Freeman Mbowe na Viongozi CHADEMA jiteteeni juu ya hoja hizi za kupotea kwa Ben Saanane

Freeman Mbowe na Viongozi CHADEMA jiteteeni juu ya hoja hizi za kupotea kwa Ben Saanane

Hivi ni kwa nini kikosi cha Red Brigade cha Chadema, hakihusishwi na suala la kupotea Ben Saanane wakati imeelezwa kwenye Katiba ya Chadema kuwa ndicho kitahusika na usalama wa viongozi na Mali za Chadema?
 
Hivi ni kwa nini kikosi cha Red Brigade cha Chadema, hakihusishwi na suala la kupotea Ben Saanane wakati imeelezwa kwenye Katiba ya Chadema kuwa ndicho kitahusika na usalama wa viongozi na Mali za Chadema?
Watakuwa na wao wanahusika hebu angalia kwa makini hizi picha then utanipa majibu baadaye kwenye inbox
image.jpg
image.jpg
 
Kama mliweza kuperuzi kwamba UKAWA walikuwa na mitambo ya kuhakiki kura zao vipi inakuwaje na hili la Ben mnashindwa nini kubaini yaliyompata ama haki ni kwa maccm only.....demons....
 
.wewe unashindwa kuhoji Lumumba hela za maafa ya bukoba ziliko na kwanini mwenyekiti wenu hakuguswa na swala zima LA maafa unahoji kwa wengine tena eti kwanini gazeti halikuandika?hivi vyombo vya usalama kazi yao nini kama si kulinda na kujua taarifa kama za kupotea binadamu,puuuuuzi kabisa
Ninyi ndiyo watu mnaojifanya mna uchungu wa kupotea kwa Ben kinafiki, hapa tunazungumzia kupotea kwa mtu wewe unaleta ushabiki wako wa kivyama kama mtoto wa chekechea. Hii Tovuti sasa isiitwe The Home Great Thinkers maana ina vilaza wengi sana tukiendelea kuliita hili tovuti The Home Of Great Thinkers tunakosea heshima kina,John Locke,Thucydide,Aristotle, Moses Maimonides, Nelson Mandela, Plato, Bill Shakespeare, Galileo Galilei n.k
 
Lizaboni hiyo ndiyo site ya ujenzi wa ofisi mpya ya Taifa ya CHADEMA?
Hahahahahaaaaaaaaa! Habari yake na maeezo kamili nitawaletea kesho. Kuna mambo mazito huko. Mkae mkao wa kula. Bado naendelea kufuatilia kwa undani zaidi. Muwe na subira. Kesho kigongo kinatoka
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wana CHADEMA wakihoji ukimya wa viongozi wa chama hicho katika kuzungumzia suala la kupotea kwa Ben Saanane. Maoni ya wana CHADEMA wengi ni kwamba pamoja na kuelekeza lawama kwa Jeshi la Polisi kutokana na kuizika miili ya watu saba bila ya kufanyiwa uchunguzi, mzigo mkubwa anashushiwa Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe. Ben kapotea huku Bosi wake Mbowe anaendelea kuponda raha huko Ulaya. Hajashtushwa na wala hataki kushtushwa na kupotea kwa Ben Saanane. Kwa wadhifa wa Ben Saanane, haiingii akilini kuona Bosi wake akiendelea kuponda raha huko Ulaya badala ya kusitisha safari yake kuungana na ndugu na marafiki wa Ben kumtafuta. Jawabu la haraka haraka ni kwamba Mbowe anajua nini kinaendelea juu ya kupotea kwa Ben.

Mapema leo asubuhi, ndugu yangu Malisa Godlisten Joseph amehoji kwa uchungu mkubwa sana and I can feel, kitendo cha Gazeti la Tanzania Daima ambalo kwa mujibu wa Malisa ni kwamba ni gazeti lao kutoipa kipaumbele taarifa ya kupotea kwa Ben kama ilivyoelezwa kwenye Press Conference ya Umoja wa Kuhoji Tanzania. Kwa mujibu wa Malisa, Gazeti la Tanzania Daima limeipuuza Taarifa yao na badala yake wamempamba Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwa Bado yupo yupo CCM. Malisa anasema kuwa hata gazeti la Kada wa CCM, Majira limewapiku Tanzania Daima.

Nikuhakikishie ndugu yangu Malisa kuwa haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya. Yamepangwa na kupangika. Awali nilipofichua uhusika wa Mbowe juu ya kupotea kwa Ben mlinishambulia na kuniona kuwa ni mchonganishi. Sasa yamewakuta. Akili imeanza kuwarejea na sasa mnaungana na Lizaboni kimya kimya.

