Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Mtoto anaenda shule ili ajue kusoma na kuandika, lakini pia kupata maarifa ya kuja kumsaidia katika maisha yake.

Lugha ni njia tu inayo tumika kumhamishia mtoto maarifa. Hivyo lugha mama humrahisishia zaidi kuelewa hayo maarifa kuliko ile lugha ya pili. (Hii ni kutokana na tafiti mbalimbali!)
Kama ni kupata maarifa ya kuja kumsaidia katika maisha yake, na lugha inayotumika kumpa hayo maarifa ni kiingereza sioni ubaya wa kufuata hilo, tusidanganyane na hiki kiswahili chetu, mwisho wake ni hapa hapa ndani tena kwa baadhi ya maeneo pekee.
 
Duuu hawa ndio wanataka kupewa nchi kwa mawazo haya.
CHADEMA tafuteni viongozi wengine hawa akina Mbowe, Mnyika na yule aliyeko nje sasa hawana jipya
 
Totally WRONG!

Sijawahi kusikia Ujerumani au Ufaransa wakiwafundisha watoto wao kwa lugha ya Kiingereza. Wala waChina waliotapakaa dunia nzima sasa hivi hawajifunzi masomo yao kwa lugha ya Kiingereza.



Hapa ndipo Mbowe na chama chake wanapolikoroga, wanapodhani Kenya ndio mfano wa kupigia chepuo kwa mambo mazuri yaliyopo huko!

Nina hofu sana juu ya chama hiki kuifanya Tanzania kuwa tegemezi wa nchi hiyo jirani kwa kila kitu. This is a very big put off about this political party.
Kazi kweli!?
 
Nae atuonyeshe mfano, anaongea kiingereza kilichonyooka? Au ni sawa na yule jamaa yangu aliyehojiwa na radio fulani ya Kenya, tulihesabu neno "actually" mara mia. Ni kweli lugha inatuendesha ila tukiweka Nia tutaweza.
Kiingereza kilichonyooka ni kipi?

Amandla...
 
Totally WRONG!

Sijawahi kusikia Ujerumani au Ufaransa wakiwafundisha watoto wao kwa lugha ya Kiingereza. Wala waChina waliotapakaa dunia nzima sasa hivi hawajifunzi masomo yao kwa lugha ya Kiingereza.



Hapa ndipo Mbowe na chama chake wanapolikoroga, wanapodhani Kenya ndio mfano wa kupigia chepuo kwa mambo mazuri yaliyopo huko!

Nina hofu sana juu ya chama hiki kuifanya Tanzania kuwa tegemezi wa nchi hiyo jirani kwa kila kitu. This is a very big put off about this political party.
Nawashangaa na aina ya mifano ya nchi mnazotaja na kuilinganisha na nchi yetu, sisi ni tegemezi, ajira zenyewe hapa kwetu bado ni shida nyingi za kugombania, na hizo ajira za kugombania ndio mnashindana na hao wa nje kama Kenya ambao wao wanakuwa na "added advantage" ya kuijua lugha ya kiingereza.

Ajabu zaidi, mnaenda kutolea mifano nchi zilizoendelea ambazo kwanza kwao tatizo la ajira sio kubwa kama kwetu, ndio maana wanawekeza kwenye aina yao ya lugha wakijua fika aina hiyo itawapa watoto wao ajira kwasababu wanazitengeneza wao.

Sasa nyie mnataka kiswahili kitumike kufundishia hapa ndani, wakati mkienda kwenye interview karibia 90% au zaidi lugha inayotumika ni kiingereza, sasa hapo mnataka kumdanganya nani na kiswahili chenu?

Mnaweza kubadilisha mambo yenu yote yawe kwa kiswahili, lakini bado mkienda kwenye kuomba ajira mkakutana na interview za kiingereza kwasababu hiyo ndio lugha ya wawekezaji mnaowapokea kila siku.

Uwezo wa kuwalazimisha watumie kiswahili chetu hatuna kwasababu hawakijui, na pili, sisi bado ni tegemezi, haya mambo lazima kwanza mjijenge kiuchumi kama hizo nchi ulizotaja kule juu.
 
