Geita: Wanafunzi Saba wafariki na wengine kujeruhiwa na Radi

Geita: Wanafunzi Saba wafariki na wengine kujeruhiwa na Radi

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
Wanafunzi wa Kidato Cha Tatu Shule ya Sekondari Businda Wilayani Bukombe Mkoani Geita, wamepoteza maisha katika msiba, huku wengine 82 wakijeruhiwa baada ya kupigwa na radi wakiwa Masomoni

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Paskas Muragili amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea leo Jumatatu Januari 27, 2025.

Miongoni mwa majeruhi hao wawili wanaripotiwa hali zao mbaya. “Wakiwa darasani wakati wa mvua, radi ilipiga na kupoteza maisha ya wanafunzi saba. Kutoka kwa uchunguzi wa awali, sita walikuwa wavulana na mmoja alikuwa msichana. Hata hivyo bado tunaendelea na uhakiki wa

vitambulisho vyao kwani bado sijafika chumba cha kuhifadhia maiti,” alisema Mkuu huyo wa Wilaya. “Bado hatujawataja marehemu wote, lakini baadhi ya majeruhi wameshatoa majina yao.

Hali inavyoendelea, tutapokea taarifa rasmi,” aliongeza. Mkuu wa Wilaya alibainisha kuwa waganga walifika shuleni hapo mara moja kufuatia tukio hilo kutoa msaada wa dharura. Hili ni tukio la tatu kutokea Mkoani Geita. Tarehe 18 Oktoba 2019, wanafunzi 39 wa Shule ya Msingi Ihumilo wilayani Geita walijeruhiwa kwa radi.

Mwaka mmoja kabla, tarehe 17 Oktoba 2018, wanafunzi sita wa Shule ya Msingi ya Emaco Vision walipoteza maisha kwa msiba, huku wengine 23 wakijeruhiwa baada ya radi kupiga darasa lao.
Chanzo .The Citizens
 
Thamani ya kiumbe mweusi anayefanana na binadamu ni ndogo mno. Mamia wanakufa na kuawa baharini wakijaribu kukimbia ardhi yao. Ila viongozi wao wapo zao kimya utadhani wanauawa ni dagaa.

Ajali za barabarani kila siku zinamaliza watu, ila hakuna jitihada za maksudi za kumaliza changamoto hiyo.

Radi Leo imechukua maisha ya watoto 8 na uenda zaidi, ila wataishia kutoa pole tu.

Ila sishangai
IMG_0729.png
 
Radi isikie tu ila ni zaidi ya umeme.

Nakumbuka wakati nasoma Advance level Bukoba mkoani kagera. Kuna mwanafunzi mwenzetu alipigwa na radi akafia na kukauka hapohapo.

Mvua ilikuwa inanyesha kubwa sana, Sasa akawa ametoka na mwamvuli wake kwenda chooni, Eeeh! Bana. Ninachokumbuka niliona mwanga mkali sana tukiwa darasani. Kisha baada ya sekunde kadhaa ilipiga ngurumo moja kubwa kila mtu alibaki ameduwaa.

Mvua kuisha kuja kumcheki jamaa kashakauka, Kawa mweusi tii!!

Niliishi kwa hofu sana hadi nahitimu kidato cha sita.

Radi za kanda ya ziwa ni balaa hasa kagera, Geita.

Pia kuna hii video hapa inaonyesha wachezaji wa mpira wakipigwa na radi uwanjani...👇
 
Radi isikie tu ila ni zaidi ya umeme.

Nakumbuka wakati nasoma Advance level Bukoba mkoani kagera. Kuna mwanafunzi mwenzetu alipigwa na radi akafia na kukauka hapohapo.

Mvua ilikuwa inanyesha kubwa sana, Sasa akawa ametoka na mwamvuli wake kwenda chooni, Eeeh! Bana. Ninachokumbuka niliona mwanga mkali sana tukiwa darasani. Kisha baada ya sekunde kadhaa ilipiga ngurumo moja kubwa kila mtu alibaki ameduwaa.

Mvua kuisha kuja kumcheki jamaa kashakauka, Kawa mweusi tii!!

Niliishi kwa hofu sana hadi nahitimu kidato cha sita.

Radi za kanda ya ziwa ni balaa hasa kagera, Geita.

Pia kuna hii video hapa inaonyesha wachezaji wa mpira wakipigwa na radi uwanjani...👇
View attachment 3215797
Mkuu hii clip siisadiki ila yote kwa yote R.I.P vijana wa shule😭
 
Back
Top Bottom