Geita: Mume amchinja mke wake na kisha yeye kujichoma kisu tumboni

Geita: Mume amchinja mke wake na kisha yeye kujichoma kisu tumboni

Kama wote wamekutwa na majeraha, kuna ushahidi gani mwanaume ndio kamchinja mkewe.
What if muuaji alitenda tukio kisha akafunga mlango na kusepa
 
Mbona siku hizi haya matukio yamezidi au ndio Chanjo ya Corona
 
Hali ya mambo imebadilika, ndoa ikifikisha miaka kumi fanya sherehe ya jubilei kana kwamba imefikisha miaka hamsini. Ndoa zimekuwa patashika nguo kuchanika, vikoba vimewatia jeuri wanawake wenye ndoa, ajira kwa mwanamke nayo ni tishio la kuvunjika kwa ndoa, kisa tu mwanamke ana hela haambiliki kwa mme wake. Wanaume wengi hawakuzoea hayo, hawataki jeuri, wanachukua maamuzi ya kijuha kumaliza kabisa jeuri ya mwanamke. Labda mwanamke mcha Mungu anaweza kuitunza ndoa yake kwa kumheshimu mume wake pamoja na kuwa amemzidi kipato. Wanaume wenye ndoa wapatiwe ushauri nasaha namna ya kuishi na wake zao wenye ajira na waliowazidi kipato, maana kwa hali ya kawaida si rahisi kudhibiti na kushikilia mapato ya mkewe na kuyatumia upendavyo hakuna maisha ya hivyo. Wanaume wasipende kujua mishahara na mapato ya wake zao, wapambane na hali zao familia ipate mahitaji. Wivu wa kimapenzi nao ni tishio na hatari kwa wanandoa.
 
Imetokea katika wilaya ya mbogwe kata ya lulembela mkoani geita, ambapo tukio limetokea mida ya saa 6 mchana.

Wawili hao wenye watoto saba imegundulika baada ya mtoto kutoka shule na kukuta nyumba imefungiwa ndani huku mziki ukiwa unapigwa (sabufa) badae mtoto akaenda kuita majirani baada ya kubomoa mlango wakakuta maiti ya mwanamke akiwa amejinjwa shingoni na pia maiti ya mwanaume huyo akiwa na alama ya kisu shingon na tumboni kilipokua kisu,

tayari polisi wameshafika eneo la tukio.


View attachment 1971274
[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]MME KAMCHINJA MKE WAKE
Labda jamaa aligundua watoto 7 sio wake
 
Imetokea katika wilaya ya Mbogwe kata ya Lulembela mkoani Geita, ambapo tukio limetokea mida ya saa 6 mchana.

Wawili hao wenye watoto saba imegundulika baada ya mtoto kutoka shule na kukuta nyumba imefungiwa ndani huku mziki ukiwa unapigwa (sabufa) badae mtoto akaenda kuita majirani baada ya kubomoa mlango wakakuta maiti ya mwanamke akiwa amejinjwa shingoni na pia maiti ya mwanaume huyo akiwa na alama ya kisu shingoni na tumboni kilipokuwa kisu.

Tayari polisi wameshafika eneo la tukio.


[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]MME KAMCHINJA MKE WAKE
Wivu wa Mapenzi! Ni kitu gani hasa hiki?
 
Hivi kuna kumchinja mtu miguuni?Ukisema "amchinja mkewe" inatosha!
 
Sasa wamejuaje kati yao yupi ndio aliyemchinja mwezie,kwani mwanamke awezi mchinja mmewe na yeye kujiuwa mnatuonea sana wanaume,kuna mijanamke mikatiliii mjue na ilo pia.....
... Watu wana taaluma zao kaka. Mfano maiti zilivyolala na silaha ilipo inaweza kutoa picha. Kwa mfano, kisu kilichotumika kimekutwa kimenasa tumboni kwa mmojawao logic ya kawaida itakutuma muuawaji ni nani?
 
wakristo tengenezeni mfumo wa taraka kuwa rafiki ili kupunguza haya mambo.
Kila siku kuuwana nyie tu kama ndio mnajua mapenz???????
Nakubaliana nawewe mkuu,biblia imeweka wazi hili Jambo


Mathayo 18:18

“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.

Tofauti na Hilo tutazidi kupoteza wapendwa wetu.
 
Kama wote wamekutwa na majeraha, kuna ushahidi gani mwanaume ndio kamchinja mkewe.
What if muuaji alitenda tukio kisha akafunga mlango na kusepa
Inaonyesha kulikua na sabufa imefunguliwa vol ya juu kabsa harafu huyo mwanaume baada ya kumchinja mke


ndipo alijaribu kujichija nayeye shingoni sijui akaona maumivu yanazidi maana pembeni kunaonekana kulikua na shati aliivua kwaajiri ya kurahisisha kitendo cha kujichoma kisu tumboni

ameacha watoto saba mmoja yupo 4m5wa kike mwingine 4m4 amehitim
 
Back
Top Bottom