Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Laiti mngejua watoto wanaotoka English medium wanavyofanya vizuri huku sekondari msingethubutu hata kidogo kumpinga Mbowe ! Watoto wanaotoka shule zetu za kiswahili mateso wanayoyapata huku sekondari laiti mngewaona mngemsapoti Mbowe mia. Ni wajibu wa serikali kutoa elimu isiyo na ubaguzi,... Kwanini wengine wasome kwa kiingereza,, wengine kwa kiswahili!?!? Kwanini watanzania wengine wajihisi wanyonge ktk nchi yao eti kisa tu wanasoma public schools!? Nafikiri hii ndo,hoja kuu ya Mbowe, nami namsapoti 100.
Huna sababu ya kumsifu Mbowe. Hayo yalishaandikwa siku nyingi sana ktk Tume ya Makweta! Yaliandikwa kwa utafiti mzuri, siyo huyo anayesema kisiasa tu bila takwimu.
 
Huna sababu ya kumsifu Mbowe. Hayo yalishaandikwa siku nyingi sana ktk Tume ya Makweta! Yaliandikwa kwa utafiti mzuri, siyo huyo anayesema kisiasa tu bila takwimu.
Sijakuelewa! Hiyo tume ilipendekeza nini!?
 
Siungi mkono hoja. Lugha nzuri ya kufundishia mtoto ni ile Lugha Mama! Na kwa bahati zuri kwa Tanzania ni Kiswahili.
Hicho kigezo cha kusema Kingereza ni Lugha ya Kimataifa, hakina mashiko. Tunaweza kukisoma kama Lugha nyingine mfano Kichina, Kifaransa, nk. Kwa ajili ya hayo matumizi ya Kimataifa.

Kuhusu ubaguzi wa kielimu nchini, yuko sahihi kabisa! Elimu yetu inawabagua watoto kwa misingi ya mwenye nacho na asiye nacho! Elimu Bure kwa Tanzania ni kichaka cha watawala kuwapumbaza Watanzania masikini! Maana watoto wao hawasomi huko! Badala yake wanawapeleka shule binafsi za mchepuo wa kiingereza, na zenye gharama kubwa.


Na hata watoto wake Mh. Mbowe bila shaka wamesoma/wanasoma shule za gharama kubwa, kama ilivyo kwa wanasiasa wenzake wengi! badala ya zile za kata.
Sasa kwanini tuna so called english mediam ambazo miaka ya karibuni kila mzazi anataman mtoto wake asome huko?????
 
Sasa kwanini tuna so called english mediam ambazo miaka ya karibuni kila mzazi anataman mtoto wake asome huko?????
Ni kwa sababu Serikali imeruhusu soko huria, huku ikishindwa kuhimili ushindani kutoka sekta binafsi! Na badala yake ikaamua kuingiza siasa kwenye shule zake na mfumo wa elimu kwa ujumla.

Ni suala tu la kuweka wazi sera ya elimu. Hata sasa katika nchi yetu kuna shule zinatumia mtaala wa Cambridge! Lakini haujasababisha elimu yetu kukosa thamani. Hivyo ni suala tu la Serikali kuamua kwa vitendo.
 
Ni kwa sababu Serikali imeruhusu soko huria, huku ikishindwa kuhimili ushindani kutoka sekta binafsi! Na badala yake ikaamua kuingiza siasa kwenye shule zake na mfumo wa elimu kwa ujumla.

Ni suala tu la kuweka wazi sera ya elimu. Hata sasa katika nchi yetu kuna shule zinatumia mtaala wa Cambridge! Lakini haujasababisha elimu yetu kukosa thamani. Hivyo ni suala tu la Serikali kuamua kwa vitendo.
Kwa vitendo vipi ivyo?
 
Wala kukó usiende, kumrahisishia kazi aingie NECTA akalinganishe matokeo ya English medium vs. Kayumba.
Sababu kubwa ya hiyo tofauti ni Serikali! Kama inabeba tu watoto wote kujiunga na shule zake, huku miundombinu ikiwa ni duni! Usitarajie maajabu kwenye matokeo.

Warudishe mchujo darasa la nne na kidato cha pili, waanzishe vyuo vya VETA kila Kata kwa ajili ya wale wanafunzi wanaopenda masomo ya ufundi na michezo, waboreshe mishahara na motisha kwa walimu, nk

Halafu uone matokeo.
 
