Pre GE2025 Gambo: Mkuu wa Wilaya asinichokonoe, ameshindwa kuwasimamia Wataalamu, aache kumsingizia Mbunge

Pre GE2025 Gambo: Mkuu wa Wilaya asinichokonoe, ameshindwa kuwasimamia Wataalamu, aache kumsingizia Mbunge

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731

Gambo amuonya Mkuu wa wilaya mbele ya Makonda, asema ameshindwa kazi

Kuna kiongozi mmoja, alisema eti mambo hayaendi kwasababu ya mgogogro wa mbunge, Baraza la Madiwani na Wataalamu, haya mlioyaona kuna sehemu mbunge anaingia hapo? Mkuu wa Mkoa kwa kuridhika na kazi yako nimetulia naomba wasinikchokonoe wasinifatefate na watimize wajibu wao.

Mkuu wa Wilaya alitakiwa akwambie kwa nini kwake mambo hayaendi, asimsingizie mbunge mimi siyomtendaji wa serikali mimi ni mwakilishi wa wananchi, hiyo ni ishara kuwa ameshindwa kuwasimimamia wataalamu ndio maana mkuu wa mkoa leo unafanya kazi kwenye wilaya mambo yote anatakiwa yeye awe ameyamaliza.

Kwa hiyo naomba Mkuu wa wilaya mimi namuheshimu sana na nimejitahidi kumkwepa kwenye kazi zake kwa sababu nataka amani kwenye jimbo letu nataka maendeleo asinichokonoe kwa sababu sina mpango wa kugombana naye. na asinilazimishe kugombana naye.

Mkuu wa Mkoa nakuunga mkono kwenye kazi unayofanya ya kupambana na wezi kupambana na mafisadi, kazi ya kupambanan na wavivu tunaopata hasara ni sisi mimi na madiwani na wenyekiti wa serikali za mtaa na Maraisi mambo yasipokwenda haya tutakaopata hasara ni sisi tutawenda kuomba kura kwa wananchi.

Nilipokuwa nasema Arusha kuna wizi, Arusha ni shamba la bibi, Arusha mambo haaendi walikuwa wanasema gambo ni mbaya, sasa leo amekaja kiboko yao. Nami naungana na kabisa na wewe unaposimamia haki, unaposimamia ukweli utapigwa vita na majungu kwenye kila kona ya nchi, lakini wanaosimamia haki mlinzi wao huwa ni Mungu na wala siyo binadamu.

Pia soma: Mkuu wa Wilaa Arusha: Migogoro baina a Baraza, menejimenti na mbunge inadhoofisha utoaji huduma au miradi ya maendeleo kwa wananchi
 
Mbunge mwenyewe ni sehemu ya Baraza la Madiwani ambalo lilitakiwa kutekeleza miradi, lakini halijatekeleza, sasa anamgeukia Mkuu wa Wilaya ambaye sio sehemu ya Baraza la Madiwani. Na hapokei fedha za maendeleo katika ofisi yake.

Madiwani ndio wanatakiwa kusimamia watendaji, sio Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya anaingia tu pale inapohitajika, Madiwani ni sawa na Bunge. Bahati mbaya yamekutana mapopoma mawili yanajaribu kufufuana kisiasa.

Kwa hiyo Gambo haelewi maana ya ugatuzi wa madaraka? Madaraka yako kwa wananchi kupitia Halmashauri zao.
 
MAKONDA BOMAYEEE, ,......wape kazi wavivu
Screenshot_20231102_120808_Remix.png
 
Wote waache u chokochoko!! Huwezi kuwa mbunge alafu kutwa unagombana na viongozi wenzio miradi haiendi kwanini naninyi ndiyo madiwani??

Mbunge hafai
 
Hakika Serikali yetu kwa kiasi kikubwa inaangushwa na watenda kazi,hawatimizi wanakwamisha wananchi mwananchi mmoja mmoja wanakwamisha maendeleo ya Taifa kwa ujumla
 
Back
Top Bottom