Ni siku ya kipekee siku ya kihistoria katika soka la nchi yetu ambapo tunaweza kushuhudia timu kutoka Tanzania kwa mara ya kwanza ikitinga hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika.
Timu hiyo si nyingine Bali ni Mabingwa wa nchi na vikombe vyote nchini na ambao ndio wawakilishi pekee wa Tanzania na Afrika Mashariki na kati katika michuano ya kimataifa Young Africans almaarufu Yanga.
Leo jioni wanashuka dimbani Estadio de Benjamini Mkapa kumenyana na Rivers United katika hatua ya robo fainali kombe la shirikisho barani Afrika.
Ikumbukwe mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa kule Nigeria, Yanga walipata ushindi wa mabao 2-0, Hivyo wataingia Uwanjani wakiwa na kiu ya kuendeleza ubabe wao mbele ya mapopo na kutinga nusu fainali ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika.
Pia Yanga watakuwa na kiu ya kulipa kisasi cha kufungwa na hawa Rivers nje ndani hivyo watakuwa na kila sababu ya kupata ushindi kwenye ardhi ya nyumbani,
Mchezo huu utapigwa mishale ya saa 1.00 usiku na utarushwa na Azam Sports kupitia channel ya ZBC2
View attachment 2604213View attachment 2604214