Gazeti la Jamhuri: Siri ya ugomvi wa Dk. Kigwangalla na Profesa Mkenda hadharani

Gazeti la Jamhuri: Siri ya ugomvi wa Dk. Kigwangalla na Profesa Mkenda hadharani

Kuna ukweli gani katika tuhuma hizi nzito, kinacho shangaza zaidi kwa nini gazeti la Jamuhuri linamkandia sana Dr.Kigwangalla, je, kuna ajenda gani nyuma ya pazia? JPM kasema Kigwangalla na katibu mkuu wa Wizara wanapaswa kulewana, actually JPM alikwenda mbali zaidi akasema Katibu Mkuu amuheshimu Kigwangalla - JPM knows what is going on - kinyume chake nyinyi mnakuja na stori zenu za kubuni tu - lengo lenu mnataka Kigwangalla afukuzwe kazi, ndio baadhi ya Watanzania tulivyo mazaba zabina tu mabingwa wa kupika majungu - wahariri magazeti wanapewa tu handdouts zenye stori za kutunga tu na wao wanazichapishwa hivyo hivyo bila ya kutafakari mambo.

Revisit mtiritiko wa tuhuma lukuki zinazo muhusu Waziri, zinaonekana wazi wazi ziko totally incoherent from highly questionable source like: majangiri wa wanyama na wale ambao hawakufanikiwa kugawiwa hunting blocks, hao ndio the brains behind machapisho ya gazeti husika.

Maneno chungu nzima, nani kawambieni kwamba kutangaza utalii ndani na nje ya Tanzania should cost nothing!! Any idea Kenya inatumia kiwango gani cha fedha kujitangaza Kimataifa?? Ukweli wa mambo Kigwangalla ni Waziri mbunifu sana sana, cha muhimu hapa gharama/matumizi ya Wizara katika masuala ya kujitangaza kiutalii yawe contained within the budget, haya mambo ya walio chini ya Waziri kujifanya ni Wakatoliki kuliko Papa hayatufikisha popote.
Ile wizara ni ngumu mno! Imejaa titan fitna! Ni muhimu kuwa makini na tuhuma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakubwa walio katika serikali wataamua nani mkweli kati ya muandishi wa story hii, katibu Mkuu Prof. Mkenda na Waziri Kigwangala.

Sidhani kama kuna makosa kutumia hela kufanya promotion ya Utalii. Suala je taratibu zimefuatwa, kama hzijafuatwa nani anahusika kumdhibiti anaechukua hela kama kweli kachukua ili afanya kwa mujibu wa utaratibu.

Kubwa kuliko vyote, kwa hayo ambayo Waziri Kigwangala kafanya, je yanaweza kuwa na return on investment. Kama dude au Stive Nyerere wakuwa kwenye media platform za utalii, watavutia Watanzania wangapi kutalii??

Au kwanini Waziri asinge-focus kama Kagame walau akapata mkataba na moja ya timu EPL tukawa na campaign visit Kilimanjaro au Visit Serengeti ili kuvutia wanadunia wanaofuatilia EPL waje Tz.

Kagame project yake na Arsenal ya visit Rwanda in positive projection kwenye return on investment. Assuming waziri katumia hela kwa kufuata utaratibu, uwepo wa akina Ebitoke na wakina wanaFA kwa gharama za TANAPA zina-project vip Return on that investment??

Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote
 
Hili linafahamika kama wanagombania fedha zetu za umma.

Kigwangalah anajaribu kupromote Utalii kupitia wasanii. Anastahili pongezi lakini haya inabidi yafuate utaratibu wa fedha na iwepo kwenye mipango ya wizara sio zimamoto pap paaap.

Hapo atamponza hata Katibu mkuu kwa magu.

Binafsi sizani kama kina Le mutuz, shilole watatushawishi watu kama sisi kwenda kutalii wakati hakuna Salary increment, small bizness zinakufa watu hatuna ongezeko la kipato huwezi kupata hela ya kutalii.

