Uchaguzi 2020 Funzo nililolipata baada ya kupata 0 kwenye kura za maoni za udiwani CCM

Uchaguzi 2020 Funzo nililolipata baada ya kupata 0 kwenye kura za maoni za udiwani CCM

Salamu zenu wakuu,

Kwa mara ya kwanza nami nikiwa Kama kijana nikatia nia ya kugombea udiwani kupitia CCM huko Katani kwetu.

Namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwangu kwa kunipa ninachostahili katika zoezi lile la kura za maoni zilizofanyika jana siku ya Jumamosi ya tarehe 25/07/2020.

Kwanza nilijitahidi kukutana na wajumbe kadhaa kuwaeleza dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia maana kata yet in changamoto sugu mno wapendwa,na hii Hali hivyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa diwani aliyekuwa akitetea kiti hana siasa zenye manufaa hata kidogo,kwa ufupi tu ni mzee,ameishia darasa la 4,si mzawa wa ile kata na mpaka sasa aslimia 80 ya shughuli na makazi yake yapo nje ya kata yetu.

Basi kwa kaelimu haka nilikopata nilamini kwamba kwa haka ka CV nilikonako basi nikirudi Kule nyumbani kuwa naamua kuiweka rehani ajira yangu kwa kuwaeleza hoja kisomi namna tunavyoguswa na changamoto za katani kwetu maana mkataa kwao ni mtumwa.

Basi kweli nikawaeleza wajumbe wengi tu wakifurahishwa na ujio na wakanipongeza Sana na wakasema hawataniangusha,basi nikawaamini na sikuona sababu ya kutoa rushwa nikiamini kuwa ukweli wangu na uadilifu mkubwa utanipa kura za kutosha kuliko wale wanaomwaga hela mtaani.

Kumbe nilikuwa najidanganya,wagombea tulikuwa 8,watatu tulikuwa watumishi wa umma,mmoja ni mstaafu,watatu ni Drs la 7 kwa elimu yao na mmoja aliishia Drs la 4(mgombea aliyekuwa anatetea nafasi yake)

Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Nimefurahi kupata hiyo 0 maana hata ningepata kura moja tu ingenisumbua kwa kuanza kujiuliza ni Nani aliyenipa hivyo Kila mmoja angekuja kinafiki kusema amenipigia yeye kumbe ni uongo.

Gharama zote nilizotumia katika mchakato huo nimechukulia kuwa ni sawa na kuwa nililipa ada ya kujifunza siasa kwa vitendo.

Sijavunjika Sana moyo na sirudi nyuma,dhamira ya kuwatumikia wananchi bado ipo hata kwa awamu nyingine huku nikisahihisha makosa yaliyonigharimu awamu hii,nitamuunga mkono yeyote atakayeteuliwa na chama,Wala sihami chama.

Wengi wamenipa pole lakini kiukomavu nimejibu kuwa wasinipe pole Bali hongera,ila pole hiyo itawarudia wao endapo wamepiga kura kinafiki kisa tu wamejazwa minoti na hivyo watakuwa wamesaliti matakwa ya wananchi lakini na endapo kweli wamepiga kura kwa uhalali basi nami naungana nao kwa baraka zote.

Kwa taarifa zilizopo sasa, jana ileile watu walianza kurudisha kadi za chama wanataka kuhamia CHADEMA. Wale wote waliopata kura nyingi Kila mtu alitengeneza kundi lake na hivyo linahatarisha sana uhai wa chama maana wananchi wanatoa kauli za kutotoa ushirikiano endapo yule diwani anayetetea nafasi akirudishwa kuwa mgombea maana hawaoni matunda yake kwa miaka yote 15 aliyotumikia. Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.

Hii ndiyo ndiyo siasa ilivyo, tukutane 2025.

Ni Mimi niyeyekuwa mtia nia Udiwani CCM.
Kata ya UHENGA
Jimbo & Wilaya ya Wanging'ombe
Mkoa NJOMBE.
.
Wasikupe pole bali hongera kwa kujaribu. I like your attitude.. Utafika mbali mzee
 
.
Wasikupe pole bali hongera kwa kujaribu. I like your attitude.. Utafika mbali mzee
Nashukuru Sana mkuu kwa kunitia moyo.
Mkuu ukiona umepata hiyo kura ujue kwanza siasa unailazimisha , pili hata ukishinda uko kwa personal interest zaid, na hautakuwa pale to serve wapigakura wako
Kwanini umeniona nipo kwa pesrsonal interests mkuu? Funguka nijirekebishe maana maana sipendi nionwe hivyo wakati Sina uchu huo wa madaraka zaidi ya dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia wananchi na ndiyo maana utaona nimeipokea hiyo sifuri kwa mikono miwili kuliko ningepata hata kura moja.
 
