Funga Juma: Masufuria ya Nyama: Siyo Wote Walioondoka Misri Walitoka Misri...

Funga Juma: Masufuria ya Nyama: Siyo Wote Walioondoka Misri Walitoka Misri...

View attachment 1800414
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya masimulizi ya kiimani ambayo yalinivutia sana tangu zamani ni safari ya wana wa Israeli kutoka Misri kwenda nchi ya ahadi wakiongozwa na Nabii Musa. Simulizi hili nimelisoma mara nyingi na kila ninapolisoma Napata mafunzo mapya. Hata hivyo mojawapo ya mafunzo ambayo naweza kutumia kuelezea siasa zetu za leo katika Tanzania ni ile tabia ya baadhi ya wana wa Israeli kulalamika lalamika kila mambo yalipokuwa magumu walipokuwa njiani.

Musa alipowajia wana wa Israeli na ujumbe kuwa kuna nchi ya ahadi inawangojea wengi walifurahia na kwa kweli walifuata maelezo yake yote na hata ile siku ya kutoka Misri jamii nzima walikuwa tayari kutoka. Wote walikuwa na hamu ya kwenda kule ambako hakuna utumwa, na kule ambapo wangekuwa hai. Waliambiwa nchi wanayoiendea ilikuwa inatiririka maziwa na asali (Kut. 3:8,17). Kwa kweli waliitamani sana hiyo nchi. Na waliondoka Misri wakifurahia kuwa wanaenda mahali ambapo watafurahia maisha kweli kweli.

Walipoondoka na kuvuka bahari ya shamu walishuhudia muujiza mkubwa wa bahari kufunguka na wao kupita kwenye nchi kavu. Lakini muujiza mkubwa ni jinsi gani majeshi ya farao yaliangamia na wana wa Israeli walikuwa wamevuka ng’ambo ya pili. Ukisoma kitabu cha Kutoka 15 utaona jinsi wana wa Israeli walivyoimba kwa shangwe wakifurahia jinsi walivyoona matendo makuu ya Mungu. Wana wa Israeli walipenda mabadiliko na mafanikio lakini hawakuwa tayari kulipa gharama.

Hili tunaliona kwenye sura mbili zinazofuatia tukio la wao kuvuka Bahari ya Shamu. Kwenye sura ya 16 na sura ya 17 tunakutana na wana wa Israeli baada ya kupata shida kidogo walipoanza kulalamika na kunung’unika. Walijisikia njaa kidogo wakaanza kukumbuka “masufuria ya nyama” waliyokuwa wakila kule utumwani Misri. Mara kadhaa katika safari yao walijikuwa wanakumbuka Misri na kutamani kurudi kule walikotoka kwa sababu walikuwa na uhakika wa kula kwao, kulala kwao – hata kama walikuwa utumwani!

Ndugu zangu, naomba kupendekeza kuwa kweli wapo Watanzania wanaotaka mabadiliko na maendeleo lakini pia wapo wengine ambao kwao mabadiliko ni lazima yawe rahisi, yasiyo na jasho na yasiyo na uchungu. Wanataka kuendelea bila kulia, wanataka kufanikiwa bila kuinama au kunyanyua! Hawa ndugu zetu miaka hii mitano kwao maisha yalikuwa magumu sana kiasi kwamba walianza kukumbuka “masufuria ya nyama”.

NI kweli maelfu walitoka Misri lakini Misri haikutoka mioyoni ma wengi katika Israeli. Hata ukisoma Qurani Tukufu utakutana na wana wa Israeli wakilalamika tena kuwa hawakuwa tayari kwenda kwenye nchi waliyoahidiwa kwa sababu walikuwa wanaogopa kuna majibut majabari kule. Kwamba, walimuambia Musa kuwa kama anataka wao waende kwenye hiyo nchi basi Musa na Mungu wake waende wakapigane na majitu hao wakati wao (wana wa Israeli) watakaa hapo hapo wakisubiria! Kwa mujibu wa Qurani hii ilikuwa ni sababu ya wana wa Israeli kuharamishwa kuingia nchi ya ahadi kwa miaka arobani wakibakia kutangatanga (Qurani 5:20-26).

Leo hii katika Tanzania wapo watu ambao wanajua kukatisha tamaa wengine; watu hawa wanabeza SGR kuwa haiwezekani; wanatuambia hatuwezi kuendelea bila kusaidiwa; wanatuambia sisi ni maskini na kuwa hatuwezi kabisa! Wanarudisha hofu na hali ya kutokujiamini miongoni mwetu na kwa bahati mbaya wapo ambao wanawaamini. Nikiri tu kuwa mojawapo ya vitu vilivyokuwa vinanipa moyo sana ni lugha ya kujiamini ya hayati Rais Magufuli. Kwa uzuri au kwa ubaya alikuwa anajiamini kupitiliza! Sidhani kama alikuwa na mazoea ya kutumia lugha ya “haiwezekani” au “hatuwezi”. Kwake yeye mengi yalikuwa ni mambo ya kuthubutu kuyafanya. Inawezekana hata sasa kuna watu hawakubali hatua mbalimbali anazochukua Rais Samia; na hawa nao wanaanza kuwa na wasiwasi kwa sababu hawaamini kuwa anaenda kuendelea kulisogeza taifa mbele.

Binafsi kwa wakati huu ninamuona Rais Samia kama Yoshua aliyechukua nafasi ya Musa. Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune walikuwa ni watu wawili ambao walileta taarifa ya kujiamini baada ya kwenda kupeleleza nchi ya ahadi. Wakati wenzao walirudi na taarifa ya kutisha ya kuwa nchi ya ahadi imejaa mijitu mikubwa kiasi kwamba wao walikuwa wadogo kama “panzi” Yoshua na Kalebu walisema hata kama hivyo ni kweli bado wao walikuwa wana uwezo wa kushinda. Yoshua hakuwa Musa na hakufanya mambo kama Musa; alijua jukumu lake lakini alienda kufanya vitu tofauti na Musa. Mama Samia – kama nilivyoeleza huko nyuma – si lazima afanye kila kitu kama Magufuli wala haitaji kuzungumza kama Magufuli; anajua ajenda anayoitekeleza na anajua Watanzania wanatarajia nini kwake.