Kwa hiyo wale wadada wa mjini wote walioenda kutalii walilipiwa na kodi zetu hii ni hatari zaidi ya umeme.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Desemba 31, mwaka jana Rais John Magufuli akiwa mapumzikoni katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo mkoani Geita aliwapa siku tano viongozi hao kupatana, vinginevyo angetengua uteuzi wao.

Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa chanzo cha ugomvi huo ni matumizi mabaya ya fedha unaofanywa na Waziri Kigwangalla, kupitia ‘utangazaji utalii’.

Miongoni mwa hayo ni matumizi yasiyo sahihi ya mali zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, zikiwamo ndege.

Katika matukio mawili ya hivi karibuni, waziri huyo ameagiza moja ya ndege za Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imfuate msanii mmoja (jina tunalo) Kigoma ili ashiriki tamasha jijini Arusha.

Katika tukio la pili, Dk. Kigwangalla aliamuru ndege ya TANAPA imfuate mwanahabari mmoja jijini Dar es Salaam na kumpeleka Arusha, Rubondo, Katavi na baadaye akarejeshwa Arusha. Ndege hiyo ilitakiwa imchukue mwanahabari huyo saa 2 asubuhi katika Uwanja wa Julius Nyerere, lakini alitokea saa 9 alasiri huku ndege ikiendelea kumsubiri kwa muda wote huo.

Wageni wake, wakiwamo wasanii wakiwa katika majiji kama Arusha hulazwa katika hoteli za kifahari za kuanzia hadhi ya nyota nne.
Chanzo cha habari kinasema Profesa Mkenda amekuwa haridhishwi na matumizi ya fedha hizo, na amekuwa akitaka taratibu zifuatwe ili kunusuru fedha za umma, lakini na yeye mwenyewe kama mtendaji mkuu na ofisa masuuli wa wizara abaki salama.

Dk. Kigwangalla, kama alivyowahi kufanya aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii wa mwisho katika Awamu ya Nne, Lazaro Nyalandu, amekuwa akiagiza apewe fedha nyingi ili kuwalipa wasanii kwa kigezo cha kuwatumia kuhamasisha utalii ndani na nje ya nchi.

Kwa kigezo hicho amekuwa akitumia makundi ya wasanii kuzunguka huku na kule nchini kufanya shughuli hiyo. Wasanii hao huzuru hifadhi za taifa na pia hushiriki matamasha mbalimbali.

Hivi karibuni alipeleka kundi la wasanii kukwea Mlima Kilimanjaro, lakini ni mmoja tu aliyefanikiwa kufika kileleni. Wengine, licha ya kushindwa, waliendelea kulipwa fedha kwa muda wote uliopangwa.

Imeelezwa kwamba Waziri Kigwangalla amekuwa akiagiza apewe fedha kutoka katika taasisi kuu zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Taasisi hizo ni Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA). Mapato ya taasisi hizo kwa mwaka ni takriban Sh bilioni 500.

“Kuna makundi ya wasanii yanapelekwa kwenye maeneo mbalimbali ya hifadhi, gharama zake ni kubwa. Waziri anadai gharama zibebwe na wizara, sawa; lakini kuwe na utaratibu, yeye hataki. Unakuta anaagiza zitolewe Sh milioni 170, zitolewe Sh milioni 80; mara zitolewe Sh milioni 100 na kadhalika. Hizi fedha ni nyingi na kwa maana hiyo lazima kuwe na utaratibu wa kifedha wa kuziomba na kuzitoa.

“Mbaya zaidi, fedha hizo hutakiwa zilipwe na wakuu wa taasisi kwa maelekezo ya waziri. Huo si utaratibu. Kule kwenye taasisi wakisema hawana mamlaka ya kufanya malipo bila maelekezo ya katibu mkuu, mgogoro huanzia hapo.

“Katibu Mkuu anapoambiwa anang’aka na kutaka fedha zisitolewe bila kufuata mfumo wa malipo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. Waziri akishajua katibu mkuu amekwamisha malipo kwa sababu hizo, basi ugomvi unalipuka,” kinasema chanzo chetu.

