Pre GE2025 Freeman Mbowe nyamaza au Ingia CCM 100% maana wewe ni mtoa taarifa

Pre GE2025 Freeman Mbowe nyamaza au Ingia CCM 100% maana wewe ni mtoa taarifa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
hakuna mtu pro samia na corrupt kama tundu lisu, kama mnafikiri tundu lisu ni mpinzani wa samia poleni sana, wote wana bosi mmoja na wametoka mbali.

mpinzani wa ukweli wa samia yuko ccm na western world hivyo 2025 si chadema wala mbowe au sijui tundu lisu kuna raisi mwingine na mpya imeshapangwa na wakuu wa Dunia kilichobakia ni utekelezaji tu na 2025 wote wanakabidhi power …
 
Aliyechangia hizo milioni 150 ni Samia kiongozi wa serikali na nchi au Samia kama raia binafsi?

Na hizo hela zimetoka wapi? Hazina au akaunti binafsi ya Samia?
Amechangia Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Rais anatoa hela mfuko wa serikali.
 
Duh!!

That makes it even worse!!
Tanzania tuna bonge la contradiction.

We are a secular country.

But religiosity is seen as a shortcut to morality and all things good.

Most people, from the populace to the power brokers, are lazy thinkers prone to shortcuts.

The shortest shortcut to popularity is through religiosity. Forget public policy and party manifesto.

Samia and Mbowe are both choosing this route of political expediency at the cost of secularity and Separation of Religion and State.

Most people cannot follow the logic to see this and its implication on good governance.
 
Mbowe ni msanii wa siasa za Chedema jamaa anapiga mpunga tu, ndio maana ni ngumu sana kuachia hichi kiti cha Uenyekiti.
Mkuu,

Ikiwa kweli Mbowe ni msanii, au si msanii hayo ni maneno ya watu tu, ukweli usio na ubishi mkubwa ni kwamba amejiweka katika mazingira ya kupewa hizo tuhuma, na tuhuma hizo zikakubalika kirahisi.

Yani kaona hapa kuna hela ya kupatikana kirahisi kutoka kwa Samia. Lakini, hela hiyo inaweza kuja na gharama kubwa sana ya shutuma za kuwa kalambishwa asali waziwazi.

Na bado akachagua kuchukua hizo hela.

Akituhumiwa kuwa kalambishwa asali, hata kama si kweli, amejitengenezea mazingira ya kupewa hizo tuhuma yeye mwenyewe.

Justice must not only be done, it must also appear to be done.

Viongozi hawatakiwi kupiga vita tu rushwa, wanatakiwa kukwepa hata muonekano wa kushiriki rushwa.

Appearances do matter.

Caesar's wife should be above suspicion.

Mbowe ameshindwa mtihani huu.
 
Kosa la Mbowe ni lipi? kuwa Mwenyekiti wa Harambee na kusoma waliotoa pesa za mchango. Maana alisoma majina karibia thelathini na la mwisho likawa la Rais Samiah. Kosa lake lipi?. Halafu Mbowe kaanza kuwa Mbunge tanguh mwaka 2000. Huko kote kaonewa huruma?. Punguza unafiki
Mbowe pasipo uruma za CCM hawezi toboa kupata hicho kiti cha ubunge,hata hivyo ubunge aliokuwa ameupata alisaidiawa na Silaa kupata uo ubunge, Sasahivi Mbowe hana mvuto tena baada ya kubadiri gia ya angani,ndio maana kila siku anajikomba kwa Samia hamwone uruma,siku hizi hauwezi sikia Mbowe anaukosoa utawala wa Samia pamoja na mambo kwenda mrama.
 
We kijambio cha msoga watz gani hao walio kuwa kitu kimoja kabla ya jpm wewe kweli ni bwege ....baba yako kauza ng'ombe wake kukusomesha kumbe kauza ng'ombe kusomesha ng'ombe.
Anamaanisha watoto wa vigogo walamba unga na wenye vyeti fyeki ndo walikuwa wammoja na walikuwa untouchable
 
Yaani mbowe aliharibu sana kutangaza mchanfo wa sa 100 Rais ujue mbowe amekinadi chama cha ccm bila yeye kujua. Pale alibidi mtu wa kutangaza mchango wa RaisSamia ni mchungaji au mwenyekiti wa ujenzi kwa sababu kila muuumini tulipewa fomu za kuchangisha michango kwa marafiki na ndugu na jamaa zetu
 
Duh!!