Wakati umefika wa kuanza kuwakatalia wale wote ambao wanataka turudi kwenye maisha ya utawala wa kifisadi ambapo baadhi yetu walikuwa wanakesha kwenye masufuria ya nyama! Kibarua alicho nacho Rais Samia ni kuweza kujua ni kina nani hawa ambao wanaotamani turudi kwenye fikra za kitumwa na za kimaskini; tukumbuke; siyo wote walioondoka Misri, walitoka kweli Misri! Kwani wengi bado walikuwa wanakumbuka Misri kwa mioyo yenye kuitamani; na wapo wanaotamani turudi kwenye ufisadi. Tukirudi tumekwisha; vinginevyo tunaweza tukajikuta tunatangatanga miaka arobaini!

Tujiandae kwa Deep Green, Tangold na Meremeta 2.0? Angalau Serikali inaonesha kushtushwa na kilichojaribiwa Wizara ya Fedha…


Niandikie:klhnews@gmail.com
Vipi wakati wa hiyo safari ya Misri Musa mwenyewe aliua waisrael wangapi safarini ??

Na je, wakati wa safari Musa aliwanyima chakula wenzake huku wakiwa safarini ilimradi punda afike Kanaan ( huku yeye Musa na kundi lake kina Yoshua wakineemeka ) ?

Kuhusu kujitegemea hakuna mtu asiyependa nchi yetu IJITEGEMEE ila kusema Magu alikuwa anapeleka nchi yetu kujitegemea ni uongo asilimia 200.

Magufuli hakuwahi kukataa misaada, na tena alikuwa anatumia mbinu zote alizoweza kuhakikisha anapewa. Mfano:
  • Uwepo wa kina Halima Mdee bungeni hata kama ni kinyume na katiba, lengo ni kuwinda misaada tena kwa gharama kubwa ya katiba na fedha
  • Pesa za COVID-19 kutoka EU alizoa na haijulikani alipekeka wapi wakati alikuwa haamini kama Tanzania kuna COVID. Tena hizo pesa alichukua kimya kimya, bila kamati ya EU yenyewe kusema tusingejua
  • Pesa za WB za elimu kwa watoto wa kike. Yaani watoto wa kike waliopata ujauzito kurudi shule hakutaka ila pesa alitaka mpaka kina Zitto kutaka kuuawa.

Magufuli alikuwa anapinga misaada ambayo aliona dalili tu kuwa haaawezi kumpa kutokana ukiukwaji mkubwa wa Demokrasia, utawala bora na haki za binadamu.

Unajifanya hukitaki kitu ambacho, mwenye nacho ameshasema hakupi. In short Magu alikuwa anaona watu kama watoto fulani wajinga.

Hata pesa za kugharamia uchaguzi mkuu, siyo kwamba nia yake ilikuwa kunitegemea.

Nia ya Magu ilikuwa ni kukwepa waangalizi wa kimataifa kwenye uchaguzi hasa ukichukua pesa za UNDP kwasababu ni moja ya masharti yao.

Na hakuna asiyejua namna Magu alivyotumia majeshi, mauaji na uporaji kuipata Dola mwaka 2020.

Namfanisha na yule Mkulima wa kwenye biblia aliyevuna sana akatia ghalani, halafu akasema sasa nafsi yake ni kunywa, kula na kufurahi. Magu alikuwa ameshamaliza, kina Lissu wameshakimbia, kila mtanzania ameshakata tamaa. Bunge, mahakama, serikali vyote vyake. Mungu akasema NO hata Urais wa awamu ya pili hajakaa sawa.

Magu alikuwa ni shetani wa damu. Alikuwa katili hasa tena wa damu.

Tena alikuwa mtu anbaye hata kama huna tatizo naye, yete analala anawaza akamuumize nani.
 
Hayati Magufuli ni mmoja wa watanzania ambao wanajitambua na yeye alikuwa ni mtu aliejitambua.

Hii ni sifa moja kubwa sana ya binadamu, kujitambua.

Hayati Magufuli alijitambua na hata wengine kama mimi Richard najitambua na naamini Paschal na Mwanakijiji pia mwajitambua.

Watanzania waafrika wengi na hata baadhi ya wazungu waliweza kuona hilo kuwa hayati Magufuli alijitambua na aliweka alama ya bara la Afrika kwenye koti lake.

Ni kweli akiwa binadamu na yeye alikuwa na kasoro zake na hilo halina ubishi ila twasimamia masuala ya msingi aloyatenda na kuyatekeleza.

Moja ya mambo mazito yanothibitisha kuwa watanzania wachache hawajitambui ni kuonyesha kushangilia kifo chake wakati waafrika wengi walisikitishwa na tukio hilo na hata kutuuliza watanzania nini kimetokea?

Sasa baadhi ya wazungu na waafrika wengine hawapendi kuona waafrika wenzao wanajitambua maana wanahisi hapatashikika.

Kama hayati Magufuli aliweza kutikisa kila mahali na pakatikisika na akaja nchini bwana mkubwa wa uchimbaji madini kutoka Canada, basi alikuwa ni yeye na hatatokea Magufuli mwingine tena ndo imetoka hiyo.

Lakini bara la Afrika bado lina waafrika na watanzania wengi ambao bado hawajajitambua na ikifika siku wanajitambua itakuwa ni siku ya kiama na tutakuwa tumechelewa maana yeye alikwishasema tumecheleweshwa mno.

Ushuhuda ni madudu ambayo yameanza kurudi baada ya kuondoka kwake duniani, mara TRA kuna mitambo imeharibika, mara TANESCO mfumo wa LUKU umeingiliwa, mara majambazi yamerudi na mara bandarini kuna figisu zimerudi hii yote ni kuonyesha kuwa watanzania bado hawajaweza kujitambua.

Hapo awali , tulisikia mara Kitalu C kilianza kuingiliwa mpaka pale mama Samia alipoamuru ulinzi uimarishwe.

Pia tumesikia wizara ya fedha watu wamesimamishwa kazi kwa ubadhilifu wa fedha na hiyo ni wizara ya FEDHA yaani hazina ya nchi!

Watanzania wenzetu hawa bila woga wameingia hazina na kukwapua fedha za walipa kodi!!

Hivyo, kwanza watanzania waweze kujitambua kuwa wao ni nani na wapo Tanzania kwa kusudio la Mungu ambae amewapa rasilimali na uwezo mkubwa wa kumiliki rasilimali hizo hivyo wahitaji usimamizi.

Kinachohitajika ni kujitambua, kisha kuhakikisha twazisimamia rasilimali hizo na kuzigeuza kuwa utajiri kiasi cha kumsaidia kila mtanzania aliezaliwa Tanzania na yule alie na vinasaba vya utanzania kwa elimu bora, makazi bora na maisha bora.
 
Wakati hao Wamisri wanalalamika njaa..., Musa alikuwa anakula peke yake na watu wake (minority) wakati wengine wana njaa (majority) au wote walikuwa wamefunga mikanda ?

Au all animals are equal but some are more equal ?
 
Uwe makini pia, awamu fulani ilikuwa haitaki wala kupenda kusikia habari mbaya zinazoihusu....hata kungekuwa na wizi kiasi gani hakuna mwandishi ambaye angeweza kuandika habari yayote wala kiongozi kuzungumzia huo ubadhirifu.....kupitia awamu hiyo kitu kinachoitwa transparency kilifutwa na hakikuwepo...

Moja ya changamoto zinazoikabili awamu hii ya Mama ni namna akili za watu zilivyojiseti baada ya kumezeshwa vitu vingi vya viongo na propaganda nyingi ambazo watu walizamishwa kuamini maana hakuna chombo cha habari ambacho kingeandika tofauti na alivyotaka bosi mkubwa mmiliki wa dola na maguvu yote..

Transparency ilimfanya JK akaonekana dhaifu na CDM kupata nguvu, lakini hata JK angeamua kuwa na tabia za jamaa kunyamazisha na kuficha mambo tusingejua kitu wala kuhoji kitu na JK tungemuita Malaika wa duniani....Mama ameamua kuuishi transparency, tunajua meeengi na kumpopoa sana Mama lakini ukweli kama Watanzania tunapaswa kukemea tabia mbovu na kuipa pressure serikali pressure itende inavyopaswa hii ni kww serikali yeyote na italeta faida kww nchi...

Siasa za kuchagua upande hazina maana kwa Watanzania na nchi...wananchi tunapaswa kupima mambo na kuyapigia kelele kwa maslahi ya umma....siasa za kuchagua upande either kwa misingi ya Dini, kabila, dhehebu nk ni mbaya sana na hazina faida kwa umma...
 
Uwe makini pia, awamu fulani ilikuwa haitaki wala kupenda kusikia habari mbaya zinazoihusu....hata kungekuwa na wizi kiasi gani hakuna mwandishi ambaye angeweza kuandika habari yayote wala kiongozi kuzungumzia huo ubadhirifu.....kupitia awamu hiyo kitu kinachoitwa transparency kilifutwa na hakikuwepo...

Moja ya changamoto zinazoikabili awamu hii ya Mama ni namna akili za watu zilivyojiseti baada ya kumezeshwa vitu vingi vya viongo na propaganda nyingi ambazo watu walizamishwa kuamini maana hakuna chombo cha habari ambacho kingeandika tofauti na alivyotaka bosi mkubwa mmiliki wa dola na maguvu yote..

Transparency ilimfanya JK akaonekana dhaifu na CDM kupata nguvu, lakini hata JK angeamua kuwa na tabia za jamaa kunyamazisha na kuficha mambo tusingejua kitu wala kuhoji kitu na JK tungemuita Malaika wa duniani....Mama ameamua kuuishi transparency, tunajua meeengi na kumpopoa sana Mama lakini ukweli kama Watanzania tunapaswa kukemea tabia mbovu na kuipa pressure serikali pressure itende inavyopaswa hii ni kww serikali yeyote na italeta faida kww nchi...

Siasa za kuchagua upande hazina maana kwa Watanzania na nchi...wananchi tunapaswa kupima mambo na kuyapigia kelele kwa maslahi ya umma....siasa za kuchagua upande either kwa misingi ya Dini, kabila, dhehebu nk ni mbaya sana na hazina faida kwa umma...
Zilikuwepo taarifa za wizi na ubadhilifu wakati huo au hukuwa unafuatilia?

Wizi khasa katika halmashauri ulikuwa ni mwingi tu na watu walikuwa wakikamatwa.

Na hata viongozi wengi walifukuzwa kazi kwa uzembe au kusababisha hasara.

Suala jingine ambalo bado ni tatizo kwa vyombo vyetu vya habari ni uandishi makini na kujitambua.

Vyombo vya habari za nje kwenye masuala yanohusu taifa au maslahi ya taifa vyombo hivyo huwa pamoja kabisa.

Kwa mfano ugonjwa COVID -19 vyombo vya habari vyapaswa kuelimisha jamii zaidi kuliko kuonekana vinasaidia propaganda kutoka nje kwani hilo ni suala linalohusu maslahi ya taifa na mstakabali wake.

Pili, vyombo vya habari vyapaswa kuchambua ni kwanini Dangote aliondoka nchini na ni kwanini anarudi mida hii?

Wanapaswa kuhoji kwanini Tanzania inaruhusu viwanda vya kigeni kuzalisha mbolea nchini?

Maana mbolea inahusika na uzalishaji vyakula na mazao mbalimbali ambavyo vyote vyaingizwa katika usalama wa vyakula yaani "Food Security" na je taratibu zote zimefuatwa?

Hivyo haya ni masuala ambayo ukitaka kuyadadavua inabidi kwanza uwe umejitambua kabla ya kuruhusu kila mtu alete malighafi za mbolea ambazo hufahamu kama zitaleta madhara kwa mazao na ardhi yetu.
 
Zilikuwepo taarifa za wizi na ubadhilifu wakati huo au hukuwa unafuatilia?

Wizi khasa katika halmashauri ulikuwa ni mwingi tu na watu walikuwa wakikamatwa.

