Pre GE2025 Freeman Mbowe: Naagiza ngazi zote za chama ziandae wagombea wa kushinda Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025

Pre GE2025 Freeman Mbowe: Naagiza ngazi zote za chama ziandae wagombea wa kushinda Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama ndivyo walivyokubaliana chamani hakuna tatizo, lakini kwa tahadhari tu, isijekutokea baada ya matokeo ya 2024 na 2025 zikaanza lawama za kuibiwa kura, huo utakuwa usanii.

Binafsi nionavyo ubaya wa hii kauli ya Mbowe, ni kama vile wanacheza ngoma ya CCM either kwa kujua au kutokujua, hasa nikikumbuka Samia alivyowahi kusema kule ndani kwao hakukaliki...

Sasa kama Chadema wameamua kushiriki uchaguzi naona ni kama vile wamemua wenyewe kujipeleka kwenye mdomo wa mamba kwa tamaa za kupata majimbo, siamini hata kidogo kama wanafikiria kwenda ikulu.

CCM wanaweza kuchakachua matokeo makusudi wakijua lawama zitarudi kwa waliochakachuliwa, yes, kama tunazijua tabia zao miaka yote kwanini tukawaamini na kushiriki uchaguzi?

Kama Chadema wangeweka mkazo kwenye Katiba mpya na Tume Huru kwa namna tuliyoona kwenye yale maandamano, naamini wangefanikiwa kupata kimojawapo kama sio vyote.

Bahati mbaya maridhiano yakageuzwa utapeli na CCM wanayoiamini sasa kwa kutaka kushiriki uchaguzi bila tume huru.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Cuf iliposusia Zanzibar ilipata nini, tiririka, Raila Odinga aliposusia Kenya alipata nini? Tiririka....
 
..ukweli ni kwamba somo la tume huru ya uchaguzi na katiba mpya bado halijaeleweka vya kutosha kwa wananchi.
Umetumia kigezo kipi kuja na hii statement? somo halijaeleweka kwa wananchi kwasababu ipi?

Chadema wameitisha maandamano ya kupinga hali ngumu ya maisha huku ndani yake wakiweka madai ya Katiba Mpya na Tume Huru, mbona watu wwlijitokeza kwa wingi kuandamana?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mbowe mjanja anajua kutafuta pesa.Anacholenga si kuwa wagombea lazima washinde anataka kuokota maokoto ya kura kila sehemu sababu chama cha siasa ili kipate ruzuku kigezo ni idadi ya kura kilizopata kwenye uchaguxi.Ndio maana kawa mkali kuwa kila sehemu wasimamishe watu wenye uwezo mkubwa wa ushindani wanaaminika waweza kukipa chama kura nyingi ambazo mwishoni zitaleta ruzuku nyingi kule makao makuu ya chama

Hapo inawindwa ruzuku hasa ndio maana kasema tutasimamisha wagombea kila eneo la uchaguzi hatuachi mahali .maokoto ya kura kwake muhimu sana akipata hapa Mia kule 20 nk si haba mwisho wa siku jumla itasaidia kwenye kikokotoo cha kupata ruzuku hata wasiposhinda nafasi yeyote
Ndio maana agenda ya kusems Chadema haitashiriki uchaguzi wowote hadi iwepo tume huru na katiba mpya ameitupilia mbali.Pesa ya ruzuku ni zaidi ya tume huru na katiba mpya kwake.Akose pesa kisa tume huru na katiba mpya .Sio Mbowe wa kilimanjaro

Chezea pesa wewe
 
Yaani ndio wanajiandaa sasa muda ukiwa umeshaenda hivi...
 
Akihutubia kwenye mkutano wa BAWACHA, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe emetoa agizo kwa Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika kuhakikisha ngazi zote za chama nchi zima zinaandaa viongozi wa kugombea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu mwaka 2025. Viongozi hawa wawe na sifa za kushinda uchaguzi.