Hahaaaaa,na wewe imekukuta?


Mimi na wasomi wenzangu tuliunda kundi la vijana na tukasajili Halmashauri.

Tukagombea nafasi mbalimbali ikiwemo kujaza nafasi za kamati ya siasa ya tawi, Halmashauri Kuu ya Tawi, EMAU na n.k.

Yale majina yalipelekwa kata.

Kata wakafanya udadisi wakagundua kuwa Katibu wa Tawi ni kijana na yupo upande wetu.

Wakamtumbua Katibu.

Kwa hasira uongozi mzima kuanzia mwenyekiti wa Tawi na jumuia zake wakajiuzulu.

Akaja kaimu Katibu akafuta mchakato wa uchaguzi ule tukachukua fomu tena ila tukafyekelewa mbali.

Nikagundua tatizo pale.

Kundi letu likagawiwa hela ila pesa ile milion 5 ikaingizwa kwenye kundi katika mtaa ule linasadikika ni la 'wajumbe'.

Kimsingi ukitaka kujua siasa za CCM wewe shiriki shughuli za chama ngazi ndogo tu ya Tawi utajua kila kitu.

Nilichoka sana.

Kumbe jamaa walihisi ujio wa wasomi ni hatari maana maamuzi tungefanya sisi na ushawishi pia.

Kimsingi Kama ulikuwa hujui ujumbe unarithishwa Kama ufalme.

Baba akifa anamwachia mtoto au mke katika baadhi ya maeneo.

Kuna jamaa zangu waligombea mwaka huu hawataki hata kunijibu imekuwaje.

Wajumbe ni wazuri kwa hulka na maongezi ya bashasha ila sasa kinyume chake ndiyo hivyo yaani Ni Wana usalama fulani na Wana Siri hatari.
 
Mkuu mpaka unapata 0 hukukumbuka hata kujipigia wewe mwenyewe?
 
Mimi na wasomi wenzangu tuliunda kundi la vijana na tukasajili Halmashauri.

Tukagombea nafasi mbalimbali ikiwemo kujaza nafasi za kamati ya siasa ya tawi, Halmashauri Kuu ya Tawi, EMAU na n.k.

Yale majina yalipelekwa kata.

Kata wakafanya udadisi wakagundua kuwa Katibu wa Tawi ni kijana na yupo upande wetu.

Wakamtumbua Katibu.

Kwa hasira uongozi mzima kuanzia mwenyekiti wa Tawi na jumuia zake wakajiuzulu.

Akaja kaimu Katibu akafuta mchakato wa uchaguzi ule tukachukua fomu tena ila tukafyekelewa mbali.

Nikagundua tatizo pale.

Kundi letu likagawiwa hela ila pesa ile milion 5 ikaingizwa kwenye kundi katika mtaa ule linasadikika ni la 'wajumbe'.

Kimsingi ukitaka kujua siasa za CCM wewe shiriki shughuli za chama ngazi ndogo tu ya Tawi utajua kila kitu.

Nilichoka sana.

Kumbe jamaa walihisi ujio wa wasomi ni hatari maana maamuzi tungefanya sisi na ushawishi pia.

Kimsingi Kama ulikuwa hujui ujumbe unarithishwa Kama ufalme.

Baba akifa anamwachia mtoto au mke katika baadhi ya maeneo.

Kuna jamaa zangu waligombea mwaka huu hawataki hata kunijibu imekuwaje.

Wajumbe ni wazuri kwa hulka na maongezi ya bashasha ila sasa kinyume chake ndiyo hivyo yaani Ni Wana usalama fulani na Wana Siri hatari.
Na hii ni kwa Tanzania nzima yaani inachekesha Sana baada ya kuhuzunisha.

Fikiri Mimi kaka yangu aliyeniachia ziwa ndiyo mwenyekiti wa kijiji chetu Sasa lakini hakunipa kura,Kuna shemeji yangu mmoja kaoa dada yangu aliyemuachia ziwa huyu kaka yangu mwenyekiti lakini hakunipa kura,Kuna mjumbe mmoja alikuwa kwenye foleni akinipa tabasamu na Mimi nikawa nafurahia kuwa kura yangu hii maana tulizungumza mengi Sana kabla ya mchakato kumbe ndo anaenda kunichinjilia huko.