Mbowe hataki kukuza lugha ya Kiswahili ili iwe lugha ya kitaaluma?
Mbona wachina, Wajapan, Warusi, Waswede, Wajerumani, wafaransa wanatumia lugha zao kufundishia watoto wao kwa nini kiswahili kisiweze?
Mbowe yuko sahihi. Miaka sitini ya uhuru tumeshindwa kufanya kiswahili lugha ya kufundishia hadi chuo kikuu. Matokeo yake vijana wetu hawana uwezo wa kujieleza kwa kiswahili au kiingereza. Hizo nchi mnazo zitolea mfano lugha zao zimekamilika na zinaweza kutoa elimu ya kiwango chochote. Ni vitabu vingapi vya elimu ya juu vimetafsiriwa kwa kiswahili? Sidhani hata vitabu vya mshindi wetu wa Nobel Prize vimetafsiriwa wakati utakuta tayari wachina, wafaransa, waswidi, wajerumani n.k. wameisha vitafsiri ili raia wake waweze kuvisoma katika lugha yao. Tukubali tu kuwa tumeshindwa katika hili na tutumie lugha ambayo watoto wetu wataweza kuitumia hadi chuo kikuu. Wakati huo huo tuwekeze katika kujenga kiswahili ili huko mbeleni watoto wetu waweze kuchagua kati ya lugha hizo mbili au kama Kitila alivyosema kuamua kutumia zote mbili.
Kutumia kiingereza kama lugha ya kufundishia hakutaua kiswahili. Marekani wanatumia kiingereza lakini watoto wanaotoka katika jamii zinazozungumza kispanish au kichina nyumbani bado wanamudu lugha zao. Aidha, ingekuwa hivyo basi hapa nyumbani wahaya wangeacha kuongea kihaya kwa sababu hakitumiki shuleni. Tuache unafik wa kupeleka watoto wetu Feza wakati tunawakazania watoto wa watanzania wenzetu wanaosoma shule za kata wasome kwa kiswahili ili wasijeweza kushindana na watoto wetu.

Amandla....

Nguruvi3 JokaKuu
 
Nawashangaa na aina ya mifano ya nchi mnazotaja na kuilinganisha na nchi yetu, sisi ni tegemezi, ajira zenyewe hapa kwetu bado ni shida nyingi za kugombania, na hizo ajira za kugombania ndio mnashindana na hao wa nje kama Kenya ambao wao wanakuwa na added advantage ya kuijua lugha ya kiingereza.

Ajabu zaidi, naenda kutolea mifano nchi zilizoendelea ambazo kwanza kwao tatizo la ajira sio kubwa kama kwetu, ndio maana wanawekeza kwenye aina yao ya lugha wakijua fika aina hiyo itawapa watoto wao ajira kwasababu wanazitengeneza wao.

Sasa nyie mnataka kiswahili kitumike kufundishia hapa ndani, wakati mkienda kwenye interview karibia 90% au zaidi lugha inayotumika ni kiingereza, sasa hapo mnataka kumdanganya nani na kiswahili chenu?

Mnaweza kubadilisha mambo yenu yote yawe kwa kiswahili, lakini bado mkienda kwenye kuomba ajira mkakutana na interview za kiingereza kwasababu hiyo ndio lugha ya wawekezaji mnaowapokea kila siku.

Uwezo wa kuwalazimisha watumie kiswahili chetu hatuna kwasababu hawakijui, na pili, sisi bado ni tegemezi, haya mambo lazima kwanza mjijenge kiuchumi kama hizo nchi ulizotaja kule juu.
Mkuu 'denooJ' nilikusoma kule juu ulipomjibu mmoja wa wachangiaji, nami nikashawishika kukujibu, lakini nikajizuia. Sasa umekuja na kunijibu hapa, kwa hiyo unanipa nafasi ya kukujibu pia.

Lugha ya Kiingereza ni lugha tu, kama lugha nyingine, pamoja na kwamba inazungumzwa na kutumika kila mahali duniani.

Kama lugha nyingine yoyote, mtu yeyote hata asiyekwenda shule anaweza kabisa kujifunza hii lugha na kuijua na kuitumia kwa mawasiliano, kama zilivyo lugha nyingine zozote, hata za kikabila zetu.

Ninakuomba unielewe: tatizo letu hapa Tanzania siyo kutojua lugha ya kiingereza. Tatizo ni elimu yetu kuwa mbovu, mbovu kabisa, kiasi kwamba wahitimu wake wanatoka bila kuiva kimasomo, bila kujali lugha waliyotumia katika kujifunza. Tatizo ni hilo.