"Niwaagize mama zangu, rudini kwenye majimbo yenu kakipangeni chama, kila kitongoji, kila kijiji, kila mtaa. Hakuna kitongoji ambacho kitapita bila kupingwa na CHADEMA katika uchaguzi ujao, hakuna"

Mbowe ameongeza kuwa viongozi wazembe ambao hawataweka watu wa kugombea nafasi za uongozi kwenye chaguzi zijazo watachukuliwa hatua.

Amesema macho yote ya watanzania yapo kwa CHADEMa hivyo ni lazima wasimamishe viongozi kwa kila ngazi.

"Naagiza, na siyo kwa BAWACHA peke yake, katibu mkuu tafadhari na mfumo mzima wa mabaraza yote ya chama, kila kiongozi ahakikishe kila nafasi inayogombewa katika serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, lazima CHADEMA iweke mgombea, na siyo mgombea tu wa kujaza nafasi, mgombea wa ushindani wa kushinda."

Amewataka kwenda kusuka chama kwa nguvu ili waizike CCM kwenye chaguzi zijazo.
Katiba Mpya imeshapatikana? 😁😁😁😁😁😂😂😂😂😂😆😆😆😆😆

Mbowe: Hatushiriki uchaguzi bila Katiba Mpya 🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Niliwaambia suseni muone na Serikali hamuwezi shika
 
Hahahaha nilikuwa namuambia mtu mmoja jana, kuwa wanasiasa wanatupanga mpaka unakosa hamu nazo,
Mnapigania katiba mpya pamoja, mnasema bila katiba hakuna uchaguzi, ghafla kila kitu kinabadilika bila ushirikishaj 😂😂😂
Wewe mjinga ndio unapangwa na ndio maana mnabuluzwa huko kwenye maandamano harafu hakuna Cha maana mnapata.Yaani uliamini kabisa Chadema watasusia Uchaguzi? 😂😂😂😂😂

Kwanza wengi wao umri umeenda,wameanza kukata tamaa na harakati zao maana hawaoni Dalili ya Mabadiliko na pia ccm inajua kucheza na akili zao na za Wananchi.

Hakuna mwanasiasa anaweza nipanga ,ukiona nafanya jambo la siasa ni kama burudani au napata faida ila siwezi kutumika kama ngazi ya mtu.
 
CCM walikuwa wanasubiri CHADEMA ijitoe wachekelee. Pia ACT walikuwa wanasubiria CHADEMA wajitoe ili wawe chama kikuu Cha upinzani. Naona wamepigwa chenga ya mawili.
Mnaoneoana ni kama mademu msuojiamini.

Si mlisema hakuna uchaguzi bila Katiba Mpya,vipi tena 😂😂😂😂

Ni hivi mtapata kile ambacho mtapangiwa na ccm na sio vinginevyo na mkiweza baada ya matokeo suseni tena muone kama Kuna jipya 😁😁
 
..hoja ya Katiba Mpya na Tume Huru haijapatiwa majibu.

..tujiulize kwanini serikali ya Samia na Ccm imegoma kuwapatia Watanzania tume huru na katiba mpya?
Kwani Katiba Mpya ndio inaleta ugali? Yaani Katiba Mpya ya kutoa mwizi X na kumleta mwizi Y Ina faida gani Kwa Mwananchi?

Ni wapi hapa Duniani Katiba Mpya imegawa pesa Kwa watu Hadi waipaparikie?
 
Kwani Katiba Mpya ndio inaleta ugali? Yaani Katiba Mpya ya kutoa mwizi X na kumleta mwizi Y Ina faida gani Kwa Mwananchi?

Ni wapi hapa Duniani Katiba Mpya imegawa pesa Kwa watu Hadi waipaparikie?
Hiyo Katiba Mpya ya kutoa mwizi X na kumleta mwizi Y umeitoa wapi?

Umekariri ubovu wa hii Katiba tuliyonayo sasa unadhani na Katiba Mpya itakuwa na ubovu huu wa sasa.

