FT: Kagera Sugar FC 2-5 Simba SC | NBC Premier League | Kaitaba Stadium | 21 Dec 2024

Ninaombea Simba wanyukwe; ila hawatabiriki. Penalty zisizokuwa na maelezo, mabao ya offside na mabao ya dakika nje ya mchezo ni kati ya silaha walizo nazo Simba. Kwa hiyo nadhani Kagera wamekalia kuti kavu.
Dakika nje ya mchezo ni zipi hizo shabik.maana mpira unaisha kwa filimbi ya mwisho ya mwamuzi.je ni timu gani iliendelea kucheza baada ya refa kumliza mpira na ikafungwa?
 
Wako wapi waliokuwa wanasema ngoma hamna kitu.

Kila nikisema kwa viungo wa simba ngoma ana nafasi kuna watu walikuwa wanatamani kushika mpaka bunduki.. Huyu ndio ngoma, mido ya boli, ana akili ya mpira.
Niliuliza juzi kuna mchezaji anayemzidi Ngoma kwa usahihi wa pasi.

Watu wakanitajia jina la mchezaji wa ajabu ajabu kutoka timu ya wapi hata sijui eti Pacome ndio anayemzidi Ngoma.

Ngoma bado tunamuhitaji sana pale msimbazi, licha ya ups and down zake ila jamaa ana class ya kiwango cha juu sana.
 
Cross ya beki wa kushoto inamaliziwa na beki wa kulia
 
Reactions: BRN
Kwa pasi za mita 15 hivi ni ana hatari.

Anapiga pasi kuliko DOBI.
 
Ninaombea Simba wanyukwe; ila hawatabiriki. Penalty zisizokuwa na maelezo, mabao ya offside na mabao ya dakika nje ya mchezo ni kati ya silaha walizo nazo Simba. Kwa hiyo nadhani Kagera wamekalia kuti kavu.
 
Kufungwa wanafungwa Kagera Sugar lakini utakuta majitu wa Uttopollo wamerundikana humu wametunisha vichwa na makalio wanatusumbua. Kudinywa anadinywa Kagera, Utto Jazz wanakata mauno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…