That makes it even worse!!
Inawezekana kabisa Samia kwa akili yake anaona anajenga umoja wa kitaifa.

Kwamba, yeye rais Muislamu, anachangia ujenzi wa kanisa la Wakristo, hana ubaguzi wa kidini.

Yeye Mwenyekiti wa CCM, anachangia sio tu kanisa la Wakristo, bali pia, kwa wito maalum wa Mwenyekiti wa CHADEMA, hivyo, sio tu anaonesha kutobagua dini, bali pia, habagui pa kuchangia kwa kuangalia chama.

Na kwa kufanya hivyo, watu waliopata maumivu mengi watampenda na kuona hiyu rais anawajali kweli watu, hata wale walio tofauti naye!

Anaimba "Sibagui, sichagui, atayenizika simjui".
 
Inawezekana kabisa Samia kwa akili yake anaona anajenga umoja wa kitaifa.

Kwamba, yeye rais Muislamu, anachangia ujenzi wa kanisa la Wakristo, hana ubaguzi wa kidini.

Yeye Mwenyekiti wa CCM, anachangia sio tu kanisa la Wakristo, bali pia, kwa wito maalum wa Mwenyekiti wa CHADEMA, hivyo, sio tu anaonesha kutobagua dini, bali pia, habagui pa kuchangia kwa kuangalia chama.

Na kwa kufanya hivyo, watu waliopata maumivu mengi watampenda na kuona hiyu rais anawajali kweli watu, hata wale walio tofauti naye!
Ila Samia atatumiaje hela za serikali/ wananchi kutoa msaada kwenye kanisa [la Mbowe]?

Mbowe naye atakubalije kupokea msaada wa kifedha toka kwa Rais wa nchi kwenda kwenye kanisa [lake]?

This is very bothersome on many levels!

Samia hajui tofauti kati ya serikali na dini?

Mbowe naye hajui tofauti kati ya dini na serikali?

Wote hawa wawili hawajui kuwa Tanzania/ serikali ya Tanzania haina dini?

Mbowe ni mwenyekiti wa chama chenye lengo la kuja kuongoza nchi na hajui kuwa serikali ya nchi haina dini?

Au wote wawili wanajua ila hawajali chochote?
 
Ila Samia atatumiaje hela za serikali/ wananchi kutoa msaada kwenye kanisa [la Mbowe]?

Mbowe naye atakubalije kupokea msaada wa kifedha toka kwa Rais wa nchi kwenda kwenye kanisa [lake]?

This is very bothersome on many levels!

Samia hajui tofauti kati ya serikali na dini?

Mbowe naye hajui tofauti kati ya dini na serikali?

Wote hawa wawili hawajui kuwa Tanzania/ serikali ya Tanzania haina dini?

Mbowe ni mwenyekiti wa chama chenye lengo la kuja kuongoza nchi na hajui kuwa serikali ya nchi haina dini?

Au wote wawili wanajua ila hawajali chochote?
Nakuelewa sana unavyosema hayo yote, na mimi ndiyo maswali yangu hayo.

Ila, nakupa possible take from Samia's rationale. Kibongobongo.

What is Sh 150 million kwenye jambo kubwa kama kujenga umoja wa kitaifa? Kwenye kuponya vidonda vya awamu ya tano, that is a bargain price.

Tena kwa kupitia kitu kizuri kitakachojenga watu kiroho kama kanisa?

I mean it's not like Samia amechangia nyumba ya kuishi Mbowe, hili ni kanisa ambalo watasali Watanzania.

After all, Mbowe alivunjiwa heshima na alifungwa muda mrefu for trumped up charges. Hapa serikali ni kama tunamlipa tu towards giving to a charity of his choice, KKKT. Mbowe hawezi kuishitaki serikali kudai fidia, tunamlipa fidia kwa njia nyingine tu.

Na hapohapo wananchi wanaona Samia mtu poa, anatoa sadaka mpaka kanisani kwa Mbowe.

Waislamu wanafundishwa kuishi vizuri na Wakristo.

CCM wanafundishwa kuishi vizuri na CHADEMA, wakileta ugomvi wanaambiwa nyie mnagombana nini mbona wenyeviti wenu damudamu mpaka Samia kachangia kujenga kanisa la kwa Mbowe.

