Foleni ya Tabata - Tazara imeanza kuwa tishio kwa uchumi wa nchi, nini kifanyike?

Foleni ya Tabata - Tazara imeanza kuwa tishio kwa uchumi wa nchi, nini kifanyike?

Akili za kipuuzi sana hizi, yani badala ya kuboresha miundo mbinu we unawazuia watu haki zao za msingi za kutumia miundo mbinu?
Kwa wale watakaoweza kulipa kwa mwezi wataendelea kufurahia miundo mbinu
 
Foleni Dar es salaam inasababishwa na

Mvua:
Mitaro kuziba na kujaa hivyo barabara kutopitika
Magari mabovu mvua yanazima [emoji28].

Poor Planning:
A.Hatuna long tern plan, majiji makubwa yana rapid buses( tunazo) na tram way, sijaona road reserve ya hii kitu na wengine mpaka metro.

B.Tumekariri flyovers bado kuna short tunnels.mfano Buguruni Unazama kwa wauza mbao pale, unaenda kuibukia kule mbele

C. Hakuna Maintenanc na Constant follow up angalia,
Vituo vya mwendokasi na magari yake, angalia barabara zake.
Njoo kwenye barabara za mitaani huku, hazifagiliwi mitaro haizibuliwi, barabar zinaharibika haraka mwisho barabara za michepuko hukosekana

D.Mamlaka husikai na makadirio: Matengenezo au marekebisho ya barabara inabidi yashirikishe na statical data kutoka kwa mamlaka zinazo control watumiaji wa barabara, tendecy a ongezeko la magari
 
Bila kufanya hivyo,foleni haitaisha, magari yanaongezeka na yanazidi kushuka bei, huko tuendako kila mmoja atakuwa na usafiri utakaosababisha msongamano.
Wapi huko magari yanazidi kushuka bei hayo magari? Wakati kodi ya magari inasimamia ukucha
 
Pale Tazara ni kama ile foleni inatengemezwa na trafiki wa pale Buguruni na Tazara
Hata mimi nilishawahi kuhisi hivyo, muda mwingine unajiuliza, ni kwanini trafiki wa buguruni na Tazara wasifanye coordination kwa radio call na kuita kwa pamoja? Unakuta wa buguruni ameruhusu lakini wa Tazara Kazuia, wa buguruni kazuia, waTazara ameruhusu, sasa si uwendawazimu huo?
 
Napendekeza wajenge flyover juu ya Tazara flyover ili zinazotokea Buguruni kwenda bandarini nazo zipite juu. Nakaribisha maoni
Foleni kubwa inasababishshwa na malori yanayotoka bandarini, tuanzishe bandari ya Bagamoyo.
 
Napendekeza wajenge flyover juu ya Tazara flyover ili zinazotokea Buguruni kwenda bandarini nazo zipite juu. Nakaribisha maoni
Pale walikosea toka mwanzo flyover sawa na zile njia za kukunja ok walichotakiwa ni kujenga Tunnel ya chini pale pale ili hawa wanaopitiliza wasisubiri kitu.
 
Foleni kubwa inasababishshwa na malori yanayotoka bandarini, tuanzishe bandari ya Bagamoyo.
Sio tukamilishe SGR ili malorry yachukulie mizigo huko mikoani badala ya kuja Dar? Au huko Bagamoyo ndio walikwambia wanataka foleni?
 
Sio tukamilishe SGR ili malorry yachukulie mizigo huko mikoani badala ya kuja Dar? Au huko Bagamoyo ndio walikwambia wanataka foleni?
Je unafikiri hiyo train inaweza kubeba mzigo wote toka bandarini?
 
Je unafikiri hiyo train inaweza kubeba mzigo wote toka bandarini?
Hatulengi kubeba yote maana mingine ni ya hapahapa Dar, ila je, unahitaji kuondoa mallory yote ili kupunguza foleni? Au ni kupunguza malorry kwa kiwango cha kutosha?
 
Njia rahisi ya kupunguza foleni kwenye majiji, ingawa itaumiza wengine, ni kuwepo na kodi au tozo ya kila mwezi kwa magari yote binafsi yasiotoa huduma kwa umma, pamoja na kuongeza tozo maeneo ya kupaki hayo magari; Mfano, kama utatumia usafiri binafsi ndani ya jiji na ukawa unatozwa shilingi milioni 1 kwa mwezi, na sehemu yoyote utakayopaki au kusimama kutozwa kodi...hapo lazima magari mengi binafsi yatabaki majumbani, na hapo utakuwa umepunguza foleni kwa asilimia kubwa...kwa sababu kwenda katika shughuli zetu tutatumia usafiri wa umma.
Safi sana mkuu. Na mazingira utakuwa umeyalinda. Uchafuzi wa hewa unaongezeka
 
Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi, nyumba na Maendeleo ya Makazi zivunjwe. Badala yake iundwe Taasisi ya kusimamia mipango miji ya Tanzania nzima. Hakuna kujenga bila kibali cha ujenzi.
Taasisi ijumuishe wataalamu wa kada zote. Taasisi ipange miji yote upya, kwa kuanzisha barabara mpya za ukubwa wa kupitia gari 12. Mifumo ya maji safi na taka kwa kila nyumba. Nyumba moja hadi nyingine kuwe na space ya kutosha kabisa—sahivi ukiongea kwako, jirani wa nyumba ya pili na tatu wanakusikia.
Serikali isiogope kutoa pesa katika kujenga miundombinu hii. Maana miundombinu bora huchochea maendeleo kwa kasi.
 
Njia rahisi kupunguza foleni ni kupunguza magari madogo.unapunza kwa kuongeza kodi kwa magari private magari binafsi. Serikali kupitia TRA Ongeza kodi
Roho ya kimasikini ni mbaya sana, inakufanya uone kama umasikini ni jambo jema,

na kuuchukia utajiri au mafanikio ya watu wengine unawaona kama waovu fulani..

Ndio maana kuna jamaa alisema anataka kuona matajiri wanaishi kama mashetani lakin hakuwahi kusema lolote juu ya anaowaita wanyonge.
 
Njia rahisi kupunguza foleni ni kupunguza magari madogo.unapunza kwa kuongeza kodi kwa magari private magari binafsi. Serikali kupitia TRA Ongeza kodi
 
Back
Top Bottom