Gari yangu ya kwanza nimenunua, Nissan Dualis

Gari yangu ya kwanza nimenunua, Nissan Dualis

1. Epuka kuoshea gari Lako maji ya Chumvi. Utaliharibu na litapauka Sana.

2. Kuwa mbahili WA kuasimisha gari Lako. Epuka Sana kuasimisha watu gari. Gari ni lako peke yako.


3. Fanya service Kwa wakati. Kama oil inabidi ubadiri baada ya kilomita 5000 zingatia Hilo.

4. Tafuta fundi wako mmoja anaejua KAZI. Acha kumpa kila fundi gari lako awe analigusa utakuja kuharibiwa gari Lako.


5. Jifunze hata namna ya kufungua tairi na baadhi ya parts za gari sio unachojua ni kuingiza ufunguo na kukunja usukani.


6. Unapokwenda Kufanya service. Oil na vifaa vingine mwambie fundi akuandikie anavyovihitaji ukanunue kwenye maduka Genuine yeye fundi KAZI yake aje kuweka kwenye gari. Kumeibuka mafundi Wasio waaminifu unawapa hela wakufanyie service wanaweka Oil na vifaa vingine feki mwisho WA siku injin ya gari inakufa.


7. Zingatia alama za barabarani ipasavyo achana na mihemko.
Hapo kwenye namba 6 ndio changamoto. Unajua hizi gereji zetu za uchochoroni tunazotumia kufanya service ndogo wamiliki wake hawapo makini wanafanya kazi kimazoea na ndipo hizi gari huharibiwa sana.

Ipo hivi, unaenda gereji mfano unataka badili oil ya gear box kwa mara ya kwanza. Meneja anamwambia dogo tu "fulani mbadilishie oil mteja" dogo anakwenda dukani anachukua oil ya Total ya Automatic ya Kawaida anakuja anaitia kwenye Dualis, au Toyota Rumion, au Vits new model, au Passo new model, au Vanguard, au kwenye Wish New model, au kwenye Xtrail new model etc gari ambazo hazitumii gear box hydraulic ya kawaida maana zote hizi na nyingine nyingi zinatumia gearbox ya mfumo wa CVT ambao hydraulic yake ni ya tofauti kabisa kimaterial na hata components zake sababu ya utofauti wa functionalities kati ya CVT transmissions na Automatic transmissions za kawaida zenye counter gearbox.

Akiweka mtumiaji tena especially wamiliki wa magari kama wanawake, watu wazima wa umri mkubwa ambao wamezoea magari ya kizamani au mtu yoyote asie mfuatiliaji wa maswala ya magari na hana elimu nayo huwa hata hawana idea nini kianendelea, analipia na kuwasha gari na kuondoka. Mita chache gari inaanza kumiss gear.

Anawaza pengine gari ni bovu, anapeleka kwa fundi anayetumia tu uzoefu ila hana ufahamu wa magari ya kisasa especially ya umeme anaanza pewa sound mara ooooh hizi Nissan ni gari mbovu sana. Ndio maana tunashauri watu kununua Toyota maana ni imara hizi ni mbovu sana.

Matokeo gari itatukanwa na kuchafuliwa jina as if ni kweli kumbe kosa ni la m'miliki na fundi wasiojua wanafanya nini.

So kimsingi ni vema sana kuzielewa hizi gari kabla haujaanza kuzitumia. Mimi nilifuatilia sana hii gari taarifa zake maana watu wanasema ni mbovu mimi kuna dada jirani na maskani kwa washua alikuwa nayo tokea 2009 namba B. Nikikuonyesha hapa picha yake utasema ameeingiza mwaka huu namna inavyowaka na kuonekana bado mpya sababu ya matunzo.

Na ukisikia akiwa ameipaki hapo ikiwa idle mode, hautasikia muungurumo wa kuchukiza yaani inatoa sauti ya chini sana almost ipo kimya yaani silent jambo limalomaanisha engine ipo safi na ipo vizuri. Ni gari nilikuwa nikipita wakati naenda shule au town nakutana na dada ndio anatoka nayo basi naitazama tu kama gari kali sana ambayo sitakuja hata kuipanda.

But recently nilianza tena kuifuatilia this time kwa kuielewa na kupata Factory instructions zake na kuijua. Aiseee nikasema shida nini, wacha nijionee. So nimekuja jua kuwa watu wengi hawajui magari wanaenda kwa mkumbo. Gari nzuri sana hii. Ingekuwa mbaya watu wasingenunua.
 
