Forojo Ganze (Master), mchawi maarufu aliyeanzisha Mwenge wa Uhuru

Forojo Ganze (Master), mchawi maarufu aliyeanzisha Mwenge wa Uhuru

kwa maana nyingine unamaanisha kuwa neno 'harambee' ni mantra? (mantra ni neno maalum lenye energy ambalo likirudiwa mara nyingi lina produce a certain effect}.
ujue hata wayahudi kina ben Gurion mwaka 1948 nchi yao waliamua waiitie ISRAEL ikiwa ni muunganiko wa majina ya miungu wao watatu ISIS, RA, na ELOHIM. Isije ikawa huyu HAR ikawa ni corruption ya jina RA au RAMA wa mahabarata.
Mkuu huyu ISISI anatofauti gani na yule wa Misri?
 
Nchi hii itatoka tu mikononi mwa shetani ngoja awaondoe kwanza vizazi vya kichawi


Mungu muumba mbingu na nchi atamalaki
 
Nchi hii itatoka tu mikononi mwa shetani ngoja awaondoe kwanza vizazi vya kichawi


Mungu muumba mbingu na nchi atamalaki
Mkuu itatoka au ndio inaelekea kwenye mikono ya Shetani.Ndugu yangu ujio wa Mpinga Kristo,the reincarnation of Satan or Satan in the body,is eminent na Covid-19 is the greatest tool the NWO cabal is using to achieve that.Nchi hii na Dunia kwa ujumla vitarudi kwa Mungu in Jesus Christ's 1000 year rule on Earth after the Great Tribulation au Dhiki Kuu,so bado.
 
"Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini, faraja palipo na huzuni, tumaini pasipo na tumaini, upendo penye chuki na heshima palipo na dharau"

Baada ya kutamka hayo mbele ya Mwl.Nyerere, Ganze alikata roho na ndipo ukaanzishwa Mwenge wa Uhuru. Kinachonishangaza hapa ni kile kipengele kisemacho"UMULIKE NJE YA MIPAKA YETU"..... Inamaana ndani ya nchi tubaki gizani kama tulivyo sasa? Na kwann Forojo Ganze hakutangazwa kama mwanzilishi wa Mwenge?
alitamta neno hata nje ya mipaka yetu na si umulike nje ya mipaka yetu
 
Kukimbiza mwenge ni agenda ya kipepo kabisa.Tunapoteza fedha nyingi sana kwenye shughuli hii ambazo zingeweza kutuongezea madarasa ya shule za msingi,zahanati au kufanya shuhuli zingine za maendeleo.

Ukiangalia kwenye Satanic symbols utaona kwamba mwenge ni moja wapo ya satanic symbols.

Kama taifa nadhani hatuna budi kutafakari upya jambo hili na kuufuta.Ajenda yake ilikuwa ovu kabisa:kupumbaza wananchi.Sidhani kama ajenda hii bado serikali yetu inayo.

Sijui ndio maana Watanzania tupo kama tulivyo!?Natafakari tu.
 
Huyu Forojo Ganze,alikuwa ni mmoja kati ya wazee waliotumwa kufanya zindiko la nchi baada ya uhuru kule bagamoyo,walipewa kazi ya kuhakikisha rais aliye madarakani hapingwi na mtu yeyote(Mwl.Nyerere),zindiko hilo lilifanyika bagamoyo ktk moja ya mashimo yanayopatikana wilayani hapo,zoezi hilo lilienda sambamba na kumuuliza shetani na malaika zake ni jambo gani lifanyike ili Tanzania iendelee.

Forojo Ganze ndiye mtu pekee aliyeingia ktk hilo shimo kwaajili ya kuuliza,alikaa huko kwa muda wa siku 10 huku akiwa amewaacha wenzake nje wakimgoja atakuja na jibu gani ili wakampatie rais na wazee wa Dar es salaam,kilichoshangaza siku ya kumi na moja alitoka akiwa hoi hajiwezi akiwa kama mtu aliyepigwa na alikuwa anaongea lugha isiyofahamika,wenzake wakiwa wanaongozwa na Yahaya Hussien walimbeba hadi ikulu Dar es salaam na walipomfikisha mbele ya mwalimu Nyerere alitamka maneno hayo yanayohusu mwenge kwa kiswahili kisha akanyoosha juu mkono wake wa kulia ambao tayari ulikuwa umeandikwa namba hii 115,kisha akakata roho,baada ya mazishi mwalimu aliyafanyia kazi maneno ya Forojo Ganze akaanzisha mwenge wa uhuru bila kujua ulikuwa na maana gani,baada ya hapo aliwagiza yahya Hussein atafasiri maana ya ile namba 115.

