Gautam Adani na kashfa ya rushwa Marekani: Je, ni nini hatma ya TANESCO na PPP ya David Kafulila, tenda apewe au atoswe?

Gautam Adani na kashfa ya rushwa Marekani: Je, ni nini hatma ya TANESCO na PPP ya David Kafulila, tenda apewe au atoswe?

Kwisha
View attachment 3157928


Mama anatafuta fedha za kuhonga!
 
Umezunguka tu. Ukweli kwa nchi zetu za dunia ya 3 wala hawana huo mpango wa kuja kukunufaisha, wanakuja kuja kuchukua zaidi kutoka kwako kuliko utachopata kwao hata akae miaka 100 story zitakua vile vile.

Kutoka hapo sio rahisi. Tuendelee tu kujipa moyo ila usitegemee maajabu yoyote. Waarabu, baadhi ya nchi asia na wazungu waliweza. Kwa huku Africa tulishakosea
Mawazo yale yale ya kimaskini, ya kudhani kila mtu anataka kukuibia!, Kujiona wewe tu ndio mwenye utajiri unaoonewa wivu unaotaka kuibiwa na wenye nacho.

Dunia hii ukimletea mwenye teknolojia maringo anaondoka kwako mchana huo huo na kwenda kufanya uwekezaji kwa mwingine.
 
Zipo sababu nyingi za kutofanya vizuri kwa mashirika hayo, mbaya kuliko zote ni kuingiza siasa kwenye masuala ya ufanisi yenye kuhitaji utaalam.

Tukubali tukatae tunalo tatizo katika taasisi nyingi haswa katika suala zima la tija kuwa ndogo, ufisadi ni mwingi watu wanavizia fursa za kuchota pesa.

DPW alikuja pale TPA na mbinu tofauti na akaanza kupigwa vita mapema sana kwani wafaidikaji wa mianya ya upigaji ni wengi na wenye misuli minene.
Tusiogope wezi jamanii kuuza mashirika yetu. Watu waadilifu wapo kabisa wapo tena wengi tu. Tatizo letu ni kuchagua rangi ya paka wakati kazi tunayotaka aifanye ni kukamata panya bila ya kujali rangi yake.
Vyuoni tunao wataalam wazuri tu na waadilifu wanaoweza endesha hayo mashirika kwa ufanisi. Tusiogope
Huwezi mwigopa mwizi kwa kugawa shamba lako kwa jirani hiyo sio sawa
Tulikuwa na akina Mchechu walioshika mashirika yaliyojufia na yakafufuka. Watu wa aina hiyo wapo wengi tu
 

===
Billionaire wa Kihindi na tajiri namba mbili barani Asia Mr Gautam Adani anayetajwa pia kuwa ni miongoni mwamatajiri kumi ( 10 ) duniani anakabiliwa na tuhuma za kuahidi kutoa rushwa ya kiasi cha US$ 250M zaidi ya TZS 650bn ili apate kazi na Mikopo toka kwa mabanki na Wawekezaji wenzake kibiashara.

Billionaire Gautam Adani anatajwa kumiliki ukwasi wa zaidi ya US$ 85.5bn zaidi ya TZS 222.3trilioni ambazo ni zaidi ya Uchumi wote wa nchi ya TANZANIA wenye wasi wasi nae kuhusu uwezo wa Kiuchumi naomba waondoe hofu.

Mtakumbuka billionaire huyu hivi karibuni alionesha nia ya kuwekeza nchini Marekani kiasi cha US$ 10bn zaidi ya TZS 26 Trilioni kwenye sekta ya nishati akiahidi kutoa ajira za moja kwa moja kwa wamarekani zaidi ya 15,000 akitaraji kupata faida ya karibu US$2bn zaidi ya TZS 5.2trlioni ndani ya miaka 20 ijayo.

