Kiswahili kimejitosheleza vipi wakati bado hatuna vitabu vya kutosha kufundishia kwenye fani mbalimbali zilizopo vyuoni?Hata kidogo.
Lugha ya kufundishia siyo tatizo kabisa. Kiswahili kimekua na kujitosheleza kabisa kuwa lugha ya kufundishia elimu iliyo bora kabisa.
Nimekusoma nikaishia kucheka tu; kimsingi umekubali hoja za Mbowe ila shida yako ni "uenyekiti" tu, tulia next year ataondoka wewe na wenzako mpumue tuone na hilo chaguo lenu mtakalotuletea.Kingereza ni lugha muhimu kwa nchi kama Tanzania na haiepukiki. Serikali iwekeze kupata walimu wazuri wa kiingereza liwe ni somo kama ilivyo sasa kuanzia chekechea. Nilikutana na jamaa mmoja anakijua kingereza vizuri. Alisoma kijijini kwetu shule hizi za kawaida na alipofika sekondari huko huko kijijini mwalimu wao wa kiingilishi akawa ni raia wa Marekani valentia.
Hivyo tusikimbilie Kiswahili kwa kukataa uwekezaji kwenye Kiingereza. Lugha zote mbili zitumike kufundishia kwa level ya msingi kingereza kiwe somo. Na ikifika sekondari kiswahili kiwe somo. Maneno haya ya wenye maslahi ya miradi ya ulaji kwenye lugha ya kiswahili yataligharimu taifa hili.
Ujumbe kwa Mbowe, CDM haiwezi kubadilika kama itaendelea kuwa na akili hizi hizi za MKT. Ni wakati umefika wapishe wengine wao wawe washauri tu. Waache tabia za ujasiriasiasa.
Chadema imepwaya sanaMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametoa msimamo wa chama chake, akisema kikifanikiwa kushika dola, lugha itakayotumika ni Kiingereza ili kuondoa alichokiita ubaguzi wa kiajira unaotokana na vijana wengi wa Kitanzania kutoijua lugha hiyo .
Akiwa wilayani Hai mkoani Kilimanjaro siku chache baada ya kutoka gerezani alipokuwa mahabusu, Mbowe alisema elimu ya Tanzania imejaa ubaguzi wa makundi kati ya wenye uwezo na masikini, huku akieleza kuwa ubaguzi huo unajidhihirisha hata katika ajira hususan kwenye taasisi na kampuni kubwa.
Akihutubia mamia ya wafuasi wake na wananchi waliojitokeza kumpokea katika viwanja vya Bomang’ombe, Mbowe alisema elimu inayotolewa kwa sasa haimjengi Mtanzania kuingia katika soko la ajira kutokana na mfumo wake ulivyo na kwamba inahitaji mabadiliko.
“Kumekuwa na ubaguzi katika elimu kwani viongozi wetu wamekuwa wakituhutubia tujifunze Kiswahili ni lugha yetu ya Taifa, lakini leo Kiswahili hicho kinazungumzwa kwenye shule zetu za kata, viongozi wote na watu wenye uwezo wanasomesha watoto katika shule za mfumo wa Kiingereza; huu ni ubaguzi,” alisema.
Kiongozi huyo anasema Chadema kikiingia madarakani, kitahakikisha watoto wote wanafundishwa kwa lugha ya Kiingereza, kwa kuwa ndiyo lugha ya kimataifa.
Anasema katika dunia inayokwenda kwa kasi huku ikichagizwa na mabadiliko ya teknolojia, maarifa ya lugha ya Kiingereza ni ya lazima na kwamba Kiswahili kitabaki kuwa kama somo la ziada.
Anatoa mfano wa namna Wakenya wanavyotamba katika soko la ajira, kwa sababu ya uwezo walionao katika kutumia Kiingereza.