Mbowe anaonekana big shot kafanikisha ujenzi wa kanisa kwa kumchangisha mpaka rais.

Samia anaonekana mtu wa maana sana, hana nongwa na mtu.

Everybody wins.

Na wewe kama una kanisa lako unajenga, mtafute Samia akuchangie kwa urefu wa kamba yako kama alivyosema mwenyewe.

Hapo vipi kibongobongo?
 
Nakuelewa sana unavyosema hayo yote, na mimi ndiyo maswali yangu hayo.

Ila, nakupa possible take from Samia's rationale. Kibongobongo.

What is Sh 150 million kwenye jambo kubwa kama kujenga umoja wa kitaifa? Kwenye kuponya vidonda vya awamu ya tano, that is a bargain price.

Tena kwa kupitia kitu kizuri kitakachojenga watu kiroho kama kanisa?

I mean it's not like Samia amechangia nyumba ya kuishi Mbowe, hili ni kanisa ambalo watasali Watanzania.

After all, Mbowe alivunjiwa heshima na alifungwa muda mrefu for trumped up charges. Hapa serikali ni kama tunamlipa tu towards giving to a charity of his choice, KKKT. Mbowe hawezi kuishitaki serikali kudai fidia, tunamlipa fidia kwa njia nyingine tu.

Na hapohapo wananchi wanaona Samia mtu poa, anatoa sadaka mpaka kanisani kwa Mbowe.

Waislamu wanafundishwa kuishi vizuri na Wakristo.

CCM wanafundishwa kuishi vizuri na CHADEMA, wakileta ugomvi wanaambiwa nyie mnagombana nini mbona wenyeviti wenu damudamu mpaka Samia kachangia kujenga kanisa la kwa Mbowe.

Mbowe anaonekana big shot kafanikisha ujenzi wa kanisa kwa kumchangisha mpaka rais.

Samia anaonekana mtu wa maana sana, hana nongwa na mtu.

Everybody wins.

Na wewe kama una kanisa lako unajenga, mtafute Samia akuchangie kwa urefu wa kamba yako kama alivyosema mwenyewe.

Hapo vipi kibongobongo?
Imebidi nicheke tu aisee!

Of course, kibongobongo that makes a ton of ‘sense’.

Ila kiuongozi tuko doomed.

Na mbaya zaidi, kwa sasa hatuna elder statesman anayeheshimika ndani na nje ya nchi [kama ilivyokuwa baada ya Nyerere kustaafu na kabla hajafariki] ambaye anaweza kuwasema Samia na Mbowe kama ambavyo Nyerere alivyowasema Malecela na Mwinyi enzi zile.
 
Imebidi nicheke tu aisee!

Of course, kibongobongo that makes a ton of ‘sense’.

Ila kiuongozi tuko doomed.

Na mbaya zaidi, kwa sasa hatuna elder statesman anayeheshimika ndani na nje ya nchi [kama ilivyokuwa baada ya Nyerere kustaafu na kabla hajafariki] ambaye anaweza kuwasema Samia na Mbowe kama ambavyo Nyerere alivyowasema Malecela na Mwinyi enzi zile.
Elder statesman Kikwete, ndiye anapanga mashambulizi yote.

Mwinyi kashapozwa na Mercedes Benz anajionea raha tu. Ndiyo kwanza anasema kutoa kanisani thawabu.
 
Kwa hivyo Mbowe ndio jeshi la polisi?. Yani jeshi la polisi lipo kimya wewe unahangaika na Mbowe. Baadala upige kelele kwa jeshi la polisi wewe unahangaika na raia .
Umeelewa nachoongelea au kwa sababu umeons jinaa la Mbowe limetajwa ukakurupuka.
 
Kabla hata ya Samia, Mbowe anajitengenezea matatizo mengi kuchanganya siasa na dini.

Tayari kuna maneno mengi ya kidini katika siasa, majungu na maneno ya msingi, habari za Mfumokristo kuongoza nchi zinasemwa sana. Habari za kampeni za kisiasa kufanyika makanisani zinasemwa sana. Habari za CHADEMA kuwa ni chama cha Wakristo zinasemwa sana.Mbowe kujiweka kimbelembele kanisani tu ni tatizo. Kunachochea habari hizi.

