Elections 2015 Freeman Mbowe atoa msimamo mzito kuhusu wanaoasi mageuzi

Elections 2015 Freeman Mbowe atoa msimamo mzito kuhusu wanaoasi mageuzi

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema Chadema siyo mali yake wala mali ya mtu yeyote bali ni mali ya wanachama.

Kutokana na hali hiyo, amesema kama kuna mtu na mkewe wana mawazo tofauti na wenzao ndani ya chama hicho, watu hao wataachwa chama kiendelee kusonga mbele.

Mbowe alitoa kauli hiyo mjini hapa jana alipohutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, waliohudhuria mkutano wa kampeni wa mgombea urais wa Ukawa kupitia Chadema, Edward Lowassa, uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Nduwa.

"Makamanda najua kuna watu wamekuwa wakiniuliza juu ya kauli iliyotolewa jana (juzi) na aliyekuwa Katibu Mkuu wetu, Dk. Wilbrod Slaa.
"Napenda niwaambie kuwa mwaka 1992 tulipoanzisha Chadema, ilikuwa ni kama safari ya treni kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma. Tulipoanza safari hiyo na kufika Pugu, abiria wengine walishuka na wengine wakapanda na tulipofika Morogoro, abiria wengine wakashuka na wengine wakapanda na mwaka huu Oktoba 25 safari yetu itafika Kigoma.

"Chadema siyo mali yangu, wala siyo mali ya mtu yeyote bali ni mali ya wanachama, anayedhani Chadema ni mali yake, ataondoka, chama atakiacha.
"Kamati Kuu, Baraza Kuu na mkutano mkuu wa Chadema viliamua Lowassa ndiye awe mgombea wa urais kupitia Chadema pamoja na Ukawa.
"Sasa, kama kuna mtu na mkewe wana mawazo tofauti na sisi, hatuna muda wa kupoteza, tutawaacha, tutasonga mbele," alisema Mbowe na kushangiliwa.

Kwa mujibu wa Mbowe, Watanzania wanahitaji mabadiliko na ili mabadiliko hayo yafikiwe ni lazima kila mmoja ashiriki kadiri atakavyoweza.
Wakati huo huo, Mbowe alisema kutokana na muda mfupi wa kampeni uliopangwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), mgombea wao wa urais na mgombea mwenza wake, Duni Haji, hawataweza kufika majimbo yote nchini.

Kutokana na hali hiyo, alisema wamelazimika kuunda vikosi vinne vya kampeni vitakavyotumia helkopta nne kuzunguka nchi nzima.
"Nchi yetu ina majimbo 215 Tanzania Bara na ina majimbo 50 Zanzibar. Katika hali ya kawaida, mgombea urais na mgombea mwenza wake hawataweza kuyafikia majimbo yote kabla ya tarehe ya uchaguzi.

"Kwa hiyo tumeunda vikosi vinne vya kampeni vitakavyotumia helkopta nne kuanzia wiki ijayo ili maeneo atakayoshindwa kufika mgombea urais na mgombea mwenza, vikosi hivyo vifike," alisema Mbowe.

Aliwataja baadhi ya watakaokuwa katika vikosi hivyo kuwa ni aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema, aliyekuwa Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje, aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na yeye mwenyewe.


Chanzo: Mtanzania
 
Wakati chadema ikitapa tapa kujinasua kwenye mgogoro wa kisiasa wa chama hicho, taarifa za ndani zinasema Mbowe kasema Slaa ataendelea kupata haki zake zote mpaka atakapoandika barua ya kujiuzulu. Habari za ndani zinasema ndani ya chadema kuna mpasuko mkubwa haswa baada ya watu wengine kuanza kulalamikia maamuzi ya chama kufanyw kw kumshirikisha gwajima wakati wao hawakupata nafasi hiyo, maandamano yanatabiriwa kutokea kila kona ya nchi. Mbowe katoa waraka kuwa Slaa asijibiwe, kama ni majibu yaelekezwe ccm anaodai ni wadhamini wake
 
Short and clear
"Kama kuna mtu na mkewe wana mawazo kuwa chama ni mali yao wataachwa waende"...

Full stop
 
Safii, tupeni sera tuu, msimzungumzie tena mtuu, wacheeni wapige kelele sisi tunawaelewa
 
Safi..tunataka taarifa nzuri kama hizi kila wakati
 
Unajua Mbowe anaweza kuongoza chama 7bu ya elimu,misimamo aliyonayo, hapimi madhara yy ni mbele daima,wasomi ni majanga
 
Udhaifu mkubwa mnakimbia kujibu issues badala yake mnajikita kwenye mambo binafsi, siasa hizi mnazidi kuonesha kwamba ubinafsi ndio umewajaa badala ya maslahi ya taifa. Kila mwanasiasa anataka kuonekana bora , badala ya kujikita kujenga nchi yetu.
 
Mboweeeee...atiii umeunda vkosi..mzee lash indies kuendelea nn?
 
Wakati chadema ikitapa tapa kujinasua kwenye mgogoro wa kisiasa wa chama hicho, taarifa za ndani zinasema Mbowe kasema Slaa ataendelea kupata haki zake zote mpaka atakapoandika barua ya kujiuzulu. Habari za ndani zinasema ndani ya chadema kuna mpasuko mkubwa haswa baada ya watu wengine kuanza kulalamikia maamuzi ya chama kufanyw kw kumshirikisha gwajima wakati wao hawakupata nafasi hiyo, maandamano yanatabiriwa kutokea kila kona ya nchi. Mbowe katoa waraka kuwa Slaa asijibiwe, kama ni majibu yaelekezwe ccm anaodai ni wadhamini wake

Mbowe amesema chama siyo mali ya mtu ni mali ya wanachama kwa hiyo ajitayarishe kuondoka kwani hajawaambia viongozi wenzake ukweli kuhusu mchakato wa kumpokea fisadi lowasa. Viongozi mwongo hafai!
 
Sasa anawatisha wanaoondoka au??
 
OTH_4428.jpg
 
Ukawa ni gari iliyo speed na haina kuchimba dawa, ukibanwa na haja ruka kutokea dirishani kama mzee slaa

Padri aliyeshindwa utumishi

Hahahahahahah mkuu, kwamaana hiyo unataka kusema kabanwa na kurukia Dirishani kisha kusambaratika viungo? Hili ni balaa!!

BACK TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom