FUNZO: Enyi vijana watafutaji mnaojiweza kiasi kiuchumi msizoeane kabisa na wenye nyumba wenu

FUNZO: Enyi vijana watafutaji mnaojiweza kiasi kiuchumi msizoeane kabisa na wenye nyumba wenu

Teslarati

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2019
Posts
2,621
Reaction score
10,466
Habari wana jamvi

Nimeona niweke huu uzi asubuhi sababu mida hii ndo wenye nyumba huwategeshea vijana wapangaji wao wanaoonekana kujiweza kdg kiuchumi na kuwaelezea shida zao ili wawasaidie.

Kuna dogo mmoja kumpa mwenye nyumba wake 30 au 20 ilikuaga kawaida. Siku mzee yule akamfuata dogo akamwambia kuwa mwanae kakosa ada, hivo amkopeshe laki 5 watakata kwenye kodi, dogo akasema laki tano hana muda ule ila akampa yule mzee laki tatu. Hadi kuombana ada ni sababu wameshawekeana mazoea ya kuombana hela.

Sasa miezi mitatu ilopita dogo aliumwa sana hadi akapewa likizo kazini kwake, kakaa pale na demu wake anauguzwa kwa miezi miwili hivi, hospitali wamezunguka sana so dogo kiuchumi akawa hayuko vizuri. Kinachofanya niandike huu uzi ni kwamba huyo mwenye nyumba kashindwa kumvumilia dogo miezi miwili tu amtafutie kodi yake.

Dem wa huyo dogo ni ndugu yangu wa mbali ndo alinitafuta nimsaidie na akanisimulia story nzima. Nimefika pale kwao juzi nikamuangalia yule mzee na alivyo hana aibu anasema eti "Wadogo zako wanakaa na mm vizuri, ni watu wazuri" lakini kumvumilia mgonjwa tu kodi, tena anaekusaidiaga imekua gumzo.

Vijana mnaoanza maisha epukeni kutoa misaada ya hovyo hasa kwa watu kama wenye nyumba wenu mlipopanga vyumba au fremu, hio sio roho mbaya bali ni kujielewa. Weka akiba kisha saidia unapoweza. Ukiwa 'nice guy' utatumika sana
 
Nafikiri ungewashauri vijana hivi;

Wajtahidi kupanga kwenye nyumba za watu wenye kipato cha ziada tofauti na hiyo nyumba anayopanga.
Namaanisha; kama umepanga kwenye nyumba ya mtu ambayo anategemea kodi yako ndio aendeshee maisha yake, ukweli hawezi kuvumilia zaidi ya mwezi kwani hana namna nyingine ya kuishi.

Kwa namna umeandika, huyo mwenye nyumba haonekani kuwa na Roho mbaya kiivyo, ila ni ugumu tu wa maisha unamsukuma kufanya hivyo; msamehe bure...

" najua vijana wakiwa singo hupenda kukaa nyumba moja na mwenye nyumba kwa sababu za usalama"
 
Nafikiri ungewashauri vijana hivi;
Wajtahidi kupanga kwenye nyumba za watu wenye kipato cha ziada tofauti na hiyo nyumba anayopanga.
Hio research mtu atafanya vp?

Na pia kuna wenye nyumba wana kazi zao, wengine waalimu lkn kila siku kulilia shida kwa wapangaji wao

Na hata kama shida ndo zimemfanya asimvumilie, tuwe na utu basi, mgonjwa unamwambia ahame na unampa wiki 2 kweli? Mie nimewaambia madogo watoke pale warudi makwao kwanza jamaa akapone, huyo mwenye nyumba hana utu, na ofcoz wengi hawana utu, ila wakija wanakuelezea shida zao wanajichekesha sana
 
Habari wana jamvi

Nimeona niweke huu uzi asubuhi sababu mida hii ndo wenye nyumba huwategeshea vijana wapangaji wao wanaoonekana kujiweza kdg kiuchumi na kuwaelezea shida zao ili wawasaidie.

Kuna dogo mmoja kumpa mwenye nyumba wake 30 au 20 ilikuaga kawaida. Siku mzee yule akamfuata dogo akamwambia kuwa mwanae kakosa ada, hivo amkopeshe laki 5 watakata kwenye kodi, dogo akasema laki tano hana muda ule ila akampa yule mzee laki tatu. Hadi kuombana ada ni sababu wameshawekeana mazoea ya kuombana hela.

Sasa miezi mitatu ilopita dogo aliumwa sana hadi akapewa likizo kazini kwake, kakaa pale na demu wake anauguzwa kwa miezi miwili hivi, hospitali wamezunguka sana so dogo kiuchumi akawa hayuko vizuri. Kinachofanya niandike huu uzi ni kwamba huyo mwenye nyumba kashindwa kumvumilia dogo miezi miwili tu amtafutie kodi yake. Dem wa huyo dogo ni ndugu yangu wa mbali ndo alinitafuta nimsaidie na akanisimulia story nzima. Nimefika pale kwao juzi nikamuangalia yule mzee na alivyo hana aibu anasema eti "Wadogo zako wanakaa na mm vizuri, ni watu wazuri" lakini kumvumilia mgonjwa tu kodi, tena anaekusaidiaga imekua gumzo.

Vijana mnaoanza maisha epukeni kutoa misaada ya hovyo hasa kwa watu kama wenye nyumba wenu mlipopanga vyumba au fremu, hio sio roho mbaya bali ni kujielewa. Weka akiba kisha saidia unapoweza. Ukiwa 'nice guy' utatumika sana
Kqbsa yaan hata mm mwenye nyumba akinifata kunidai hela ya umeme kabla ya tareh moja haijafka siwezi kumpa
anidai hela ya kodi kabla ya trh husika siwezi kumpa hata niwe na nayo ndani na akija nikopa siwez kumkopeaha hyo ndp principle yngu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya yalishanikuta kipindi napanga ,mwenye nyumba unampa kodi ya mwaka au miezi sita ,Wiki anakuomba laki mbili au tatu unampa ,Ukidhani kunsaidia naye atakusaidia ukikwama ,Ila hawa watu si watu wenye utu ,Urafiki wenu ukiwa unampa kodi yake kwa wakati ,ila ukikwama anasahau yote
 
Haya yalishanikuta kipindi napanga ,mwenye nyumba unampa kodi ya mwaka au miezi sita ,Wiki anakuomba laki mbili au tatu unampa ,Ukidhani kunsaidia naye atakusaidia ukikwama ,Ila hawa watu si watu wenye utu ,Urafiki wenu ukiwa unampa kodi yake kwa wakati ,ila ukikwama anasahau yote
Kaka inategemea..mm mwenye nyumba wangu usipompigia siku ya kodi anakuacha hata mwez mzima.
 
Kaka inategemea..mm mwenye nyumba wangu usipompigia siku ya kodi anakuacha hata mwez mzima.
Kumi kwa mmoja mzee ,na haya manyanyaso yao yamenipelekea kujenga kwangu haraka na kuhamia ,wengi ni watu wasiokuwa na Utu kabisa wala huruma ,Yaani huwa wanaona kila ambaye hajajenga hana akili ,Ila hawajui kila kitu kina muda wake
 
Muda mwingine hata wapangaji hukosa wema Kuna ndugu yangu alimpangisha mtu nyumba anaishi mkoa mwingine na nyumba iko mkoa mwingine akalipa kodi awamu ya kwanza na ya pili vizuri tu ilipofika awamu ya tatu akaanza danada a kuwa mambo hayaendi vizuri amvumilie yule mwenye nyumba akamvumilia mpaka miezi sita kumbe kipindi anasingizia ugumu wa mambo alikuwa anajenga kwake mwisho wa siku kilichofuata alihama kimya kimya bila hata kuaga na kumblock mwenye nyumba ikawa imeisha.Cha msingi uaminifu binadamu hatuna lkn pia unavyopata changamoto kutoka kwa wenye nyumba ndio iwe chachu ya wewe kupambana kujenga kwako sio kuendelea kupanga
 
Wewe unaongelea mwenye nyumba,Kuna kipindi Mimi nilikuwa naamua kumsaidia mtu hata kwa kujibana,Ila sahiz jibu langu ni Sina hata km Sina kweli
 
Back
Top Bottom