Caesar's wife should be above suspicion. Mbowe anajipeleka kwenye religious political controversies na suspicion bila sababu.

Mbowe kama kiongozi wa kisiasa aliyejiweka kimbelembele kanisani, ni mnufaika wa huu mchango. Watu wanamuona big shot kamleta rais kuchangia kanisa, anatumia umaarufu huo kisiasa. Unafikiri akijinadi kafanikisha ujenzi wa kanisa mpaka kamleta rais, watu wamkubali kisiasa, watu hawatakuwa influenced?

Hivi huoni wanasiasa wanavyotumia dini kujikosha na kufanya kampeni za umaarufu hapa? Wote wawili Mbowe na Samia?

Hivi huoni Samia anavyojitengenezea mazingira ya kuwa na influence KKKT, kesho wakiwa na migogoro waende kwake awachagulie maaskofu chawa watakaotuambia "Samia chaguo la Mungu" kwa sababu za kupewa asali ya kutoka Ikuku?

Mbowe kamualika Samia. Samia hajajipeleka tu kwa kina Mbowe. Kuna makanisa mangapi yanahitaji ujenzi Tanzania? Kwa nini Samia kaenda kujenga kanisa la kwa Mbowe?

Kama hujui kusoma, hata picha huoni hapo?

Kanuni za rule of law and good governance zinataka nchi secular iendeshwe in a secular way, kusiwe na hata muonekano wa watu fulani au dini fulani kupendelewa. Sasa hivi serikali imejiingiza kujenga makanisa. Hii si kazi ya serikali. Kila mtu anayetaka kanisa lake lijengwe kwa mchango wa Ikulu wa Sh 150 milioni akijipanga apate mgao huo, rais hataweza kututimizia wote.

Hapa kuna muonekano wa Mbowe kupendelewa, kwa nini? Mbowe kahongwa ili awe mpole kwenye siasa.

Nyerere amekuwa rais kwa miaka 24. Alikuwa Mkatoliki kindakindaki.Tulikuwa tunamuona St. Peters Oysterbay kila siku asubuhi.Hakuwahi kuchangia ujenzi wa kanisa wala msikiti kwa namna hii. Kwa nini?

Alijua kanuni za Separation of Religion and State. Alijua hiki jambo ni scandal.

Mbowe hajui? Samia hajui?

Kama hawajui, hawafai kuwa viongozi, kwa sababu hawajui misingi muhimu ya uongozi katika a secular state.

Ama wanajua wanadharau tu?

Kama wanajua, ila wanadharau tu, hawafai kuwa viongozi katika a secular state. Kwa sababu wanadharau misingi ya Separation of Religion and State.
Mkuu you should have cried so loud and wide when Magufuli started going in bed with several churches on the same issue! As of now it's too late for you to come out and hypocritically point fingers and blames where it is not necessary!

Mbowe sio Askofu Mkuu wa KKKT na sio Rais, yeye ni muumini aliyeshirikisha marafiki zake wa karibu na wa mbali wakiwemo Samia kufanikisha changisho Kanisani kwake! Habari ya siasa na dini ipo wapi hapo! Acha hizo propaganda mbovu!

Mkuu mbona huku sema chochote wakati Samia alipomzawadia Mwinyi Mercedes Benz mpyaaa yenye thamani ya zaidi ya milioni mia tatu! Acha unafiki na roho mbaya!

Nakuambia chuki haimwachi salama mwenye nayo! Tua gunia la miiba ulilobeba!
 
Wengi walio ktk umri wa Mbowe walikuwa wana CCM. Kuwa na kadi ya CCM haina maana ya kuwa mwanachama wa CCM. Kadi ya CCM kwa sasa ni kumbukumbu tu ya historia ya kisiasa.
👍👏👏
 
Mkuu you should have cried so loud and wide when Magufuli started going in bed with several church on the same issue! As of now it's too late for you out and hypocritically point fingers and blames where it is not necessary!

Mbowe sio Askofu Mkuu wa KKKT na sio Rais, yeye ni muumini aliyeshirikisha marafiki zake wa karibu na wa mbali wakiwemo Samia kufanikisha changisho Kanisani kwake! Habari ya siasa na dini ipo wapi hapo! Acha hizo propaganda mbovu!

