Freeman Mbowe na Viongozi CHADEMA jiteteeni juu ya hoja hizi za kupotea kwa Ben Saanane

Freeman Mbowe na Viongozi CHADEMA jiteteeni juu ya hoja hizi za kupotea kwa Ben Saanane

Hivi nyie wana chadema, gazeti la TzDaima ni kipeperushi cha chama?
Sie tusio wanachama habari za Saanane zinatuhusu nini?

Na kama hili gazeti ni habari za chama chenu tu, basi liuzwe pale Ufipa tu, na lisiruhusiwe kuitwa gazeti huru bali memo ya chama kwa wanachama wake.
 
Hivi nyie wana chadema, gazeti la TzDaima ni kipeperushi cha chama?
Sie tusio wanachama habari za Saanane zinatuhusu nini?

Na kama hili gazeti ni habari za chama chenu tu, basi liuzwe pale Ufipa tu, na lisiruhusiwe kuitwa gazeti huru bali memo ya chama kwa wanachama wake.
Kaka angu, ukiona hivyo ujue mambo yamewafika hapaaaaaa!
 
Kinachosikitisha ni kiwa watu wsliolivalia njuga swala la Ban ni watu baki tu washkaji wake wa karibu hawajalichukulia kwa uzito hili swala upepo ukipungua makali tutajua tu mbivu na mbichi SITAKI SHARI
 
Malisa haminiki, juzi alitudanganya kuwa Ben Saanane siyo Mkurugensi wa sera na utafiti wa Chadema. Halafu leo ndo wanakubali Tanzania Daima ni gazeti lao?
 
Malisa haminiki, juzi alitudanganya kuwa Ben Saanane siyo Mkurugensi wa sera na utafiti wa Chadema. Halafu leo ndo wanakubali Tanzania Daima ni gazeti lao?
Nadhani anatafuta cheo cha PA kama Ben asipopatikana
 
baada ya lizaboni kumsakama sana saanane miezi miwili iliyopita,muda mfupi baadae akapotea
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wana CHADEMA wakihoji ukimya wa viongozi wa chama hicho katika kuzungumzia suala la kupotea kwa Ben Saanane. Maoni ya wana CHADEMA wengi ni kwamba pamoja na kuelekeza lawama kwa Jeshi la Polisi kutokana na kuizika miili ya watu saba bila ya kufanyiwa uchunguzi, mzigo mkubwa anashushiwa Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe. Ben kapotea huku Bosi wake Mbowe anaendelea kuponda raha huko Ulaya. Hajashtushwa na wala hataki kushtushwa na kupotea kwa Ben Saanane. Kwa wadhifa wa Ben Saanane, haiingii akilini kuona Bosi wake akiendelea kuponda raha huko Ulaya badala ya kusitisha safari yake kuungana na ndugu na marafiki wa Ben kumtafuta. Jawabu la haraka haraka ni kwamba Mbowe anajua nini kinaendelea juu ya kupotea kwa Ben.

Mapema leo asubuhi, ndugu yangu Malisa Godlisten Joseph amehoji kwa uchungu mkubwa sana and I can feel, kitendo cha Gazeti la Tanzania Daima ambalo kwa mujibu wa Malisa ni kwamba ni gazeti lao kutoipa kipaumbele taarifa ya kupotea kwa Ben kama ilivyoelezwa kwenye Press Conference ya Umoja wa Kuhoji Tanzania. Kwa mujibu wa Malisa, Gazeti la Tanzania Daima limeipuuza Taarifa yao na badala yake wamempamba Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwa Bado yupo yupo CCM. Malisa anasema kuwa hata gazeti la Kada wa CCM, Majira limewapiku Tanzania Daima.

Nikuhakikishie ndugu yangu Malisa kuwa haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya. Yamepangwa na kupangika. Awali nilipofichua uhusika wa Mbowe juu ya kupotea kwa Ben mlinishambulia na kuniona kuwa ni mchonganishi. Sasa yamewakuta. Akili imeanza kuwarejea na sasa mnaungana na Lizaboni kimya kimya.

Wapo pia wanaosema kuwa Freeman Mbowe anastahili kuhojiwa kutokana na upotevu wa Ben. Naungana nao moja kwa moja kwani familia yake iliwajibika ila Mbowe na viongozi wenzake hawakuwajibika na hawapo tayari kuwajibika.

Kurasa zao za facebook hakika zimechafuka. Mashambulizi kwa Mbowe yamepamba kila kona. Wapo wanaosema waziwazi lakini wengine wanahoji kimya kimya. Mwisho wa siku akili itawarejea na wataanza kupaza sauti.

Nimalizie kwa kusema kuwa kabla hujamtafuta mbaya wako nje ya nyumba, jaribu kutafakari kwa kina mahusiano yako na watu wa ndani ya nyumba yako.

View attachment 445613 View attachment 445614 View attachment 445615
.wewe unashindwa kuhoji Lumumba hela za maafa ya bukoba ziliko na kwanini mwenyekiti wenu hakuguswa na swala zima LA maafa unahoji kwa wengine tena eti kwanini gazeti halikuandika?hivi vyombo vya usalama kazi yao nini kama si kulinda na kujua taarifa kama za kupotea binadamu,puuuuuzi kabisa
 
Hivi nyie wana chadema, gazeti la TzDaima ni kipeperushi cha chama?
Sie tusio wanachama habari za Saanane zinatuhusu nini?

Na kama hili gazeti ni habari za chama chenu tu, basi liuzwe pale Ufipa tu, na lisiruhusiwe kuitwa gazeti huru bali memo ya chama kwa wanachama wake.
Wanafichana wenyewe kwa figisu figisu zao halafu wanataka iwe habari ya mjini
 
Narudia tena tuzungumze issues ambazo ni maslahi kwa taifa ili tuweze songa mbele na maisha yetu yawe na tija,, mpaka sasa hatujui tulipo,, tunahoji upotevu wa mtu mmoja!? Shame on u,, tutulize akili jamani oh oh tutaachwa huu muda siyo wa porojo za siasa jamani,,,
 
.wewe unashindwa kuhoji Lumumba hela za maafa ya bukoba ziliko na kwanini mwenyekiti wenu hakuguswa na swala zima LA maafa unahoji kwa wengine tena eti kwanini gazeti halikuandika?hivi vyombo vya usalama kazi yao nini kama si kulinda na kujua taarifa kama za kupotea binadamu,puuuuuzi kabisa
Mkuu una maana wa kuhoji ya BEN ni Chadema pekee? Hapo ndipo tunapokuwa na mashaka na Bosi wa Saanane. Kauli zenu zinazidi kudhihirisha hilo.
 
.wewe unashindwa kuhoji Lumumba hela za maafa ya bukoba ziliko na kwanini mwenyekiti wenu hakuguswa na swala zima LA maafa unahoji kwa wengine tena eti kwanini gazeti halikuandika?hivi vyombo vya usalama kazi yao nini kama si kulinda na kujua taarifa kama za kupotea binadamu,puuuuuzi kabisa
Mkuu, yaelekea kuwa umekuja kwa pupa kuchangia ama hujui nini unachangia. Malalamiko ya kwa nini Tanzania Daima hawajaipa uzito taarifa ya kupotea kwa Ben Saanane sijayatoa mimi. Katoa Malisa GJ nami nimenukuu tu kile alichosema. Bahati nzuri nimeattach kile alichoandika. Akili yako ikikaa sawa utaelewa nini nimeandika
 
Back
Top Bottom