Mgombea mwenzangu mmoja naye mwajiriwa mjumbe mmoja ni mpwa wake kabisa,wawili ni wakwe zake hivyo akawa anahesabia kuwa ni kura zake ajabu alipata kura moja aliyojipigia yeye mwenyewe maana alikuwa ni mjumbe.

Sasa msikilize Steve Nyere ndo unacheka balaa alichofanyiwa.
 
Wajumbe , hawasikilizi hotuba yako ya kujinadi.

Kweli umejilipia kujifunza siasa, sasa yule atakayeteuliwa wewe jipendekeze kuwa mshirika wake.

Piga kampeni za nguvu kumnadi hiyo ndiyo njia ya kujitambulisha kwa wananchi.
 
Wajumbe , hawasikilizi hotuba yako ya kujinadi.

Kweli umejilipia kujifunza siasa, sasa yule atakayeteuliwa wewe jipendekeze kuwa mshirika wake.

Piga kampeni za nguvu kumnadi hiyo ndiyo njia ya kujitambulisha kwa wananchi.
Na nimeahidi kufanya hivyo bila kinyongo.
 
Hapo
Na nimeahidi kufanya hivyo bila kinyongo.
Hapo sasa ndo unajiwekea hazina uchaguzi ujao.

Usisahau takrima mdogomdogo, madaftari kwa wanafunzi, penseli ,ufutio gawa mwenyewe kwa wanafunzi hao ni watoto wa wajumbe salamu zinafika.
 
Na hii ni kwa Tanzania nzima yaani inachekesha Sana baada ya kuhuzunisha.

Fikiri Mimi kaka yangu aliyeniachia ziwa ndiyo mwenyekiti wa kijiji chetu Sasa lakini hakunipa kura,Kuna shemeji yangu mmoja kaoa dada yangu aliyemuachia ziwa huyu kaka yangu mwenyekiti lakini hakunipa kura,Kuna mjumbe mmoja alikuwa kwenye foleni akinipa tabasamu na Mimi nikawa nafurahia kuwa kura yangu hii maana tulizungumza mengi Sana kabla ya mchakato kumbe ndo anaenda kunichinjilia huko.

Mgombea mwenzangu mmoja naye mwajiriwa mjumbe mmoja ni mpwa wake kabisa,wawili ni wakwe zake hivyo akawa anahesabia kuwa ni kura zake ajabu alipata kura moja aliyojipigia yeye mwenyewe maana alikuwa ni mjumbe.

Sasa msikilize Steve Nyere ndo unacheka balaa alichofanyiwa.
[emoji23][emoji23][emoji23] wajumbe mwaka huu sio walirogwa na Nani wamekula hela za wengi na wakawatosa nadhani mpaka warogwe
 
Kali kuliko you're majibu ya wajumbe was ccm kwa wagombea ,wakiulizwa mtanipa kura kura? Wanajibu tuko pamoja kuja kuhesabu kura unaambulia 0.
 
Salamu zenu wakuu,

Kwa mara ya kwanza nami nikiwa Kama kijana nikatia nia ya kugombea udiwani kupitia CCM huko Katani kwetu.

Namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwangu kwa kunipa ninachostahili katika zoezi lile la kura za maoni zilizofanyika jana siku ya Jumamosi ya tarehe 25/07/2020.

Kwanza nilijitahidi kukutana na wajumbe kadhaa kuwaeleza dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia maana kata yet in changamoto sugu mno wapendwa,na hii Hali hivyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa diwani aliyekuwa akitetea kiti hana siasa zenye manufaa hata kidogo,kwa ufupi tu ni mzee,ameishia darasa la 4,si mzawa wa ile kata na mpaka sasa aslimia 80 ya shughuli na makazi yake yapo nje ya kata yetu.

Basi kwa kaelimu haka nilikopata nilamini kwamba kwa haka ka CV nilikonako basi nikirudi Kule nyumbani kuwa naamua kuiweka rehani ajira yangu kwa kuwaeleza hoja kisomi namna tunavyoguswa na changamoto za katani kwetu maana mkataa kwao ni mtumwa.

Basi kweli nikawaeleza wajumbe wengi tu wakifurahishwa na ujio na wakanipongeza Sana na wakasema hawataniangusha,basi nikawaamini na sikuona sababu ya kutoa rushwa nikiamini kuwa ukweli wangu na uadilifu mkubwa utanipa kura za kutosha kuliko wale wanaomwaga hela mtaani.