Na hata viongozi wengi walifukuzwa kazi kwa uzembe au kusababisha hasara.

Suala jingine ambalo bado ni tatizo kwa vyombo vyetu vya habari ni uandishi makini na kujitambua.

Vyombo vya habari za nje kwenye masuala yanohusu taifa au maslahi ya taifa vyombo hivyo huwa pamoja kabisa.

Kwa mfano ugonjwa COVID -19 vyombo vya habari vyapaswa kuelimisha jamii zaidi kuliko kuonekana vinasaidia propaganda kutoka nje kwani hilo ni suala linalohusu maslahi ya taifa na mstakabali wake.

Pili, vyombo vya habari vyapaswa kuchambua ni kwanini Dangote aliondoka nchini na ni kwanini anarudi mida hii?

Wanapaswa kuhoji kwanini Tanzania inaruhusu viwanda vya kigeni kuzalisha mbolea nchini?

Maana mbolea inahusika na uzalishaji vyakula na mazao mbalimbali ambavyo vyote vyaingizwa katika usalama wa vyakula yaani "Food Security" na je taratibu zote zimefuatwa?

Hivyo haya ni masuala ambayo ukitaka kuyadadavua inabidi kwanza uwe umejitambua kabla ya kuruhusu kila mtu alete malighafi za mbolea ambazo hufahamu kama zitaleta madhara kwa mazao na ardhi yetu.
Waandishi wengi wa taifa hili ni makasuku mkuu
 
Hakuna cha nchi ya ahadi wala Mussa na Yoshua...

Ufisadi unalelewa na kutopenda kukosolewa na kuminya uhuru wa habari...

Huyo 'Mussa ' alijenga airport Kwa bajeti ipi iliyopitishwa na Bunge lipi na transparency ipi?

Labda Mussa wa imagination zako...

Ufisadi ulikuwepo mkubwa awamu ya tano...
Hapa huyo myunani hawezi kukujibu maana Musa hakuwa mroho/mbinafsi wala mungu mtu
 
Tatizo la binadamu ni kiburi chake cha asili. Huwa anapanga mipango yake halafu Mungu anatekeleza makusudio yake ambayo humuacha Binadamu akiwa mdomo wazi haamini anachokiona.

Usiku ule wa tarehe 17 March mtu mmoja alituma message kwenye group la whatsapp kwamba Mama Samia anatangaza kifo cha JPM, nikamwambia asiweke kitu kwenye group pasipo kuwa na uhakika, ndani ya dakika chache ikathibitika kuwa kweli msiba umelikumba taifa.

Kumwangalia Mama Samia anaongea mbele ya kamera akielezea kuhusu msiba, ndio kichwani ikaja picha ya ukuu wa Mungu, kwamba yule Mama ambaye alionekana ni msaidizi tu wa Rais JPM kuanzia dakika ile alikuwa ndio Rais wa nchi mpaka 2025.

Ukuu wa Mungu hauwezi kuhojiwa na kuelezewa kwa akili za kawaida za binadamu. Siku zote unazidi uwezo wetu, mipango yetu, tamaa zetu. Ni ukuu ulio juu kuzidi namna tunavyoweza kuuelezea.

Sasa jamaa wengi tu bado ni kama hawakubaliani na uhalisia wa kinachoendelea. Rais Samia hakutegemea kuja kuwa rais lakini cha muhimu sio kuangalia upungufu wake halafu mtu akadhani anaikomoa Tanzania. Hii nchi tunaiacha na hatujui ni lini.
 
View attachment 1800414
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya masimulizi ya kiimani ambayo yalinivutia sana tangu zamani ni safari ya wana wa Israeli kutoka Misri kwenda nchi ya ahadi wakiongozwa na Nabii Musa. Simulizi hili nimelisoma mara nyingi na kila ninapolisoma Napata mafunzo mapya. Hata hivyo mojawapo ya mafunzo ambayo naweza kutumia kuelezea siasa zetu za leo katika Tanzania ni ile tabia ya baadhi ya wana wa Israeli kulalamika lalamika kila mambo yalipokuwa magumu walipokuwa njiani.

Musa alipowajia wana wa Israeli na ujumbe kuwa kuna nchi ya ahadi inawangojea wengi walifurahia na kwa kweli walifuata maelezo yake yote na hata ile siku ya kutoka Misri jamii nzima walikuwa tayari kutoka. Wote walikuwa na hamu ya kwenda kule ambako hakuna utumwa, na kule ambapo wangekuwa hai. Waliambiwa nchi wanayoiendea ilikuwa inatiririka maziwa na asali (Kut. 3:8,17). Kwa kweli waliitamani sana hiyo nchi. Na waliondoka Misri wakifurahia kuwa wanaenda mahali ambapo watafurahia maisha kweli kweli.

Walipoondoka na kuvuka bahari ya shamu walishuhudia muujiza mkubwa wa bahari kufunguka na wao kupita kwenye nchi kavu. Lakini muujiza mkubwa ni jinsi gani majeshi ya farao yaliangamia na wana wa Israeli walikuwa wamevuka ng’ambo ya pili. Ukisoma kitabu cha Kutoka 15 utaona jinsi wana wa Israeli walivyoimba kwa shangwe wakifurahia jinsi walivyoona matendo makuu ya Mungu. Wana wa Israeli walipenda mabadiliko na mafanikio lakini hawakuwa tayari kulipa gharama.

Hili tunaliona kwenye sura mbili zinazofuatia tukio la wao kuvuka Bahari ya Shamu. Kwenye sura ya 16 na sura ya 17 tunakutana na wana wa Israeli baada ya kupata shida kidogo walipoanza kulalamika na kunung’unika. Walijisikia njaa kidogo wakaanza kukumbuka “masufuria ya nyama” waliyokuwa wakila kule utumwani Misri. Mara kadhaa katika safari yao walijikuwa wanakumbuka Misri na kutamani kurudi kule walikotoka kwa sababu walikuwa na uhakika wa kula kwao, kulala kwao – hata kama walikuwa utumwani!

