Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Mwambie hiviiii," KUNA MTU KAAGA BBC LEO", HOMU KAMINGI
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Ndugu yangu nimepandwa na hasira hapa.

Hii kauli ni msumari kwenye box la CCM.

Kauli hii ni aibu kubwa
 
Watanzania wengi wana mihemko na hawako objective, ndio maana serikali huwa inapuuza na kungojea mijadala ife yenyewe, kubishana nao ni kupoteza muda.

Msigwa ameongea ukweli mtupu, wenye uzoefu na ripoti za CAG wanayajua hayo, huwa zina makosa mengi tu, na ndio maana baadhi ya hoja zake huwa zinafutwa na kufungwa kabisa.

Wanaofanya ukaguzi ni watumishi wa umma wa kawaida tu, tena wengine wameajiriwa juzi juzi hapa hata uzoefu hawana. Watu huwa wanadhani Kichere mwenyewe ndio anakwenda 'site'.

Hatusemi kuwa ripoti yote imejaa makosa, tunachosema ni kuwa watu wawe watulivu utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria ufuatwe, wenye makosa watachukuliwa hatua na wale wasio na makosa hoja zao zitafutwa.

Kwa hisia kali za watanzania ni bora Msigwa angekaa kimya, sometimes it doesn't matter if you are correct.
Utaratibu wa utoaji wa Ripoti ya Ukaguzi,hupitia hatua mbalimbali.Kwanza wahusika(watuhumiwa) hujibu hoja hizo kwa maandishi (pengine zaidi za mara moja).Mpaka unaona hoja zinakuja kwenye Ripoti humo,maana yake hazikuweza kutatuliwa (outstanding issues) mpaka wanapotoa Ripoti.Pia zinafungwa(closed) na CAG mwenyewe kama zina majibu ya kuridhisha na wala sio Bunge au Serikali.Zinakwenda Bungeni na Serikalini kwa ajili na "kuchukua hatua stahiki" kwa mujibu wa sheria.Kuwa na "dhana" kwamba unaweza kubishia Ripoti ya CAG "hewani" au kwenye Jamii forum ni kukosa uelewa wa taarifa za Ukaguzi namna zinavyofanya kazi.
 
Unadhani wanakaa kwenye taasisi moja kwa muda gani? CAG hana workforce ya kukagua taasisi zote kwa pamoja, wanatumia muda mfupi sana kwenye kila eneo.

Mbali na hapo watumishi wa ofisi ya CAG wanaweza kuwa na changamoto za uelewa wa baadhi ya mambo, jambo ambalo ni kawaida kwa watumishi wote serikali, wao sio malaika. Kuna vitu wanaibua kama dosari ambavyo sio dosari.

Hata wakipewa maelezo na vielelezo haisaidii, ndio maana kwa mujibu wa sheria ripoti ya CAG ni 'input' kule bungeni, sio final.

Lazima kamati za bunge zipitie kwa umakini hoja zote, na wakihitaji maelezo zaidi pande zote mbili zinaitwa, upande CAG na taasisi husika.

Mara nyingi tu CAG mwenyewe anaridhia baadhi ya hoja zifutwe baada ya wote kukalishwa na kamati ya bunge.

CAG ni kama mwendesha mashtaka, kushtakiwa haimaanishi una hatia. Bunge ndio mahakama, na taasisi zenye kasoro ni watuhumiwa.

It's basic stuff, but somehow people don't get it. Ndio maana nasema watanzania wengi ni wajinga.
Wenzio walitaka siku ile kesho yake waone makarandinga yamejaza watuhumiwa pale kisutu. Au wasukie CAG amefukuzwa kazi kama alivyofukuzwa ASSAD Hapo ahhh ungesikia raisi anapinga ufisadi kwa vitendo. Wajinga tu hawa wabongo
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
MSIGWA hana uwezo kiakili wa kuwa hata Msemaji wa mkoa.
 
CAG huwa hafukuzwi acha kupotosha. Yule alimaliza awamu yake ya Kwanza ila haukuongezewa muda, baada ya kupasua ufisadi wa trioni 1.5
Lakini unajua kwamba kwenye kesi ya kikatiba iliyofunguliwa Mahakama ilitamka wazi kuwa aliondolewa ofisini kinyume Cha katiba Sheria na Taratibu ambapo kwa neno moja Ni kufukuzwa?
 
Miaka yote mbona iko hivyo, bunge la hili huwa ni la bajeti.
Basi waambieni wabadilishe sheria tunataka baada ya report ya CAG kutoka, mapungufu yafanyiwe kazi kwa haraka sana na wezi wa Mali za Umma wafikishwe Mahakamani kwa haraka sana ili kuleta nidhamu kwa Watumishi wengine watakao taka tafuna Mali ya Umma! Mali ya Umma lazima iogopewe na kila Mtu!!
 
Yani hoja km yako, zinatia kichefu chefu. Hivi unajua maana collective responsibility? Ebu nikuulize, wakati Mwinyi anajiuzulu nafasi yake alikuwa ametenda yeye kosa au watendaji wake wa chini? Mzee Lowasa wakati anajiuzulu alikuwa ametenda yeye makosa au watendaji wake wa chini? Walimu 6 huko Tabora waliotuhumiwa kuvujisha mtihani na hatimae kukaa jela takribani miaka mitatu na baadae mahakama kusema hawakuwa na makosa na kuachiliwa hivi majuzi wao hawakuwa watu?

Kinachosemwa na wananchi ni kuona waliotuhumiwa wote wanaachia ofisi kupisha uchunguzi juu ya tuhuma zao, na ikibainika hawakuwa na makosa wataendelea na kazi km awali. Kwanini wao wana dinda kuachia ofisi kwani ni mali Yao. Kwani hao niliowatolea mfano hapo juu wao hawakuwa na moyo wa nyama?

Achana na ushaabiki wa kisiasa kwenye mambo ya msingi na nyeti kuliko hata nyeti ulizonazo. Watu wajifunze kuishi bila gari za serikali, mafao ya serikali, nyumba za serikali, na kupenda ubwanyenye mbele ya Watanzania wenzao. Tabia za baadhi ya viongozi wa Kitanzania kupenda kunyanyua makwapa na kupandisha mabega huku wakilamba asali kwa ncha ya kisu ndivyo vinavyosababisha ugumu wa kujiuzuru kwa manufaa ya umma pindi anapotuhumiwa.

Nimemaliza.
Nikupe tu pole. Audit queries zinatolewa then zinajibiwa na hapo mjadala unafanyika kuhusisha audit query na majibu. Kama unafikiri audit query ni verdict, you simply miss the point. Na ni lazima upate kichefuchefu.
 
Back
Top Bottom