JAMHURI limeelezwa kuwa baada ya Waziri Kigwangalla kuona anakwamishwa na katibu mkuu, alianza kutumia utaratibu wa kumwagiza msaidizi wake kuwasiliana moja kwa moja na wakuu wa taasisi hizo ili wafanye malipo.

“Hilo nalo lilionekana kuwa ni ukiukwaji wa taratibu, kwa sababu msaidizi wa katibu hana mamlaka ya kuwasilisha maelekezo ya kufanyika malipo. Utoaji fedha za umma una taratibu zake,” kinasema chanzo chetu.

Fedha zinazochotwa kutoka kwenye taasisi hizo zinatumika kugharimia usafiri, malazi na posho za wasanii. Hata hivyo, baadhi ya waliozungumza na JAMHURI wanasema kinachofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuwatumia wasanii kinavuka mipaka ya ‘utangazaji utalii’, badala yake kuna mkakati wa kisiasa kwa ajili ya siku zijazo.

“Ninachoweza kukuhakikishia ni kuwa kuna mpango wa watu kuwania nafasi kubwa zaidi mwaka 2025, kwa hiyo kinachofanyika sasa ni kuwavuta wasanii ili wawe karibu nao kwa ajili ya mwaka 2025. Hili halina ubishi kwa sababu tumo humu tunajua mengi. Kinachofanywa sasa ni kujenga mtandao wa kuungwa mkono na ndiyo maana unaona wanaotumika hapa ni wasanii na watu wa online, ” kinasema chanzo chetu na kuongeza:

“Angalia hata wajumbe wa bodi, baadhi yao wanateuliwa kwa sababu ni marafiki wa wakubwa wizarani.”

Mwanzoni mwa Desemba, mwaka jana wasanii saba walifanya ziara katika baadhi ya hifadhi kwa kile kilichoelezwa kuwa ni sehemu ya kujionea vivutio ili kuvitangaza, hivyo kuhamasisha wageni na wenyeji kutalii.

Ziara hiyo ilianzia katika Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato na kuendelea hadi hifadhi za taifa za Ibanda – Kyerwa na Rumanyika – Karagwe. Kiongozi mkuu wa msafara alikuwa Dk. Kigwangalla mwenyewe. Wasanii wa muziki na maigizo (Bongo Movie) walioshiriki ni Steve Nyerere, Dude, Richie, Shilole, Ebitoke, Shetta na mwakilishi kutoka Muziki AT (Zanzibar). Baadaye walizuru Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.

Rais Magufuli akizungumza na wahifadhi wa Rubondo, alisema: “Ninafahamu, watendaji wenu wa juu, Katibu Mkuu na Waziri kila siku wanagombana, ninawatazama taratibu na nilishampa kazi Katibu Mkuu Kiongozi awaite na awaeleze, lakini wasipobadilika nitawaondoa… Siwezi kuwa na watendaji ambao nimewateua mwenyewe halafu wanagombana, na kuna mambo mengi hayaendi. Katibu Mkuu hamheshimu waziri na waziri hataki kwenda na katibu mkuu, siwezi kuvumilia hilo.

“Leo nawaambia wajirekebishe na ikiwezekana wajirekebishe ndani ya siku tano, wawe wanasalimiana na wanazungumza, mimi ninafahamu, nina vyombo, ninajua nani hafai zaidi,” alisema Rais Magufuli.

Baada ya kauli ya Rais Magufuli, Waziri Kigwangalla kupitia akaunti yake ya Twitter alisema: “Kazi ya urais ni ngumu sana. Tulioteuliwa na Mheshimiwa Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea Rais frustration nyingine zaidi. Sisi kwenye wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary (Katibu Mkuu Kiongozi) tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari!”

Gazeti la JAMHURI limemtafuta Dk. Kigwangalla kwa njia zote za mawasiliano ili kupata maoni yake, lakini hakupokea simu wala kujibu maswali aliyoandikiwa. Katibu Mkuu, Profesa Mkenda, hakuwa tayari.