Ndugu zangu, naomba kupendekeza kuwa kweli wapo Watanzania wanaotaka mabadiliko na maendeleo lakini pia wapo wengine ambao kwao mabadiliko ni lazima yawe rahisi, yasiyo na jasho na yasiyo na uchungu. Wanataka kuendelea bila kulia, wanataka kufanikiwa bila kuinama au kunyanyua! Hawa ndugu zetu miaka hii mitano kwao maisha yalikuwa magumu sana kiasi kwamba walianza kukumbuka “masufuria ya nyama”.

NI kweli maelfu walitoka Misri lakini Misri haikutoka mioyoni ma wengi katika Israeli. Hata ukisoma Qurani Tukufu utakutana na wana wa Israeli wakilalamika tena kuwa hawakuwa tayari kwenda kwenye nchi waliyoahidiwa kwa sababu walikuwa wanaogopa kuna majibut majabari kule. Kwamba, walimuambia Musa kuwa kama anataka wao waende kwenye hiyo nchi basi Musa na Mungu wake waende wakapigane na majitu hao wakati wao (wana wa Israeli) watakaa hapo hapo wakisubiria! Kwa mujibu wa Qurani hii ilikuwa ni sababu ya wana wa Israeli kuharamishwa kuingia nchi ya ahadi kwa miaka arobani wakibakia kutangatanga (Qurani 5:20-26).

Leo hii katika Tanzania wapo watu ambao wanajua kukatisha tamaa wengine; watu hawa wanabeza SGR kuwa haiwezekani; wanatuambia hatuwezi kuendelea bila kusaidiwa; wanatuambia sisi ni maskini na kuwa hatuwezi kabisa! Wanarudisha hofu na hali ya kutokujiamini miongoni mwetu na kwa bahati mbaya wapo ambao wanawaamini. Nikiri tu kuwa mojawapo ya vitu vilivyokuwa vinanipa moyo sana ni lugha ya kujiamini ya hayati Rais Magufuli. Kwa uzuri au kwa ubaya alikuwa anajiamini kupitiliza! Sidhani kama alikuwa na mazoea ya kutumia lugha ya “haiwezekani” au “hatuwezi”. Kwake yeye mengi yalikuwa ni mambo ya kuthubutu kuyafanya. Inawezekana hata sasa kuna watu hawakubali hatua mbalimbali anazochukua Rais Samia; na hawa nao wanaanza kuwa na wasiwasi kwa sababu hawaamini kuwa anaenda kuendelea kulisogeza taifa mbele.

Binafsi kwa wakati huu ninamuona Rais Samia kama Yoshua aliyechukua nafasi ya Musa. Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune walikuwa ni watu wawili ambao walileta taarifa ya kujiamini baada ya kwenda kupeleleza nchi ya ahadi. Wakati wenzao walirudi na taarifa ya kutisha ya kuwa nchi ya ahadi imejaa mijitu mikubwa kiasi kwamba wao walikuwa wadogo kama “panzi” Yoshua na Kalebu walisema hata kama hivyo ni kweli bado wao walikuwa wana uwezo wa kushinda. Yoshua hakuwa Musa na hakufanya mambo kama Musa; alijua jukumu lake lakini alienda kufanya vitu tofauti na Musa. Mama Samia – kama nilivyoeleza huko nyuma – si lazima afanye kila kitu kama Magufuli wala haitaji kuzungumza kama Magufuli; anajua ajenda anayoitekeleza na anajua Watanzania wanatarajia nini kwake.

Wakati umefika wa kuanza kuwakatalia wale wote ambao wanataka turudi kwenye maisha ya utawala wa kifisadi ambapo baadhi yetu walikuwa wanakesha kwenye masufuria ya nyama! Kibarua alicho nacho Rais Samia ni kuweza kujua ni kina nani hawa ambao wanaotamani turudi kwenye fikra za kitumwa na za kimaskini; tukumbuke; siyo wote walioondoka Misri, walitoka kweli Misri! Kwani wengi bado walikuwa wanakumbuka Misri kwa mioyo yenye kuitamani; na wapo wanaotamani turudi kwenye ufisadi. Tukirudi tumekwisha; vinginevyo tunaweza tukajikuta tunatangatanga miaka arobaini!

Tujiandae kwa Deep Green, Tangold na Meremeta 2.0? Angalau Serikali inaonesha kushtushwa na kilichojaribiwa Wizara ya Fedha…


Niandikie:klhnews@gmail.com
Na Kundi kubwa ktk waliotamani kurudi Misri ni watendaji wa serikali ambao kwa Tamaaa ya nyama ya kwenye sufuria walisahau maumivu ya mijeledi mwilini mwao na mateso yasiyo na mwisho.
Hawa ndo walilalamika maji,umeme usio wa uhakika,foleni zisizoisha,uwizi na ujambazi,mauaji holela ya ma albino,posho kubwa za mabosi wao,ada kubwa za shule za private n.k,Hawa ndo wamesahau kurudi kwao Misri utumwani Basi ni mateso yasiyo na mwisho kwa vizazi vyao.

Ila tumewajua,wamejazana mtandaoni wakimdemsha mama wakati huku mtaani hali ni tofauti,watu wakimkumbuka Mussa aliyeanza kuwapeleka nchi ya ahadi.
 
View attachment 1800414
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya masimulizi ya kiimani ambayo yalinivutia sana tangu zamani ni safari ya wana wa Israeli kutoka Misri kwenda nchi ya ahadi wakiongozwa na Nabii Musa. Simulizi hili nimelisoma mara nyingi na kila ninapolisoma Napata mafunzo mapya. Hata hivyo mojawapo ya mafunzo ambayo naweza kutumia kuelezea siasa zetu za leo katika Tanzania ni ile tabia ya baadhi ya wana wa Israeli kulalamika lalamika kila mambo yalipokuwa magumu walipokuwa njiani.

Musa alipowajia wana wa Israeli na ujumbe kuwa kuna nchi ya ahadi inawangojea wengi walifurahia na kwa kweli walifuata maelezo yake yote na hata ile siku ya kutoka Misri jamii nzima walikuwa tayari kutoka. Wote walikuwa na hamu ya kwenda kule ambako hakuna utumwa, na kule ambapo wangekuwa hai. Waliambiwa nchi wanayoiendea ilikuwa inatiririka maziwa na asali (Kut. 3:8,17). Kwa kweli waliitamani sana hiyo nchi. Na waliondoka Misri wakifurahia kuwa wanaenda mahali ambapo watafurahia maisha kweli kweli.