Kuuliza Katiba Mpya ina manufaa gani kwa mwananchi unaonesha hujiamini, unatembea kichwani na maswali ya kukariri toka kwa wajinga wenzio.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hiyo Katiba Mpya ya kutoa mwizi X na kumleta mwizi Y umeitoa wapi?

Umekariri ubovu wa hii Katiba tuliyonayo sasa unadhani na Katiba Mpya itakuwa na ubovu huu wa sasa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kenya wapi Kuna Katiba Mpya haijawahi leta ugali Wala kudhibiti Ufisadi.

Nkasisitiza Katiba Mpya ni Kwa Ajili ya mwizi X kutaka kumtoa mwizi Y ila Haina maana yeyote Kwa Wananchi.
 
Akihutubia kwenye mkutano wa BAWACHA, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe emetoa agizo kwa Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika kuhakikisha ngazi zote za chama nchi zima zinaandaa viongozi wa kugombea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu mwaka 2025. Viongozi hawa wawe na sifa za kushinda uchaguzi.

"Niwaagize mama zangu, rudini kwenye majimbo yenu kakipangeni chama, kila kitongoji, kila kijiji, kila mtaa. Hakuna kitongoji ambacho kitapita bila kupingwa na CHADEMA katika uchaguzi ujao, hakuna"

Mbowe ameongeza kuwa viongozi wazembe ambao hawataweka watu wa kugombea nafasi za uongozi kwenye chaguzi zijazo watachukuliwa hatua.

Amesema macho yote ya watanzania yapo kwa CHADEMa hivyo ni lazima wasimamishe viongozi kwa kila ngazi.

"Naagiza, na siyo kwa BAWACHA peke yake, katibu mkuu tafadhari na mfumo mzima wa mabaraza yote ya chama, kila kiongozi ahakikishe kila nafasi inayogombewa katika serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, lazima CHADEMA iweke mgombea, na siyo mgombea tu wa kujaza nafasi, mgombea wa ushindani wa kushinda."

Amewataka kwenda kusuka chama kwa nguvu ili waizike CCM kwenye chaguzi zijazo.
Walidhani Tutawasusia Nyani Shamba la Mahindi😂😂😂
 
Kenya wapi Kuna Katiba Mpya haijawahi leta ugali Wala kudhibiti Ufisadi.

Nkasisitiza Katiba Mpya ni Kwa Ajili ya mwizi X kutaka kumtoa mwizi Y ila Haina maana yeyote Kwa Wananchi.
Unaweweseka.......We ndio una wasi wasi Katiba Mpya itakuondolea Ugali
 
..Tume Huru ya uchaguzi ni kwa faida ya kila Mtanzania bila kujali vyama vyao.

..hebu fikiria tuwe na ligi kuu ya mpira wa miguu halafu timu moja kubwa, kwa mfano Simba, wawe wanapanga waamuzi, usajili wa wachezaji, na matokeo. ligi ya aina hiyo haitakuwa na mvuto hata kidogo.

..Waliokwamisha Katiba Mpya sio Chadema wala kundi la Ukawa. Mchakato wa Katiba Mpya uliendelea hata baada ya Chadema na Ukawa kususia. Katiba Mpya pendekezwa iliandikwa na wana-Ccm waliobaki ktk bunge maalum. Baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, serikali ya Ccm haikuendelea na hatua iliyofuatia ambayo ilikuwa ni kuitisha kura ya maoni.

..Wanaolaumu kwamba Chadema walizuia upatikanaji wa Katiba Mpya wanajilazimisha upumbavu kwa kufumbia macho ukweli kwamba Mchakato ulikamilika kwa kuandikwa kwa Katiba Pendekezwa.
Katiba iliyopendekezwa mliigeuzia jina mkaiita Katiba inayodekezwa !!! Mkawa mnataka ile rasimu ya maoni ya warioba ndio iwe katiba kamili hivi mlikuwa serious??? Kuleni chuma hicho hakuna cha katiba mpya 😃😃
 
Back
Top Bottom