Kuna jamaa yangu nesi alichukuaga mkopo akalichukua hilo dude Dualis, ikawa mda wote maspeed tu.. Umbali mdogo tu anataka amalize sahani.. Alikuja kulibwaga, bahati nzuri akipata tu michubuko.

Kuna mwamba mwingine alikua daktari, nae Dualis ilikua gari yake ya kwanza.. Sijui lilimkuta jambo gani maana tuliishia kuambiwa amesha-R.I.P na alikua ktk barabara iliyonyooka ila gari ilitoka nyang'a nyang'a hakuna kilichopona!

Ushauri wangu jitahidi kua na nidhamu road.
Aiseee sio yule daktari amefariki mwaka huu nadhani kama sio mwaka jana. Alikuwa kama sio muhimbili hapo upanga basi ni muhimbili ile ya kule njia ya mkoa nimesahau jina.

Sio yule jamaa?!
 
Jambo la kwanza kwenye oil ya gear box. Fanya ubahiri wote ila sio hilo eneo. Usije ukaweka brand ya oil nje ya ile ya Nissan au ipo moja ya mobil ila sidhani kama inapatikana sana hapa Bongo. Ukiweka nje ya hiyo utakuja hapa kulia lia kuwa gari hizi ni mbovu kumbe ni wewe unashida.

Oil ya engine pia tumia yenyewe ya Nissan zinajulikana maana zipo za gear box na za engine. Asije akatokea fundi akakuchanganyia hiyo taarifa na kusema oil ni oil unaweza mix HAPANA. Kataaa. Tumia hizo oil za Nissan tuuu.

Gear box ya hiyo gari ni CVT so haitumii gear box oil (hydraulic) nyingine nje ya recommended ambayo ni zake na brand ya mobil. Utakutana na CVT oil (hydraulic) za brand zingine na mafundi wanaweza kushawishi kutia tu kwa sababu yoyote kataaaaaaaaa weka only ya Nissan.

Kingine, zingatia kutunza movements zako. Ni bora upite njia ndefu ya lami ukaingia gharama isiyozidi elfu 5 au 10 ya mafuta kuliko kufosi kupita njia fupi yenye mashimo makubwa na rough ambayo itaweza kukuchakazia gari yako na kuja kununua spare isivyo lazima. Ukiheshimu unapoipitisha ina uimara wa kutokukusumbua spare hata kwa miaka 2 bila shida yoyote.

Mengine nitakushauri kulingana na wachangiaji wanavyochangia. Karibu kwenye familia ya Nissan Dualis. For anything unaweza uliza tu bila shaka.

Safi Mkuu.
 
Kuna jamaa yangu nesi alichukuaga mkopo akalichukua hilo dude Dualis, ikawa mda wote maspeed tu.. Umbali mdogo tu anataka amalize sahani.. Alikuja kulibwaga, bahati nzuri akipata tu michubuko.

Kuna mwamba mwingine alikua daktari, nae Dualis ilikua gari yake ya kwanza.. Sijui lilimkuta jambo gani maana tuliishia kuambiwa amesha-R.I.P na alikua ktk barabara iliyonyooka ila gari ilitoka nyang'a nyang'a hakuna kilichopona!

Ushauri wangu jitahidi kua na nidhamu road.
Hizi gari zina handling nzuri sana. Sasa ukiendesha kizembe inajibu kwa namna unaendesha. Ipo flexible na very comfortable kuiendesha. Nimeona hata wadada wengi wanakimbilia huku sasa maana wanaona comfortability na urahisi wa kuitumia.
 
Fundi ngongo ndo atakuharibia hilo gari. Pale litakapowasha check engine ukampelekea akapima na mashine uchwara software ipo outdated akakuambia limeua coil na valves na themostat ni ya kutoa sababu iliwekwa kwa ajili ya nchi zenye barafu.
 
Hizi gari zina handling nzuri sana. Sasa ukiendesha kizembe inajibu kwa namna unaendesha. Ipo flexible na very comfortable kuiendesha. Nimeona hata wadada wengi wanakimbilia huku sasa maana wanaona comfortability na urahisi wa kuitumia.
Mkuu Vitz new model recommend oil, ni ipi ?

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
[emoji23][emoji23] kisahani ni speedometer wazee wa kulala kwenye kona na 120km/H wanaelewa. Anyway maneno yasiwe mengi kumaliza kisahani ni kutembea hadi mshale wa speedometer ufike mwisho
Kwakweli ata mimi nisingemaliza hicho kisahani
 
Mkuu Vitz new model recommend oil, ni ipi ?

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Kuna hiii 1.
download.jpg
 
Back
Top Bottom