Walipoondoka na kuvuka bahari ya shamu walishuhudia muujiza mkubwa wa bahari kufunguka na wao kupita kwenye nchi kavu. Lakini muujiza mkubwa ni jinsi gani majeshi ya farao yaliangamia na wana wa Israeli walikuwa wamevuka ng’ambo ya pili. Ukisoma kitabu cha Kutoka 15 utaona jinsi wana wa Israeli walivyoimba kwa shangwe wakifurahia jinsi walivyoona matendo makuu ya Mungu. Wana wa Israeli walipenda mabadiliko na mafanikio lakini hawakuwa tayari kulipa gharama.

Hili tunaliona kwenye sura mbili zinazofuatia tukio la wao kuvuka Bahari ya Shamu. Kwenye sura ya 16 na sura ya 17 tunakutana na wana wa Israeli baada ya kupata shida kidogo walipoanza kulalamika na kunung’unika. Walijisikia njaa kidogo wakaanza kukumbuka “masufuria ya nyama” waliyokuwa wakila kule utumwani Misri. Mara kadhaa katika safari yao walijikuwa wanakumbuka Misri na kutamani kurudi kule walikotoka kwa sababu walikuwa na uhakika wa kula kwao, kulala kwao – hata kama walikuwa utumwani!

Ndugu zangu, naomba kupendekeza kuwa kweli wapo Watanzania wanaotaka mabadiliko na maendeleo lakini pia wapo wengine ambao kwao mabadiliko ni lazima yawe rahisi, yasiyo na jasho na yasiyo na uchungu. Wanataka kuendelea bila kulia, wanataka kufanikiwa bila kuinama au kunyanyua! Hawa ndugu zetu miaka hii mitano kwao maisha yalikuwa magumu sana kiasi kwamba walianza kukumbuka “masufuria ya nyama”.

NI kweli maelfu walitoka Misri lakini Misri haikutoka mioyoni ma wengi katika Israeli. Hata ukisoma Qurani Tukufu utakutana na wana wa Israeli wakilalamika tena kuwa hawakuwa tayari kwenda kwenye nchi waliyoahidiwa kwa sababu walikuwa wanaogopa kuna majibut majabari kule. Kwamba, walimuambia Musa kuwa kama anataka wao waende kwenye hiyo nchi basi Musa na Mungu wake waende wakapigane na majitu hao wakati wao (wana wa Israeli) watakaa hapo hapo wakisubiria! Kwa mujibu wa Qurani hii ilikuwa ni sababu ya wana wa Israeli kuharamishwa kuingia nchi ya ahadi kwa miaka arobani wakibakia kutangatanga (Qurani 5:20-26).

Leo hii katika Tanzania wapo watu ambao wanajua kukatisha tamaa wengine; watu hawa wanabeza SGR kuwa haiwezekani; wanatuambia hatuwezi kuendelea bila kusaidiwa; wanatuambia sisi ni maskini na kuwa hatuwezi kabisa! Wanarudisha hofu na hali ya kutokujiamini miongoni mwetu na kwa bahati mbaya wapo ambao wanawaamini. Nikiri tu kuwa mojawapo ya vitu vilivyokuwa vinanipa moyo sana ni lugha ya kujiamini ya hayati Rais Magufuli. Kwa uzuri au kwa ubaya alikuwa anajiamini kupitiliza! Sidhani kama alikuwa na mazoea ya kutumia lugha ya “haiwezekani” au “hatuwezi”. Kwake yeye mengi yalikuwa ni mambo ya kuthubutu kuyafanya. Inawezekana hata sasa kuna watu hawakubali hatua mbalimbali anazochukua Rais Samia; na hawa nao wanaanza kuwa na wasiwasi kwa sababu hawaamini kuwa anaenda kuendelea kulisogeza taifa mbele.

Binafsi kwa wakati huu ninamuona Rais Samia kama Yoshua aliyechukua nafasi ya Musa. Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune walikuwa ni watu wawili ambao walileta taarifa ya kujiamini baada ya kwenda kupeleleza nchi ya ahadi. Wakati wenzao walirudi na taarifa ya kutisha ya kuwa nchi ya ahadi imejaa mijitu mikubwa kiasi kwamba wao walikuwa wadogo kama “panzi” Yoshua na Kalebu walisema hata kama hivyo ni kweli bado wao walikuwa wana uwezo wa kushinda. Yoshua hakuwa Musa na hakufanya mambo kama Musa; alijua jukumu lake lakini alienda kufanya vitu tofauti na Musa. Mama Samia – kama nilivyoeleza huko nyuma – si lazima afanye kila kitu kama Magufuli wala haitaji kuzungumza kama Magufuli; anajua ajenda anayoitekeleza na anajua Watanzania wanatarajia nini kwake.

Wakati umefika wa kuanza kuwakatalia wale wote ambao wanataka turudi kwenye maisha ya utawala wa kifisadi ambapo baadhi yetu walikuwa wanakesha kwenye masufuria ya nyama! Kibarua alicho nacho Rais Samia ni kuweza kujua ni kina nani hawa ambao wanaotamani turudi kwenye fikra za kitumwa na za kimaskini; tukumbuke; siyo wote walioondoka Misri, walitoka kweli Misri! Kwani wengi bado walikuwa wanakumbuka Misri kwa mioyo yenye kuitamani; na wapo wanaotamani turudi kwenye ufisadi. Tukirudi tumekwisha; vinginevyo tunaweza tukajikuta tunatangatanga miaka arobaini!

