?

Faida yake msongamano utapungua, athari yake je! ni ipi? Aisee si rahisi kama unavyodhani, ukitafuta picha ya kariakoo enzi hizo haikua na mafuriko ya watu kama unayoyaona sasa, mambo hubadilika kadiri miji inavyokua. Muhimu ifanyike study ya uhakika ili kuja na solutions za uhakika kulingana na hali na mazingira yetu na sio kusema nchi flan wanafanya hivi au vile wamefanikiwa halafu unasahau utamaduni, desturi na mazingira ya kiuchumi tunatofautiana.
 
Malori yale sijui ,yaani kutoka mwananchi mpaka Tazara ni kero sana.Nchi inaingia hasara kwa maeneo yale tuu
Yaani muda mwingine foleni inaaniza external hadi uhasibu, hii nchi hii, wajenge flyover juu ya Tazara flyover , masaa matatu mtu hujavuka hata Tazara!!??
 
Kuondoa biashara barabarani itakuwa na matokeo chanya kwa Sana!! Ila hawa Tanroad Kama hayana msaada kabisa
 
Njia rahisi ya kupunguza foleni kwenye majiji, ingawa itaumiza wengine, ni kuwepo na kodi au tozo ya kila mwezi kwa magari yote binafsi yasiotoa huduma kwa umma, pamoja na kuongeza tozo maeneo ya kupaki hayo magari; Mfano, kama utatumia usafiri binafsi ndani ya jiji na ukawa unatozwa shilingi milioni 1 kwa mwezi, na sehemu yoyote utakayopaki au kusimama kutozwa kodi...hapo lazima magari mengi binafsi yatabaki majumbani, na hapo utakuwa umepunguza foleni kwa asilimia kubwa...kwa sababu kwenda katika shughuli zetu tutatumia usafiri wa umma.

Halafu vituo vya mafuta vife? Mafundi magari na wauza vipuli warudi mtaani na car wash zote zifungwe.
 
Napendekeza wajenge flyover juu ya Tazara flyover ili zinazotokea Buguruni kwenda bandarini nazo zipite juu. Nakaribisha maoni
NAUNGA MKONO, ijengwe fly over nyingine juu ya TAZARA, kwa upande wa Tabata serikali wakati wa mwenda zake ilikuwa imeahidi kujenga flyover pale, sijui kama bibi mkubwa kapotezea au la
 
NAUNGA MKONO, ijengwe fly over nyingine juu ya TAZARA, kwa upande wa Tabata serikali wakati wa mwenda zake ilikuwa imeahidi kujenga flyover pale, sijui kama bibi mkubwa kapotezea au la
Tatizo pesa yote inaenda kwenye chanjo, ile sehemu imefikia critical level, ijengwe kama walivyofanya ubungo
 
 
Hali ni mbaya sana muda huu, malorry ni mengi mno, foleni ni kali, uchumi utakua vipi kwa style hii?!
 
Hali ni tete, je, serikali inampango wowote wa kutatua janga hili hapo Tazara?, kama upo, ni upi? Na kama haupo, watupe sababu ni kwanini tuendelee kuwaacha madarakani?!
 
Napendekeza wajenge flyover juu ya Tazara flyover ili zinazotokea Buguruni kwenda bandarini nazo zipite juu. Nakaribisha maoni

Foleni haitokei Tazara ile foleni ni ya buguri pale junction ya manyanya na kwenda ilala
 
Napendekeza wajenge flyover juu ya Tazara flyover ili zinazotokea Buguruni kwenda bandarini nazo zipite juu. Nakaribisha maoni
Foleni ktk eneo tajwa kwa kiasi kikubwa lina chochewa na malori mengi yatokayo na yaingiayo bandarini ....binafsi nikiona vile ni indicator ya kuwa bandari yetu ina piga kazi kwa maana wateja wana ikubali

Lkn pia solution ni ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na ujenzi wa bandari kavu kule mkoa wa pwani kwa kiasi zitapunguza huu msururu wa malori...
 
Back
Top Bottom