Nimetumia mfano wa waChina hapo juu uliponijibu kwa maksudi kabisa, kwa sababu ya kuwa na uzoefu nao watu hao. Vijana wao wengi walitapakaa sana katika vyuo vya nchi za magharibi kwenye miaka ya 80, 90 hadi leo hii 2022. Wengi wa hawa wanafunzi walikuwa wakiingia kwenye vyuo hivyo vya magharibi,(soma hapa, kama Uingereza na Marekani nilikokutana nao) wakiwa hawajui kabisaaaaa, lugha ya Kiinereza. Hawa watu walikuwa wanawekwa kwenye 'program' ya kujifunza kiingereza kwa miezi mitatu, ndiyo, miezi mitatu, tena wakiendelea na kozi zao za masomo darasani.
Kwa vile hawa vijana walikuwa na msingi mzuri wa elimu, waliokuwa wamejifunzia nyumbani kwao kwa kichina, darasani hawakuathirika vyovyote kwa kutojua lugha ya kiingereza. Na baada ya hiyo miezi mitatu, pamoja na kwamba bado hawakuwa wamenyoosha lugha ya kiingereza vizuri sana, lakini waliweza kuendelea na masomo yao yote bila ya shida yoyote
Na hadi walipofikia mwisho wa masomo yao kabla ya kuhitimu, mtu usingeweza kutambua kabisa kwamba mwanzo hawakuwa na ufahamu wa lugha hiyo ya Kiingereza walipoanza.

Na sisemi wachina tu, Waarabu wengi pia hili lilikuwa linawahusu, hasa kutoka Iraq na kwingine. Huu ni uzoefu nilioupata, siyo kwa kuambiwa, bali kwa kushuhudia mwenyewe kwa muda mrefu sana.

Lugha yetu ya Kiswahili inatosha kabisa kuwafundisha watoto wetu tukiwa na mfumo wa elimu unaomfanya mwanafunzi kuelewa na kujua alichojifunza, na kuweza kutumia elimu hiyo katika maisha yake, bila kujali mazingira ya lugha nyingine itakayopaswa kutumiwa; mradi tu awe na basis (basic) ya matumizi ya lugha hiyo.
 
Uwezo wa kuwalazimisha watumie kiswahili chetu hatuna kwasababu hawakijui, na pili, sisi bado ni tegemezi, haya mambo lazima kwanza mjijenge kiuchumi kama hizo nchi
Kwani mchina anayekuja kuwekeza hapa, mojawapo ya kigezo anachotakiwa kuwa nacho ni kujua lugha ya kiingereza?

Mhandisi yeyote kwa mfano, aliyeiva vyema katika nyanja yake, akienda kwenye 'interview' ambayo inafanyika kwa lugha ya kiingeraza, na kama mhandisi huyo ametumia lugha ya kiingereza kujifunza Chuo Kikuu, ashindwe 'interview' hiyo kwa vile hajui lugha ya Kiingereza?

Hii itakuwa kuna sababu nyingine zaidi ya lugha inayotumika kwenye usaili huo.
 
Namuunga mkono Mh. Mbowe.Hata mimi napinga ubaguzi huu.ni zaidi ubaguzi wa rangi. Kwanini watoto wa matajiri na viongozi serikali wawapeke watoto wao English medium. Huku watoto wa kidato cha chini wawafundishe kiswahili. Kiswahili kuwafundishia watoto wa masikini .ni kiwanyima furusa za nje.
 
Mkuu 'denooJ' nilikusoma kule juu ulipomjibu mmoja wa wachangiaji, nami nikashawishika kukujibu, lakini nikajizuia. Sasa umekuja na kunijibu hapa, kwa hiyo unanipa nafasi ya kukujibu pia.

Lugha ya Kiingereza ni lugha tu, kama lugha nyingine, pamoja na kwamba inazungumzwa na kutumika kila mahali duniani.

Kama lugha nyingine yoyote, mtu yeyote hata asiyekwenda shule anaweza kabisa kujifunza hii lugha na kuijua na kuitumia kwa mawasiliano, kama zilivyo lugha nyingine zozote, hata za kikabila zetu.

Ninakuomba unielewe: tatizo letu hapa Tanzania siyo kutojua lugha ya kiingereza. Tatizo ni elimu yetu kuwa mbovu, mbovu kabisa, kiasi kwamba wahitimu wake wanatoka bila kuiva kimasomo, bila kujali lugha waliyotumia katika kujifunza. Tatizo ni hilo.