Tujiandae kwa Deep Green, Tangold na Meremeta 2.0? Angalau Serikali inaonesha kushtushwa na kilichojaribiwa Wizara ya Fedha…


Niandikie:klhnews@gmail.com

Tuko pamoja kabisa ndugu yangu.
Umetaja watu hatari ambao licha ya kwamba wako jangwani, mioyo na akili zao bado zinaota Misri. Wanakumbuka matikiti maji, makoma manga, mapande ya nyama n.k. Lkn pia kuna wengine ambao wako jangwani, lkn wao kazi yao ni kufuata umati. Wenyewe wakisikia "kazi iendelee" kuelekea Kanaan kweli wanaongoza kuelekea nchi ya ahadi. Lkn pia wakisikia sauti za wale wanaokumbuka matikiti maji na mapande ya nyama wakinung'unika, nao bila kuwaza wamaanza kulia kwa sauti kubwa kuikumbuka Misri. Hawaeleweki wanataka nini, ama kwenda mji mpya au kurudi Misri. Lkn pia hawajui ya kuwa wale ambao wana mahaba na Misri walikuwa wakifaidika au kuwa na masilahi fulani huko. Lkn hawa fuata upepo wamekuwa wakiwaiga bila kujua sababu za kwa nini wanakumbuka mambo ya kale!! Ndivyo ilivyo kwa Tanzania, kuna wengine kipindi cha JPM walikuwa wakiiga mkumbo wa kulalamika bila kujua wale walioanzisha kulalamika kwa nini walifanya hivyo, pia walipoteza kitu gani kutokana na ule mfumo wa kale mpaka wanalalamikia mfumo mpya. Hawakujisumbua kujiuliza maswali hayo, wakabakia kulalamika tu, bila ya kujua kuwa wanatumika kama kikuza na kipaza sauti cha wanufaika wa mfumo wa kale.
Tuna tatizo la watu wengi tu kutokuwa na subira na kuzipa nafasi nafsi zao kabla ya kulaumu au kushutumu. Hilo sitalifafanua maana kila mmoja anajua. Wengi wetu tumeingia kwenye mtego huo wa kutamka tu jambo bila kujipa muda wa kutosha kuona mambo. Kwani wahenga walisema muda/wakati ni hakimu mzuri.

NB: Tabia ya ulalamishi na kunung'unika ni mbaya sana. Kama unakumbuka kunung'unika na lawama za waisraeli, ndizo zilizosababisha Musa kutoingia nchi ya ahadi. Naye alikufa jangwani. Hivyo kulaumu kuna athiri utendaji wa viongozi wetu.

CC: gwandumi Mwakatobe nakualika uje usikilize hadithi ya hadithi ya Musa na Waisraeli jangwani.
 
Na sio lazima tuone sisi, bali hata wajukuu wetu wataona tunayoyatamani.
Hiyo ndo "mindset" ya mtu tumuitae "mzungu".

Wazungu walijenga Ulaya kwa gharama na taabu nyingi na leo hii wametulia na wajukuu hawana shida ya maji, umeme wa uhakika, miundombinu imara na kila tukionacho Ulaya na Marekani kilitokana na mababu zao kutolea jasho na kutaabika.

Kwanza Ulaya au Marekani mtu hujiuliza mara mbili atachezea vipi mfumo wa umeme kama Luku, au mifumo ya kutoa mizigo bandarini au kule TRA (kama kweli kulitokea zengwe).

Si kama hayafanywi, lakini hutendwa katika maneo ya watumiaji. Kwa mfano wahalifu huweza kurekebisha kifaa cha umeme na kutolipa bili ya umeme ili kustawisha zao la bangi nyuma ya maeneo ya viwanda.

Lakini kutokana na mfumo imara huweza kugunduliwa na kukamatwa mara moja maana mfumo imara wa tehama huweza kugundua bili kubwa ya umeme kutoka katika nyumba au jengo fulani.

Sasa hiyo ni mifumo imara na iliyo thabiti.

Au mzungu atajiuliza aanzie wapi kwenda hazina kama ya Federal Reserve ya Marekani au Treasury ya Uingereza aingie na aandike hundi za kughushi na watu walipane malipo yasoeleweka?

Wajukuu na vitukuu vyetu vitakuwa na shida sana maana bado matatizo ya kufikiri nje ya boksi kwa sisi babu zao bado ni kitendawili.
 
View attachment 1800414
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya masimulizi ya kiimani ambayo yalinivutia sana tangu zamani ni safari ya wana wa Israeli kutoka Misri kwenda nchi ya ahadi wakiongozwa na Nabii Musa. Simulizi hili nimelisoma mara nyingi na kila ninapolisoma Napata mafunzo mapya. Hata hivyo mojawapo ya mafunzo ambayo naweza kutumia kuelezea siasa zetu za leo katika Tanzania ni ile tabia ya baadhi ya wana wa Israeli kulalamika lalamika kila mambo yalipokuwa magumu walipokuwa njiani.

Musa alipowajia wana wa Israeli na ujumbe kuwa kuna nchi ya ahadi inawangojea wengi walifurahia na kwa kweli walifuata maelezo yake yote na hata ile siku ya kutoka Misri jamii nzima walikuwa tayari kutoka. Wote walikuwa na hamu ya kwenda kule ambako hakuna utumwa, na kule ambapo wangekuwa hai. Waliambiwa nchi wanayoiendea ilikuwa inatiririka maziwa na asali (Kut. 3:8,17). Kwa kweli waliitamani sana hiyo nchi. Na waliondoka Misri wakifurahia kuwa wanaenda mahali ambapo watafurahia maisha kweli kweli.

Walipoondoka na kuvuka bahari ya shamu walishuhudia muujiza mkubwa wa bahari kufunguka na wao kupita kwenye nchi kavu. Lakini muujiza mkubwa ni jinsi gani majeshi ya farao yaliangamia na wana wa Israeli walikuwa wamevuka ng’ambo ya pili. Ukisoma kitabu cha Kutoka 15 utaona jinsi wana wa Israeli walivyoimba kwa shangwe wakifurahia jinsi walivyoona matendo makuu ya Mungu. Wana wa Israeli walipenda mabadiliko na mafanikio lakini hawakuwa tayari kulipa gharama.

