TANZIA Gardner G Habash mtangazaji wa Clouds Media afariki dunia

TANZIA Gardner G Habash mtangazaji wa Clouds Media afariki dunia

Mara kwanza kumuona Gardner ilikuwa miaka ya 90, alikuja Kahama Mining kwenye kampuni ya Tanzoro Diomond Drilling kama Accountant akitokea Mwanza ,akatukuta pale wazee wa drilling rigs.
Alikuwa kijana mtanashati checkibobu, aliletwa pale na mke wa mmiliki wa wa kampuni, alikuwa mcanada Mzee Georgre Graham.
Mara tunaona pilika zake na mke wa bosi zimezidi, kumbe tukaja kujua ni tokea zamani, yule mzee wa canada alikuwa analiwa hela tu na yule demu.
Yule demu alikuwa na mpango wake wa kuleta ndugu zake pale, basi hata hatukudumu, akatutengenezea gozi mpaka tukafukuzwa kazi, lakini nakumbuka Gadner ndio alikuwa mhasibu pale akatuandia cheki nzuri ya kama jiwe na upuuzi.
Ndio ikawa mwisho wa kumuona Gardner, mara nashangaa namuona kwenye TV na kumsikia redioni,
R.I.P
Very interesting story Mkuu

Ukiweza imalizie tujue how it ended up

Apumzike salama le captain 😭
 
Mkuu, hii unaithibitisha vipi kwamba mtu akifa anaenda kukutana na watu wengine? Na ni wapi huko?

Samahani lakini..
Hiyo mistari Kibonde na Gardner walikuwa wanapenda kuitumia wakiwa kwenye kipindi ila walikuwa wanaongea hivyo kwasababu mmojawapo wa wadhamini wa kipindi Chao ilikuwa ni kampuni ya pombe .
 
George Bantu, huyu naye kwa muonekano ni mgonjwa, wanatangaza kipindi kimoja, mwingine simkumbuki, ila alikuwa na kipindi cha mambo ya uswazi, nadhani anaitwa Mussa, wote walevi wa kutupwa.

May be Wasafi wampe angalizo Edo Kumwembe, anaingia kwenye kipindi akiwa mlevi kabisa mpaka sura yake imeshachakaa
George bantu ni kijana mdogo sana ila sura na mwili wake umeshaanza kuchoka sijui kwa nn hawajifunzi kuna siku alikesha baa mpaka asubuh akaenda kulala clouds ofisini ili kipindi cha jahazi kikianza wamuamshe na aliona ni kawaida tu.
 
Hivi Gadner alikuwa bado kijana? Maana sie wazee tinahisi alikuwa mzee mwenzetu🤣🤣
Mimi binafsi nahesabu mtu wa chini ya miaka 60 bado ni kijana aliyekomaa kifikra na kiakili......

Mtu wa huo umri bado ana nguvu na siha njema kabisa..........

Vijana wanachakaa si kutokana na umri bali na mitindo mibovu ya maisha......

Vijana hawaihurumii miili yao wanaibebesha mizigo mikubwa Sana

Imagine ini lako na figo kila siku inakumbana mipombe mikali kuchuja........

Mfumo wako wa chakula kila siku inakutana na mavyakula ambayo hayana faida mfumo wa insulins unachoka kiasi gani.........

Matokeo yake ndani ya miaka 20 Tu tayari mwili unakupa ishara kuwa karibu tunaagana...........

Hata chombo cha moto matumizi yako ya rafu ndio yanapunguza life span yake..........

Watu wawe makini Sana na miili yao.......

Mimi naamini life span ya mwili wa mwanadamu kuanza ku notice uzee na uchakavu wa mwili ni kuanzia miaka 70 kwenda chini ya hapo ni wewe mwenyewe na circumstances chache za kimazingira
 
Back
Top Bottom