Nimetumia mfano wa waChina hapo juu uliponijibu kwa maksudi kabisa, kwa sababu ya kuwa na uzoefu nao watu hao. Vijana wao wengi walitapakaa sana katika vyuo vya nchi za magharibi kwenye miaka ya 80, 90 hadi leo hii 2022. Wengi wa hawa wanafunzi walikuwa wakiingia kwenye vyuo hivyo vya magharibi,(soma hapa, kama Uingereza na Marekani nilikokutana nao) wakiwa hawajui kabisaaaaa, lugha ya Kiinereza. Hawa watu walikuwa wanawekwa kwenye 'program' ya kujifunza kiingereza kwa miezi mitatu, ndiyo, miezi mitatu, tena wakiendelea na kozi zao za masomo darasani.
Kwa vile hawa vijana walikuwa na msingi mzuri wa elimu, waliokuwa wamejifunzia nyumbani kwao kwa kichina, darasani hawakuathirika vyovyote kwa kutojua lugha ya kiingereza. Na baada ya hiyo miezi mitatu, pamoja na kwamba bado hawakuwa wamenyoosha lugha ya kiingereza vizuri sana, lakini waliweza kuendelea na masomo yao yote bila ya shida yoyote
Na hadi walipofikia mwisho wa masomo yao kabla ya kuhitimu, mtu usingeweza kutambua kabisa kwamba mwanzo hawakuwa na ufahamu wa lugha hiyo ya Kiingereza walipoanza.

Na sisemi wachina tu, Waarabu wengi pia hili lilikuwa linawahusu, hasa kutoka Iraq na kwingine. Huu ni uzoefu nilioupata, siyo kwa kuambiwa, bali kwa kushuhudia mwenyewe kwa muda mrefu sana.

Lugha yetu ya Kiswahili inatosha kabisa kuwafundisha watoto wetu tukiwa na mfumo wa elimu unaomfanya mwanafunzi kuelewa na kujua alichojifunza, na kuweza kutumia elimu hiyo katika maisha yake, bila kujali mazingira ya lugha nyingine itakayopaswa kutumiwa; mradi tu awe na basis (basic) ya matumizi ya lugha hiyo.
Kwenye jibu langu kwako hapo juu nimeweka factors kama mbili zinazotulazimu sisi kukimbilia kiingereza, (1) utegemezi wetu kiuchumi (kuvutia wawekezaji) (2) ushindani.

Nakusoma vizuri sana ulipozungumzia hao jamaa hususan wachina waliotoka kwao wakaenda nje Marekani na kwingineko kujifunza lugha za kule kwa miezi mitatu, then after wakaendelea na masomo yao mapaka vyuo vikuu na kupata elimu bora.iliyowasaidia kurudi kwao na kupata ajira.

Hapa ni sawa na umetolea mfano wa kikundi kidogo cha wazazi wenye uwezo kiuchumi hapa kwetu wanaopeleka watoto wao nje wakapate elimu bora then wakirudi nyumbani wapate ajira, na hawa wengi wao huzipata kwasababu hukidhi viwango vya ushindani.

Lakini vipi kuhusu hawa watoto wa shule za kata? wangapi huwa na uwezo aa kuahindana na hao wanaosoma nje au wageni waliotoka nje kuja kutafuta ajira Tanzania? simply hakuna.

Nimeona unazungumzia ubovu wa elimu yetu kwa ujumla sana, hujawa specific, hapa ningependa zaidi uwe specific ubovu kwenye eneo gani hasa?

Kwasababu mimi binafsi kwa uzoefu wangu, kesi nyingi zinazokuja toka kwa waajiri kwanini wanafunzi wa kayumba hawapati ajira, wengi husema wanakosa uwezo wa kujieleza kwa lugha ya kiingereza, hili kwangu ndio tatizo kuu ambalo hawa jamaa hukutana nalo.

Na nikiangalia kwa undani, naona kweli, mitaala yetu kwa shule za primary huwa mostly ni kiswahili, mtoto hujifunza kiingereza kwa somo moja tu English itself.

Huyu mpak aende secondary ndio akakutane na kiingereza, kumbuka ametoka primary school na kiswahili kwa miaka 7, then aende secondary aka adopt kiingereza kwa miaka 4.

Then A level 2 yrs tena asome arts, akienda masomo ya science ndio balaa kabisa, then chuo nako akienda kusoma hizo fani za ufundi ndio balaa, wengi hushindwa interview pale wanapokutanishwa na hao waliotoka nje.

Hapo bado hata walimu wanaowafundisha hao watoto ni wabovu kwenye kiingereza, nakumbuka kama miak miwili au mitatu nyuma, wanafunzi wengi walifeli somo la kiingereza kwenye mitihani yao ya form four waliyofanya, sasa huyu mwanafunzi atapata lini uwezo wa kuijua lugha hiyo?