Ni kwa sababu Serikali imeruhusu soko huria, huku ikishindwa kuhimili ushindani kutoka sekta binafsi! Na badala yake ikaamua kuingiza siasa kwenye shule zake na mfumo wa elimu kwa ujumla.

Ni suala tu la kuweka wazi sera ya elimu. Hata sasa katika nchi yetu kuna shule zinatumia mtaala wa Cambridge! Lakini haujasababisha elimu yetu kukosa thamani. Hivyo ni suala tu la Serikali kuamua kwa vitendo.
Mkuu sera ya Elimu ipô wazi , lugha mbili,kiingereza au kiswahili vitatumika kutekeleza mtaala, chaguo ni lako
 
Sababu kubwa ya hiyo tofauti ni Serikali! Kama inabeba tu watoto wote kujiunga na shule zake, huku miundombinu ikiwa ni duni! Usitarajie maajabu kwenye matokeo.

Warudishe mchujo darasa la nne na kidato cha pili, waanzishe vyuo vya VETA kila Kata kwa ajili ya wale wanafunzi wanaopenda masomo ya ufundi na michezo, waboreshe mishahara na motisha kwa walimu, nk

Halafu uone matokeo.
Kwahiyo unasimamia kipi!? Kiswahili au Kiingereza ktk kutekeleza mtaala!?
 
Kwahiyo unasimamia kipi!? Kiswahili au Kiingereza ktk kutekeleza mtaala!?
Mimi naamini katika Lugha Mama (Mother tongue)! Mtoto anaelewa zaidi ukimfundisha kwa kutumia lugha aliyo kua nayo, kuliko ile aliyo jifunza ukubwani.

Hivyo namatani kuona siku moja Kiswahili kikitumika katika ngazi zote za elimu. Na kama kuna watu wataamua kiwapeleka watoto wao shule za mchepuo wa kiingereza, waachwe.

Ila tu elimu itakayo tolewa kwa kutumia Lugha Mama, iwe na ubora unaotakiwa! Na isifanyiwe dhihaka kama ilivyo sasa.
 
Hili la lugha ya kufundishia serikali ya kijani..imefeli pakubwa..nadhani ni moja ya mipango yao miovu ya kuharibu elimu ya wananchi ili waendelee kutawala.

Muhimu kwa na lugha moja yakifundishia kuanzia shule za awali hadi chuo kikuuu.

Hili nalo kijani mmeshindwa kabisa kulifanyia maamuzi?
Katiba mpya muogope
Hata mfumo wa elimu nao kuboresha mnaogopa.
Absurd

#MaendeleoHayanaChama
 
Awaombe radhi wa kanda ya ziwa.

Alisema Magufuli aliwabagua watu wa Kilimanjaro maana yake na yeye akiwa rais atawabagua wa kanda ya ziwa.
Hivi huwa hamuwezi kujikita kwenye hoja..hata kama m alipwa sometimes tumieni akili...au id zenu zipo lumumba mmeshikiwa akili.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mbowe hataki kukuza lugha ya Kiswahili ili iwe lugha ya kitaaluma?
Mbona wachina, Wajapan, Warusi, Waswede, Wajerumani, wafaransa wanatumia lugha zao kufundishia watoto wao kwa nini kiswahili kisiweze?
Kiswahili chenyewe kinatushinda..sijui tutaweza..

#MaendeleoHayanaChama
 
Laiti mngejua watoto wanaotoka English medium wanavyofanya vizuri huku sekondari msingethubutu hata kidogo kumpinga Mbowe ! Watoto wanaotoka shule zetu za kiswahili mateso wanayoyapata huku sekondari laiti mngewaona mngemsapoti Mbowe mia. Ni wajibu wa serikali kutoa elimu isiyo na ubaguzi,... Kwanini wengine wasome kwa kiingereza,, wengine kwa kiswahili!?!? Kwanini watanzania wengine wajihisi wanyonge ktk nchi yao eti kisa tu wanasoma public schools!? Nafikiri hii ndo,hoja kuu ya Mbowe, nami namsapoti 100.
Halafu wajinga wanalazimishwa kupiga makofi eti Elimu Bure...hao wanaoshadadia Elimu Bure ,mbonahawapeleki watoto wao.kwenye Shule hizo !
Ubaguzi unaoengenezwa ni hatari Kwa siku zijazo!
Nenda vijijini uone Hilo zao la Shulee za Kata wanafanyaa Nini!?
 
Back
Top Bottom