Not only FOXEX mkuu, si kila fundi viatu atakua kama Bahressa. Tatizo la Tanzania ni Watanzania Wenyewe, tunamihemko sana kwenye Biashara za Mezani bila kufanya analysis.Mkuu Deadbody Forex ilikuwepo kabla hata Ontario hajazaliwa, Forex ipo na itaendelea kuwepo. Wenye akili zao zilizotulia wanapiga hela na wataendelea kupiga hela. Niliwahi kuandika humu, na ninaandika tena, Forex trading is not for everyone.
Biashara ya Forex haifanywi na kila mtu, hii biashara inahitaji uelewa mkubwa sana wa mambo ya kiuchumi yanayotokea kila siku kwenye soko la fedha. Ni Watanzania wachache sana wenye akili ya kujua hivyo vitu na kuvifuatilia kwa karibu. Watanzania wengi wanapenda habari za udaku na umbea, habari za biashara za kimataifa hawazijui wala solo la fedha la kimataifa hawalijui achilia mbali misamiati inayotumiwa katika soko hili kwa Watanzania wengi ni giza nene.
Mimi nilijua tu Wabongo wengi wataanguka katika hii biashara sababu wengi kutokana na kutokuelewa mambo wanaiona Forex kama kamari, na ndivyo ilivyo, kama huna uelewa mzuri Forex trading itakuwa kama kamari kwako, lakini kama unaouelewa mzuri, Forex trading ni biashara kama biashara zingine.
Kuna watu wanavuta mkwanja na wametulia kimya kabisa.
Kweli kabisa mkuu.Not only FOXEX mkuu, si kila fundi viatu atakua kama Bahressa. Tatizo la Tanzania ni Watanzania Wenyewe, tunamihemko sana kwenye Biashara za Mezani bila kufanya analysis.