Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wakuu!
Naona vijana wanaendelea nguvu ya uchawa kawa Rais maana kila kitu sasa utasikia Samia hivi na vile yani hashitag kibao kumuhusu Rais Samia.
Sasa ndiyo njia pekee ya kufanikiwa kwenye mambo yao? Hii ni to much
======================
Programu mpya ya vijana inayojulikana kama Generation Samia (Gen S) imezinduliwa rasmi, Disemba 2, 2024, jijini Dodoma, kwa lengo la kuwaunganisha vijana wa Kitanzania kutoka sekta mbalimbali na kuwajengea mtandao wa fursa za maendeleo.
Akizungumza katika uzinduzi huo, msemaji wa @Gen_samia, Sonata Nduka, amesema programu hiyo inalenga kuwa chachu ya mafanikio kwa vijana, ikiwakutanisha kutoka nyanja tofauti kama wajasiriamali, wafanyabiashara, wanamichezo, wasafirishaji, na wajenzi.
Sonata amesema Gen S inalenga kufanikisha ndoto za vijana kupitia juhudi za pamoja huku ikichagiza matumizi ya mazingira rafiki yaliyowekwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha uchumi wa vijana.
Soma Pia: Samia Kagera CUP Yahitimishwa kwa Kuwahamasisha Vijana Kushiriki Uchaguzi Serikali za Mitaa
Katika hatua ya kuimarisha mtandao wa vijana, Gen S imeandaa tukio la mbio za pamoja lijulikanalo kama Gen S Jogging, litakalofanyika Jumamosi, Disemba 7, 2024, kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Mbio hizo zitaanza saa 12 asubuhi na kumalizika saa 3 asubuhi, zikiwaleta pamoja vijana kutoka makundi tofauti, ikiwa ni pamoja na vikundi vya jogging, wafanyabiashara, wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali, pamoja na wanamichezo.
Sonata amesema tukio hilo si tu fursa ya kujenga mtandao wa kijamii na kiuchumi bali pia litakuwa sehemu ya burudani kwa vijana wa mjini.
Naona vijana wanaendelea nguvu ya uchawa kawa Rais maana kila kitu sasa utasikia Samia hivi na vile yani hashitag kibao kumuhusu Rais Samia.
Sasa ndiyo njia pekee ya kufanikiwa kwenye mambo yao? Hii ni to much
======================
Programu mpya ya vijana inayojulikana kama Generation Samia (Gen S) imezinduliwa rasmi, Disemba 2, 2024, jijini Dodoma, kwa lengo la kuwaunganisha vijana wa Kitanzania kutoka sekta mbalimbali na kuwajengea mtandao wa fursa za maendeleo.
Akizungumza katika uzinduzi huo, msemaji wa @Gen_samia, Sonata Nduka, amesema programu hiyo inalenga kuwa chachu ya mafanikio kwa vijana, ikiwakutanisha kutoka nyanja tofauti kama wajasiriamali, wafanyabiashara, wanamichezo, wasafirishaji, na wajenzi.
Sonata amesema Gen S inalenga kufanikisha ndoto za vijana kupitia juhudi za pamoja huku ikichagiza matumizi ya mazingira rafiki yaliyowekwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha uchumi wa vijana.
Soma Pia: Samia Kagera CUP Yahitimishwa kwa Kuwahamasisha Vijana Kushiriki Uchaguzi Serikali za Mitaa
Katika hatua ya kuimarisha mtandao wa vijana, Gen S imeandaa tukio la mbio za pamoja lijulikanalo kama Gen S Jogging, litakalofanyika Jumamosi, Disemba 7, 2024, kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Mbio hizo zitaanza saa 12 asubuhi na kumalizika saa 3 asubuhi, zikiwaleta pamoja vijana kutoka makundi tofauti, ikiwa ni pamoja na vikundi vya jogging, wafanyabiashara, wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali, pamoja na wanamichezo.
Sonata amesema tukio hilo si tu fursa ya kujenga mtandao wa kijamii na kiuchumi bali pia litakuwa sehemu ya burudani kwa vijana wa mjini.