-Jamhuri (Toleo 07/01/2020)
Haya matumizi yanayofanywa na mleta hoja yana tija kwenye kuutangaza utalii; hata Coca Cola pamoja na kujulikana na kila mtu hawajawahi kuacha matangazo. Shida ninayoiona hapa hilo ni jukumu la Tanzania Tourist Board na siyo shughuli inayohitaji kusimamiwa na waziri moja kwa moja. Waziri angeelekeza hizo taasisi zipeleke michango hiyo TTB ili kuimarisha juhudi za kuvitangaza vivutio vyetu
 
Watu wameanza kufukua makaburi _joy__joy__joy_ kosa la  @hamisi_kigwangalla amewaambia wa ( 62...jpg
 
Alikataa kupokea simu habari imetoka anasema amechafuliwa anataka milini 500, Kigwangala mjanja sana ameona sasa ulaji unakata wizarani anataka apate jamuhuri, jamaa anafanya kazi kishamba sana.
 
Napendekeza tufanye kama Rwanda tuandike "Kilimanjaro" kwenye jezi za Barcelona.
Itatugharimu pesa lakini outcome yake itakua kubwa sana.
Tutafute na timu ndogo za Hispania na Uingereza ila tupromote utalii wa mbuga zetu na vivutio vingine.
Utalii wa ndani tuwaachie Safari Chanel.
 
By the way usipokubali kuliwa huli.....biashara ua utalii inahitaji utumie fedha kuitangaza utalii hivyo hizi pesa kama zinatumika kutangaza utalii shida ipo wapi

Asubiri baada ya miaka 5 asipoona matokeo chanya alalamike kwangu me naona sasa hivi kumekuwepo na mwamko mkubwa sana kwa utalii wa ndani hivyo si mbaya


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa namna tunavyokwenda kipindi hiki sidhani kama yanayoandikwa kwenye bajeti zetu ndio yanayofuatwa,naona kila mmoja anajikurupukia tu kufanya mambo. Twendeni tu hivyo hivyo si ndio tulivyoamua tutafika tu yakiharibika tutarekebisha mbele ya safari.
Hivi utangazaji huo wa utalii uliandaliwa na kitengo cha masoko cha wizara ( kama kipo) ama yalikuwa mawazo binafsi ya waziri mwenye dhamana!? Na malipo hayo yanayosemwa yalikuwa halali ama lah!? Kama utaratibu wa malipo ulikuwa na shida, wahusika wa kutoa fedha wachukua hatua gani ela zitoke kwa wakati?
====
Kwa waliosoma habari nzima kwenye gazeti, mwandishi wa habari alimpa furusa mheshimiwa waziri kujibu yuhuma hizi..!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla ya kutoa habari hii kiungwana na kitaaluma ya uandishi wa habari makini na wenye weledi walitakiwa wahakikishe wamempata Kigwangala kwanza ilk kubalansi stori.
Kinachoonekana ni mkakati wa Balile na Adolf Mkenda kummaliza Kigwangala kisiasa,
Huyu Balile pia alitumika na kina Nape Nnauye kummaliza Makonda alichemka.

Naona anarudia yaleyale aliofanya kea Makonda.
,Ninavyofahamu Kigwangalah ni kijana mtiifu wa rais Magufuli,na anafanya kazi zake kwa nidhamu ya hali ya juu.

Angalizo,
Kuhusu Adolf Mkenda Rais Magufuli siku anamuapisha kuwa katibu mkuu wa hiyo wizara alimwambia nakupeleka huko nako ukafanye yako,ukivurunda ndio basi tena.

Ngoja tuone nani ataibuka kidedea,Uzuri wa vyanzo vya taarifa vya Rais Magufuli huwa makini sana.
Mwisho ,
Balile toka usifiwe na rais Magufuli kipindi kile kwenye sakata la mafuta kuhusu kodi ulivimba kichwa ,muda mwingine unaitumia kalamu yako vibaya.

Na mwisho kabisa si kwa umuhimu, wasanii ni muhimu sana kuwa nao karibu kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, si kwa Kigwangalah tu ,hata Rais Magufuli anawahitaji sana tu
Desemba 31, mwaka jana Rais John Magufuli akiwa mapumzikoni katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo mkoani Geita aliwapa siku tano viongozi hao kupatana, vinginevyo angetengua uteuzi wao.

Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa chanzo cha ugomvi huo ni matumizi mabaya ya fedha unaofanywa na Waziri Kigwangalla, kupitia ‘utangazaji utalii’.

Miongoni mwa hayo ni matumizi yasiyo sahihi ya mali zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, zikiwamo ndege.

Katika matukio mawili ya hivi karibuni, waziri huyo ameagiza moja ya ndege za Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imfuate msanii mmoja (jina tunalo) Kigoma ili ashiriki tamasha jijini Arusha.

Katika tukio la pili, Dk. Kigwangalla aliamuru ndege ya TANAPA imfuate mwanahabari mmoja jijini Dar es Salaam na kumpeleka Arusha, Rubondo, Katavi na baadaye akarejeshwa Arusha. Ndege hiyo ilitakiwa imchukue mwanahabari huyo saa 2 asubuhi katika Uwanja wa Julius Nyerere, lakini alitokea saa 9 alasiri huku ndege ikiendelea kumsubiri kwa muda wote huo.

Wageni wake, wakiwamo wasanii wakiwa katika majiji kama Arusha hulazwa katika hoteli za kifahari za kuanzia hadhi ya nyota nne.
Chanzo cha habari kinasema Profesa Mkenda amekuwa haridhishwi na matumizi ya fedha hizo, na amekuwa akitaka taratibu zifuatwe ili kunusuru fedha za umma, lakini na yeye mwenyewe kama mtendaji mkuu na ofisa masuuli wa wizara abaki salama.

Dk. Kigwangalla, kama alivyowahi kufanya aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii wa mwisho katika Awamu ya Nne, Lazaro Nyalandu, amekuwa akiagiza apewe fedha nyingi ili kuwalipa wasanii kwa kigezo cha kuwatumia kuhamasisha utalii ndani na nje ya nchi.

Kwa kigezo hicho amekuwa akitumia makundi ya wasanii kuzunguka huku na kule nchini kufanya shughuli hiyo. Wasanii hao huzuru hifadhi za taifa na pia hushiriki matamasha mbalimbali.

Hivi karibuni alipeleka kundi la wasanii kukwea Mlima Kilimanjaro, lakini ni mmoja tu aliyefanikiwa kufika kileleni. Wengine, licha ya kushindwa, waliendelea kulipwa fedha kwa muda wote uliopangwa.

Imeelezwa kwamba Waziri Kigwangalla amekuwa akiagiza apewe fedha kutoka katika taasisi kuu zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Taasisi hizo ni Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA). Mapato ya taasisi hizo kwa mwaka ni takriban Sh bilioni 500.

“Kuna makundi ya wasanii yanapelekwa kwenye maeneo mbalimbali ya hifadhi, gharama zake ni kubwa. Waziri anadai gharama zibebwe na wizara, sawa; lakini kuwe na utaratibu, yeye hataki. Unakuta anaagiza zitolewe Sh milioni 170, zitolewe Sh milioni 80; mara zitolewe Sh milioni 100 na kadhalika. Hizi fedha ni nyingi na kwa maana hiyo lazima kuwe na utaratibu wa kifedha wa kuziomba na kuzitoa.

“Mbaya zaidi, fedha hizo hutakiwa zilipwe na wakuu wa taasisi kwa maelekezo ya waziri. Huo si utaratibu. Kule kwenye taasisi wakisema hawana mamlaka ya kufanya malipo bila maelekezo ya katibu mkuu, mgogoro huanzia hapo.

“Katibu Mkuu anapoambiwa anang’aka na kutaka fedha zisitolewe bila kufuata mfumo wa malipo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. Waziri akishajua katibu mkuu amekwamisha malipo kwa sababu hizo, basi ugomvi unalipuka,” kinasema chanzo chetu.

JAMHURI limeelezwa kuwa baada ya Waziri Kigwangalla kuona anakwamishwa na katibu mkuu, alianza kutumia utaratibu wa kumwagiza msaidizi wake kuwasiliana moja kwa moja na wakuu wa taasisi hizo ili wafanye malipo.

