Uchaguzi 2020 Funzo nililolipata baada ya kupata 0 kwenye kura za maoni za udiwani CCM

Uchaguzi 2020 Funzo nililolipata baada ya kupata 0 kwenye kura za maoni za udiwani CCM

Sasa mkuu ajira yangu na udiwani kipi kina maslahi zaidi?
Unajua nivigumu mwanasiasa yeyote kukiri au kukubali kuwa kipaumbele cha kwanza chake ni malengo binafsi na pili kuwatumukia wananchi kama kipaumbele chake chamwisho.. Mfano kuacha ukuu wa mkoa nakuja kugombania ubunge . huhitaji akili kubwa kufumbua hili fumbo
 
Salamu zenu wakuu,

Kwa mara ya kwanza nami nikiwa Kama kijana nikatia nia ya kugombea udiwani kupitia CCM huko Katani kwetu.

Namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwangu kwa kunipa ninachostahili katika zoezi lile la kura za maoni zilizofanyika jana siku ya Jumamosi ya tarehe 25/07/2020.

Kwanza nilijitahidi kukutana na wajumbe kadhaa kuwaeleza dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia maana kata yet in changamoto sugu mno wapendwa,na hii Hali hivyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa diwani aliyekuwa akitetea kiti hana siasa zenye manufaa hata kidogo,kwa ufupi tu ni mzee,ameishia darasa la 4,si mzawa wa ile kata na mpaka sasa aslimia 80 ya shughuli na makazi yake yapo nje ya kata yetu.

Basi kwa kaelimu haka nilikopata nilamini kwamba kwa haka ka CV nilikonako basi nikirudi Kule nyumbani kuwa naamua kuiweka rehani ajira yangu kwa kuwaeleza hoja kisomi namna tunavyoguswa na changamoto za katani kwetu maana mkataa kwao ni mtumwa.

Basi kweli nikawaeleza wajumbe wengi tu wakifurahishwa na ujio na wakanipongeza Sana na wakasema hawataniangusha,basi nikawaamini na sikuona sababu ya kutoa rushwa nikiamini kuwa ukweli wangu na uadilifu mkubwa utanipa kura za kutosha kuliko wale wanaomwaga hela mtaani.

Kumbe nilikuwa najidanganya,wagombea tulikuwa 8,watatu tulikuwa watumishi wa umma,mmoja ni mstaafu,watatu ni Drs la 7 kwa elimu yao na mmoja aliishia Drs la 4(mgombea aliyekuwa anatetea nafasi yake)

Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Nimefurahi kupata hiyo 0 maana hata ningepata kura moja tu ingenisumbua kwa kuanza kujiuliza ni Nani aliyenipa hivyo Kila mmoja angekuja kinafiki kusema amenipigia yeye kumbe ni uongo.

Gharama zote nilizotumia katika mchakato huo nimechukulia kuwa ni sawa na kuwa nililipa ada ya kujifunza siasa kwa vitendo.

Sijavunjika Sana moyo na sirudi nyuma,dhamira ya kuwatumikia wananchi bado ipo hata kwa awamu nyingine huku nikisahihisha makosa yaliyonigharimu awamu hii,nitamuunga mkono yeyote atakayeteuliwa na chama,Wala sihami chama.

Wengi wamenipa pole lakini kiukomavu nimejibu kuwa wasinipe pole Bali hongera,ila pole hiyo itawarudia wao endapo wamepiga kura kinafiki kisa tu wamejazwa minoti na hivyo watakuwa wamesaliti matakwa ya wananchi lakini na endapo kweli wamepiga kura kwa uhalali basi nami naungana nao kwa baraka zote.

Kwa taarifa zilizopo sasa, jana ileile watu walianza kurudisha kadi za chama wanataka kuhamia CHADEMA. Wale wote waliopata kura nyingi Kila mtu alitengeneza kundi lake na hivyo linahatarisha sana uhai wa chama maana wananchi wanatoa kauli za kutotoa ushirikiano endapo yule diwani anayetetea nafasi akirudishwa kuwa mgombea maana hawaoni matunda yake kwa miaka yote 15 aliyotumikia. Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.

Hii ndiyo ndiyo siasa ilivyo, tukutane 2025.

