Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Kwe
Mbowe hataki kukuza lugha ya Kiswahili ili iwe lugha ya kitaaluma?
Mbona wachina, Wajapan, Warusi, Waswede, Wajerumani, wafaransa wanatumia lugha zao kufundishia watoto wao kwa nini kiswahili kisiweze?
Kwenye soko la dunia sisi utatfananinisha na wachina? Ata wahindi na ukubwa wao wanatumia english! Kiswahili hakiwezi kutusukuma mbele kitaaluma na kikitumika kitaaluma sio Kama ndo kitakuwa dhaifu
 
Mimi naamini katika Lugha Mama (Mother tongue)! Mtoto anaelewa zaidi ukimfundisha kwa kutumia lugha aliyo kua nayo, kuliko ile aliyo jifunza ukubwani.

Hivyo namatani kuona siku moja Kiswahili kikitumika katika ngazi zote za elimu. Na kama kuna watu wataamua kiwapeleka watoto wao shule za mchepuo wa kiingereza, waachwe.

Ila tu elimu itakayo tolewa kwa kutumia Lugha Mama, iwe na ubora unaotakiwa! Na isifanyiwe dhihaka kama ilivyo sasa.
Hapo sasa tunasema,kwa kimombo 'until then' !
 
Labda chama kingene ila mbowe na ubaguzi was kikanda
 
Basi kiswahili kitumike kufundishia Awali Mpk Chuo kikuu na kusiwe na English medium ndani ya Nchi Ili tukuze kiswahili,ila Kwa hali ya Sasa Bora tuwe na English mwanzo mwisho
Mbona kinatumika tu kwenye kufundishia na mtu anaelewa vizuri
 
Laiti mngejua watoto wanaotoka English medium wanavyofanya vizuri huku sekondari msingethubutu hata kidogo kumpinga Mbowe ! Watoto wanaotoka shule zetu za kiswahili mateso wanayoyapata huku sekondari laiti mngewaona mngemsapoti Mbowe mia. Ni wajibu wa serikali kutoa elimu isiyo na ubaguzi,... Kwanini wengine wasome kwa kiingereza,, wengine kwa kiswahili!?!? Kwanini watanzania wengine wajihisi wanyonge ktk nchi yao eti kisa tu wanasoma public schools!? Nafikiri hii ndo,hoja kuu ya Mbowe, nami namsapoti 100.
Uongo mtupu
 
Hili la lugha ya kufundishia serikali ya kijani..imefeli pakubwa..nadhani ni moja ya mipango yao miovu ya kuharibu elimu ya wananchi ili waendelee kutawala.

Muhimu kwa na lugha moja yakifundishia kuanzia shule za awali hadi chuo kikuuu.

Hili nalo kijani mmeshindwa kabisa kulifanyia maamuzi?
Katiba mpya muogope
Hata mfumo wa elimu nao kuboresha mnaogopa.
Absurd

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu kuna ka msemo kanasema,,'kama elimu ni gharama,jaribu ujinga'.. CCM miaka 60 baadae baada ya uhuru ilichagua UJINGA!
 
Mtoto anaenda shule ili ajue kusoma na kuandika, lakini pia kupata maarifa ya kuja kumsaidia katika maisha yake.

Lugha ni njia tu inayo tumika kumhamishia mtoto maarifa. Hivyo lugha mama humrahisishia zaidi kuelewa hayo maarifa kuliko ile lugha ya pili. (Hii ni kutokana na tafiti mbalimbali!)
Point
 
Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.

Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.


Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.
Mkuu, makabils 120+ Kiswahili siyo lugha mama. Ni lugha ya pili.
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametoa msimamo wa chama chake, akisema kikifanikiwa kushika dola, lugha itakayotumika ni Kiingereza ili kuondoa alichokiita ubaguzi wa kiajira unaotokana na vijana wengi wa Kitanzania kutoijua lugha hiyo .