Hao uliowataja wanaoenda kusoma Marekani na kwingineko wao hawakutani na matatizo haya, ndio maana nakubaliana na hoja ya Mbowe kwa maana kwamba tuwekeze kwenye kiingereza, kuanzia vitabu, walimu, na vyote watoto waanze kupata elimu bora ya kiingereza wakashindane na hao wanaotoka nje, lkn sio tupoteze muda na kiswahili chetu.
 
Kwani mchina anayekuja kuwekeza hapa, mojawapo ya kigezo anachotakiwa kuwa nacho ni kujua lugha ya kiingereza?

Mhandisi yeyote kwa mfano, aliyeiva vyema katika nyanja yake, akienda kwenye 'interview' ambayo inafanyika kwa lugha ya kiingeraza, na kama mhandisi huyo ametumia lugha ya kiingereza kujifunza Chuo Kikuu, ashindwe 'interview' hiyo kwa vile hajui lugha ya Kiingereza?

Hii itakuwa kuna sababu nyingine zaidi ya lugha inayotumika kwenye usaili huo.
Kiingereza ndio lugha ya dunia, huu ndio ukweli, kiswahili chetu mpaka kifikie kiwango hiki tutasubiri sana, hao wachina pamoja na kukijua kichina lakini wengi wao hukijua kiingereza pia, na kwasababu hiyo interview zao hutumia kiingereza kama lugha ya kuunganisha pande zote mbili kwenye interview.

Halafu unaonekana mgeni hapa Tanzania, wapo wanafunzi wengi wanaomaliza vyuo vikuj wasiojua kujieleza kwa kiingereza, huu ndio ukweli, wengi hutetemeka kwenye interview mpaka wanatoka jasho hata kama chumba walichopo kina AC.
 
Nakusoma vizuri sana ulipozungumzia hao jamaa hususan wachina waliotoka kwao wakaenda nje Marekani na kwingineko kujifunza lugha za kule kwa miezi mitatu, then after wakaendelea na masomo yao mapaka vyuo vikuu na kupata elimu bora.iliyowasaidia kurudi kwa
Hapana.
Naomba unisome vizuri, au pengine sikujieleza vyema juu ya hili.

Hawa wachina/Waarabu ninaotoa mifano yao hapa, hawakupelekwa na wazazi wao wakasome Kiingereza, halafu wahitimu vyuo vikuu vya huko ili wakatumie lugha hiyo huko kwao kama turufu ya kupata ajira.

Hawa ni vijana waliohitimu kwenye vyuo vya China/Arabuni hadi chuo kikuu na kusoma digrii zao za mwanzo.
Hawa walipelekwa na serikali ya China/ Iraq, kuchukua masomo kwenye fani maalum za uhitaji maalum katika nchi zao. Pia naomba uelewe kwamba nimetumia Uingereza/Marekani kama mifano tu wa nchi za magharibi walikopelekwa. Wengi zaidi walikwenda nchi kama Ujerumani, Ufaransa, n.k.
 
Nimeona unazungumzia ubovu wa elimu yetu kwa ujumla sana, hujawa specific, hapa ningependa zaidi uwe specific ubovu kwenye eneo gani hasa
Nitakupa mfano mdogo sana, tena usiohitaji jasho kabisa kuwa mahili ndani ya fani hiyo. Uandishi wa habari.

Ukitaka mfano wa masomo ya sayansi, pia nitakupa mifano mingi tu. Angalia watu tunaotazamiwa kuwategemea na kuwapa heshima zote kwa kusimamia elimu yetu, wao ndio wakitoa mifano mibovu kabisa.
Sijasoma Ripoti ya Tume iliyoundwa kuchunguza chanzo cha uharibifu wa mazingira kilichosababisha samaki kufa ziwani na mto mara. Lakini kama yanayosemwa kwamba ndiyo yaliyomo kwenye ripoti hiyo, ninasikitika sana.
 
Huna sababu ya kumsifu Mbowe. Hayo yalishaandikwa siku nyingi sana ktk Tume ya Makweta! Yaliandikwa kwa utafiti mzuri, siyo huyo anayesema kisiasa tu bila takwimu.
Yanasubiri Yesu arudi ili yatekelezwe?
 
a Tanzania, wapo wanafunzi wengi wanaomaliza vyuo vikuj wasiojua kujieleza kwa kiingereza, huu ndio ukweli, wengi hutetemeka kwenye interview mpaka wanatoka jasho hata kama chumba walichopo kina AC.
Sasa sijui tunapishana wapi.
Huu mfano uliotoa hapa, unaweza kweli kusema ni kutojua lugha?

