FT: Ligi Kuu Bara | Simba SC 1-0 Namungo FC | Stade de Benjamin Mkapa 16/11/2022

FT: Ligi Kuu Bara | Simba SC 1-0 Namungo FC | Stade de Benjamin Mkapa 16/11/2022

Unajua maana ya kujihusisha na dawa za Kulevya? Au akili yako ni Kiutopolo topolo huwezi Kung'amua hilo

Halafu mbona kama umeng' aka mno shida ni nini.!?
Tuhuma za kujihusisha?kiswahili mbona rahisi sana hicho bwana ngada? anyway leo kibu apunguziwe kiwango cha ngada nna uhakika atatupia.
 
ALikutwa na kilo ngapi za ngada? Maana huko kwa SImba mwamba kakutwa na kilo 34.89..!! Haya taja kilo alizokutwa nazo Manji
Jamaani nimeleta tu kumbukizi kuwa haya mambo yanazunguka na nimefunga mjadala kuanzia sasa

Na kama nimewatekenya Kiungo basi niwie radhi wakuu [emoji16]

Simba SC Vs Namungo FC ndo muda wake yaani.. Nguvu Moja [emoji881]
 
Unajua maana ya kujihusisha na dawa za Kulevya? Au akili yako ni Kiutopolo topolo huwezi Kung'amua hilo

Halafu mbona kama umeng' aka mno shida ni nini.!?
Kolo a.k.a mbumbumbu a.k.a mwana ngada FC, tofautisha tuhuma za kujihusisha na ngada na kudakwa na ngada..!! Unakumbuka LISU alikataa kupimwa mkojo?? Unajua sababu??
 
Kama si Mbiringe bila shaka ni Patashika ya Ligi Kuu Tanzani Bara [emoji1241] kuendelea kupigwa leo Jumatano ya Novemba 16, 2022 kwa Mnyama Mkali Mwituni Simba SC [emoji881] kukiwasha vilivyo na Wababe wa Kusini Namungo FC, katika Uwanja wa Stade de Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam [emoji2522]

Mchezo unatarajiwa kuwa ngumu kwa pande zote mbili kulingana na maandalizi na ubora wa vikosi vyao huku makocha wote wakisema kuwa wapo tayari kwa mchezo huo. Kocha Mkuu wa Simba SC, Juma Mgunda amesema kuwa maandalizi ya mchezo yapo vizuri.

"Kwa ujumla ni kwamba maandalizi ya mchezo wa leo yanakwenda vizuri, kwa maana kuwa tupo tayari kucheza mchezo wetu na mpinzani wetu kutoka Lindi". alisema Kocha Mgunda.

Naye Kocha Msaidizi wa Namungo FC Shadrack Nsajigwa kuelekea kwenye mchezo huo amesema kuwa wamejiandaa kushindana na Simba SC.

"Kimsingi tumekuja kushindana na Simba SC, tumepata muda wa kujiandaa kiasi cha siku 8 kwahivyo timu yetu ipo tayari kwa ajili ya kushindana na Simba SC". amesema Kocha Shadrack.

Tutegemee kuona ushindani wa kweli ndani ya dakika 90 za jasho na damu kutoka pande zote mbili katika kugombea alama tatu muhimu za Ligi Kuu Tanzania Bara..[emoji288]Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1;00[emoji354] Usiku.. Usikose Ukaadithiwa Yaani.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana.[emoji2424][/B]
Mchezo utakua mgumu kwa pande zote mbili
 
Anakuja na Style tofauti baadala ya ile ya Kunyunyiza. Pape Sakho
20221116_131617.jpg
 
Back
Top Bottom