Mkuu mbona huku sema chochote wakati Samia alipomzawadia Mwinyi Mercedes Benz mpyaaa yenye thamani ya zaidi ya milioni mia tatu! Acha unafiki na roho mbaya!

Nakuambia chuki haimwachi salama mwenye nayo! Tua gunia la miiba ulilobeba!
Mkuu,

Mimi nimekuwa nikikemea hii tabia tangu enzi za Magufuli. Nimekemea sana Magufuli kuchanganya siasa na dini. Nimekemea Magufuli alivyosimama kanisani St. Peters na kuanza kuhubiri akimsema Jaji Thomas Mihayo kuvaa barakoa kanisani. Unajihakikishiaje sikukemea? Umesoma posts zangu zote?

Au wewe ni kati ya wale watu wazembe wanaokwenda kwa assumptions tu?

Unasema sikusema lolote Samia alipomzawadia Mwinyi Mercedes Benz, unajuaje hilo? Unahakikishaje mimi sikusema lolote?

Au unajikubalisha tu hivyo kivivuvivu tu?

Ukitaka tufukue nyuzi tutafukua hapa.

What are you talking about?

Unaniita mnafiki kama umechunguza posts zangu zote hapa JF?

Mbowe ni kiongozi wa chama cha upinzani. Kwa nini anamkaribisha rais kuchangia kujenga kanisa kama vile hajui kanuni za Separation of Religion and State?

Au una kasumba ya kufikiri kila mtu anayemsema Mbowe ni mshabiki wa CCM?

Wengine tuko consistent hapa, tunasimamia principle bila kujali mtu.

Nimemsema Magufuli, nimemsema Samia, nimemsema Mbowe kwenye hili.

Consistently.

Wanaonifuatilia watajua hilo.

Ni wewe tu unarukia mada na kutoa shutuma jumlajumla bila hata kuuliza au uhakiki.
 
Kitu cha kwanza kabisa, rais hatakiwi kuchangia shughuli za dini. Hili linaharibu Separation of Church and State.

Kitu cha pili, kila mtu mwenye kanisa lake akitaka rais achangie shilingi milioni 150 rais hataweza. Rais anajiwekea mazingira ya kuonekana anapendelea sehemu fulani kisiasa.

Kitu cha tatu, denokrasia si tu inatakiwa ifanyike, bali pia inatakuwa kuonekana kuwa imefanyika. Hapa kuna muonekano wa kumuhonga Mbowe. Kqma mchango ninwa KKKT kwa nini Samia hakuchangia Uyole kaenda kuchangia kanisa la kwa Mbowe?

Kitu cha nne, Samia hajachaguliwa kujenga makanisa. Hili halimo katika ilani ya CCM. Katika nchi ambayo haifuati dini, haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi. Waacheni waumini wachangishane wenyewe makanisani.

Kitu cha tano, Mbowe anajiwekea mazingira ya kutoweza kumkemea Samia inavyotakiwa. Utamkemea vipi Boss Lady anayekufadhili mpaka kwenye kujenga kanisa?

Kwa sasa niishie hapa tu.
Mkuu haya yote ulioainisha hapa ni haramu kwa sheria ipi? Mbowe alisema mchango umetoka kwa Samia na familia yake, sio serikalini.

Mkuu naona hapo ndipo unapo changanya mada! Na umechanganyikiwa kweli kweli!

Mkuu mbali na Samia, waziri mkuu Majaliwa na Naibu waziri mkuu Biteko walichangia harambee ya ujenzi huo wa Kanisa la KKKT; Je, nao wamechanganya siasa na dini?

Kuna wafanyabiashara na watu mashuhuri mbali mbali walichangia ujenzi huo wa Kanisa; Je, nao wamechanganya biashara na dini?

Mkuu kama wanasiasa kuchangia ujenzi wa Kanisa au msikiti ni kuchanganya siasa na dini, na kwa mtazamo wako ni haramu;

Je, wafanyabiashara wakichangia jambo la namna hiyo nao wanachanganya biashara na dini?

Je mchango wao nao ni haramu?

Je, wafanyakazi na watumishi nao wasichangie jambo la namna hiyo maana watakuwa wanachanganya kazi na dini?

Je, nao mchango wao ni haramu?

Tuna subiri majibu yako Mkuu!
 
Back
Top Bottom