Akiwa wilayani Hai mkoani Kilimanjaro siku chache baada ya kutoka gerezani alipokuwa mahabusu, Mbowe alisema elimu ya Tanzania imejaa ubaguzi wa makundi kati ya wenye uwezo na masikini, huku akieleza kuwa ubaguzi huo unajidhihirisha hata katika ajira hususan kwenye taasisi na kampuni kubwa.

Akihutubia mamia ya wafuasi wake na wananchi waliojitokeza kumpokea katika viwanja vya Bomang’ombe, Mbowe alisema elimu inayotolewa kwa sasa haimjengi Mtanzania kuingia katika soko la ajira kutokana na mfumo wake ulivyo na kwamba inahitaji mabadiliko.

“Kumekuwa na ubaguzi katika elimu kwani viongozi wetu wamekuwa wakituhutubia tujifunze Kiswahili ni lugha yetu ya Taifa, lakini leo Kiswahili hicho kinazungumzwa kwenye shule zetu za kata, viongozi wote na watu wenye uwezo wanasomesha watoto katika shule za mfumo wa Kiingereza; huu ni ubaguzi,” alisema.

Kiongozi huyo anasema Chadema kikiingia madarakani, kitahakikisha watoto wote wanafundishwa kwa lugha ya Kiingereza, kwa kuwa ndiyo lugha ya kimataifa.

Anasema katika dunia inayokwenda kwa kasi huku ikichagizwa na mabadiliko ya teknolojia, maarifa ya lugha ya Kiingereza ni ya lazima na kwamba Kiswahili kitabaki kuwa kama somo la ziada.

Anatoa mfano wa namna Wakenya wanavyotamba katika soko la ajira, kwa sababu ya uwezo walionao katika kutumia Kiingereza.

‘’Vijana wa Kenya wamelikamata soko kubwa hata katika nchi zenye uchumi mzuri ndani ya Afrika tofauti na Watanzania, ambao licha ya kuwa na uwezo, wanakwamishwa na suala la lugha,’’ anaeleza.

Ilivyo sasa nchini, wanafunzi wa shule za awali hadi darasa la saba, wanafundishwa kwa lugha ya Kiswahili, huku Kingereza kikiwa kama somo.

Pia kuna shule za mchepuo wa Kingereza katika ngazi hiyo ya elimu, hata hivyo, nyingi zinamilikiwa na watu au taasisi binafsi. Wanafunzi hao wote wanapomaliza darasa la saba, wanalazimika kutumia Kiingereza kama lugha ya kufundishia.
Mbowe atuambie alienda kufanya nini Ikulu baada kutoka jela bila hata kufika nyumban kwake?

Asiudanganye ulimweng na wananchi Chadema sasa haina tena mpango wa kushika dola baada ya manusura

Chadema walikubali kuongea na mama mchana kweupe, biashara ishamaliza
 
Laiti mngejua watoto wanaotoka English medium wanavyofanya vizuri huku sekondari msingethubutu hata kidogo kumpinga Mbowe ! Watoto wanaotoka shule zetu za kiswahili mateso wanayoyapata huku sekondari laiti mngewaona mngemsapoti Mbowe mia. Ni wajibu wa serikali kutoa elimu isiyo na ubaguzi,... Kwanini wengine wasome kwa kiingereza,, wengine kwa kiswahili!?!? Kwanini watanzania wengine wajihisi wanyonge ktk nchi yao eti kisa tu wanasoma public schools!? Nafikiri hii ndo,hoja kuu ya Mbowe, nami namsapoti 100.
Huko mbeleni wanapofika vyuoni mwenye akili zinajionyesha bila kujali alisoma english media au kiswahili media
 
Akihutubia mamia ya wafuasi wake na wananchi waliojitokeza kumpokea katika viwanja vya Bomang’ombe, Mbowe alisema elimu inayotolewa kwa sasa haimjengi Mtanzania kuingia katika soko la ajira kutokana na mfumo wake ulivyo na kwamba i
Wanaomshauri Mbowe, wawe makini sana.