‘’Vijana wa Kenya wamelikamata soko kubwa hata katika nchi zenye uchumi mzuri ndani ya Afrika tofauti na Watanzania, ambao licha ya kuwa na uwezo, wanakwamishwa na suala la lugha,’’ anaeleza.
Ilivyo sasa nchini, wanafunzi wa shule za awali hadi darasa la saba, wanafundishwa kwa lugha ya Kiswahili, huku Kingereza kikiwa kama somo.
Pia kuna shule za mchepuo wa Kingereza katika ngazi hiyo ya elimu, hata hivyo, nyingi zinamilikiwa na watu au taasisi binafsi. Wanafunzi hao wote wanapomaliza darasa la saba, wanalazimika kutumia Kiingereza kama lugha ya kufundishia.
Naomba nikupinge katika elimu bure, elimu bure imesaisia sana watanzania,shule za kata zinatoa elimu bora kabisa kulingana na mitaala yetu,labda shule iwe haina walimu.Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.
Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.
Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.
sidhani kama suala hapa ni lugha bali mfumo mzima wa elimu katika hizo English medium. Mfumo wa uchaguzi wa wanafunzi na mazingira ya ufundishaji kama uwezo wa walimu, idadi yao, vifaa vya kufundishia na ubora wa madarasa. Haya hayapo kwenye shule zetu wananchi.
mngejua watoto wanaotoka English medium wanavyofanya vizuri huku sekondari msingethubutu hata kidogo kumpinga Mbowe ! Watoto wanaotoka shule zetu za kiswahili mateso wanayoyapata huku sekondari laiti mngewaona mngemsapoti Mbowe mia. Ni wajibu wa serikali kutoa elimu isiyo na ubaguzi,... Kwanini wengine wasome kwa kiingereza,, wengine kwa kiswahili!?!? Kwanini watanzania wengine wajihisi wanyonge ktk nchi yao eti kisa tu wanasoma public schools!? Nafikiri hii ndo,hoja kuu ya Mbowe, nami namsapoti 10
Tuachane nao tu! Aliyewaroga ni Nyerere na kashakufa!Ndugu Data! Mitanzania mingi ni mijinga Sana. Mi ni mwl English medium. Watoto wanaelewa Sana. Tatizo Mwl Nyerere watu walimdanganya kuwa ukiendelea na Kiingereza watu wataerevuka na watajua mengi ya nje watakupindua! Akabadili gia angani Kiswahili tu tofauti na nchi zilizotawaliwa na Mwingereza. Sasa ccm inafurahia cnn, bbc world, sky news etc wakiongea watz ni hola! Shenzi type!
Mkuu Una shule binafsi?Kwa Mara ya kwanza najitokeza NAYAPINGA MAWAZO YA MBOWE[emoji848][emoji848]
Haya ndo Watanzania tunahitaji kuyasikia yakitugusa moja kwa moja siyo kila kukicha oooh Katiba mpyaaMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametoa msimamo wa chama chake, akisema kikifanikiwa kushika dola, lugha itakayotumika ni Kiingereza ili kuondoa alichokiita ubaguzi wa kiajira unaotokana na vijana wengi wa Kitanzania kutoijua lugha hiyo .
Akiwa wilayani Hai mkoani Kilimanjaro siku chache baada ya kutoka gerezani alipokuwa mahabusu, Mbowe alisema elimu ya Tanzania imejaa ubaguzi wa makundi kati ya wenye uwezo na masikini, huku akieleza kuwa ubaguzi huo unajidhihirisha hata katika ajira hususan kwenye taasisi na kampuni kubwa.
Akihutubia mamia ya wafuasi wake na wananchi waliojitokeza kumpokea katika viwanja vya Bomang’ombe, Mbowe alisema elimu inayotolewa kwa sasa haimjengi Mtanzania kuingia katika soko la ajira kutokana na mfumo wake ulivyo na kwamba inahitaji mabadiliko.
