MWANA WA NGURUMO
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 228
- 473
Very professional advice. Nimependa sana uchambuzi wako huu kk.Hii ni kwa ajili yako mkuu sana Lodrick Thomas pamoja na infant traders wengine.
Naona umeingia live, hongera sana kwa uthubutu uliochukua, so impressing. Lakini nashangaa unafanya makosa ambayo ni very obvious hutakiwa kufanya. As I said earlier, There's a very thin line separating forex and gambling, mstari unaotenganisha FX na betting ni mwembamba sana. Kuna picha (screen shot) ulishare, 1 kwa 1 niseme unachokifanya si financial trading bali ni gambling.
Edited: screen shot ya Lodrick![]()
Kwenye fx, Ukifanya analysis unatoka na conclusion 1 tu; Either to buy or to sell or to stay away from the market... and the most important thing is ni kuanalyse entry point and exit point. Lazima utambue kuwa it takes the same skills and efforts to realise there isn't a trade as it takes to find a trade
Ulichokifanya kwenye hiyo screen shot ni indiscipline, utovu wa nidhamu. Haiwezekani same currency EURUSD ukasell na ukaBuy [emoji23] [emoji23] . Yani ni utovu wa hali ya juu sana in forex. Yani hapo maana yake ni liwalo na liwe - cha kufia nini (kama ulipita jeshi). Hapo ulipaswa ufunge trades za sell na kuacha za buy zirun or vise versa. Na kama haukua na uhakika bora ungelikimbia soko hadi opportunity ije.
FX ni kama biashara zingine boss, kama hakuna fursa basi hakuna haja ya kufanya biashara. Ni jambo la ajabu sana mtu akaenda Rorya vijijini huko kisha akafungua massage parlour, sawa na FX yani hauoni fursa lkn unalazimisha kutrade.
Kuuza na kununua currency pair 1 boss ni kosa litakuja kuunguza a/c yako kama ukiliendekeza. Yani ni jambo la ajabu sana unakuta mtu yupo kwenye Buy ya XAU/USD at the same time yupo kwenye sell ya AUDUSD. Au unakuta mtu anauza Aussie (AUDUSD) na muda huo huo ananunua kiwi (NZDUSD). Yani ni nidhamu ya kiwango cha standard gauge. Au unakuta mtu amebuy Brent oil (USOIL) at the same time yupo ktk buy ya USDCAD.
●●But usiwe na presha ndipo tulipotoka bro... Tutaelezeana mdogo mdogo - lkn ukiwa na haraka haraka, unaeza kujifunza kwa njia ngumu na ndefu sn.
Wiki iliyopita currencies zilikua hazijakaa poa sana, hasa pairs za USD. Kuna yule Kijana wangu mmoja akaingia buy USDCAD alivyonitumia screen shot, nikashtuka sana maana tyr alikua ana loss ya -60 USD. Nikamwambia funga positions zote, kisha nikamwambia nunua mafuta chap chap - Dogo akaingia sokoni akanunua mafuta, ndani ya muda wa km siku 2 akagonga zake $140 tukaifunga wiki kwa amani.
Edited: screen shot ya jamaa'ngu.![]()
==============================
Edited:
Pia kwa lot size unayotumia eeishhh. Itakuchukua muda mfupi sana kutia kiberiti account yako. Kijana wangu alianza $150 (though sikukubaliana naye - hakukua na jinsi) mpk leo account yake ina balance ya 437... lkn anatumia lot za 0.01 mwisho kbs ni 0.02 kama nikimruhusu. Unachokifanya wewe kwa account ya $70 kutumia lot ya 0.23 ni uncalculated risk ama uroho. Boss forex ukiiletea uhoro inakuchambua kama karanga.
Nami ktk kujifunza kwangu demo niligundua kuwa kama nime buy EUR/USD I don't expect at all nikafungua Sell position ya GBP/USD.
Salute boss