Billionaire huyo kwa kupita kampuni yake Adan Green Energy Ltd pamoja na kampuni ya Gridworks Development Partners LLP toka Uingereza kwa nyakati tofauti tofauti wameonesha nia ya kutaka kuwekeza kwenye mradi wa kusafirisha na kusambaza Umeme kwa gharama ya zaidi ya TZS 3.3Trilioni ikiwa ni baada ya Tanzania kuwa na Umeme wa ziada wa zaidi ya 600MW hii ni baada ya bwawa la Mwl Nyerere (JNHPP) kukamilika na kuanza kufua umeme wa zaidi ya 2,100MW na kuziba nakisi ya umeme iliyokuwepo kwa miongo mingi na hivyo kuilazimu Tanzania kuuza umeme nje ya nchi.
Kufuatia kashfa hii ya kibiasha ya makampuni ya billionaire Gautam Adani na yanayoendelea katika Mitandao ya Kijamii hasa jukwaa hili na vyombo mablimbali vya habari vya ndani na nje ya Tanzania hasa kwa kuishambulia Serikali ya TANZANIA na watendaji wake,

Haya ni maoni yangu,

1. Tuhuma hizi kwa Serikali ya Tanzania ni ama zimewahi ama hazina msingi wowote kwakuwa billionaire Gautam Adani hana mkataba wowote na Serikali ya Tanzania japo ameonesha nia ya kuwekeza kwa kutumia Sheria , kanuni na taratibu za PPPC.

2. Hata hivyo kinachomsibu Gautam Adani Kwa sasa ni tuhuma tu tena za Upande mmoja na kwa kuzingatia dunia hii ya mnyukano wa vita za Kiuchumi tusiende mbio kwenye lawama badala yake tujiuluze kwanini Marekani yenyewe imruhusu billionaire Gautam Adani awekeze kiasi Cha US$ 10bn na hivyo kutoa ajira zaidi ya 15,000 kwa wamarekani?

3. Hata hivyo, hakuna mahali Serikali ya Tanzania wala Mkurugenzi wa PPP Bw David Kafulila wamemtetea billionaire Gautam Adani au mwekezaji mwingine yeyote.

4. Kwa msiofahamu kazi mojawapo ya PPPC ni kuueleza umma wa Tanzania ( Public ) kuhusu uwekezaji na wawekezaji wenye nia ya kuwekeza kwenye PPP kwa kuzingatia zaidi masilahi mapana ya Taifa la Tanzania.

5. Lazima tufahamu kwanini PPPC anafanya hivi, lengo na nia ni kuufanya Umma ( Public) uelewe kila kitu tangu mwanzo kabisa wa mradi hasa kwenye hatua ya mwekezaji kuonesha nia badala ya Umma kuja kuletewa mkataba ulosainiwa bila kujua mchakato wa uwekezaji huo ulianza lini na kwa namna gani na masilahi kwa Taifa ni yepi hivyo kupoteza maana ya neno Public-Private

Tukumbuke Transparency ndio nguzo kuu katika ndoa yoyote ile ya PPP na faida yake ni hii Leo Watanzania wanamjadili Adani nje ndani ni kwa sababu wameshirikishwa mapema na kwa uwazi kabisa juu ya nia yake hiyo.

Pia soma Bilionea Gautam Adani ambaye Kafulila anataka kumpa shirika la TANESCO ashitakiwa kwa utapeli huko Marekani



#SAMIAMITANOTENA
Watu washakula hela sasa wanaangalia upepo unavyoenda.
 
Mawazo yale yale ya kimaskini, ya kudhani kila mtu anataka kukuibia!, Kujiona wewe tu ndio mwenye utajiri unaoonewa wivu unaotaka kuibiwa na wenye nacho.

Dunia hii ukimletea mwenye teknolojia maringo anaondoka kwako mchana huo huo na kwenda kufanya uwekezaji kwa mwingine.
Unauzungumza umaskini sehemu ambayo haihusiani. Nimekueleza kama unasubiri mwekezaji aje Africa kukupa zile ndoto tunaota kufika basi hatutafika kwenye hizo ndoto. Mwekezaji ataweza kukupa ndoto iliwa tayari wewe mwenyewe umeanza kuzitimiza

Dunia hii ukimletea mwenye teknolojia maringo anaondoka? Huu ni uongo, Hakuna mtu atataka kuondoka kirahisi sehemu anayopata sawa na bure. Ndio maana unaona hadi leo ExxonMobil, Equinor wanabembeleza serikali isaini haraka mkataba wa gesi Lindi. Fikiria tu kwa miaka 8 sasa tunawapiga chenga lakini bado wanabembeleza. Kwa maneno yako wangekua washaacha kutaka huo mradi
 
Unaushahidi wowote jombaa
All circumstantial evidence points to that.