Kumbe nilikuwa najidanganya,wagombea tulikuwa 8,watatu tulikuwa watumishi wa umma,mmoja ni mstaafu,watatu ni Drs la 7 kwa elimu yao na mmoja aliishia Drs la 4(mgombea aliyekuwa anatetea nafasi yake)

Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Nimefurahi kupata hiyo 0 maana hata ningepata kura moja tu ingenisumbua kwa kuanza kujiuliza ni Nani aliyenipa hivyo Kila mmoja angekuja kinafiki kusema amenipigia yeye kumbe ni uongo.

Gharama zote nilizotumia katika mchakato huo nimechukulia kuwa ni sawa na kuwa nililipa ada ya kujifunza siasa kwa vitendo.

Sijavunjika Sana moyo na sirudi nyuma,dhamira ya kuwatumikia wananchi bado ipo hata kwa awamu nyingine huku nikisahihisha makosa yaliyonigharimu awamu hii,nitamuunga mkono yeyote atakayeteuliwa na chama,Wala sihami chama.

Wengi wamenipa pole lakini kiukomavu nimejibu kuwa wasinipe pole Bali hongera,ila pole hiyo itawarudia wao endapo wamepiga kura kinafiki kisa tu wamejazwa minoti na hivyo watakuwa wamesaliti matakwa ya wananchi lakini na endapo kweli wamepiga kura kwa uhalali basi nami naungana nao kwa baraka zote.

Kwa taarifa zilizopo sasa, jana ileile watu walianza kurudisha kadi za chama wanataka kuhamia CHADEMA. Wale wote waliopata kura nyingi Kila mtu alitengeneza kundi lake na hivyo linahatarisha sana uhai wa chama maana wananchi wanatoa kauli za kutotoa ushirikiano endapo yule diwani anayetetea nafasi akirudishwa kuwa mgombea maana hawaoni matunda yake kwa miaka yote 15 aliyotumikia. Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.

Hii ndiyo ndiyo siasa ilivyo, tukutane 2025.

Ni Mimi niyeyekuwa mtia nia Udiwani CCM.
Kata ya UHENGA
Jimbo & Wilaya ya Wanging'ombe
Mkoa NJOMBE.
Mkuu acha ujivuni,kwani kuwa diwani lazima uwe msomi,na je hizo ndio sifa zinazotakiwa kuwa diwani,kumbuka hao hao wa darasa la nne ndio wapiga kura,wanawajua nyie wasomi kwa kuleta mbwembwe za kijinga, kuna mheshimiwa mmoja ni waziri kaporomka,alipokuwa kwenye kijiji kimoja akawa anajinasibu kwa mengi ya kitoto oh mara mimi ni tajiri,mimi nina pesa ,nina magorofa huko Dar,sasa kikaja kipindi cha maswali akaulizwa mh tulikusikia ukijinasibu kuwa wewe ni tajiri na maneno mengi je utajirika wako sisi unatusaidia nini?na kama tajiri huku unafuata nini?akaishia kufoka na kudai wewe wa darasa la pili unataka uniambie nini, matokeo akaangukia pua.
 
Salamu zenu wakuu,

Kwa mara ya kwanza nami nikiwa Kama kijana nikatia nia ya kugombea udiwani kupitia CCM huko Katani kwetu.

Namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwangu kwa kunipa ninachostahili katika zoezi lile la kura za maoni zilizofanyika jana siku ya Jumamosi ya tarehe 25/07/2020.

Kwanza nilijitahidi kukutana na wajumbe kadhaa kuwaeleza dhamira yangu ya dhati ya kuwatumikia maana kata yet in changamoto sugu mno wapendwa,na hii Hali hivyo kutokana na ukweli usiopingika kuwa diwani aliyekuwa akitetea kiti hana siasa zenye manufaa hata kidogo,kwa ufupi tu ni mzee,ameishia darasa la 4,si mzawa wa ile kata na mpaka sasa aslimia 80 ya shughuli na makazi yake yapo nje ya kata yetu.

Basi kwa kaelimu haka nilikopata nilamini kwamba kwa haka ka CV nilikonako basi nikirudi Kule nyumbani kuwa naamua kuiweka rehani ajira yangu kwa kuwaeleza hoja kisomi namna tunavyoguswa na changamoto za katani kwetu maana mkataa kwao ni mtumwa.

