Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakuna kitu hapoo, yaan wachezaji wengi wa Simba hawastahili kuwepo hata kwenye benchi.Bora kapama ni mzuri kwenye holding,sawadogo hana match fitness kabisa yaani.
SIMBA itabaki kuwa kileleniMajira ya Saa 10:00 Alasiri kwa masaa ya Afrika Mashariki, Ihefu Fc itawakaribisha Simba Sc katika dimba lao la Highland Estates katika muendelezo wa Ligi Kuu ya NBC.
Habari kubwa leo, nani wa kumzuia Jean Baleke ambaye amekuwa hazuiliki sasa, kwa taarifa yako Baleke kwasasa anafunga kila mechi, alifunga mecho iliyopita hat trick na atafunga leo na mechi ijayo atafunga kama ilivyoada.
Ihefu iliyopo nafasi ya 8 itajaribu kulipa kisasi baada ya kufanyiwa mauaji ya Sharubela juzi dhidi ya Mnyama mkubwa mwituni, Simba SC, Ihefu aliloa mabao 4-1.
Simba iliyopo nafasi ya pili, itajaribu kupunguza alama dhidi ya Yanga wanaoongoza ligi kwa tofauti ya alama 8 huku ikisalia michezo sita kabla ya ligi kutamatika.
Ewe mwanasimba uliyepo Dodoma, Nakuru, Bukoba, Mwanakwerekwe, Jinja, Eldoret, Kivu na maeneo mengine usipitwe na mchezo huu mtamu.
Mchezo utakuwa mubashara Azam Sports 1HD na tutakuletea updates hapa JamiiForums kupitia uzi huu...
View attachment 2583336
Mchezo umeanza
2' Wenyeji wanamiliki mpira muda mwingi
8' Bado Ihefu wanaonekana kuwa na nguvu zaidi kuliko Simba
16' Simba wanafanya shambulizi kali, Baleke anapaisha mpira juu licha ya kufanya kazi nzuri ya kuwatoka walinzi
19' Shuti la Sakho linatoka nje kidogo ya lango
21' Mabadiliko kwa Simba, Sawadogo anatoka, anaingia Kapama,
Kwa mchezo huu wa Simba itoshe kusema Wydad watajipigia kama vile wanapiga mlevi
Kwa mechi hizi za kujitoa sadaka, wenzio huwa tunaweka mzigo baada ya kujua kikosi. Binafsi nilitegemea kuona kikosi cha namna hii kwa kuzingatia mechi mbili zijazoSimba jitahidini hata droo asee nimewapa 2x
Sasa kwani kwa upeo wako unadhani kitacheza kikosi hiki?Kwa mchezo huu wa Simba itoshe kusema Wydad watajipigia kama vile wanapiga mlevi
Hao wamewekwa kama reserve kwa ajili ya mechi kubwa ya CAF japo Okra nadhani anaweza akawa na sababu nyingine pengine ni match fitnessWapi
Banda
Okra
Ntibayonkiza
Phili
Kikosi kipi kinachoweza kuogopwa na Wydad?Sasa kwani kwa upeo wako unadhani kitacheza kikosi hiki?
Na lengo sio kuogopeshanaKikosi kipi kinachoweza kuogopwa na Wydad?