Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.
Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.
Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.