Gen Z wa Tanzania wapewe ajira maana ukosefu wa ajira ni chanzo cha maandamano tunayoshuhudia Kenya na sasa Uganda

Gen Z wa Tanzania wapewe ajira maana ukosefu wa ajira ni chanzo cha maandamano tunayoshuhudia Kenya na sasa Uganda

Maandamano ya General Z wa Tanzania hayana sababu za msingi ajira zinatangazwa Kila kukicha na Serikali na sekta binafsi lakini yote kwa yote Serikali haina uwezo wa kuajiri vijana wote wa Tanzania hii isipokuwa watu kujiajiri wenyewe na ukizingatia Serikali inatafuta masoko ya mazao Kila leo mfano kusini watu wanapiga pesa ya korosho,ufuta na mbaazi,wakulima wa mahindi Zambia wanahitaji Tani 650,000/= NFRA wananunua kilo moja ya mahindi shs.700 kwa mjini na vijijini 600 ,ardhi imejaa tele nchi nzima,mvua za uhakika halafu kijana anaililia Serikali eti maisha magumu vijana wa Kenya wangekuwa na ardhi kama hii yetu tusingewaona kwenye maandamano zaidi ya kuwepo mashambani.
 
Wadau Asalam aleykum.

Wanasema mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Nawashauri viongozi wangu mlioko kwenye vyombo vya kutunga sera, mfanye kuwaajiri vijana walioko mtaani wenye ujuzi na wasio na ujuzi pia watafutiwe kazi za kufanya.

Hii itawafanya kuwa bize na hivyo kuwasahaulisha na ugumu wa maisha wanaokabiliana nao sasa.

Viongozi wangu, msijiamini kupitiliza kwamba nyinyi mna mifumo imara kuliko huko kunakofuka moto sasa.

Wanasema mwenye njaa mara zote huwa na hasira.

Pia wanasema kama huna kazi ya kufanya, basi chochote kinachokuja mbele yako unaweza kujikuta unakifanya! Shetani huwatumia sana wasio na kazi kutimiza agenda zake ovu.

Maandamano ni kama ugonjwa wa kuambukiza. Mara nyingi nchi nyingi zenye matatizo kama vile Libya, Tunisia, Misri, Sudan, na sasa Kenya na Uganda, maandamano huwa yanaanza kidogo kidogo na baadaye kusambaa nchi nzima!

Kama hali ikiendelea hivi ilivyo, basi tusishangae kuwaona Gen Z wetu nao wakiingia barabarani kuandamana.
Naomba kuwasilisha.


Ajira zinatokana na uwekezaji. Uwekezaji unakuja kama kuna mazingira mazuri ya biashara na mfumo imara. Tanzania haina mazingira mazuri ya biashara na mifumo mizuri. Tukipigania hapa mabadiliko ya mifumo bora na mazingira mazuri ya biashara mnatakiwa kuelewa tunapigania vijana wetu lakini wengi wenu hamuelewi na kuishia kubeza beza tu na wajinga jinga sana. Kazi haziokotwi na serikali inapata pesa kutoka kwenye kodi kazi yake sio kuajiri watu bali watu wachacha tu watekelezaji. Ajira zinatoka sekta binafsi.
 
Bora yaje tuanze upya, kuna koo Tanzania hazizidi 10 zinaishi kwenye sayari nyingine tofauti na sisi yaani zinaogelea kwenye utajiri na raha kwa kodi za watanzania wanyonge
 
Wasingoje ajira za serikali tu, waingie mitaani kwenye sekta binafsi.
wewe mbona hukuingia kwenye hiyo sekta binafsi? acheni ujinga, familia zenu zimejazana serikalini na mitaji mnayo ya kuwapa watoto wenu tena mikubwa, mbona hamuwapi hiyo mitaji watoto wenu waingie sekta binafsi?
 
MTU akikunyima ELIMU BORA

Akakupa simba na yanga

Ukaanza kufatilia connection

Na mwisho ukaamini umerogwa
 
mkuu ajira hazitoki kwakua serikali yetu haina hela.... na kwanini haina hela ni matumizi makubwa ya fedha kwenye uendeshaji wake...

mfano swala kama mwenge lingeweza kulipa watumishi wangapi? japo watumishi hao hao hulazimishwa kuuchangia mwenge kwenye wilaya husika.
ununuzi wa magari ya viongozi unashuhudia msafara wa lc 300 kama 30 zinampitisha kiongozi.
unadhani haya matumizi ni lazima au viongozi wanataka kutuonyesha kwamba hatuna la kufanya?