Hiyu jamaa Adani ndoyo tabia yake kutembeza pesa na viongozi wa Watanzania wanapenda sana pesa.

Sasa unafikiri watampa contract burebure bila kupiga pesa?

Unataka waweke wazi hii hapa rushwa katoa tumeifurahia sana?

Serikali ina wajibu wa kuweka mambo wazi, kwa nini haikuweka?
 
All circumstantial evidence points to that.

Hiyu jamaa Adani ndoyo tabia yake kutembeza pesa na viongozi wa Watanzania wanapenda sana pesa.

Sasa unafikiri watampa contract burebure bila kupiga pesa?

Unataka waweke wazi hii hapa rushwa katoa tumeifurahia sana?

Serikali ina wajibu wa kuweka mambo wazi, kwa nini haikuweka?
Kafulila hawezi kukubali rushwa ya aina yoyote namfahamu vema tuwe watulivu tu
 
Kafulila hawezi kukubali rushwa ya aina yoyote namfahamu vema tuwe watulivu tu
Angekuwa hawezi kukubali rushwa ya aina yoyote asingetuletea huyu mtu anayenuka rushwa.

Kutuletea huyu mtu na kampuni yake maana yake hakufanya due diligence ya kutosha.

Sasa hakufanya due diligence ya kutosha kwa sababu gani?

Unataka kusema Kafulila ni mjinga hivyo hakujua kwamba huyu mtu na kampuni yake wananuka rushwa?

Haya mambo mbona yameandikwa kirefu miezi mingi tu na whistleblowers wa Kenya.

Kafulila hakujua tuhuma hizi?
 
Angekuwa hawezi kukubali rushwa ya aina yoyote asingetuletea huyu mtu anayenuka rushwa.

Kutuletea huyu mtu na kampuni yake maana yake hakufanya due diligence ya kutosha.

Sasa hakufanya due diligence ya kutosha kwa sababu gani?

Unataka kusema Kafulila ni mjinga hivyo hakujua kwamba huyu mtu na kampuni yake wananuka rushwa?

Haya mambo mbona yameandikwa kirefu miezi mingi tu na whistleblowers wa Kenya.

Kafulila hakujua tuhuma hizi?
Kafulila ndio maana Jesca alimwacha kisa hajui kupiga pesa, Kafulila ni mwadilifu sana hata hivyo
 
Kafulila ndio maana Jesca alimwacha kisa hajui kupiga pesa, Kafulila ni mwadilifu sana hata hivyo
Uadilifu wake haukumfanya afanye due diligence ya kutosha kuepukana na watu waliogubikwa na rushwa. Hivyo hautoshi.

Katika sheria kuna msemo kwamba "Justice must not only be done, it must appear to be done".

Mtu muadilifu hatakiwi tu kuwa muadilifu, anatakiwa kuonekana kuwa muadilifu.

Sasa mnasema Kafulila muadilifu, halafu hapo hapo anampigia debe huyu mtu anayejulikana kwa kugawa rushwa popote anapokwenda. Hapo tukiangalia tunahitimisha kuwa Kafulila naye ama kapewa rushwa, ama ni mjinga sana hakujua kuwa huyu mtu ananuka rushwa despite all the press.

Sasa Kafulila ni mjinga sana hivyo kweli?
 
Kwani tuliingia mkataba na yeye au kampuni zake?

USA siwaamini sana linapokuja suala la maslahi yao, wanakuundia zengwe tu.

Tanzania tutazame maslahi ya nchi kwanza kabla ya yote.
 
William Ruto amekwisha vunja kandarasi ya huyu mtoa rushwa kuendesha uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta
Hapa Tz kunanuka uvundo.
Madame FaizaFoxy sijui waziri na Abdul ukwasi wao umetokana hapa au la ila huyu muhindi ni mtoa rushwa mkubwa.
 
20241121_200215.jpg
 
Back
Top Bottom