Formula 1® Grand Prix special thread

Formula 1® Grand Prix special thread

Bahrain GP 2018: Classification
  1. Vettel - Ferrari
  2. Bottas - Mercedes
  3. Hamilton - Mercedes
  4. Gasly - Toro Rosso
  5. Magnussen - Haas

Mkuu leo sijaangalia F1 nilikuwa stadium ila nimesikia ice man kamuumiza mtu inbox.pia hongera timu yetu toro rosso
 
Mkuu leo sijaangalia F1 nilikuwa stadium ila nimesikia ice man kamuumiza mtu inbox.pia hongera timu yetu toro rosso
Kimi kapata bahati mbaya sana leo... Hopefully huyo mechanic hajapata madhara makubwa!

Zaidi nuksi leo ilikuwa kwa Red bull , gari zote mbili nje!

Gasly wa Toro Rosso kashindana kwa utulivu bila matatizo....
 
Kimi kapata bahati mbaya sana leo... Hopefully huyo mechanic hajapata madhara makubwa!

Zaidi nuksi leo ilikuwa kwa Red bull , gari zote mbili nje!

Gasly wa Toro Rosso kashindana kwa utulivu bila matatizo....

[emoji106][emoji106]yaani ofisi yangu mkuu na toro rosso ni karibu mno najua kesho itakuwa sherehe
 
Adrian Newey leo gari zake zimetoka zoote dahh ila jamaa ni genius sana kila timu aliyowahi kwenda nasikia aliwahi kushinda ubingwa wa dunia kama ukiwa na muda mcheki historia yake huyu jamaa miaka aliyoshinda vettel na Redbull ni yeye alikuwa anaitwa ubongo wa Redbull
 
Chinese Grand Prix 2018: Qualifying Results
  1. Vettel
  2. Räikkönen
  3. Bottas
  4. Hamilton
  5. Verstappen
  6. Ricciardo
 
Chinese Grand Prix 2018: Classification
  1. Ricciardo - Red Bull
  2. Bottas - Mercedes
  3. Räikkönen - Ferrari
  4. Hamilton - Mercedes
  5. Verstappen - Red Bull
  6. Hulkenberg - Renault
  7. Alonso - McLaren
  8. Vettel - Ferrari
  9. Sainz - Renault
  10. Magnussen - Haas
 
Vesterpen akiona rangi nyekundu ya Ferrari kichwa kinamruka safety car leo imewasaidia timu ya Milton keyes(Redbull) Lewis inabidi aamke sasa bahati nzuri vettel leo kafika wa nane vinginevyo leo tena ingekuwa kilio kwake.
 
Namkubali sana bottas...sema mda mwingi anafunikwa na kivuli cha hamilton!

Bottas kachukuliwa awe namba 2 pale tu ikitokea Hamilton ana tatizo yeye anatakiwa azibe pengo.F1 ukiwa na jogoo wawili kwenye tundu moja inakuwa ngumu kuwadhibiti angalia 2014 na 2016 Nico Rosberg na Lewis Hamilton walikuwa wao magari yao yapo fiti zaidi ya wengine ila walikuwa wanatupana nje kama kule hispania round ya 1 waligongana wenyewe wakatoka nje haikuishia hapo kule austria na uhasama ulianzia kule Spa Francorchamps,Rosberg alimgonga mwenzake.na ndivyo ilivyo F1 toka kina Ayrton Senna na Alan Prost.Ferrari hili hawalitaki ndiyo maana wana dereva namba 1 na 2 dereva namba 2 kazi yake ni kumlinda namba 1 tu anatakiwa achukue kazi ya dereva namba 1 pale likimtokea tatizo dereva mwenzake namba 1. Kama hawa madereva wawili yaani 1 na 2 wote wawe huru lazima ugomvi utakuwepo sana.kama mwaka jana ukiangalia Force India kati ya sergio Perese na Esteban Ocon walikuwa wanapambana wenyewe kwa wenyewe mpaka walikuwa wanagongana.mpaka team principal anashindwa kuwapa muongozo nani ampishe mwenzake ndiyo huwa inatokea lile munapambana ndugu kwa ndugu.
 
