Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Ipo mikasa mingi ya wezi ambao baada ya kuiba hujikuta wametegeshewa na hawawezi kuutua tena mzigo wao mpaka makubaliano na mwenye mali yafanyike.
Iko mikasa mingine ya wazinifu na wachawi inayofanana na mikasa ya wizi. Gaza ni mfano wa mzigo Israel iliyojitwisha ikitaraji kuufikisha ilipotaka mapema na baadae wapumzike.
Hali imekuwa tofauti na mara Israel imejikuta imebeba mzigo wa tego ambao sasa wanatamani wautue na hawawezi kufanya hivyo. Wameporomosha majengo karibu robo tatu ya jiji la Gaza na hakuna kilichopatikana.
Baadae wakaanza kubomoa mahospitali yote makubwa na kupiga wagonjwa na bado hakuna tija yoyote iliyopatikana. Baada ya kushindwa kuutua mzigo upande wa Gaza kaskazini wakaelekea kusini ya Gaza wamefanya kama walivyofanya kaskazini na haikuwezekana kuutua mzigo wao wa Gaza.
Vizuizi walivyoweka Israel kuzuia watu wa maeneo tofauti wasitoke na kurudi wanakotaka navyo wameshindwa kuvilinda.
Israel ililpojaribu kuhamisha vikosi kurudisha nyumbani ili kuutua mzigo wa Gaza haikusaidia kabisa na ndipo mzigo ulipozidi kuielemea kwa kuongezeka mapigano.
Hatimae Israel ili kuutua mzigo wake wa tego inajaribu kufikia makubaliano ili kumaliza vita na kubaki huru wapate kupumua.
Iko mikasa mingine ya wazinifu na wachawi inayofanana na mikasa ya wizi. Gaza ni mfano wa mzigo Israel iliyojitwisha ikitaraji kuufikisha ilipotaka mapema na baadae wapumzike.
Hali imekuwa tofauti na mara Israel imejikuta imebeba mzigo wa tego ambao sasa wanatamani wautue na hawawezi kufanya hivyo. Wameporomosha majengo karibu robo tatu ya jiji la Gaza na hakuna kilichopatikana.
Baadae wakaanza kubomoa mahospitali yote makubwa na kupiga wagonjwa na bado hakuna tija yoyote iliyopatikana. Baada ya kushindwa kuutua mzigo upande wa Gaza kaskazini wakaelekea kusini ya Gaza wamefanya kama walivyofanya kaskazini na haikuwezekana kuutua mzigo wao wa Gaza.
Vizuizi walivyoweka Israel kuzuia watu wa maeneo tofauti wasitoke na kurudi wanakotaka navyo wameshindwa kuvilinda.
Israel ililpojaribu kuhamisha vikosi kurudisha nyumbani ili kuutua mzigo wa Gaza haikusaidia kabisa na ndipo mzigo ulipozidi kuielemea kwa kuongezeka mapigano.
Hatimae Israel ili kuutua mzigo wake wa tego inajaribu kufikia makubaliano ili kumaliza vita na kubaki huru wapate kupumua.