“Kumekuwa na ubaguzi katika elimu kwani viongozi wetu wamekuwa wakituhutubia tujifunze Kiswahili ni lugha yetu ya Taifa, lakini leo Kiswahili hicho kinazungumzwa kwenye shule zetu za kata, viongozi wote na watu wenye uwezo wanasomesha watoto katika shule za mfumo wa Kiingereza; huu ni ubaguzi,” alisema.
Kiongozi huyo anasema Chadema kikiingia madarakani, kitahakikisha watoto wote wanafundishwa kwa lugha ya Kiingereza, kwa kuwa ndiyo lugha ya kimataifa.
Anasema katika dunia inayokwenda kwa kasi huku ikichagizwa na mabadiliko ya teknolojia, maarifa ya lugha ya Kiingereza ni ya lazima na kwamba Kiswahili kitabaki kuwa kama somo la ziada.
Anatoa mfano wa namna Wakenya wanavyotamba katika soko la ajira, kwa sababu ya uwezo walionao katika kutumia Kiingereza.
‘’Vijana wa Kenya wamelikamata soko kubwa hata katika nchi zenye uchumi mzuri ndani ya Afrika tofauti na Watanzania, ambao licha ya kuwa na uwezo, wanakwamishwa na suala la lugha,’’ anaeleza.
Ilivyo sasa nchini, wanafunzi wa shule za awali hadi darasa la saba, wanafundishwa kwa lugha ya Kiswahili, huku Kingereza kikiwa kama somo.
Pia kuna shule za mchepuo wa Kingereza katika ngazi hiyo ya elimu, hata hivyo, nyingi zinamilikiwa na watu au taasisi binafsi. Wanafunzi hao wote wanapomaliza darasa la saba, wanalazimika kutumia Kiingereza kama lugha ya kufundishia.
Ni wapi nimedharau lugha. Kiswahili siyo lugha?Hebu nikumbushe hilo swali lako, mambo yalikuwa mengi wakati mwingine ni rahisi kusahau jambo.
Bado kwangu nakushauri usidharau umuhu wa lugha kwenye fani yoyote kama chombo cha mawasiliano, hicho ndio kiunganishi kikuu.
Kuwa na vitabu vya kutosha ni swala tofauti, ambalo ufumbuzi wake ni rahisi.Kiswahili kimejitosheleza vipi wakati bado hatuna vitabu vya kutosha kufundishia kwenye fani mbalimbali zilizopo vyuoni?
"Ponda ponda lugha si hoja mradi ujue unachofanya"Ni wapi nimedharau lugha. Kiswahili siyo lugha?
Mpaka huo ufumbuzi wake utakapopatikana ndio hilo jambo litakuwa rahisi, kwasasa sioni urahisi wowote, sisi bado ni tegemezi, kiswahili kitaendelea kutumika mitaani pekee, sio kwenye uwanja wa soko la ajira.Kuwa na vitabu vya kutosha ni swala tofauti, ambalo ufumbuzi wake ni rahisi.
Basi tuseme upo sawa!Mpaka huo ufumbuzi wake utakapopatikana ndio hilo jambo litakuwa rahisi, kwasasa sioni urahisi wowote, sisi bado ni tegemezi, kiswahili kitaendelea kutumika mitaani pekee, sio kwenye uwanja wa soko la ajira.
Huu ni ubishi. Sina la zaidi."Ponda ponda lugha si hoja mradi ujue unachofanya"
Sijui kama ulijua maana ya hayo maneno uliyotumia "ponda ponda" maana yake ni kama kulipua, ...fanya bora liende, sasa kama kwako huku sio kudharau lugha sijui ni nini.
Huwezi "ponda ponda" halafu ukawasiliana na mlengwa, lugha ni chombo cha mawasiliano, ukiponda ponda unapoteza maana ya mawasiliano.
Kwani ni uongo?Utasikia gaidi alifeti kidato cha sita.![emoji1493][emoji1493]