“Hilo nalo lilionekana kuwa ni ukiukwaji wa taratibu, kwa sababu msaidizi wa katibu hana mamlaka ya kuwasilisha maelekezo ya kufanyika malipo. Utoaji fedha za umma una taratibu zake,” kinasema chanzo chetu.

Fedha zinazochotwa kutoka kwenye taasisi hizo zinatumika kugharimia usafiri, malazi na posho za wasanii. Hata hivyo, baadhi ya waliozungumza na JAMHURI wanasema kinachofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuwatumia wasanii kinavuka mipaka ya ‘utangazaji utalii’, badala yake kuna mkakati wa kisiasa kwa ajili ya siku zijazo.

“Ninachoweza kukuhakikishia ni kuwa kuna mpango wa watu kuwania nafasi kubwa zaidi mwaka 2025, kwa hiyo kinachofanyika sasa ni kuwavuta wasanii ili wawe karibu nao kwa ajili ya mwaka 2025. Hili halina ubishi kwa sababu tumo humu tunajua mengi. Kinachofanywa sasa ni kujenga mtandao wa kuungwa mkono na ndiyo maana unaona wanaotumika hapa ni wasanii na watu wa online, ” kinasema chanzo chetu na kuongeza:

“Angalia hata wajumbe wa bodi, baadhi yao wanateuliwa kwa sababu ni marafiki wa wakubwa wizarani.”

Mwanzoni mwa Desemba, mwaka jana wasanii saba walifanya ziara katika baadhi ya hifadhi kwa kile kilichoelezwa kuwa ni sehemu ya kujionea vivutio ili kuvitangaza, hivyo kuhamasisha wageni na wenyeji kutalii.

Ziara hiyo ilianzia katika Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato na kuendelea hadi hifadhi za taifa za Ibanda – Kyerwa na Rumanyika – Karagwe. Kiongozi mkuu wa msafara alikuwa Dk. Kigwangalla mwenyewe. Wasanii wa muziki na maigizo (Bongo Movie) walioshiriki ni Steve Nyerere, Dude, Richie, Shilole, Ebitoke, Shetta na mwakilishi kutoka Muziki AT (Zanzibar). Baadaye walizuru Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.

Rais Magufuli akizungumza na wahifadhi wa Rubondo, alisema: “Ninafahamu, watendaji wenu wa juu, Katibu Mkuu na Waziri kila siku wanagombana, ninawatazama taratibu na nilishampa kazi Katibu Mkuu Kiongozi awaite na awaeleze, lakini wasipobadilika nitawaondoa… Siwezi kuwa na watendaji ambao nimewateua mwenyewe halafu wanagombana, na kuna mambo mengi hayaendi. Katibu Mkuu hamheshimu waziri na waziri hataki kwenda na katibu mkuu, siwezi kuvumilia hilo.

“Leo nawaambia wajirekebishe na ikiwezekana wajirekebishe ndani ya siku tano, wawe wanasalimiana na wanazungumza, mimi ninafahamu, nina vyombo, ninajua nani hafai zaidi,” alisema Rais Magufuli.

Baada ya kauli ya Rais Magufuli, Waziri Kigwangalla kupitia akaunti yake ya Twitter alisema: “Kazi ya urais ni ngumu sana. Tulioteuliwa na Mheshimiwa Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea Rais frustration nyingine zaidi. Sisi kwenye wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary (Katibu Mkuu Kiongozi) tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari!”

Gazeti la JAMHURI limemtafuta Dk. Kigwangalla kwa njia zote za mawasiliano ili kupata maoni yake, lakini hakupokea simu wala kujibu maswali aliyoandikiwa. Katibu Mkuu, Profesa Mkenda, hakuwa tayari.