Mtu anayejua fani yake vyema, hawezi kutetemeka kwa vile hawezi kusema lugha.

Hao niliokueleza kama mifano huko juu, wakitetea hoja zao kwa kuponda ponda lugha, bado wanaeleweka kabisa wanachokizungumzia.

Naomba tu kama unaweza, unieleze, kwa nini mtu mmoja anaweza akatumia lugha kwa 'confidence' kabisa kueleza kitu anachokijua baada ya kujifunza lugha kwa miezi mitatu tu; na mwingine, ambaye ametumia lugha miaka zaidi ya miaka mitatu akijifunza masomo aliyohitimu, halafu asiweze kabisa kujieleza, hata kwa kuponda ponda lugha inayotumika.

Tunaweza kuacha mengine yote, nieleze tu hili.
 
Hapana.
Naomba unisome vizuri, au pengine sikujieleza vyema juu ya hili.

Hawa wachina/Waarabu ninaotoa mifano yao hapa, hawakupelekwa na wazazi wao wakasome Kiingereza, halafu wahitimu vyuo vikuu vya huko ili wakatumie lugha hiyo huko kwao kama turufu ya kupata ajira.

Hawa ni vijana waliohitimu kwenye vyuo vya China/Arabuni hadi chuo kikuu na kusoma digrii zao za mwanzo.
Hawa walipelekwa na serikali ya China/ Iraq, kuchukua masomo kwenye fani maalum za uhitaji maalum katika nchi zao. Pia naomba uelewe kwamba nimetumia Uingereza/Marekani kama mifano tu wa nchi za magharibi walikopelekwa. Wengi zaidi walikwenda nchi kama Ujerumani, Ufaransa, n.k.
Ok, kama unazungumzia wanaopelekwa kwa ajili ya mahitaji maalum hili nalo kwangu sio tatizo, mbona hata kwetu hufanya hivyo, lakini hawa tayari wanakuwa na guarantee ya ajira.

Vipi kuhusu wale ambao hawapelekwi huko ambao ndio kundi kubwa zaidi na ndio wanaozungumziwa kwenye mada hii, wao wasaidiwe vipi ili waondokane na tatizo la ajira kwa nchi hii yenye nafasi chache za ajira tena za kushindaniwa na watu toka nje?
 
Kwani mtoto unampeleka shule kwa lengo gani? ajue lugha na elimu na kukaa nayo nyumbani? au ajue lugha pamoja na elimu vitakavyo muwezesha kuyamudu mazingira atakayokabiliana nayo mbele ya safari yake ya kimaisha?

Uko sahihi kuuliza maswali kama hayo lakini umekosa msingi wa unachokiita “elimu” na umeweka ufinyu katika namna ya kupata elimu na kuiona iko “shuleni”. Uzuri umetaja “kumudu mazingira”. Nitakukumbusha haya:
1. Hakuna mtu anayetumia elimu ya shule ya msingi kufanya chochote. Hata hajira rasmi hazina watu hao na ndio maana walifoji vyeti na wakafurushwa na JPM.
2. Mazingira ya sasa yanamtaka mtu akabiliane nayo sio kwa bidii tu, bali ufahamu. Tuna EAC na hivo mipaka ya ajira iko wazi. Ndio kusema hukusoma Mbowe anazungumzia watu wajuzi wa kiingereza wakichukua kazi kubwa kubwa? Ina msaada gani kama ajira za watanzania itakuwa ni kufagia ofisi, kumwagilia maua eti kwa sababu hawaajiriki kwa hawa wajuzi wa kiingereza???
3. Amezungumzia ubaguzi. Wewe unadhani wazazi wanaowapeleka watoto kwenye shule za mchepuo wa kiingereza hawajaamua kuwatofautisha watoto wao na wa shule za serikali??

Sababu ya kutaka kiingereza ni kupanua uwigo wa ushindani!! Sio kwamba Kiswahili hakina maana. Kwa kiswahili tu, maana yake uwigo unakuwa finyu. Kiingereza kina wigo mpana wa maarifa kwa sababu ndio lugha inayoongewa (hata kama si kwa ufasaha) na watu wengi kuliko lugha nyingine yoyote!!
 
Back
Top Bottom