Ni Mimi niyeyekuwa mtia nia Udiwani CCM.
Kata ya UHENGA
Jimbo & Wilaya ya Wanging'ombe
Mkoa NJOMBE.
Umeandika vzr Ila ulipochemsha Ni kusema diwani anayetetea kiti n
Sio mzawa wa kata yenu hii Ni lugha ya kibaguzi kwa sababu Maendeleo sio lazima yaletwe na mzawa wa pale,kuishi nje ya kata Sio hoja yenye mashiko kwa sababu tuna wabunge na madiwan hawaishi kwenye majimbo na kata zao Ila wanafanya kazi nzuri Sana.Wananchi wanataka hoja na mipango ya Maendeleo sio siasa za kibazazi et fulan sio mzawa
 
Umeandika vzr Ila ulipochemsha Ni kusema diwani anayetetea kiti n
Sio mzawa wa kata yenu hii Ni lugha ya kibaguzi kwa sababu Maendeleo sio lazima yaletwe na mzawa wa pale,kuishi nje ya kata Sio hoja yenye mashiko kwa sababu tuna wabunge na madiwan hawaishi kwenye majimbo na kata zao Ila wanafanya kazi nzuri Sana.Wananchi wanataka hoja na mipango ya Maendeleo sio siasa za kibazazi et fulan sio mzawa
Na bado nalisisitiza Hilo kuwa sio mzawa maana hata yeye mwenyewe alishanaswa mahali akizungumza huko kwao maelezo yanayotafsirika kwa kifupi kuwa yeye hajazaliwa katani kwetu na taarifa tulizipata vizuri kabisa.Lakini pia bado wapiga kura wakawa wanalisisitiza hilo.
 
Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.
Hii ni porojo tu. Hivi kweli mtoa mada unataka waachwe waliopigiwa kura uteuliwe wewe uliyepata sifuri? Kama hata ujanja wa kutoa rushwa umezidiwa na huyo wa darasa la saba, basi tafsiri yake Ni kwamba wewe una elimu lkn huna akili.

Kwenye michakato ya uchaguzi wanaoshinda ni wenye akili siyo wenye elimu.
 
Na bado nalisisitiza Hilo kuwa sio mzawa maana hata yeye mwenyewe alishanaswa mahali akizungumza huko kwao maelezo yanayotafsirika kwa kifupi kuwa yeye hajazaliwa katani kwetu na taarifa tulizipata vizuri kabisa.Lakini pia bado wapiga kura wakawa wanalisisitiza hilo.
Ndio maana ulipata zero kwa akili hii.Wewe mbona unafanya kazi sehem ambayo wewe sio mzawa? Rud ufanye hyo ajira kwenu
 
Nini kinakusukuma hadi uangaike hivo kwani kata yenu ni wewe tu? bilashaka ni tumbo.
 
Ndio maana ulipata zero kwa akili hii.Wewe mbona unafanya kazi sehem ambayo wewe sio mzawa? Rud ufanye hyo ajira kwenu
Sawa ndugu mjumbe,mwisho wa siku niliamua kuyaweka hadharani yaliyokuwa yakisemwa na wananchi kutuaminisha kuwa tunaweza kushinda kumbe walikuwa wanatuchora tu,mwisho wa siku sikuyaweka kwa ubaya,ila Kama Kama nilikosea kuyaweka au umenielewa vibaya basi uniwie radhi mkuu ili unijenge zaidi.
 
Shu
Hii ni porojo tu. Hivi kweli mtoa mada unataka waachwe waliopigiwa kura uteuliwe wewe uliyepata sifuri? Kama hata ujanja wa kutoa rushwa umezidiwa na huyo wa darasa la saba, basi tafairi yake Ni kwamba wewe una elimu lkn huna akili.

Kwenye michakato ya uchaguzi wanaoshinda ni wenye akili siyo wenye elimu.
Shukrani Sana kwa mchango wako.
 
Nini kinakusukuma hadi uangaike hivo kwani kata yenu ni wewe tu? bilashaka ni tumbo.
Tupo wengi,ila wasomi wengi wamekususa kwao na si kila mtu Ana wito Kama wangu.Na Sasa baada ya kukosa naendelea na ajira yangu.
 
Salamu zenu wakuu,

Kwa mara ya kwanza nami nikiwa Kama kijana nikatia nia ya kugombea udiwani kupitia CCM huko Katani kwetu.

Namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwangu kwa kunipa ninachostahili katika zoezi lile la kura za maoni zilizofanyika jana siku ya Jumamosi ya tarehe 25/07/2020.

Kwanza nilijitahidi kukutana na wajumbe kadhaa kuwaeleza dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia maana kata yet in changamoto sugu mno wapendwa,na hii Hali hivyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa diwani aliyekuwa akitetea kiti hana siasa zenye manufaa hata kidogo,kwa ufupi tu ni mzee,ameishia darasa la 4,si mzawa wa ile kata na mpaka sasa aslimia 80 ya shughuli na makazi yake yapo nje ya kata yetu.

Basi kwa kaelimu haka nilikopata nilamini kwamba kwa haka ka CV nilikonako basi nikirudi Kule nyumbani kuwa naamua kuiweka rehani ajira yangu kwa kuwaeleza hoja kisomi namna tunavyoguswa na changamoto za katani kwetu maana mkataa kwao ni mtumwa.

Basi kweli nikawaeleza wajumbe wengi tu wakifurahishwa na ujio na wakanipongeza Sana na wakasema hawataniangusha,basi nikawaamini na sikuona sababu ya kutoa rushwa nikiamini kuwa ukweli wangu na uadilifu mkubwa utanipa kura za kutosha kuliko wale wanaomwaga hela mtaani.