-Jamhuri (Toleo 07/01/2020)

Zaidi, soma:

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla ya kutoa habari hii kiungwana na kitaaluma ya uandishi wa habari makini na wenye weledi walitakiwa wahakikishe wamempata Kigwangala kwanza ilk kubalansi stori.
Kinachoonekana ni mkakati wa Balile na Adolf Mkenda kummaliza Kigwangala kisiasa,
Huyu Balile pia alitumika na kina Nape Nnauye kummaliza Makonda alichemka.

Naona anarudia yaleyale aliofanya kea Makonda.
,Ninavyofahamu Kigwangalah ni kijana mtiifu wa rais Magufuli,na anafanya kazi zake kwa nidhamu ya hali ya juu.

Angalizo,
Kuhusu Adolf Mkenda Rais Magufuli siku anamuapisha kuwa katibu mkuu wa hiyo wizara alimwambia nakupeleka huko nako ukafanye yako,ukivurunda ndio basi tena.

Ngoja tuone nani ataibuka kidedea,Uzuri wa vyanzo vya taarifa vya Rais Magufuli huwa makini sana.
Mwisho ,
Balile toka usifiwe na rais Magufuli kipindi kile kwenye sakata la mafuta kuhusu kodi ulivimba kichwa ,muda mwingine unaitumia kalamu yako vibaya.

Na mwisho kabisa si kwa umuhimu, wasanii ni muhimu sana kuwa nao karibu kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, si kwa Kigwangalah tu ,hata Rais Magufuli anawahitaji sana tu


Sent using Jamii Forums mobile app
Ni vema mtu unapozungumza jambo uwe una uhakika nalo,Jamhuri imetoa tuhuma kama izo,Wazir yupo na Katibu yupo wasijifiche wajibu hoja!

Unapoanza kumtetea mtu kwamba lengo ni kumchafua,aende Mahakamani.

Na umesema Balile ametumika kumchafua Makonda hebu weka wazi hapa tujadili kama hizo tuhuma ni za uongo?na Makonda alishaenda mahakamani kuhusiana na tuhuma hizo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wazi kwamba vijana bado hatuko tayari kupewa uongozi wa juu katika nchi. Vijana wote wakipewa nafasi wanafanya vibaya. Huyu nae anaingia kwenye list ya viongozi vijana wasio na vision wala charisma kama nilivyoeleza hapa chini

 
Umri ni kigezo muhim sana kuwa katika nafasi kubwa za maamuzi.

Vijana bado wanahitajo kuwa monitored,mihemuko bado ipo juu ya kuwa na utajiri na tamaa za madaraka makubwa. Hivyo wapo tayr kwa gharama yoyote kuona wanafikia hayo malengo.

Mojawapo ni hii ya matumizi mabaya ya fedha za umma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umri ni kigezo muhim sana kuwa katika nafasi kubwa za maamuzi.

Vijana bado wanahitajo kuwa monitored,mihemuko bado ipo juu ya kuwa na utajiri na tamaa za madaraka makubwa. Hivyo wapo tayr kwa gharama yoyote kuona wanafikia hayo malengo.

Mojawapo ni hii ya matumizi mabaya ya fedha za umma.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nakubaliana na wewe. Katiba inabidi iseme

ilikugombea urais lazima uwe na miaka 50
Ili kuwa waziri, naibu waziri au mkuuwa mkoa lazima uwe na miaka 45
 
Yule ni kiwanda cha pombe aina ya Spirit inaitwaga .....shim nani na maji ya habari unajua ushuru wa spirit upo juu sana? Pia biashara ya pombe inalipa sana? Kitimoto ndio the best Baddest Animal?
Ok ila JAMHURI mie nawaomba mfuatilie na lile sakata la mfanyabiashara wa Shinyanga aliyewaachisha kazi RPC na Meneja wa TRA mkoa huo!

Hiyo kesi ilianza upya? Jamaa ni nani? etc

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaah...! Siasa zina pesa jamani asikuambie mtu. Sasa hizi hela zote zinatolewa bila mpangilio milioni 170,hapa zinatumika milioni 20,150 mfukoni mwa wajanja ,mara 100,zinatumika 10,90 mfukoni,mara 200,zinatumika 20,180 kwa wajanja. Jamani,jamani hii nchi ni bure kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom