Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Status
Not open for further replies.
Me nilidhani kuwa huyu Ontario na malaika fulani hiki ametumwa na mungu aje aniondolee tatizo la pesa.
Nikasoma page 1 baada ya nyingine aisee.Kwa kifupi nilikesha nikiwaza kuwa baada ya miezi kadhaa walionidharau wataniheshimu sasa.

Ukifungua threads za FOREX namwona malaika wangu anasisitizo tena ni kwamba kama halazimishi watu kuhudhulia class maana mahela aliyokuwa nayo yanamtosha.

Habari zikaenea kila kona JF ni FOREX.Hata ukifungua jukwaa la mapenzi huko utaona wakina SHUNIE wanachati FOREX.Yaani kwa kifupi niliona bomba la mihela inaellekea kwangu.

Haijakaa sawa namuona mahondaw anatumiwa reply za FOREX na MARIO wake Smart911 kuhusu FOREX hadi ikawa sio siri tena .

Mtaani kwetu Ukonga hadi Bombani namsikia jamaa yangu Stereo ananielezea kuwa tujiunge Forex baada ya kuona mziki haulipi.Yani wa kifupi ilikuwa ni mchakamchaka nguo kuchanika kuelekea safari mpya ya kuitwa boss kupitia TMT.

Dah na hii sehemu ikanifanya niamini hata urais haulipi

View attachment 773863

Maisha yakaanza kuchange pale tu tulipoanza kutrade "Live ".

Kasha nyingi zikaibuliwa mapema kabisa kama hizi zifuatavyo:

SHAHIDI: Majibu kwa Ontario kuhusu kuitwa tapeli wa Biashara ya Forex kupitia TMT (II)

Majibu kwa Ontario kuhusu kuitwa tapeli wa Biashara ya Forex kupitia TMT




Soma zaidi>>>Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!


View attachment 773851
Pole Sana mkuu, FOREX ni biashara ya ukweli Sana, tatizo Ontario aliwaonyesha Dalali tapeli (fake Broker) wapo madalali wazuri mno wa FOREX, Ontario pumbavu sana akashawishi watu wajiunge na JP markets kumbe ana kamisheni kila watu wakiunguziwa akaunt, FOREX ni lazima uijue vizuri kwanza inahitaji ujisomee sana kuijua FOREX na uwe na smart mind, na siyo kukurupuka tu hapo lazima uichukie FOREX, ukiijua vyema, hakuna biashara yenye pesa Duniani kama FOREX, yaani Hakuna.
 
Hivi "Double Entry" system ya Forex imekaaje?
Niki-Debit kwangu, wapi kunakua Credited?
Yaani niki-gain, nani ana loose?, na niki-loose nani ana-gain?
uki gain ume gain Hakuna anaye loose, ni pesa yako imezaa, na Broker naye ana gain 12% ya pesa yako uliyotumia ku trade, mfano $5 per single trade wewe unapata $4 na Broker $1,uki loose Broker anakula yote $5,FOREX tamu Sana hakyanani.
 
Mkuu Deadbody Forex ilikuwepo kabla hata Ontario hajazaliwa, Forex ipo na itaendelea kuwepo. Wenye akili zao zilizotulia wanapiga hela na wataendelea kupiga hela. Niliwahi kuandika humu, na ninaandika tena, Forex trading is not for everyone.

Biashara ya Forex haifanywi na kila mtu, hii biashara inahitaji uelewa mkubwa sana wa mambo ya kiuchumi yanayotokea kila siku kwenye soko la fedha. Ni Watanzania wachache sana wenye akili ya kujua hivyo vitu na kuvifuatilia kwa karibu. Watanzania wengi wanapenda habari za udaku na umbea, habari za biashara za kimataifa hawazijui wala solo la fedha la kimataifa hawalijui achilia mbali misamiati inayotumiwa katika soko hili kwa Watanzania wengi ni giza nene.

Mimi nilijua tu Wabongo wengi wataanguka katika hii biashara sababu wengi kutokana na kutokuelewa mambo wanaiona Forex kama kamari, na ndivyo ilivyo, kama huna uelewa mzuri Forex trading itakuwa kama kamari kwako, lakini kama unaouelewa mzuri, Forex trading ni biashara kama biashara zingine.

Kuna watu wanavuta mkwanja na wametulia kimya kabisa.
Nadhani sasa amekuelewa, Hakuna biashara tamu na yenye pesa Kama FOREX Duniani, mimi kwa mtaji wa $100 tu kila siku nakuja $45 faida sawa na sh 110,000 Kwa siku, niliteseka Sana kujifunza na wakati naanza nilikula loss zaidi ya mara tatu lakini sikukata tamaa, Leo nakula bata tu.
 
Forex iko na faida kama utakubali kufuata taratibu zake.

Ila ukiingia kwa pupa, umeliwa
 
Kujaribu hutaki inaishia kusikiliza wanayosema watu. Watu mwataka mlishwe kilichotafutwa na wengine, shughuli gani duniani hapa isiyohitaji kutumia akili, fedha na muda kuifanikisha?
 
Forex iko na faida kama utakubali kufuata taratibu zake.

Ila ukiingia kwa pupa, umeliwa
Ukiwa na akili kama za jiwe utaichukia mno FOREX, lakini ukiwa na bongo iliyotulia Kama ya Obama au Clinton ,aisee FOREX ni tamu mno, "you should treat FOREX just like any other business that has Profit and Loss".Ukijua hiyo slogan, FOREX inakutajirisha asubuhi tu.
 
Nadhani sasa amekuelewa, Hakuna biashara tamu na yenye pesa Kama FOREX Duniani, mimi kwa mtaji wa $100 tu kila siku nakuja $45 faida sawa na sh 110,000 Kwa siku, niliteseka Sana kujifunza na wakati naanza nilikula loss zaidi ya mara tatu lakini sikukata tamaa, Leo nakula bata tu.
Kuna mwenzako humu jf anaitwa anaitwa CCNP ENGINEER alikua anasema anapiga sio chini ya ma million kila wiki huko FOREX mara paap kafungua thread anaomba ushauri anataka kukopa mil 5 aache kazi akafanye ujasiriamali,hahah
 
Mitaa niliyokulia mimi hakuna mtu anatapeliwa kizembe kuanzia mtoto mdogo hadi wazee,maana matapeli nguli wametokea huko.
Kuna kanuni za maisha ambazo ukizifuata hutakaa utapeliwe.
1.hakuna mtu atakaye kuunganisha kwenye fursa zaidi ya watu wako wa karibu,baba,mama,dada etc.sio mtu baki,we hujiulizi mtu akute mfereji wa hela saa ngapi anapata muda kuwatangazia humu jf?,binaadamu yuko radhi akuonyeshe matumizi yake na sio anapopatia hela.

2.If its sounds too good to be true,its definately not true.Ukiona/kukutana na 'fursa' ambayo inasisimua na kuonekana iko perfect sana basi weka alama ya kiulizo,jamani hakuna namna utaweza kupata mihela kirahisirahisi,ize touch,yaani upakuwa tu mshiko kama una nawa,hela kuipata lazima uminyike one way or another.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom