Frederick Mpendazoe atimkia CCJ...

Frederick Mpendazoe atimkia CCJ...

Kweli huenda wengi wakitoka Msekwa na kundi lake wataona kuwa Mpendazoe si ndoo moja ya maji katika mto rufiji kama alivyoongea na mwandidhi wa BBC, Ila Msekwa anaoneka ana sauti ya woga na kuanza kulalamika bila kujibu maswali, wengi watafuata- eti akutukutanae hakuchagulii tusi na Mpendazoe kawatukana kusema chama kimeingiliwa na wafanyabiashara wanaolinda masilahi yao.
http://www.bbc.co.uk/mediaselector/check/swahili/meta/tx/swahili_1530?size=au&bgc=003399&lang=sw&nbram=1&nbwm=1

Ukitaka kupata mahojiano na BBC peleka player mbele karibu na mwisho, maana haya ni matangazo ya saa nzima na mahojiano nafikiri yapo katika dakika za 50+
 
Mpendazoe hakuhamia ccj kwa maslahi ya watanzania wenzake, bali ni kwa ajili ya matakwa yake binafsi, na kwa kutegemea maslahi binafsi kutoka CCJ. Hakunas mtanzania yeyote mwenye akili timamu anayeweza kushawishiwa na maoni ya mbunge huyo, kwamba amehamia huko kwa ajili ya kuwakomboa watanzania wenzake!
 
Ndugu mwanafalsafa umeuliza swali au maswali ambayo hayatakiwa
kulizwa kwa kipindi hiki.

Sijaona sababu ya wewe kuitwa au kuonekana unatetea mafisadi post yako ya kwanza ilionyesha unavyowaza wewe. Kuna vitu viwili vinavyoendelea sasa hivi

ambavyo ni

1. CCM iondoke no matter what
2. Any one who supports CCM ni fisadi

Hizo issue mbili hapo juu ni kubwa mno na utakuja kugundua kuwa unachosema si sahihi kama tunaangalia point number moja tu. kwa sababu tumechoka then CCM iondoke! I am also agreeing with this , hivyo kwa hali ya sasa hongera na shukrani zimwendee Mpendazoe

Point ya pili ni paradox na ambayo kwa sasa is not applying due to our current situation. Hivyo kuita fisadi haimaanishi ni fisadi, au kuambiwa mtetea fisadi kwenye forum haimaainishi uko hivyo. Point number ya pili ni kuwa we need to evaluate every move ya siasa zinazoendela nchini mwetu.

Mpendazoe kaondoka well and good. the next questions is. His he for real? what makes him to decide this time? why is going to CCJ? what is he planning? CCJ inaweza isifanye uchaguzi mwaka huu, hivyo na yeye anaweza asichaguliwe, je lengo hapa ni nini? kwa nini hakwenda chadema au CUF ? Sijaona na kamwe sitaona ubaya wa kuuliza haya maswali!!! kama nina uhuru wa fikra maswali yako hayakwepeki kabisa!

- Mpaka hapo tupo pamoja sana mkuu na hasa hayo maswali.

Nilichofurahia sana kuhusu issue ya Mpendazoe ni kuwa kawaanika wana JF wengi sana ambao ni wanafiki wa fikra na nafasi zao

1. Kuna tabia humu ya kusifia baadhi ya wabunge na waliitwa wapiganaji, je hawa wapiganaji leo hii ukiwaweka mizani moja na mpendazoe nani zaidi?

2. Je kusifiwa kwa wale wabunge wa CCM ni upungufu wa akili zetu? kwa nini usifie baadhi ya watu ndani ya CCM na leo akiondoka huyu CCM inapondwa? ina maana wale waliokuwa wanamwaga sifa kwa wabunge wapiganaji walikuwa wanafanya hivyo kama jadi? kufuata mkumbo, au ni nini hasa?

- Hapa hapana, kwanza bado kujua ni kwa nini Mpendazoe ameondoka na besides kila chama duniani huwa kina makundi ya aina mbali mbali tupo kwenye dunia ya mwaka 2010 unaondoka na sababu na una uhakika na unakokwenda, sio kuondoka tu kama Mrema binafsi ninawaunga mkono sana wapiganaji walioko ndani ya CCM ninaamini bila wao wananchi tungeishia kuliwa viboko na kina Lowassa, ambaye mpaka leo angekwua bado kwenye power.

- Mimi ninawa-support wapiganaji na wewe huwa-support ongea hoja lakini sio matusi kama ulivyoanza tayari, tatizo sio kuondoka CCM tatizo ni unakwenda wapi? kwa nini na kwa masilahi ya nani?

Respect


FMEs!
 
- CCJ watapata usajili mwaka huu na watashiriki uchaguzi kwa nguvu ya wafadhili, lakini are they for real au? ni yale yale tu, binafsi simfahamu vizuri huyu Mpendazoe vipi ikiwekwa record yake kama ipo?

Respect.


FMEs!

Mkuu
mie nafikiri wakijienguwa wengi bila kujali ni mafisadi ama sio mafisadi,ccm itakosa nguvu na hatimaye kubalansi mambo na sie watoto wa masikini we can do something ktk system iliyo balansi.

Na hata rostam na lowasa wakijiengua na wakaanzisha chama chao ni bora pia maana equilibriamu itapatikana.

Kutafuta mtu msafi ktk viongozi waliopo wenda wasiwepo kabisa. Saihiz cha kufanya nikuivunja vunja system ili kuwe na equal chansi, lakini mkianza kuwa filter sidhani kama ni njia sahihi, maana karibu wote watawala na wapinzani ni si wasafi wasiofuta kanuni na sheria.
 
Mpendazoe hakuhamia ccj kwa maslahi ya watanzania wenzake, bali ni kwa ajili ya matakwa yake binafsi, na kwa kutegemea maslahi binafsi kutoka CCJ. Hakunas mtanzania yeyote mwenye akili timamu anayeweza kushawishiwa na maoni ya mbunge huyo, kwamba amehamia huko kwa ajili ya kuwakomboa watanzania wenzake!

Kunradhi, sijakuelewa hapo Winche. Hivi **** masilahi gani CCJ ambayo Fred anayafuata? Kama ni fedha za michoto, hiyo si iko tele CCM? Unatuchanganya hapa ndugu.
 
Mpendazoe hakuhamia ccj kwa maslahi ya watanzania wenzake, bali ni kwa ajili ya matakwa yake binafsi, na kwa kutegemea maslahi binafsi kutoka CCJ. Hakunas mtanzania yeyote mwenye akili timamu anayeweza kushawishiwa na maoni ya mbunge huyo, kwamba amehamia huko kwa ajili ya kuwakomboa watanzania wenzake!

- Mkuu heshima mbele sana, vipi una facts za ku-back up au hata dataz japo kidogo?

Respect.


FMEs!
 
Mpendazoe hakuhamia ccj kwa maslahi ya watanzania wenzake, bali ni kwa ajili ya matakwa yake binafsi,

Wanaotafuta maslahi binafsi hubaki CCM, hawahami.

na kwa kutegemea maslahi binafsi kutoka CCJ. Hakunas mtanzania yeyote mwenye akili timamu anayeweza kushawishiwa na maoni ya mbunge huyo,

Maslahi hayo yaliyo CCJ ni yapi ? Mwenye akili timamu hawezi kuandika upuuzi kama huu wako.

kwamba amehamia huko kwa ajili ya kuwakomboa watanzania wenzake!

Lolote lile linalolidhoofisha CCM ni hatua katika ukombozi wa Mtanzania. Katika wale asilimia 70%, Mpendazoe sasa hayumo, amejikomboa.
 
habari hizi ni za kweli kabisa,mh kashindwa gemu kaamua aende CCJ-haya karibu lakini hatuna mashangingi huku.
 
Kwanza hili la Mpendazoe huenda likafungu chapter mpya kabisa katika historia ya nchi yetu. Mfumo wa CCM ulivyokuwa ulikuwa decoy ya kuwadanganya wananchi kuwa wao ni wamoja hata kama unatofautiana nao, as longer as ni mwanachama wa wao! Nyamaza!!!! Tumeyaona kuanzia kwa Horace Korimba, Mzee wetu Mangula, Kitine. Hilo kwa sasa halipo tena and the party will no longer be the same again! Manake yameibuka makundi ndani ya chama lipo kundi la Makabaira na Mapebari wao hukaa kwaye Meza ya Mfalme na hula pamoja na mfalme. Wanataka kuiendesha nchi kwa remote control huku wakijilimbikizia na ku-expand himaya yao
Lipo kundi la Wana wa chama watetezi wa wanyonge, ndani ya chama eti wanataka kunyamazishwa, sijui wameamshwa na nani! Wamechachamaa!! Thanks to Dr Harison Jina lako litaingia kwenye Historia ya nchi yetu! Unapewa kazi unaifanya na Matokeo yanaanikwa hadharani bila kupindisha hata sentenso moja licha ya kutaka kunyamazishwa kwa gharama yeyote!
Kundi hili tambueni nguvu yenu iko kwa wananchi, Mnaweza msiwe na pesa kama wao lakini tuko pamoja.
12Fight the good fight of the faith. Take hold of the eternal life to which you were called when you made your good confession in the presence of many witnesses. Timothy 6:12
May the grace of our lord Jesus be with you Amen
 
Naomba mwongozo wa kisheria::

Tanzania tunachagua mbunge na sio chama, sasa ni kweli kwamba huyu mbunge akiondoka CCM automatically anaukosa ubunge au???

Kuhusu mafao, si lazima kisheria alipwe hata kama ni prorated hadi siku atakayokuwa sio mbunge rasmi????
 
Wanaotafuta maslahi binafsi hubaki CCM, hawahami.



Maslahi hayo yaliyo CCJ ni yapi ? Mwenye akili timamu hawezi kuandika upuuzi kama huu wako.



Lolote lile linalolidhoofisha CCM ni hatua katika ukombozi wa Mtanzania. Katika wale asilimia 70%, Mpendazoe sasa hayumo, amejikomboa.
Naungana nawewe, nchi hii haitapata maendeleo kama CCM haitapata mtikisiko mkubwa. Kama hakuna mabadiliko hakuna maendeleo, na njia ya kuleta mabadiliko Tanzania ni CCM kupata mtikisiko utakao kidhoofisha sana. Tunahitaji wabunge wengine wengi wajiengue ili kidhoofike na mabadiliko yatokee.
 
Na ni vizuri watu kuwa na vitu mnavyoamini na kusimamia ili wakati mtu usije kuumbuliwa kwa matendo. KWA imani yangu CCM wote ni mafisadi na nothing good can come out of CCM! wakitokea kama hawa ninafurahi kuwa wanahukumiwa na asili !

Waberoya, you are missing the bigger picture. Yawezekana kuna wanaoamini kuwa CCM ikimeguka, viongozi wazuri wataweza kupatikana humo humo. Lakini mimi siamini hivyo bali naamini katika mmommonyoko wowote ule unaoipunguzia nguvu CCM. Mathalani leo hii wakijiengua Lowassa, Rostamu, Karamagi na wengineo - kwangu mimi nitapiga vigelegele siyo kwa sababu nawapenda hao la hasha, ni kwa sababu kitendo chao kinaidhoofisha CCM. Vivyo hivyo wakiondoka hao wanaojiita wapiganaji, pia nitashangilia kwani CCM itakuwa imedhoofika kwa kiasi fulani. Nyumba yenye nyufa haiwezi kustahimili kishindo chochote kile na kwa kupuliza tu twaweza kuitikisa kama si kuiangusha kabisa.
 
Naomba mwongozo wa kisheria::

Tanzania tunachagua mbunge na sio chama, sasa ni kweli kwamba huyu mbunge akiondoka CCM automatically anaukosa ubunge au???

Ndiyo; lakini to set it straight.. tunachague mbunge aliyependekezwa na chama; Mbunge akipoteza Ubunge hapotezi uanachama wake, ila akipoteza uanachama wake anapoteza Ubunge. Kwa vile tuko tayari ndani ya muda wa uchaguzi basi hata akipoteza Ubunge hakuna uchaguzi mdogo kufanyika kwa hiyojimbo lake litakuwa wazi hadi uchaguzi mkuu.


Kuhusu mafao, si lazima kisheria alipwe hata kama ni prorated hadi siku atakayokuwa sio mbunge rasmi????

