Papaa Azonto
JF-Expert Member
- Jun 30, 2013
- 319
- 277
Nilijiuliza sana sana kwanini ipande. Hii pair ya usdjpy imenitenda. Anyway sehemu ua kujifunza zaidi.Habari za mda huu wadau??
Nadhani wote tunajua kinachoendelea huko kwa wenzetu hasa kati ya N.Korea na Japan!! Jana N.Korea alivurumisha kombora juu ya anga la Japan na kutua kwenye bahari jiran kabisa na pwani ya japan!! Kwa kifupi kuna hali tetea huko mashariki ya mbali!!
Anyways, kama ukiangalia baada ya N.Korea kutangaza kurusha kombora, Yen ilianza kupanda nabaada ya kurusha kombora Yen ikapanda maradufu, nadhani USDJPY ilitoka 109 mpaka 108 within very short period of time!! kilichonishangaza kwanini Yen ipande badala ya kushuka hasa ukizingatia Japan ndio ilikua kwenye hali ya kushambuliwa??
Katika pita pita zangu kwenye huu uzi na kwenye sites nyingine, Yen inajulikana kama "Safe haven" na mara nyingi inakua kimbilio la wawekezaji kipindi cha machafuko! Baada ya kugundua hili sikushangaa what happened yesterday!!
EURUSD ime-hit 1.2 na bado inaelekea north!!
Mpaka sasa naona dola ya Marekani inafanya vibaya. Nangoja reaction ya USA, China na Urusi kuhusu tukio la jana....
Sent using Jamii Forums mobile app