Wapo pia wanaosema kuwa Freeman Mbowe anastahili kuhojiwa kutokana na upotevu wa Ben. Naungana nao moja kwa moja kwani familia yake iliwajibika ila Mbowe na viongozi wenzake hawakuwajibika na hawapo tayari kuwajibika.

Kurasa zao za facebook hakika zimechafuka. Mashambulizi kwa Mbowe yamepamba kila kona. Wapo wanaosema waziwazi lakini wengine wanahoji kimya kimya. Mwisho wa siku akili itawarejea na wataanza kupaza sauti.

Nimalizie kwa kusema kuwa kabla hujamtafuta mbaya wako nje ya nyumba, jaribu kutafakari kwa kina mahusiano yako na watu wa ndani ya nyumba yako.

View attachment 445613 View attachment 445614 View attachment 445615
Nahisi hili deal limeharibiwa na familia ya Ben, maana lilipangwa vizuri sana lilipuliwe wakati jamaa wako nje ya nchi halafu walizungumzie wakiwa ughaibuni ili serikali ilaumiwe katika ngazi ya kimataifa lakini wanafamilia hawakutonywa hivyo imebidi kina Mbowe wakae kimya. Unaonaje mkuu Lizaboni?
 
Hahahahahaaaaaaaaa! Habari yake na maeezo kamili nitawaletea kesho. Kuna mambo mazito huko. Mkae mkao wa kula. Bado naendelea kufuatilia kwa undani zaidi. Muwe na subira. Kesho kigongo kinatoka


Niite tafadhali kikiwa tayari...
 
Wanafichana wenyewe kwa figisu figisu zao halafu wanataka iwe habari ya mjini
Chacha Wangwe alivyojidai "kuchongoa mdomo" kuhusu utaratibu wa chama
Mawazo aliyekuwa mwenyekiti wa chama Geita alivyokula hela akaharibu utaratibu wa kampeni za mgombea urais na kuingia doa
 
Kumbe Tanzania Daima ni "gazeti letu"?!!!
 
Kuna mtu na kitu hakisemwi hapa, hata unashindwa kuamini ukweli uko wapi.
 
Mumkamate huyo Mbowe km kuna ishara ya ushiriki wake ktk hilo tukio! Mnashindwa nini?

Jamani hebu tuacheni propaganda chafu na tufanye siasa safi na si za kiaharamia kwa mustakabali Wa maendeleo ya taifa letu huku kila mtanzania akiwa sawa na mtanzania mwingine iwe wapinzani au watawala maana kwa kufurahia hivi vitendo iwe vimetokea kwa Ben kwa namna yoyote ile sio vzr. Sote ni watz na wote tuna haki sawa ya kufurahia kuishi ktk hii nchi yetu.
tumkamate!! kwani Ben amewahi kutufurahisha nini? kama panzi wamepotezana halafu eti kunguru akashtaki
 
Mmempeleka wapi rafiki yangu Ben-Rabiu Ben-Rabiu Wa Saanane

Amewatumikia kwa muda mrefu na kwa hali ngumu

Hotuba mnazozisikia Mbowe akihutubia si zake ni za rafiki yangu Ben

Kwenye mambo ya mikakati na sera anajitolea kwa kiasi kikubwa

Kiufupi Ben ndiye kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani

Nililiona Kundi la Wanasheria lililokwenda kumtetea mtu anayetukana watu na anayetaka Rais afe Kule Arusha lakini nasikitika sijaona kiongozi wa Chadema akizungumzia kuhusu Ben.

Nawaona wakila bata Ulaya huku Ben asifahamike mahali alipo,
Naamini safari hii Joyce Mukya hajasafiri naye kama ilivyo kawaida yake if other things remain constant!

Binafsi nimeumia sana na hili na litawarudisha nyuma vijana wenu wengi kwasababu Ikiwa huyu ni Ben mnayeshinda naye Makao makuu mnamfanyia hivi vipi kuhusu mdogo wangu Mwanakijiji Lugusi, ama Charles Francis, ama Malisa na Eliza Beth si ndio mtafanya sherehe kabisa siku wakipotea?

Hivi nyie viongozi mnaweza kukaa kimya siku Lema akipotea?
Mnaweza kukaa kimya siku Joyce Mukya akipotea?
Mnaweza kukaa kimya siku Lowassa akipotea ingawa ametoka Ccm juzi na yupo kwenu kwa ajili ya Urais tu, au kwasababu Lowassa ana pesa na rafiki yangu Ben hana?
Ndio maana mkampa na Ujumbe wa kamati kuu!