Bottas kachukuliwa awe namba 2 pale tu ikitokea Hamilton ana tatizo yeye anatakiwa azibe pengo.F1 ukiwa na jogoo wawili kwenye tundu moja inakuwa ngumu kuwadhibiti angalia 2014 na 2016 Nico Rosberg na Lewis Hamilton walikuwa wao magari yao yapo fiti zaidi ya wengine ila walikuwa wanatupana nje kama kule hispania round ya 1 waligongana wenyewe wakatoka nje haikuishia hapo kule austria na uhasama ulianzia kule Spa Francorchamps,Rosberg alimgonga mwenzake.na ndivyo ilivyo F1 toka kina Ayrton Senna na Alan Prost.Ferrari hili hawalitaki ndiyo maana wana dereva namba 1 na 2 dereva namba 2 kazi yake ni kumlinda namba 1 tu anatakiwa achukue kazi ya dereva namba 1 pale likimtokea tatizo dereva mwenzake namba 1. Kama hawa madereva wawili yaani 1 na 2 wote wawe huru lazima ugomvi utakuwepo sana.kama mwaka jana ukiangalia Force India kati ya sergio Perese na Esteban Ocon walikuwa wanapambana wenyewe kwa wenyewe mpaka walikuwa wanagongana.mpaka team principal anashindwa kuwapa muongozo nani ampishe mwenzake ndiyo huwa inatokea lile munapambana ndugu kwa ndugu.
Okkk...leo ndo nmeelewa sasa, ila marcedes wanaelewana sana na wako vizur!!

BTW uko vizur mzee....unafuatilia sana haya mambo....me napenda sana F1 ila majukum tu na hivi ving'amuz vyetu hawaonyeshi mda mrefu!
 
Okkk...leo ndo nmeelewa sasa, ila marcedes wanaelewana sana na wako vizur!!

BTW uko vizur mzee....unafuatilia sana haya mambo....me napenda sana F1 ila majukum tu na hivi ving'amuz vyetu hawaonyeshi mda mrefu!

Ndiyo hivyo aisee waswahili wanasema mafahari wawili hawakai zizi moja na hii iliwahi pia kutokea kwa Maclaren 2007 wakati inaitwa Maclaren Mercedes.Ron Dennis alimchukua Lewis Hamilton kama mwanafunzi wake toka drive academy akamuunga na Fernando Alonso kipindi hicho Alonso alikuwa bingwa wa dunia alishinda 2006,wakati Hamilton ni mwaka wa kwanza kuingia Katika F1.kabla ya hapo alikuwa kwenye mashindano yanaitwa Kart ni mbio za magari nazo ila zinaibua madereva wadogo.Ron Dennis alimuona anafaa akamchukua akamuweka kama dereva namba (2) namba (1) alikuwa ni Alonso sasa wakaanza vizuri tu Australia Hamilton alijitahidi ila history ni ndefu mpaka mwaka ule Alonso ulivyoisha akahama timu.kuna mambo mengi yalitokea ikiwemo lile skendo la Spy Story na ni mwaka ambao Alonso na Hamilton walimaliza kwa point sawa ushindi wa dunia alishinda kimi raikonen kwa point 1 na ndiyo alikuwa dereva wa mwisho kushinda ubingwa wa dunia na Ferrari.2007 mambo mengi yalitokea ikiwa lile la Alonso kumfanyia mwenzake makusudi ndani ya box.Alonso alibadilishwa matairi akapewa ruhusa yeye akawa amebaki tu pale halafu nyuma yake alikuwa Hamilton na unajua kwenye mashindano haya hata sekunde moja ni muhimu kwa kumchelewesha mwenzake na ilikuwa Q3 Lewis akashindwa kuzunguuka muda uliisha sasa team principal akakasirika na injinia wa Alonso.maneno yalikuwa mengi mpaka Alonso akasema Maclaren timu ya uingereza inampendelea muingereza Lewis.na ilikuwa tafrani Lewis alisema Alonso au mimi mmoja ataondoka. Kawaida ya mashindano haya mukiwa na point sawa inaangaliwa nani kashinda mashindano mengi na kama mmmeshinda sawa inaangaliwa nani ana pole posizione sana. Mwaka 2007 Hamilton alikuwa mbele ya Alonso na ni kwa mara ya kwanza Alonso kuwa nyuma ya dereva mwenzake yaani namba 2.mwaka ule Lewis na Alonso ubingwa waliutupa wenyewe tu.kulikuwa na matatizo ya timu mwanzo walimuona Alonso ni kiranja baadae wakageuza upande wakaona kumbe hata dogo naye ni mtaalam.ilifikia kipindi kama sikosei itakuwa 2008 mwaka ambao Hamilton alishinda ubingwa wake wa kwanza wa dunia ilikuwa hispania akawa analindwa na walinzi kwa sababu ya mashabiki wa Alonso.
 
Azerbaijan Grand Prix 2018: Qualifying Results
  1. Vettel
  2. Hamilton
  3. Bottas
  4. Ricciardo
  5. Verstappen
  6. Räikkönen
 
Azerbaijan Grand Prix 2018: Race Results
  1. Hamilton
  2. Räikkönen
  3. Perez
  4. Vettel
  5. Sainz
  6. Leclerc
  7. Alonso
  8. Stroll
  9. Vandoorne
  10. Hartley
 
Huu uzi hasa umenigusa hasa na nitautendea haki hapo mbeleni. nahusika moja kwa moja ndani ya Grad prix katika hii nchi husika mwanzo mwisho. stay tuned.
 
Back
Top Bottom