Hili tunaliona kwenye sura mbili zinazofuatia tukio la wao kuvuka Bahari ya Shamu. Kwenye sura ya 16 na sura ya 17 tunakutana na wana wa Israeli baada ya kupata shida kidogo walipoanza kulalamika na kunung’unika. Walijisikia njaa kidogo wakaanza kukumbuka “masufuria ya nyama” waliyokuwa wakila kule utumwani Misri. Mara kadhaa katika safari yao walijikuwa wanakumbuka Misri na kutamani kurudi kule walikotoka kwa sababu walikuwa na uhakika wa kula kwao, kulala kwao – hata kama walikuwa utumwani!

Ndugu zangu, naomba kupendekeza kuwa kweli wapo Watanzania wanaotaka mabadiliko na maendeleo lakini pia wapo wengine ambao kwao mabadiliko ni lazima yawe rahisi, yasiyo na jasho na yasiyo na uchungu. Wanataka kuendelea bila kulia, wanataka kufanikiwa bila kuinama au kunyanyua! Hawa ndugu zetu miaka hii mitano kwao maisha yalikuwa magumu sana kiasi kwamba walianza kukumbuka “masufuria ya nyama”.

NI kweli maelfu walitoka Misri lakini Misri haikutoka mioyoni ma wengi katika Israeli. Hata ukisoma Qurani Tukufu utakutana na wana wa Israeli wakilalamika tena kuwa hawakuwa tayari kwenda kwenye nchi waliyoahidiwa kwa sababu walikuwa wanaogopa kuna majibut majabari kule. Kwamba, walimuambia Musa kuwa kama anataka wao waende kwenye hiyo nchi basi Musa na Mungu wake waende wakapigane na majitu hao wakati wao (wana wa Israeli) watakaa hapo hapo wakisubiria! Kwa mujibu wa Qurani hii ilikuwa ni sababu ya wana wa Israeli kuharamishwa kuingia nchi ya ahadi kwa miaka arobani wakibakia kutangatanga (Qurani 5:20-26).

Leo hii katika Tanzania wapo watu ambao wanajua kukatisha tamaa wengine; watu hawa wanabeza SGR kuwa haiwezekani; wanatuambia hatuwezi kuendelea bila kusaidiwa; wanatuambia sisi ni maskini na kuwa hatuwezi kabisa! Wanarudisha hofu na hali ya kutokujiamini miongoni mwetu na kwa bahati mbaya wapo ambao wanawaamini. Nikiri tu kuwa mojawapo ya vitu vilivyokuwa vinanipa moyo sana ni lugha ya kujiamini ya hayati Rais Magufuli. Kwa uzuri au kwa ubaya alikuwa anajiamini kupitiliza! Sidhani kama alikuwa na mazoea ya kutumia lugha ya “haiwezekani” au “hatuwezi”. Kwake yeye mengi yalikuwa ni mambo ya kuthubutu kuyafanya. Inawezekana hata sasa kuna watu hawakubali hatua mbalimbali anazochukua Rais Samia; na hawa nao wanaanza kuwa na wasiwasi kwa sababu hawaamini kuwa anaenda kuendelea kulisogeza taifa mbele.

Binafsi kwa wakati huu ninamuona Rais Samia kama Yoshua aliyechukua nafasi ya Musa. Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune walikuwa ni watu wawili ambao walileta taarifa ya kujiamini baada ya kwenda kupeleleza nchi ya ahadi. Wakati wenzao walirudi na taarifa ya kutisha ya kuwa nchi ya ahadi imejaa mijitu mikubwa kiasi kwamba wao walikuwa wadogo kama “panzi” Yoshua na Kalebu walisema hata kama hivyo ni kweli bado wao walikuwa wana uwezo wa kushinda. Yoshua hakuwa Musa na hakufanya mambo kama Musa; alijua jukumu lake lakini alienda kufanya vitu tofauti na Musa. Mama Samia – kama nilivyoeleza huko nyuma – si lazima afanye kila kitu kama Magufuli wala haitaji kuzungumza kama Magufuli; anajua ajenda anayoitekeleza na anajua Watanzania wanatarajia nini kwake.

Wakati umefika wa kuanza kuwakatalia wale wote ambao wanataka turudi kwenye maisha ya utawala wa kifisadi ambapo baadhi yetu walikuwa wanakesha kwenye masufuria ya nyama! Kibarua alicho nacho Rais Samia ni kuweza kujua ni kina nani hawa ambao wanaotamani turudi kwenye fikra za kitumwa na za kimaskini; tukumbuke; siyo wote walioondoka Misri, walitoka kweli Misri! Kwani wengi bado walikuwa wanakumbuka Misri kwa mioyo yenye kuitamani; na wapo wanaotamani turudi kwenye ufisadi. Tukirudi tumekwisha; vinginevyo tunaweza tukajikuta tunatangatanga miaka arobaini!

Tujiandae kwa Deep Green, Tangold na Meremeta 2.0? Angalau Serikali inaonesha kushtushwa na kilichojaribiwa Wizara ya Fedha…

Niandikie:klhnews@gmail.com
Kongole sana mkuu kwa andiko lako hili lililojaa mantiki na kufikirisha pia. Wajuzi wengi katika masuala ya "organisation behaviour" wanakubaliana kuwa "vision statement" ya kale kabisa katika kumbukumbu za kihistoria ni hii ya wana wa Israeli walipokuwa utumwani Misri, yaani kwa kuinukuu;

"Tuondoke Misri (utumwani) na tuelekee nchi mpya ya ahadi (Kaanani) iliyojaa maziwa na asali"

"Vision statement" ndiyo dira yenye kusimamia njozi ama ndoto ya matamanio ya jumuiya yoyote ile ambayo ipo kwenye mkwamo ama hitaji la wakati la kuhama kutoka hatua moja kwenye nyingine ya maendeleo. Ni vyema wahusika kwa pamoja wakashikamana na dhamira hiyo kupitia ktk umoja wao.

Ni kosa kubwa kwa wanajumuiya mmojamoja ama baadhi yao kwenda kinyume na dhamira hiyo. Ni usaliti kurudi nyuma ama kukwamisha wengine pale mnapoamua kuianza safari hiyo ya matamanio ili mkapate kufikia ndoto iliyokusidiwa yaani matokeo chanya (maziwa na asali).
 
Back
Top Bottom