3.2.1 Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) mara moja
wachukue hatua ya kumkamata Bwana Harbinder Singh Sethi na
kumfikisha mahakamani kwa makosa ya Anti money laundering,
ukwepaji kodi na wizi. Kamati pia inaelekeza Serikali kutumia
sheria za Nchi, ikiwemo sheria ya Proceeds of Crime Act
kuhakikisha kuwa Bwana Harbinder Singh Sethi anarejesha fedha
zote alizochota kutoka Benki Kuu ya Tanzania. Kwa kuwa suala hili
ni suala la utakatishaji wa fedha haramu, Mamlaka ziwasiliane na
mamlaka za Nchi nyingine kuhakikisha mali za Bwana huyu
zinakamatwa na kufidia fedha hizo.