Sidhani kwa kiongozi mwenye akili timamu aliyepata sifa kutokana na uwezo wa maandiko ya Ben, anayeonekana Msomi kutokana na Elimu ya Ben kusafiri kwenda Ughaibuni huku msaidizi wako akiwa hajulikani mahali alipo!

Niliwahi kumshauri Ben achana nacho hiki Chama, hiki Chama ni cha kihuni hakina fadhila,kilimuacha Dr Slaa na kumtukana na kumuita msaliti huku dada yangu Josephine Mushumbusi akitukanwa kila aina ya tusi kwasababu ya pesa za Lowassa.

Leo wamemuacha rafiki yangu bila kuuthamini utu wake,akili na nguvu zake alizozitumia kuiinua Chadema!

Nakumbuka ndoto zako za kumrithi Comrade Joseph Selasini kule Rombo lakini Viongozi wako wa Chadema hawalioni hili!
Wapo Ulaya wanastarehe!

Naishukuru serikali kwa kuonesha ushirikiano mkubwa wa kukutafuta na naiomba iendelee kushughulikia suala hili!

Nakuombea Popote ulipo rafiki yangu uwe salama

Safety be upon you in the almighty name of JESUS CHRIST!

Aluta Continua, Victory Ascerta!
mlikuwa hamjui eeh, mkiambiwa chadema wapiga dili, mnabisha
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wana CHADEMA wakihoji ukimya wa viongozi wa chama hicho katika kuzungumzia suala la kupotea kwa Ben Saanane. Maoni ya wana CHADEMA wengi ni kwamba pamoja na kuelekeza lawama kwa Jeshi la Polisi kutokana na kuizika miili ya watu saba bila ya kufanyiwa uchunguzi, mzigo mkubwa anashushiwa Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe. Ben kapotea huku Bosi wake Mbowe anaendelea kuponda raha huko Ulaya. Hajashtushwa na wala hataki kushtushwa na kupotea kwa Ben Saanane. Kwa wadhifa wa Ben Saanane, haiingii akilini kuona Bosi wake akiendelea kuponda raha huko Ulaya badala ya kusitisha safari yake kuungana na ndugu na marafiki wa Ben kumtafuta. Jawabu la haraka haraka ni kwamba Mbowe anajua nini kinaendelea juu ya kupotea kwa Ben.

Mapema leo asubuhi, ndugu yangu Malisa Godlisten Joseph amehoji kwa uchungu mkubwa sana and I can feel, kitendo cha Gazeti la Tanzania Daima ambalo kwa mujibu wa Malisa ni kwamba ni gazeti lao kutoipa kipaumbele taarifa ya kupotea kwa Ben kama ilivyoelezwa kwenye Press Conference ya Umoja wa Kuhoji Tanzania. Kwa mujibu wa Malisa, Gazeti la Tanzania Daima limeipuuza Taarifa yao na badala yake wamempamba Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwa Bado yupo yupo CCM. Malisa anasema kuwa hata gazeti la Kada wa CCM, Majira limewapiku Tanzania Daima.

Nikuhakikishie ndugu yangu Malisa kuwa haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya. Yamepangwa na kupangika. Awali nilipofichua uhusika wa Mbowe juu ya kupotea kwa Ben mlinishambulia na kuniona kuwa ni mchonganishi. Sasa yamewakuta. Akili imeanza kuwarejea na sasa mnaungana na Lizaboni kimya kimya.

Wapo pia wanaosema kuwa Freeman Mbowe anastahili kuhojiwa kutokana na upotevu wa Ben. Naungana nao moja kwa moja kwani familia yake iliwajibika ila Mbowe na viongozi wenzake hawakuwajibika na hawapo tayari kuwajibika.

Kurasa zao za facebook hakika zimechafuka. Mashambulizi kwa Mbowe yamepamba kila kona. Wapo wanaosema waziwazi lakini wengine wanahoji kimya kimya. Mwisho wa siku akili itawarejea na wataanza kupaza sauti.

Nimalizie kwa kusema kuwa kabla hujamtafuta mbaya wako nje ya nyumba, jaribu kutafakari kwa kina mahusiano yako na watu wa ndani ya nyumba yako.

View attachment 445613 View attachment 445614 View attachment 445615
Tanzania Daima ni gazeti "lenu" UGT au la Chadema
 
Back
Top Bottom