Basi kweli nikawaeleza wajumbe wengi tu wakifurahishwa na ujio na wakanipongeza Sana na wakasema hawataniangusha,basi nikawaamini na sikuona sababu ya kutoa rushwa nikiamini kuwa ukweli wangu na uadilifu mkubwa utanipa kura za kutosha kuliko wale wanaomwaga hela mtaani.

Kumbe nilikuwa najidanganya,wagombea tulikuwa 8,watatu tulikuwa watumishi wa umma,mmoja ni mstaafu,watatu ni Drs la 7 kwa elimu yao na mmoja aliishia Drs la 4(mgombea aliyekuwa anatetea nafasi yake)

Baada ya kura za maoni matokeo yakawa kama ifuatavyo:

- Anayetetea kura 23 (Drs la 4)
- Wa pili kura 22 (elimu VII)
- Watatu kura 14(elimu VII)
- Wa nne kura 1(mwajiriwa) nayo alijipigia mwenyewe kwa sababu ni mjumbe.
- Wa tano kura 0 (elimu VII)
- Mstaafu kura 0.
- Mimi na mwenzangu kura 0 (vijana wasomi na waajiriwa)

Wapiga kura walikuwa 63, kura tatu ziliharibika.

FUNZO NILILOLIPATA
1. Katika kugombea kitu Cha kwanza ni MTAJI WA FEDHA KWA AJILI YA RUSHWA.
2. Jambo la pili ni UNAFIKI.
3. CV ni na ukweli ni Jambo la ziada tu.

Nimefurahi kupata hiyo 0 maana hata ningepata kura moja tu ingenisumbua kwa kuanza kujiuliza ni Nani aliyenipa hivyo Kila mmoja angekuja kinafiki kusema amenipigia yeye kumbe ni uongo.

Gharama zote nilizotumia katika mchakato huo nimechukulia kuwa ni sawa na kuwa nililipa ada ya kujifunza siasa kwa vitendo.

Sijavunjika Sana moyo na sirudi nyuma,dhamira ya kuwatumikia wananchi bado ipo hata kwa awamu nyingine huku nikisahihisha makosa yaliyonigharimu awamu hii,nitamuunga mkono yeyote atakayeteuliwa na chama,Wala sihami chama.

Wengi wamenipa pole lakini kiukomavu nimejibu kuwa wasinipe pole Bali hongera,ila pole hiyo itawarudia wao endapo wamepiga kura kinafiki kisa tu wamejazwa minoti na hivyo watakuwa wamesaliti matakwa ya wananchi lakini na endapo kweli wamepiga kura kwa uhalali basi nami naungana nao kwa baraka zote.

Kwa taarifa zilizopo sasa, jana ileile watu walianza kurudisha kadi za chama wanataka kuhamia CHADEMA. Wale wote waliopata kura nyingi Kila mtu alitengeneza kundi lake na hivyo linahatarisha sana uhai wa chama maana wananchi wanatoa kauli za kutotoa ushirikiano endapo yule diwani anayetetea nafasi akirudishwa kuwa mgombea maana hawaoni matunda yake kwa miaka yote 15 aliyotumikia. Wote watatu walitoa Sana rushwa ima walizidiana viwango.

Hii ndiyo ndiyo siasa ilivyo, tukutane 2025.

Ni Mimi niyeyekuwa mtia nia Udiwani CCM.
Kata ya UHENGA
Jimbo & Wilaya ya Wanging'ombe
Mkoa NJOMBE.
KUMBESOL JNAIJUÀ MSITUMALIZIE.MB ZETU
KAJIPANGE
1) 2025 UWE NA FEDHA ZA RUSHWA A KUTOSHA
2))JIFUNZE UNAFIKI...HILI SIKUTARAJIA LIMEKUSHINDA

MAANA MA.MC WENGI WANASIFIKA KWA UNAFIKI ILI KAZI ZAO ZIENDELEE HAPO TAFUTA MKONGWE AKUSAIDIE UNAFIKI GAN UNATAKIWA

3))HILII NDILOO LINAWAMALIZA WENGI SIASA N LAZIMA UCHAGUE.MAWILI KUWA NA MUNGU MPAKA.MWISHO AMA.KUWA NA SHETAN😁😁😁

UWEZI KUSALI NA KUTOA RUSHWA UKATEGEMEA UTASHINDA

WENZENU WANASHINDA WAMEJIKITA.MAZIMA.UPANDE WAPILI

UKIWA VUGUVUGU UNAISHA MAZIMA KWENYE SIASA HILI USILISAHAU 2025
KILA.LA KHERI MPWAAA
 
Back
Top Bottom