Kumbe nilikuwa najidanganya,wagombea tulikuwa 8,watatu tulikuwa watumishi wa umma,mmoja ni mstaafu,watatu ni Drs la 7 kwa elimu yao na mmoja aliishia Drs la 4(mgombea aliyekuwa anatetea nafasi yake)

Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Nimefurahi kupata hiyo 0 maana hata ningepata kura moja tu ingenisumbua kwa kuanza kujiuliza ni Nani aliyenipa hivyo Kila mmoja angekuja kinafiki kusema amenipigia yeye kumbe ni uongo.

Gharama zote nilizotumia katika mchakato huo nimechukulia kuwa ni sawa na kuwa nililipa ada ya kujifunza siasa kwa vitendo.

Sijavunjika Sana moyo na sirudi nyuma,dhamira ya kuwatumikia wananchi bado ipo hata kwa awamu nyingine huku nikisahihisha makosa yaliyonigharimu awamu hii,nitamuunga mkono yeyote atakayeteuliwa na chama,Wala sihami chama.

Wengi wamenipa pole lakini kiukomavu nimejibu kuwa wasinipe pole Bali hongera,ila pole hiyo itawarudia wao endapo wamepiga kura kinafiki kisa tu wamejazwa minoti na hivyo watakuwa wamesaliti matakwa ya wananchi lakini na endapo kweli wamepiga kura kwa uhalali basi nami naungana nao kwa baraka zote.

Kwa taarifa zilizopo sasa, jana ileile watu walianza kurudisha kadi za chama wanataka kuhamia CHADEMA. Wale wote waliopata kura nyingi Kila mtu alitengeneza kundi lake na hivyo linahatarisha sana uhai wa chama maana wananchi wanatoa kauli za kutotoa ushirikiano endapo yule diwani anayetetea nafasi akirudishwa kuwa mgombea maana hawaoni matunda yake kwa miaka yote 15 aliyotumikia. Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.

Hii ndiyo ndiyo siasa ilivyo, tukutane 2025.

Ni Mimi niyeyekuwa mtia nia Udiwani CCM.
Kata ya UHENGA
Jimbo & Wilaya ya Wanging'ombe
Mkoa NJOMBE.
Kwahiyo awamu zijazo nawe utatoa rushwa ama? Kumbuka mkono mtupu........
 
Mkuu pole sana, lakini nimetatizwa na sentensi yako kwamba "sijavunjika moyo, nitajaribu awamu nyingine huku nikisahisha makosa yaliyonigharimu awamu hii" mwisho wa kunukuu. Kwa maelezo yako makosa yaliyokugharimu ni kutokutoa rushwa na kutokuwa mnafiki.Kwahiyo unataka kutuambia awamu ijayo utatoa rushwa na kuwa mnafiki?
Nimewaza kama wewe
 
Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Yote matatu siyo mafunzo kwa sababu zifuatazo 🙁1) Uongozi mwingi kwenye CCM nunendana na Rushawa na kila mtu anyegombea alitakiwa alijue hilo (2) Unachota unfiki siyo kweli bali ni nguvu ya ushawisi; sisa siku zote zinahusisha unafiki (3) CV siyo jambo la muhimu sana katika shughuli zote za kisiasa. Utakuwa ulifanya makesa kuwaomba wapiga kura wako kwa kuwaambia wewe ni msomi kuliko wao. Angalia yaliyomkuta Mwakyembe; unatakiwa utumie elimu yako kujenga ushawishi
 
Ushukuru kama hujachomolewa kwenye payroll,

Ila kaa standby waweza futwa any time.

Hii ya kusema ki cv mara ki elimu pia ni sababu kuwa hata wewe hujiamini. Ona std iv anakugalagaza.

Wenzio licha ya rushwa pia wanaroga wengine wanatoa pia matambiko.

Fanyeni kazi ikija kutokea automatically umeingia siasa itokee tu.

Mbona hamriziki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua naweza kukuambia kuwa siasa za nchi za dunia ya 3 nikama kichochoro cha watu flani kwaajili ya mambo flani, namaanisha kuwa huku ndio viongozi huwatapeli wananchi ya kutowatendea haki kama kusaini mikataba mibovu. Na kiongozi ni mfano mzuri kama baba wa familia ambaye hayuko tayari kuona familia inapata taabu sasa ni viongozi wangapi ambao wakimaliza uongozi wao wanawaachia wananchi stress za madeni mikataba mibovu n.k

Unaonyesha kuwa unaamini siasa ndio mafanikio yako ,yani hapa tayari umeshaanza waibia wananchi hata kabla hawajakuchagua

Sasa mkuu ajira yangu na udiwani kipi kina maslahi zaidi?
 
Back
Top Bottom