Pre GE2025 Gambo: Mkuu wa Wilaya asinichokonoe, ameshindwa kuwasimamia Wataalamu, aache kumsingizia Mbunge

Pre GE2025 Gambo: Mkuu wa Wilaya asinichokonoe, ameshindwa kuwasimamia Wataalamu, aache kumsingizia Mbunge

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
DC anatakiwa afahamu mkuu wa mkoa na mmbunge ni washikaji kitambo toka wanajitafuta wakiwa CCM.

Mmoja hapo alienda azima suit ya harusi kwa mwenzake wote wakiwa apeche alolo; majungu ya mmbunge kwa mkuu wa mkoa ni sawa kumchomea Mchengerwa kwa ‘bi-tozo’.

Imenikumbusha msanii mmoja marekani zama hizo kaenda kutafuta deal la label yake iwe chini ya Columbia Records amekutana na president anamwaga sera zake tunataka kuwa wakubwa kushinda So-So def records, kwanza Jermaine Dupri is overrated na kamsagia humo ndani.

Jamaa mkutano umeisha karudi kwa washakaji zake anawaadithia jinsi president alivyokuwa anamsikiliza kwa makini anadhani watapatq deal lao la label, washkaji zake wakamwambia huyo president Columbia records ‘Michael Mauldin’ ndio baba yake mzazi Jermaine Dupri kama umempondo hivyo mtoto wake sahau ilo deal.
 

Gambo amuonya Mkuu wa wilaya mbele ya Makonda, asema ameshindwa kazi

Kuna kiongozi mmoja, alisema eti mambo hayaendi kwasababu ya mgogogro wa mbunge, Baraza la Madiwani na kila kona ya nchi, lakini wanaosimamia haki mlinzi wao huwa ni Mungu na wala siyo binadamu.
Hapo kwenye kuchokonolewa tu.
 
DC anatakiwa afahamu mkuu wa mkoa na mmbunge ni washikaji kitambo toka wanajitafuta wakiwa CCM.

Mmwakamwambia huyo president Columbia records ‘Michael Mauldin’ ndio baba yake mzazi Jermaine Dupri kama umempondo hivyo mtoto wake sahau ilo deal.
Nimeipenda hii!, haswa hiyo ya kutaka kumchonganisha baba na mwana, kwa kuichonganisha record label ya baba na mwana, Columbia Records ya Michael Mauldin ambaye ni baba mtu, na Def Jam Records ya Jermaine Dupri ambaye ni mwanae!. Thanks for this, I didn't know this!.

Baada ya Makonda kuletwa Arusha, Lema, Gambo na Ole Sambaya, wanajitafakari sana kuhusu ubunge wa 2025!, kama Konda Boy aliachia mkoa wa Dar kugombea Ubunge, akidumu Arachuga hadi 2025, akaamua kutinga mjengoni kutokea Arusha, Lema, Gambo na Ole Sambaya hawana chao!.
P
 
Nimeipenda hii!, haswa hiyo ya kutaka kumchonganisha baba na mwana, kwa kuichonganisha record label ya baba na mwana, Columbia Records ya Michael Mauldin ambaye ni baba mtu, na Def Jam Records ya Jermaine Dupri ambaye ni mwanae!. Thanks for this, I didn't know this!.
!.
P
Makonda na Gambo ni ndugu wa kufikia.

Gambo ndio alimuazima suti yake Makonda siku ya harusi yake.

Ndio maana kapewa mic hapo amsute DC mbele ya wananchi, wanajuana hao kitambo; walishawahi simulia historia yao wote wakiwa wakuu wa mikoa.
 

Gambo amuonya Mkuu wa wilaya mbele ya Makonda, asema ameshindwa kazi

Kuna kiongozi mmoja, alisema eti mambo hayaendi kwasababu ya mgogogro wa mbunge, Baraza la Madiwani na Wataalamu, haya mlioyaona kuna sehemu mbunge anaingia hapo? Mkuu wa Mkoa kwa kuridhika na kazi yako nimetulia naomba wasinikchokonoe wasinifatefate na watimize wajibu wao.