Tatizo siyo kujua lugha ya kiingereza.
Tatizo ni hili hapa lililoelezwa katika mstari huo hapo juu.

Awe mwangalifu sana na jambo hili, kwa sababu inaonekana anachanganya mambo hapa.

Tatizo siyo lugha inayotumika katika kufundisha, ni ubovu wa mfumo wa elimu kiujumla.

Natumaini CHADEMA hili jambo wataliwekea maanani zaidi na kulifanyia uchambuzi ulio makini, kuliko kuja na matamko ya kijumla jumla kama haya yanayosemekana yamesemwa na mwenyekiti wa chama hicho.

Itasikitisha sana kama CHADEMA watakuwa wanatafuta umaarufu kwa wananchi kwa kugusia matatizo makubwa kama kuporomoka kwa elimu yetu bila ya kuelewa tatizo ni nini na bila kuwa na ufumbuzi sahihi wa tatizo lenyewe.

Lazima wawe waangalifu sana kwa mambo kama haya.
 
Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.

Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.


Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.

kwa kiasi kikubwa sisi ndio tunauhitaji kwa sasa, kukomaa na kiswahili itatutesa sana na tutahitaji karne nyingi sana ili tuweze kusurvive, na itawezekana tu kama tutakuwa na uwezo wa kiteknolojia na kiuchumi hapo watu wengi watatuhitaji kuliko tunavyowahitaji...Kwa sasa tunaihitaji sana dunia inayotumia kiingereza kwa kiasi kikubwa kuliko yenyewe kutuhitaji sisi tunaoongea kiswahili....

Kwasasa Kiingereza kitiliwe mkazo jamii ijifunze iweze kuchangamana na dunia ili watu wetu waweze kuishi, kuliko sasa ambapo dunia kwa kiasi kikubwa inahitaji watu wazungumze kiingereza na ukiwa haujua automatically unakosa soko...

Mataifa mengi yanayotumia lugha zao, historically wana maguvu kiuchumi na wanajitegemea kwa kiasi kikubwa na program hizi walizianza zamani kabla dunia haijafika huku..
 
Kumbe kampeni za uchaguzi mkuu zimeanza eh?

anyway; amehama ktk kampeni ya katiba amehamia ktk kiswahili🤗
 
Anasema katika dunia inayokwenda kwa kasi huku ikichagizwa na mabadiliko ya teknolojia, maarifa ya lugha ya Kiingereza ni ya lazima na kwamba Kiswahili kitabaki kuwa kama somo la ziada.

Anatoa mfano wa namna Wakenya wanavyotamba katika soko la ajira, kwa sababu ya uwezo walionao katika kutumia Kiingereza.

‘’Vijana wa Kenya wamelikamata soko kubwa hata katika nchi zenye uchumi mzuri ndani ya Afrika tofauti na Watanzania, ambao licha ya kuwa na uwezo, wanakwamishwa na suala la lugha,’’ anaeleza.

Ilivyo sasa nchini, wanafunzi wa shule za awali hadi darasa la saba, wanafundishwa kwa lugha ya Kiswahili, huku Kingereza kikiwa kama somo
Totally WRONG!

Sijawahi kusikia Ujerumani au Ufaransa wakiwafundisha watoto wao kwa lugha ya Kiingereza. Wala waChina waliotapakaa dunia nzima sasa hivi hawajifunzi masomo yao kwa lugha ya Kiingereza.



Hapa ndipo Mbowe na chama chake wanapolikoroga, wanapodhani Kenya ndio mfano wa kupigia chepuo kwa mambo mazuri yaliyopo huko!

Nina hofu sana juu ya chama hiki kuifanya Tanzania kuwa tegemezi wa nchi hiyo jirani kwa kila kitu. This is a very big put off about this political party.
 
Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.

Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.

Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.
80% ya maarifa ya ulimwengu yameandikwa kwa lugha ya kiingereza ....st kayumba maarifa km ya kwenye kitabu rich dad poor dad hawezi kuyaelewa.
 
Back
Top Bottom