Kwa Mara ya kwanza naomba nikukosee heshima Leo wewe ni mchawi aiseee
Jamaa na kuelezea kote juu ya kifo cha General tyre wewe unapinga tu
....Wakiristooooo ! NgongoHaaa haaa aliuza formula ya 7.50 - 16 HCT YANA ni Kipingu swala tano aliyesimamia zoezi na kufanya safari za kwenda Kenya mara kwa mara ni Philip Mweta Quality Assurance Manager wakati kabla hajapelekwa sales huyu naye ni muislam swala tano usibabishwe na hilo jina ni la kusomea tu alichukua nafasi ya mgalatia aliyefaulu baada ya yeye kufail.
Sales and Marketing Manager enzi za Mwl Nyerere alikuwa Kibwana swala tano huyu kazi yake kubwa ilikuwa ni kuoa akina Mama kila mwaka.Mke wake wa mwisho alikuwa mrembo wa Air Tanzania baada ya kuiba vya kutosha akakimbilia kugombea ubunge akashindwa mwanamke mrembo akamkimbia siku hizi nasikia kaolewa na Maulid Kitenge kama mke wa pili.
Suala ya kufa viwanda halina uhusiano na dini ya mtu lakini kwakuwa umekimbilia mkondo huo si vibaya nikikupa za uso.
Serekali baada ya kushindwa kuyasimamia mashirika yaliyokuwa yakiwaingizia fedha nyingi kupitia kodi mbali mbali na kuyaacha yajifie kifo cha mende siku hizi imekimbilia kunyakua fedha kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF,PPF...........matokeo yake wachangiaji wa hii mifuko inayokaribia kufilisika ni kutunga sheria na kanuni za kuwabana wachangiaji ambao ni wafanyakazi.
hichi kiwanda juzijuzi kinana alienda kukitembelea akakuta ni ghala tu siku hizi....ukipita pale ni kama gofu tuNgongo
Samahani kaka mkubwa naomba unijuze tu!! Hivi kiwanda kilichokuwa jirani wa kiwanda cha General Tyre cha KILITEX kilichokuwa kinatengeneza nguo kipo au nacho ndo tumeshakula mtaji??
Watanzania waliokosa uzalendo wamelaghaiwa na wahindi na Waarab kulifilisi hili taifa chunguza viwanda mfu vyote vimenunuliwa na wahindi na Waarab then wakawa ma supplier na wagavi wa bidhaa zilizokuwa zikizalishwa na viwanda hivyo kutoka nje.
Wahindi sio watu wema kabisa na uchumi wa nchi yetu.
.. ndugu yangu Ngongo, unashangaza sana kama ambavyo watanzania wengi wamekuwa wakishangaza, mnamsifia Nyerere upande mmoja halafu hapo hapo mnamkosoa upande pili. Umesema Nyerere alianzisha General tyre kwa makubaliano ya umiliki wa 74% kwa TZ na 26% USA, lakini hapo hapo, nanukuu kauli yako: "WATANZANIA BADALA YA KUINGIZA VICHWA VYA UKWELI TUKAWAPA UJUMBE WA BODI AKINA GULLAMAL, SHELLUKINDO NA WABUNGE WENGINE WENGI KWA AJILI YA KULIPANA POSHO" mwishi wa kunukuu
Wajumbe wa bodi za mashirika ya umma wanateuliwa na mh rais, kwa maana hiyo hao waliokuwa wajumbe wa bodi ya General Tyre, walioua shirika hilo waliteuliwa na Nyerere kwa ajili ya kulipana posho. Halafu kumbuka kila walipoharibu hakuwawajibisha ndiyo maana mashirika yote kufa hata kabla Nyerere hajaondoka madarakani ila alikuwa anayanusuru kwa usanii wa kuyapa ruzuku ili yaonekane yapo hai.
Wewe wacha porojo za ajira. Hapa inaongelewa General Tyre. Wajomba na shangazi zako waliokuwa wanapendelewa kwa kuchaguliwa kuendelea na masomo ndiyo hao hao wakaviua viwanda mpaka Serikali ikaamuwa kujitowa kwenye biashara.
Nini usichokifahamu, sasa mkatafute ajira kwenye makampuni binafsi, kama mlikuwa mnategemea mtarithi kwenye mawizara, mashirika ya umaa na idara za Serikali, sasa hivi huko ajira ni chache sana, almost hakuna.
Kuweni wabunifu mzinduwe kazi za kufanya si kungoja Serikali iwafanyie kila kitu. Anza kwa kuuza kashata kisomi.
Hivi hizo shule mnaenda kusomea ujinga?
naungana nawe sana. kweli unaweza enda shule na usieleimike, watu wamebaki na ushabiki wa kisiasa tu, ndio mambo machafu yametendeka ila ninauhakika karibu 90% ya wale wanaishutumu serikali nao ni mafisadi vile vile. Nina hakika ndio wa kwanza kukwepa kodi, kupokea hongo na rushwa kupitisha magendo kusoma magazeti siku nzima ofisini na kubia makampuni ila wanakaa kando na kunyoosha vidole serikali. Tunakuwaje watu tusio weza kujisimamia na kujiendesha wenyewe?!
Kuokoa taifa ni jukumu letu sote lazima kila mtanzania avae uzalendo na kusimama katika nafasi yake kuitetea nchi tuwe na uchungu basi japo kidogo tu, nakwambia hata kije chama gani kipya mambo ni yaleyale tuu maana watu waliopo kwenye system ya uchumi uwe serikalini au shirika la umma au binafsi hamweki maslahi ya taifa mbele mnasumbuliwa na ubinafi, uchoyo, ulafi na umimi tu.
Na ni vyema kumwangalia mgombea kama mgombea na kueka uchama pembeni maana sidhani kama wote wa ccm ni wachafu au wote wa upinzani ni wasafi na waadilifu.
Be wise people, it begins with you.
asingeamini kwamna hivi sasa nyama ya ng'ombe inauzwa 6,000/- badala ua sh.5, shillingi inaporomoka mno kwa ukosefu wa viwanda..Dah.....laiti mwalimu nyerere akipewa bahati ya kufufuka akiiona Tanzania yake ilivyo na akiwaona watanzania wake walivyokata matumaini anaweza akafa tena kwa mstuko.......