Kama kawaida ya shehe Yahaya alitafasiri akamwambia kuwa namba hiyo inamaanisha "utakufa ukiwa na umri wa miaka 77 na taifa la Tanzania kwa kipindi hicho litakuwa na umri wa miaka 38,hii inamanisha ukichukua 77 umri wa mwalimu jumlisha 38 umri wa taifa utapata 115,na hii ndivyo ilivyokuwa,mwaka 1999 mwalimu alikufa akiwa na miaka 77 na taifa lilikuwa na miaka 38 ya uhuru (77+38=115) pia utamaduni wa rais kuongea na wazee wa Dar es salaam unaendelea hadi sasa na wamekuwa na maamuzi ya kitaifa na husikilizwa sana wanachokisema,mbona haijawahi kutokea rais akaongea na wazee wa bukoba jambo la kitaifa?,zindiko la bagamoyo linafanya kazi ,Safu hii ilikuwa ya watu 5 ambao ni. 1.mzee ramadhan,alizaliwa mwaka 1920,2.Ally tarazo(1929),3.Komwe wa Komwe(1918),4.Sheihe Yahya Hussein(1925),na 5.Forojo Ganze (1902)
Hii story niliipitia nikaona kama imekaa ki-propaganda zaidi na ki-danganyifu zaidi sababu kama ni kweli hao wazee walikuwa wana uwezo huo iweje tutawaliwe kwa muda mrefu kiasi hicho? Na pia iweje wajitokeze kipindi cha mwishoni wakati tunapambania uhuru wakati wangemaliza kazi before hata kutawaliwa?
 
FOROJO GANZE vipi hakuwa na watoto,Kama wapo, wapo wapi na wanafanya nini
 
Natamani hiyo historia ya kilwa,mkuu tuletee tafadhari au ni tag ukiweka uzi wake mpya
 
ooohhh....thanks for ellaborating. Sasa unaona jinsi watu walivyokuwa misled. I thought they pray 'to' rocks not 'on' rocks

haha niliuliza kama waislamu wamekuja na mapepo au na mapepo walikuwepo huku toka zamani? Siajabu hata maana yangu ya mapepo ni tofauti na yako
mapepo yalikuwepo kabla ya ADAM hajaumbwa
 
Hii story niliipitia nikaona kama imekaa ki-propaganda zaidi na ki-danganyifu zaidi sababu kama ni kweli hao wazee walikuwa wana uwezo huo iweje tutawaliwe kwa muda mrefu kiasi hicho? Na pia iweje wajitokeze kipindi cha mwishoni wakati tunapambania uhuru wakati wangemaliza kazi before hata kutawaliwa?
Rudia tena kusoma, bandiko linasema ni zindiko kwa rais Nyerere maana yake uhuru ulikuwa tayari, sio zindiko kwa ajiri ya kuwaondoa wakoloni, hata hivyo hao wakoloni mpaka wametucolonize maana yake walituzidi kila kitu mpaka nguvu za kichawi.
 
Rudia tena kusoma, bandiko linasema ni zindiko kwa rais Nyerere maana yake uhuru ulikuwa tayari, sio zindiko kwa ajiri ya kuwaondoa wakoloni, hata hivyo hao wakoloni mpaka wametucolonize maana yake walituzidi kila kitu mpaka nguvu za kichawi.
Hapa kuna hoja mbili mkuu kwa jinsi nilivyo elewa kutoka kwenye maandishi yako na kutoka kwenye maandishi yangu ya mwanzo.

1. Hoja ya pili ni kuwa zindiko lilikuwa ni kwa ajili ya Mwl pekee na ilikuwa ni baada ya uhuru,.. hii ina maana ya kuwa taifa halijazindikwa/ kuwekwa kwenye maagano na shetani kama mleta mada & wachangiaji kadhaa jinsi walivyodai,...... Swali,., mwenge ulionzishwa mbona umeanzishwa kwa ajili ya taifa na sii Mwl.? Na pia mbona inadaiwa mambo ya mazindiko yalianza hata kabla ya uhuru?

2. Hoja ya kwanza( kutoka kwenye andiko langu)---- Hao akina Forojo walianza kazi zao kabla ya kupata uhuru ila nchi ilikuwa kwenye harakati za kupata uhuru (rejea habari za wazee wa Pwani & Dar es salaam), .................... ilikuwaje washinde kufanya hayo mambo toka enzi za vita za majimaji au kabla ya hapo kama ni kweli mazindiko yao yalikuwa ni ya kweli? na yana uwezo huo unao zungumzwa hapa?
 
Hii story niliipitia nikaona kama imekaa ki-propaganda zaidi na ki-danganyifu zaidi sababu kama ni kweli hao wazee walikuwa wana uwezo huo iweje tutawaliwe kwa muda mrefu kiasi hicho? Na pia iweje wajitokeze kipindi cha mwishoni wakati tunapambania uhuru wakati wangemaliza kazi before hata kutawaliwa?
Uchawi wa kiafrika haufanyi kazi kwa Mzungu.
 
Ungeendelea kutujuza, sasa wewe unatupa somo kabla hatujajua linahusu nini unatuswalika maswali..!? ngoja waje wajuzi, mine is an ordinary mind...!
Labda alikata moto baada ya kuanza andiko
 
Back
Top Bottom