Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Nyie watu vipi?Mahakama inaenda kusikiliza madai ya Mwenyekiti kwamba amechafuliwa.
Hoja za msigwa zinapaswa kujibiwa na chama kupitia katibu mkuu kama ambavyo Lissu alipendekeza.
Tuanze na za ndugai kwanzaHOJA ZA MSIGWA ZIJIBIWEbo
Hata kwa Kinana alisema hivyo hivyo mwisho wa siku akamuangukia Kinana
Ni vyema Wanasiasa Vijana wakajifunza kuhusu hayoSolemba na Gundu juu. Leo hii kina Samson Mwigamba wapo wapi. Nani anayejali leo hii Vincent Mashinji anafanya nini huko alipo!?
Sio wote lakiniCCM ni chama cha Utulivu na amani, ukiwemo ukawekwa bench, Tulia kimya, elewa unapimwa imani, 😊, ukifaulu hapo elewa umefaulu. Kaa mkao, ona yule mkulima wa nyanya, mifano ni mingi sana.
Hata kauli na misimamo yake kuhusu Wamasai kuhamishwa Ngorongoro zilionyesha wazi kuwa anataka kuwafurahisha watawala.Huyu tangia JPM amlipie kutoka segerea ilikuwa wenda wazimu
kuendelea kumwamini kuwa ni mwenzetu
Masahihisho- Alipata kura 1 tuTangu alipopata kura mbili (2) kwenye kura za maoni huko Kawe kwenye chama chao, sijawahi kujua CCM walimtupia kwenye jalala la wapi.
Hata kauli na misimamo yake kuhusu Wamasai kuhamishwa Ngorongoro zilionyesha wazi kuwa anataka kuwafurahisha watawala.
Shida ukishakua ccm akili sijui inaendaga wapi? Apa unaweza kuona Mzee wa watu Mzee Lowassa ( R.I.P) alivyokua smart. alipe tu ili akomeMkubwa tunaweza kuona chanzo cha habari yako kama hautajali?
By the way ni jambo jema kumtaka alipe hiyo fidia ama akathibitishe madai yake
Maana Mchungaji Msigwa Kila Siku yeye na Mbowe, Mbowe na yeye
Utasema wana ugomvi wa kuibiana mali ama Wapenzi 🙌
1 Kwamba anaiba pesa za chama kwa kutumia Mbowe Foundation
2. Amegeuza chama kuwa SACCOS yake
3. Chadema digital inamilikiwa na Mbowe kwa manufaa yake
My take: hilo nililitegemea and that is the right way to go!
=====
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amempa siku tano aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyassa, Mchungaji Peter Msigwa, kuomba radhi, asipfanya hivyo ajiandae kulipa kulipa fidia ya shilingi bilioni 5 Mahakamani kutokana na madai ya kumkashifu na kuharibu chapa yake kutokana na matamshi ya Msigwa yaliyotolewa hadharani baada ya kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika barua (notisi ya madai) iliyotolewa Septemba 2, 2024 ikiwa na sahihi ya tarehe 4 Septemba, 2024, mawakili wa Mbowe ambao ni Hekima Mwasipu na wenzake kutoka Matwiga Law Chambers, Msigwa anadaiwa kutoa matamshi ya uongo na kumchafua Mbowe mbele ya umma.
“Msigwa alitumia majukwaa ya mikutano, vyombo vya habari, na hata mitandao ya kijamii kutoa madai ya kumkashifu mteja wetu,” ameleza Wakili Mwasipu.
Imeelezwa kuwa Msigwa alidai kuwa Mbowe ameanzisha "Mbowe Foundation," na anatumia chama cha CHADEMA kwa manufaa yake binafsi. Katika moja ya mikutano yake, Msigwa alinukuliwa akisema, "Mwenyekiti wa CHADEMA amegeuza chama kuwa SACCOS, fedha za chama zinaishia kwenye taasisi binafsi na si kwenye akaunti za chama.”
Mawakili wa Mbowe wameeleza kuwa matamshi hayo yameathiri sifa ya Mbowe ndani na nje ya Tanzania, hasa kutokana na nafasi zake mbalimbali kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuwa Naibu Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia vya Afrika (DUA).
“Mteja wetu anaona maneno yote yanayozungumzwa na kunukuliwa hapo juu katika maana yake ya asili, muktadha na misemo kuwa ni kashfa, dharau na kudhuru sio tu sifa yake binafsi bali pia kwa familia yake yote, marafiki, taaluma (Siasa), Jumuiya ya Biashara, Jumuiya ya Kidini, marafiki na rika. Maneno haya si chochote lakini ushahidi dhahiri wa nia mbaya dhidi ya mteja wetu”, imeelezwa na mawakili.