Mkuu wa Wilaya alitakiwa akwambie kwa nini kwake mambo hayaendi, asimsingizie mbunge mimi siyomtendaji wa serikali mimi ni mwakilishi wa wananchi, hiyo ni ishara kuwa ameshindwa kuwasimimamia wataalamu ndio maana mkuu wa mkoa leo unafanya kazi kwenye wilaya mambo yote anatakiwa yeye awe ameyamaliza.

Kwa hiyo naomba Mkuu wa wilaya mimi namuheshimu sana na nimejitahidi kumkwepa kwenye kazi zake kwa sababu nataka amani kwenye jimbo letu nataka maendeleo asinichokonoe kwa sababu sina mpango wa kugombana naye. na asinilazimishe kugombana naye.

Mkuu wa Mkoa nakuunga mkono kwenye kazi unayofanya ya kupambana na wezi kupambana na mafisadi, kazi ya kupambanan na wavivu tunaopata hasara ni sisi mimi na madiwani na wenyekiti wa serikali za mtaa na Maraisi mambo yasipokwenda haya tutakaopata hasara ni sisi tutawenda kuomba kura kwa wananchi.

Nilipokuwa nasema Arusha kuna wizi, Arusha ni shamba la bibi, Arusha mambo haaendi walikuwa wanasema gambo ni mbaya, sasa leo amekaja kiboko yao. Nami naungana na kabisa na wewe unaposimamia haki, unaposimamia ukweli utapigwa vita na majungu kwenye kila kona ya nchi, lakini wanaosimamia haki mlinzi wao huwa ni Mungu na wala siyo binadamu.

Pia soma: Mkuu wa Wilaa Arusha: Migogoro baina a Baraza, menejimenti na mbunge inadhoofisha utoaji huduma au miradi ya maendeleo kwa wananchi
Naunga mkono hoja,Gambo amekuwa anafichua Ufisadi Arusha mara Kwa mara kuanzia Bungeni na kwingine lakini Serikali haichukui hatua.

Pale Arusha kulikuwa na syndicate ya Ufisadi kuanzia Halmashauri, Watumishi Hadi viongozi wa CCM.

Nakumbuka walimtenga Gambo ila Sasa ujio wa Makonda Gambo amefurahi sana ngoja awafyatue.
 
Nadhani ilikuwa ni story tuu, suti ya Gambo ni mwembamba haiwezi kumtosha Makonda ana kifua kipana!.
P
Sio Makonda huyu wa leo, ndoa yake Makonda kafanyia Arusha ghafla ghafla tu, ilibidi aende kwa Gambo zama hizo.

Kama ni story sawa Iła kuna siku waliwahi simulia walipotokea.

Nadhani ilikuwa kwenye mkutano wa Makonda dar akiongea na vijana dar au UVCCM akamwalika na Gumbo akiwa mkuu wa mkoa Arusha. Kwenye kuhamasisha wasikate tamaa na ndoto zao ndio wakakumbushia wao walipotokea.
 
Hii nchi imegeuka kuwa ya wasanii na wapenda maigizo.
Na hii ni toka juu hadi chini.
Kinachofanyika sasa hivi ni kuwekwa wazi ubovu wa serikali ya CCM na waweka wazi ni wanaccm wenyewe.
Wakati wapinzani walipokuwa wanasema ilionekana ni kelele na kuwa wanapinga kila kitu, sasa hao wanaounga mkono kila kitu ndio wanaoweka sasa uchafu wao wote hadharani
 
Huyo hata kipindi akiwa mkuu wa wilaya Uvinza alipandisha bei viwanja mpaka watu wa chini wameshindwabkununia
 
Back
Top Bottom