Donnie Charlie
JF-Expert Member
- Sep 16, 2009
- 16,908
- 19,123
Mama anasema anazunguka sana kufanya tz iwe bora.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mama anasema anazunguka sana kufanya tz iwe bora.
Wakenya wamebadili mawazo. Rutto ametangaza kuwa dili ya kumwachia huyo Adnan AirPort yao aiendeshe kwa miaka 30 imesitishwa baada ya hiyo kashfa kule Marekani.Dp world ni mafia zaidi ya huyo lakini amepewa tenda hakuna kitakachobadilika hapo.
Imeisha hiyo.Kwisha
View attachment 3157928
Kampuni ya Adani yasaini Mkataba wa miaka 30 kuendesha Gati ya 2 ya Bandari (Zamani TICTS)
Adani itafanya kazi na kusimamia Gati ya 2 ya Kontena katika Bandari ya Dar es Salaam, Tanzania, kupitia kampuni tanzu ya Adani International Ports Holdings Pte Ltd. Mkataba huo wa miaka 30 umesainiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania. ==== The concession agreement for 30 years has been signed...www.jamiiforums.com
Fisadi, mwizi, jangili. Marekani washatoa arrest warrant ya kumkamata huyo msimbe. Kwa nini hatujifunzi? Mpaka litutokee?Kwanini atoswe toa sababu mujarabu
Noma sana 🤣 itakuwa tajiri Gautamu katoa Asali tamu sana.Imeisha hiyo.
We unafikiri zile milioni mia saba saba anazogawagawa ovyo kwenye mpira na zile milioni mia, mia hamsini anazogawa makanisani/misikitini zote ni pesa za walipa kodi?
Hii nchi kwa Sasa ipo mikononi mwa wahuniUsipotoshe.
Kinacho pingwa ni ufisadi. Miradi inayo ingiwa gizani kwa kuficha kila kitu ili madudu yasionekane.
Wewe mwenyewe humu ulisha sema na kumhimiza Samia kila kitu afanye gizani, watu wasijue kinacho endelea!
Sasa mnageuza stori na kulalamikia watu na makundi yanayo pigania maslahi ya wananchi.
Sasa wewe tueleze, ni waTanzania wangapi wanajuwa kwamba gesi ya Mtwara (Ntor) Samia alikwisha wagawia Omani; ni waTanzania wangapi wanajuwa Adani huyo huyo alisha pewa mradi wa kuzalisha umeme wa makaa ya mawe. Huko bandarini, nani anaye juwa ni makubaliano gani huyo Adani aliingia nayo na serikali yetu.
Kila kitu mnafanya gizani, halafu mnawaona waTanzania kama majuha!
Lord have mercy on Tanganyika
Toa upumbavu wako hapa.Kila Mkataba unajitegemea
Watanganyika AmkeniHii nchi ni shamba la bibi mjomba
Nchi inauzwa mchana na usiku utazan kesho hakuna kizazi
Kizimkazi kaamua sijawahi ona uuzaji wa nchi namna hii mimi toka nizaliwe
Endelea kukariri 🐼Toa upumbavu wako hapa.
Tangu 1961 tunapata uhuru wasomi wetu wanazo akili za wizi tu, ni kwa bahati mbaya sana kila mwaka CAG anapotoa report ya mwaka inajaa uchafu mtupu.Tusiogope wezi jamanii kuuza mashirika yetu. Watu waadilifu wapo kabisa wapo tena wengi tu. Tatizo letu ni kuchagua rangi ya paka wakati kazi tunayotaka aifanye ni kukamata panya bila ya kujali rangi yake.
Vyuoni tunao wataalam wazuri tu na waadilifu wanaoweza endesha hayo mashirika kwa ufanisi. Tusiogope
Huwezi mwigopa mwizi kwa kugawa shamba lako kwa jirani hiyo sio sawa
Tulikuwa na akina Mchechu walioshika mashirika yaliyojufia na yakafufuka. Watu wa aina hiyo wapo wengi tu