Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kama si Mbiringe bila shaka ni Patashika ya Ligi Kuu Tanzani Bara [emoji1241] kuendelea kupigwa leo Novemba 16, 2022. Mnyama Mkali Mwituni Simba SC [emoji881] kukiwasha na Wababe wa Kusini Namungo FC, katika Uwanja wa Stade de Benjamin Mkapa Dar es salaam [emoji2522]
Mchezo unatarajiwa kuwa ngumu kwa pande zote mbili kulingana na maandalizi na ubora wa vikosi vyao huku makocha wote wakisema kuwa wapo tayari kwa mchezo huo. Kocha Mkuu wa Simba SC, Juma Mgunda amesema kuwa maandalizi ya mchezo yapo vizuri.
"Kwa ujumla ni kwamba maandalizi ya mchezo wa leo yanakwenda vizuri, kwa maana kuwa tupo tayari kucheza mchezo wetu na mpinzani wetu kutoka Lindi". alisema Kocha Mgunda.
Naye Kocha Msaidizi wa Namungo FC Shadrack Nsajigwa kuelekea kwenye mchezo huo amesema kuwa wamejiandaa kushindana na Simba SC.
"Kimsingi tumekuja kushindana na Simba SC, tumepata muda wa kujiandaa kiasi cha siku 8 kwahivyo timu yetu ipo tayari kwa ajili ya kushindana na Simba SC". amesema Kocha Shadrack.
Tutegemee kuona ushindani wa kweli ndani ya dakika 90 za jasho na damu kutoka pande zote mbili katika kugombea alama tatu muhimu za Ligi Kuu Tanzania Bara..[emoji288]Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1;00[emoji354] Usiku.. Usikose Ukaadithiwa Yaani.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana.[emoji2424][/B]
=====================
Wachezaji wa Timu zote mbili wapo uwanjani wakipasha misuli moto tayari kwa mchezo..!
00' Naaam mpira umeanza | Simba SC 0-0 Namungo FC
02' Simba wanapata Kona ambayo haikuzaa bao.. Inaokolewa na Namungo FC
09' Simba wanafanya mashambulizi mawili ya kasi, moja Kibu akishindwa kufunga bao la kichwa huku mpira wa Kichwa wa Henock ukigonga Mlingoti
15' Dakika hizi za mwanzo Simba SC wameweza kumiliki mchezo kwa mashambulizi kadhaa
Namungo wanafanya shambulizi lakini Onyango anatokea na kucheza mpira na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.
23' Kanoute anapiga shutii lakini linapaa nje ya lango la Namungo FC.
25' Pasi nzuri ya Kichuya, Namungo FC wanashindwa kufunga bao..!
31' [emoji460] Phiri Goooooooooooooaaal gooal
Moses Phiri anahesabu bao la kwanza akipokea V' pasi murua kutoka kwa Hussein
35' Asante anapiga shutii la chini chini lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick.
40' Kikoti kwake Masawe mbele kuleee lakini wanapoteza mpira ule.
Kichuya anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Hussein
Sakho anapiga shutii la chini chini lakini golikipa Munishi anaruka na anadaka.
43' Namungo FC wanapata Free Kick, unapigwa mpira mrefu na kutoka nje ya lango.
45+1' Kuelekea kuwa mapumziko Uwanja wa Benjamin Mkapa
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba SC wapo mbele ya bao moja kwa bila dhidi ya Namungo FC
HT: Simba SC 1-0 Namungo FC
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Mkapa.. Hakuna mabadiliko kwa wachezaji wa Timu zote mbili
49' Magingi anapiga kichwa lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick
52' Sakho yupo chini akipatiwa matibabu baada kuchezewa vibaya, ameinuka mpira unaendelea
Simba wanashindwa kuifungua ngome ya Namungo, Phiri na Mzamiru walikuwa na nafasi nzuri ya kufunga.
59' Masawe anashindwa kuunganisha mpira wa Krosi kutoka kwa Kichuya
Hashim Manyanya anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Hussein
62' Kichuya na Kikoti wametoka na wameingia Mohamed Issa na Lusajo
Phiri yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kupata rabsha.. Mpira upo mbele kuleee kwake Lusajo
68' Mohamed Issa anaonyeshwa Kadi ya Njano baada ya kumchezea madhambi Kanoute
Kassim ameingia kuchukua nafasi ya Masawe, upande wa Namungo FC
75' Namungo FC wamemka kwa sasa kutafuta bao la kusawazisha, wanamiliki mpira.
78' Ametoka Okrah na ameingia Akpan huku Simba wakifanya majaribio kadhaa
Ni Free Kick kuelekea Simba eneo karibu na box la 18, Akpan anafanya faulo.. Inapigwa mpira unababatiza mabeki wa Simba
Asante anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Kibu
85' Simba wanaweka bao lakini Refa anakataa anasema ni Offside kwa Henock
88' Lusajo anapiga shutii lakini golikipa Manula anacheza vizuri, ilikuwa hatari langoni kwa Simba SC
90+2' Kuelekea kumalizika kwa mchezo
Almanusura Lusajo afunge bao, ilikuwa hatari sana lango la Simba Manula anacheza vizuri.. Lakini yupo chini akipatiwa matibabu
Kona kuelekea Simba, inapigwa kulee lakini Kanoute anaokoa, mpira wa kurusha sasa.
Naaam mpira umekwishaaaaaa
FT: Simba SC 1-0 Namungo FC
....... Ghazwat...
Mchezo unatarajiwa kuwa ngumu kwa pande zote mbili kulingana na maandalizi na ubora wa vikosi vyao huku makocha wote wakisema kuwa wapo tayari kwa mchezo huo. Kocha Mkuu wa Simba SC, Juma Mgunda amesema kuwa maandalizi ya mchezo yapo vizuri.
"Kwa ujumla ni kwamba maandalizi ya mchezo wa leo yanakwenda vizuri, kwa maana kuwa tupo tayari kucheza mchezo wetu na mpinzani wetu kutoka Lindi". alisema Kocha Mgunda.
Naye Kocha Msaidizi wa Namungo FC Shadrack Nsajigwa kuelekea kwenye mchezo huo amesema kuwa wamejiandaa kushindana na Simba SC.
"Kimsingi tumekuja kushindana na Simba SC, tumepata muda wa kujiandaa kiasi cha siku 8 kwahivyo timu yetu ipo tayari kwa ajili ya kushindana na Simba SC". amesema Kocha Shadrack.
Tutegemee kuona ushindani wa kweli ndani ya dakika 90 za jasho na damu kutoka pande zote mbili katika kugombea alama tatu muhimu za Ligi Kuu Tanzania Bara..[emoji288]Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1;00[emoji354] Usiku.. Usikose Ukaadithiwa Yaani.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana.[emoji2424][/B]
=====================
Wachezaji wa Timu zote mbili wapo uwanjani wakipasha misuli moto tayari kwa mchezo..!
00' Naaam mpira umeanza | Simba SC 0-0 Namungo FC
02' Simba wanapata Kona ambayo haikuzaa bao.. Inaokolewa na Namungo FC
09' Simba wanafanya mashambulizi mawili ya kasi, moja Kibu akishindwa kufunga bao la kichwa huku mpira wa Kichwa wa Henock ukigonga Mlingoti
15' Dakika hizi za mwanzo Simba SC wameweza kumiliki mchezo kwa mashambulizi kadhaa
Namungo wanafanya shambulizi lakini Onyango anatokea na kucheza mpira na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.
23' Kanoute anapiga shutii lakini linapaa nje ya lango la Namungo FC.
25' Pasi nzuri ya Kichuya, Namungo FC wanashindwa kufunga bao..!
31' [emoji460] Phiri Goooooooooooooaaal gooal
Moses Phiri anahesabu bao la kwanza akipokea V' pasi murua kutoka kwa Hussein
35' Asante anapiga shutii la chini chini lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick.
40' Kikoti kwake Masawe mbele kuleee lakini wanapoteza mpira ule.
Kichuya anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Hussein
Sakho anapiga shutii la chini chini lakini golikipa Munishi anaruka na anadaka.
43' Namungo FC wanapata Free Kick, unapigwa mpira mrefu na kutoka nje ya lango.
45+1' Kuelekea kuwa mapumziko Uwanja wa Benjamin Mkapa
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba SC wapo mbele ya bao moja kwa bila dhidi ya Namungo FC
HT: Simba SC 1-0 Namungo FC
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Mkapa.. Hakuna mabadiliko kwa wachezaji wa Timu zote mbili
49' Magingi anapiga kichwa lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick
52' Sakho yupo chini akipatiwa matibabu baada kuchezewa vibaya, ameinuka mpira unaendelea
Simba wanashindwa kuifungua ngome ya Namungo, Phiri na Mzamiru walikuwa na nafasi nzuri ya kufunga.
59' Masawe anashindwa kuunganisha mpira wa Krosi kutoka kwa Kichuya
Hashim Manyanya anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Hussein
62' Kichuya na Kikoti wametoka na wameingia Mohamed Issa na Lusajo
Phiri yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kupata rabsha.. Mpira upo mbele kuleee kwake Lusajo
68' Mohamed Issa anaonyeshwa Kadi ya Njano baada ya kumchezea madhambi Kanoute
Kassim ameingia kuchukua nafasi ya Masawe, upande wa Namungo FC
75' Namungo FC wamemka kwa sasa kutafuta bao la kusawazisha, wanamiliki mpira.
78' Ametoka Okrah na ameingia Akpan huku Simba wakifanya majaribio kadhaa
Ni Free Kick kuelekea Simba eneo karibu na box la 18, Akpan anafanya faulo.. Inapigwa mpira unababatiza mabeki wa Simba
Asante anaonyeshwa Kadi ya Njano kwa kumchezea madhambi Kibu
85' Simba wanaweka bao lakini Refa anakataa anasema ni Offside kwa Henock
88' Lusajo anapiga shutii lakini golikipa Manula anacheza vizuri, ilikuwa hatari langoni kwa Simba SC
90+2' Kuelekea kumalizika kwa mchezo
Almanusura Lusajo afunge bao, ilikuwa hatari sana lango la Simba Manula anacheza vizuri.. Lakini yupo chini akipatiwa matibabu
Kona kuelekea Simba, inapigwa kulee lakini Kanoute anaokoa, mpira wa kurusha sasa.
Naaam mpira umekwishaaaaaa
FT: Simba SC 1-0 Namungo FC
....... Ghazwat...