Mbali na hilo, Msigwa alidai kuwa CHADEMA Digital ambayo ni huduma ya usajili wa wanachama, inamilikiwa na kampuni binafsi na kwamba Mbowe anatumia fedha za chama kwa manufaa binafsi.
“Hali hii imeleta hasara kubwa kwa mteja wetu kwani sifa yake ya kiongozi wa kisiasa, mfanyabiashara na mwanafamilia imeathirika sana,” alisema Mwasipu.
Kwa mujibu wa notisi hiyo, Msigwa anatakiwa kuomba radhi kupitia machapisho katika magazeti mawili; moja lenye kuweza kufikia nchi nzima na lingine ambalo linaweza kuwafikia watu walau wa kanda, na kulipa fidia ya Shilingi bilioni 5, la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
Pia soma
View attachment 3088571View attachment 3088572View attachment 3088573View attachment 3088574View attachment 3088575View attachment 3088576View attachment 3088577
- Freeman Mbowe amdai Mchungaji Peter Msigwa bilioni 5 kwa kumkashifu na kumchafulia jina lake
- Peter Msigwa: Msajili wachunguze CHADEMA, wana vikundi vinaitwa ZOO na JOB. Mbowe ni Nkurunziza
- Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA
- Mchungaji Msigwa: Mbowe siyo Msakata Rhumba maarufu ndio sababu hadi sasa bado yuko Jukwaani japo muda umeisha!
- Peter Msigwa: CHADEMA idhibitiwe kabla haijaleta vurugu nchini
- Mchungaji Msigwa akiri kumsingizia Kinana ujangili, amwangukia na kumwomba radhi
Political tolerance kwenye maneno ya uongo, sasa msigwa akadhibitishe au alipe iyo B5Sasa kutajwa na msigwa tu alipwe bil5 siku akiwa rais huyo mbowe wenu wananchi si tutalipishwasana hozo bil5? Ina maana mbowe na wafuasi wenu hamna political tolerance?
Hatari sana MkuuShida ukishakua ccm akili sijui inaendaga wapi? Apa unaweza kuona Mzee wa watu Mzee Lowassa ( R.I.P) alivyokua smart. alipe tu ili akome
Katibu Mkuu akijibu kwa maelezo tu mtadai haaminiki; atoe ushahidi wa nyaraka. Nyaraka za chama haziwezi kutolewa kwenye media. Kuna confidentiality na pia wako watakaodai ni feki. Inabidi zitolewe na kuhakikiwa mahakamani kumaliza ubishi.Mahakama inaenda kusikiliza madai ya Mwenyekiti kwamba amechafuliwa.
Hoja za msigwa zinapaswa kujibiwa na chama kupitia katibu mkuu kama ambavyo Lissu alipendekeza.
Ushahidi wa nyaraka ndyo kitu muhimu, pia naamini mpaka Lissu kusema hayo anajua kinacho endelea ndani ya chama, kuna Madudu yanafanyika na yanachafua taswira ya chama kwa ujumla.Katibu Mkuu akijibu kwa maelezo tu mtadai haaminiki; atoe ushahidi wa nyaraka. Nyaraka za chama haziwezi kutolewa kwenye media. Kuna confidentiality na pia wako watakaodai ni feki. Inabidi zitolewe na kuhakikiwa mahakamani kumaliza ubishi.
.
CCM wamemtupia Msigwa mjusi wa hii kesi ili zile hela walizmlipa kwenye biashara ya kumnunua ziishe kwenye kesi maana wanaona hakuna la maana aliloleta CCM toka Chadema kwani yote anayosema yalishasemwa na wote walionunuliwa kama bidhaa. Msigwa ameyatimba, hili ni la kwake mwenyewe.
Ccm watamlipia ,apa ndo kuna mtego kama kweli ccm wanampenda msigwa au la, wasipo mlipia basi Msigwa ondoka ccm achana na siasa, ukiomba msamaha tu tiyari iyo ni pigo kwako na ccm waliokutuma,Yale yale kama ya kinana na Msigwa hadi akaomba poo... ndilo linaloenda kutokea... Msigwa fanya uungwana mapema kabla mambo hayajawa mambo... kuomba msamaha nayo ni heri, sijui kama unazo hizo billion tano, labda kama mpango ni kukufilisi hadi nyumba....
mbona hamna kesi mule gentleman,Zitajibiwa mahakamani