Ndiyo.. mafao ya Ubunge hayapotezi kwa sababu ameamua kuacha chama au kuacha ubunge, kuna muda ambao atapewa mafao hayo kwa mujibu wa sheria.
 
Acha utani mkuu; tofauti yao ni sawa na mchana na usiku!

kweli ukipenda hata chongo utaita kengeza............... the same mrema (or a number of mremas) is (are) back.................. mi nadhani hata mrema alikuwa na hekima kidogo, alijiunga na chama ambacho kiko hai, saasa huyu anajiunga na mimba ya chama!!!!!!!!!!! chama kisipozaliwa? au kiizaliwa njiti?.......... mbona mmeirahisishia kazi CCM, ikiona tishio lolote inacheza na wakunga tu, wakati wa ku-deliver wananjyonga katoto kwisha kazi............ hahah..... hizi domokrasia very funy................
 
Waberoya, you are missing the bigger picture. Yawezekana kuna wanaoamini kuwa CCM ikimeguka, viongozi wazuri wataweza kupatikana humo humo. Lakini mimi siamini hivyo bali naamini katika mmommonyoko wowote ule unaoipunguzia nguvu CCM. Mathalani leo hii wakijiengua Lowassa, Rostamu, Karamagi na wengineo - kwangu mimi nitapiga vigelegele siyo kwa sababu nawapenda hao la hasha, ni kwa sababu kitendo chao kinaidhoofisha CCM. Vivyo hivyo wakiondoka hao wanaojiita wapiganaji, pia nitashangilia kwani CCM itakuwa imedhoofika kwa kiasi fulani. Nyumba yenye nyufa haiwezi kustahimili kishindo chochote kile na kwa kupuliza tu twaweza kuitikisa kama si kuiangusha kabisa.

Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah! kaka nikisema hivyo nina wachoma wale wana CCM walio wasafi waondoke! tuko pamoja ! nikisema upinzani wako butu maana yake ninawaamsha! napata coca cola taratibu hapa!

Achilia mbali kandoka kwa sababu gani, lets me assume ni clean na akina Kilango, na wale wote wanaoongea kwa 'uchungu' sana wahame, wasipohama basi wanakutana na maneno yangu kuwa ni mafisadi!

Kikubwa mtu yeyote anayeulizwa haya maswali asionekane ni mfisadi kwa sababu ni forums mtu akitoa hoja ajibiwe kwa hoja, kumekuwa na utaratibu wa watu kurusha makombora na ku-attack mtu simply kwa sababu anauliza maswali nje ya mstari wetu. People are different wnd will always be. Kama askari tuko vitani yapasa pia kujua mbinu ya adui CCM ni kama simba angurumaye akizunguka huku na huku ammeze mtu!

cheers!
 
Mawazo finyu! Sidhani kwamba Mpendazoe alichowaza ni kupata ushindi wa aina yoyote. Anajua yaliyo mbele yake lakini ameamua liwalo na liwe. Tunapenda watu ambao wako tayari ku-sacrifice 'luxuries' za kuwemo ndani ya CCM kwa ajili ya kutetea misimamo yao. Hongera Mpendazoe!

Hii imenikumbusha hili andiko hasa baada ya kupata habari rasmi leo; "Kwa Imani Musa alipokuwa mtu mzima,akakataa kuitwa mwana wa Binti Farao; akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo," Ebr. 1125

Asante sana Mpendazoe, Mungu akutangulie na kukufanikisha katika maono na malengo yako!
 
Ila kwa mtizamo wangu, CCJ nina mashaka kama ni chama imara cha upinzani halisi. Upinzani wa kweli ni lazima utokane na mpasuko ndani ya Chama cha Mapinduzi tu. Yaani ni sawa na kuchora mstari, kundi moja la SSM kule na la pili kule!!


Mkuu huo ndoi mwanzo, wengine utawaona.
 
Nyie bin adam mnaletewa mpaka picha amuamini jamani?????

Leo nimefurahi sana kila nikisoma naona thanks ya mwana mapinduzi wetu ""mwana kijiji""naona amefurahi sana

sala zake zimeanza kujibiwa

asieamini mungu yupo !!!!!akaamini misukule

mambo yameanza subiri wiki ijayo lista inakuja!!!!mmoja mmoja
 
Back
Top Bottom