leo tunakopa nje na bado tumewekwa kwenye nchi maskini zaidi na sio kuwekwa ndio uhalisia

ogopa nchi ambayo wanatenga bajeti ya kununua magari mapya wakati yaliyopo bado yanalipa vizuri tu ninkamfumo ka kujimilikisha kanatafutwa
Kwanza kwa nchi masikini kama Tanzania hapakupaswa kuwa na mtumishi wa umma wa ngazi yoyote ile anayelipwa zaidi ya milioni 3 kama kweli ni uzalendo na siyo wizi wa mali za umma, badala ake kuna watu wanalamba mpk milioni 50 kwa mwezi nje na posho kibao, milioni 50 ingeweza kulipa graduate zaidi ya 60, nje na matumizi makubwa na ya anasa + wizi wa mali za umma.
 
Wadau Asalam aleykum.

Wanasema mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Nawashauri viongozi wangu mlioko kwenye vyombo vya kutunga sera, mfanye kuwaajiri vijana walioko mtaani wenye ujuzi na wasio na ujuzi pia watafutiwe kazi za kufanya.

Hii itawafanya kuwa bize na hivyo kuwasahaulisha na ugumu wa maisha wanaokabiliana nao sasa.

Viongozi wangu, msijiamini kupitiliza kwamba nyinyi mna mifumo imara kuliko huko kunakofuka moto sasa.

Wanasema mwenye njaa mara zote huwa na hasira.

Pia wanasema kama huna kazi ya kufanya, basi chochote kinachokuja mbele yako unaweza kujikuta unakifanya! Shetani huwatumia sana wasio na kazi kutimiza agenda zake ovu.

Maandamano ni kama ugonjwa wa kuambukiza. Mara nyingi nchi nyingi zenye matatizo kama vile Libya, Tunisia, Misri, Sudan, na sasa Kenya na Uganda, maandamano huwa yanaanza kidogo kidogo na baadaye kusambaa nchi nzima!

Kama hali ikiendelea hivi ilivyo, basi tusishangae kuwaona Gen Z wetu nao wakiingia barabarani kuandamana.
Naomba kuwasilisha.
Kila mmoja anaboda yake
 
Kwanza kwa nchi masikini kama Tanzania hapakupaswa kuwa na mtumishi wa umma wa ngazi yoyote ile anayelipwa zaidi ya milioni 3 kama kweli ni uzalendo na siyo wizi wa mali za umma, badala ake kuna watu wanalamba mpk milioni 50 kwa mwezi nje na posho kibao, milioni 50 ingeweza kulipa graduate zaidi ya 60, nje na matumizi makubwa na ya anasa + wizi wa mali za umma.
Wewe ni mchochezi
 
wewe mbona hukuingia kwenye hiyo sekta binafsi? acheni ujinga, familia zenu zimejazana serikalini na mitaji mnayo ya kuwapa watoto wenu tena mikubwa, mbona hamuwapi hiyo mitaji watoto wenu waingie sekta binafsi?
Sijawahi kuajiriwa na serikali.
 
Tupo katika wakati ambao vijana wetu wengi wanapitia hali ya sintofahamu hatima ya maisha yao kutokana tatizo kubwa ukosefu wa ajira.

Ni vyema watu wote wenye mamlaka wajue wanatatua vipi tatizo wanahaidi Nini na hatua gani watakazoenda kuzichukua
Hali kwa sasa inaonekana ni shwari mana watawala wameshajihakikishia ulinzi kutoka kwa polisi

Itafika muda ambao vijana watakuwa hawana Cha kupoteza vijana wengi wamekosa matumaini itafika mahali ambapo ata mtu ataona yeye akifa hana atakalolipoteza
 
Watawala wanajiaminisha kuwa vijana wa TZ bado sana hawajitambui ndio maana wana promote boda boda kama kipaumbele cha ajira.
 
Mimi kama muwakilishi wa Generation Z nasema ya kwamba HATUTO ANDAMANA WALA KUFANYA VURUGU UNAYOIHAMASISHA!! KAMA wewe kweli unataka ufanye VURUGU nenda ofisi ya serikali iliyokaribu ukajitokeze kuliko kujificha nyuma ya keyboard
 
Mimi kama muwakilishi wa Generation Z nasema ya kwamba HATUTO ANDAMANA WALA KUFANYA VURUGU UNAYOIHAMASISHA!! KAMA wewe kweli unataka ufanye VURUGU nenda ofisi ya serikali iliyokaribu ukajitokeze kuliko kujificha nyuma ya keyboard
Mkuu umesoma na kuelewa kilichoandikwa? Au umerukia gari kwa mbele? Soma kwa kutafakari na kutulia sijaona alipohamasisha vurugu.
 
Back
Top Bottom