FT: Niger 0-1 Tanzania. Kufuzu Kombe la Dunia. Novemba 18, 2023

FT: Niger 0-1 Tanzania. Kufuzu Kombe la Dunia. Novemba 18, 2023

Wewe hizi taarifa za best loser umezitolea wapi? Africa tunapeleka timu 6 tu na makundi yapo 6 tu.
Kweli? Mbona walisema zimeongezwa timu? Au yale ya mbele?. Ngoja nifuatilie tena,huenda nimechanganya na kombe la dunia la mbele
 
Wewe hizi taarifa za best loser umezitolea wapi? Africa tunapeleka timu 6 tu na makundi yapo 6 tu.
Hivi hapa umeandika kutokana na kutojua au unabishana? Kwa nini kabla hujaonyesha u... Usingeenda hata LiveScore au google ukajiridhisha na ulichotaka kuandika? Kukusaidia tu, jumatatu (20/11/2023) kutakuwa na mechi za group I, sasa rejea herufi I ni ya ngapi kutoka herufi A.
 
Kwa mpira waliocheza stars ni matumaini hakuna.
Bado inaonekana tuna shida ya kocha
 
Kwenye kundi letu wangejituma kidogo tu,ukiachana na Morocco,wengine wote ni wa kawaida sana. Kwa sasa sisi tunaweza kuwa level moja na Zambia.

Nimeangalia mechi ya DRC na Zambia. Hawa DRC wepesi mno. Hapo za kuwekana sawa inatakiwa iwe Zambia na Moroco tu. Wachezaji wakikaza kidogo tu hawa Niger ni wetu hawa,inatakiwa tuwatupie nje,ndani. DRC pia kwa walivyo sasa tuwatupie nje,ndani. Hapo inatakiwa wakija Moroco tupige nao patulo sale. Kwao acha watufunge. Tupambane na Zambia kwao sare,hata kwetu tukipata nao sare.

Hapo tayari tutakuwa tumemaliza na point 11[emoji3581] . Tutakuwa tumepita nafasi ya pili. Hata tukiangukia nafasi ya 3,kwa kundi letu ksbb ziko 5 maana yake timu ya 3 kuna timu itacheza nayo best rooser mtoano ndani na nje.

Kizuri zaidi timu sasa kutoka Afrika zimeongezwa nafikiri zitakuwa kati ya timu 9 au 10 hapo. Kwa hiyo sidhani kama tutakosa. Kocha kama mjanja waangalie sana mechi za DRC na Zambia,maana huko kuna point zetu wachezaji wakiongeza moto kidogo tu
Jana nmeona timu ya taifa mpya kabisa, ile iliyocheza na Algeria imeenda wapi?

maana wamecheza hovyooo mnooo hawakutahli kupewa ndege kabisa

Ile kama ndyo tim ya taifa kunahaja ya kufanya review

au watatuletea tim nyingne itakayo cheza na Morocco?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatuna Wachezaji hasa kule mbele.Samata hamna kitu Huo ndio ukweli.
Kubali tu mkuu kuwa kocha ni tatizo stars. Hata huyo Samata mbovu anapangwa na kocha.
Kocha ndie anaamua timu ichezeje
 
Hatuna Wachezaji hasa kule mbele.Samata hamna kitu Huo ndio ukweli.

Mkuu mechi ya jana timu ilikua haijengi mashambulizi
Mipira karibu yote ilikua inaishia katikati ya uwanja
Sasa hao akina mbwana mipira itawafikiaje?

Mfumo ulikua kujilinda zaidi na mashambulizi ya kushtukiza lakini penetration pasi zote zilikua fyongo

Hata hivyo tushukuru plan ya mwalimu ililipa tulipata nafasi tukaitumia na tukalinda vizuri sana
 
Kubali tu mkuu kuwa kocha ni tatizo stars. Hata huyo Samata mbovu anapangwa na kocha.
Kocha ndie anaamua timu ichezeje
Kuna jamaa anasema plan ya Mwalimu ilikuwa kujilinda!
 
Samatta na Manonga walikosa magoli ya wazi kabisa.Samattta alibaki na kipa na Manonga alibaki na goli bila kipa wakakosa!
 
Huyu haji Mnoga anakimbiakimbia na kuanguka hovyo Kama mtoto hajui Hata kukwepa poor stamina poor fitness inamfanya Achoke hoi Kama amekimbia maili 300!
Amemuangukia Job na kumuumiza bila sababu yoyote .
Shauri ngozi nyeupe ndiyo maana kocha anampanga lakini Kiwango kidogo kuliko wachezaji wa ligi ya Tanzania , nafuu Hata wachezaji wa Ihefu au kmc .
Inasemekana anachezea timu ya daraja la nne huko England .
Fei Toto mzito amenenepa hana speed na uchu wa mashambulizi na mashuti kama zamani
Umeonekana kabisa wewe ni yanga
 
Tukiongeza mazoezi ya pumzi na kukaba tukashikilia bomba hatufungwi na Morocco, ila tukifunguka tutapigwa nyingi. Lazima tuwaheshimu, faulo nje ya box hazitakiwi kabisa. Hawa mpira wao kama waarabu wengine hawana jipya na hawajui tunachezaje itatubeba!

Feisal bado sio yule, hivi sasa ni mzito sana muda wote anawaza kurudisha mipira nyuma sijui mbele anaogopa nini , mechi ya Morocco inamhitaji Mudathir tu katikati.

Samatta aache utozi, goli alilokosa akiwa yeye na kipa ni la kijinga kabisa, ila bado ni tegemeo letu mpira anaujua na amebadilika hivi sasa anakaba sana na kusaidia sana timu kule mbele. Kipa wa Niger alisumbuliwa sana na Samatta big up!

Ushindi dhidi ya Morocco pia upo tukitulia mwarabu anakaa tu kwa Mkapa hatoki Mtu, namuona Msuva akipiga goli mbili safi. Point 3 za Morocco tuzipambanie zitatubeba sana. Hii timu iko vizuri sana kushikilia bomba lazima tuseme ukweli
Mbona fei ndiyo kaongoza kupiga pass za macho
 
Back
Top Bottom