Gerson Msigwa: Matunda Matamu Ya Siku 150 Za DP World Bandarini, Serikali Yakusanya Billion 325

Gerson Msigwa: Matunda Matamu Ya Siku 150 Za DP World Bandarini, Serikali Yakusanya Billion 325

Ujinga mtupu, serikali ilitakiwa ikusanye trillion 1 kwa mwezi kutoka bandarini
Hela ndogo sana aese! Najiuliza hivi wabongo tunaweza kusimamia kitu gani? Maana mambo yanaenda hovyo hovyo tu!
 
Hizo ela anaingiza mo kwa biashara zake tuu ...
 
Yani Bil 2.16 ni hela ya kufurahia kupata mapata ya bandari kama Dsm ambapo nchi zaid ya 8, wanategemea bandari hii? 😳 Tafsiri yake hata icho kiasi kimepikwa na wameona ni hela nyingi, hivyo mwanzoni ilikuwa pungufu zaidi ya hapo, Aiseee 🤔 huku sio kuiba nikusombelea hela mifukoni kwa watu😳😳🥺
 
Yani Bil 2.16 ni hela ya kufurahia kupata mapata ya bandari kama Dsm ambapo nchi zaid ya 8, wanategemea bandari hii? 😳 Tafsiri yake hata icho kiasi kimepikwa na wameona ni hela nyingi, hivyo mwanzoni ilikuwa pungufu zaidi ya hapo, Aiseee 🤔 huku sio kuiba nikusombelea hela mifukoni kwa watu😳😳🥺
Acha wivu wako hapa wewe
 
Kwa hakika Watanzania wamefurahi sana kuona namna jitihada na juhudi za Mheshimiwa Rais kuvutia wawekezaji na uwekezaji zikizaa matunda ndani ya muda mfupi sana.
Vipi shati lako la ccm limeboreshwa au ni Lile Lile la kitenge Hela si imeingia. Mama atakushonea na suruali ya kitenge
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika Mama ameifungua Nchi na Sasa Asali na Maziwa vinatiririka na kumiminika Tu hapa Nchini.kwa hakika kila mmoja analamba asali Kiganjani mwake.Embu nisiwachoshe na kuwapunguzia Utamu .

soma hapo chini👎

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema matunda ya uwekezaji wa DP World katika Bandari ya Dar es salaam yameanza kuonekana ambapo katika kipindi cha miezi mitano tangu ianze kuendesha Bandari hiyo Serikali ya Tanzania imekusanya Tsh. bilioni 325

Akiongea Jijini Dar es salaam leo December 19,2024, Msigwa amesema “Tumeanza kuona matunda matamu ya DP World ndani ya kipindi kifupi sana, tangu kampuni ya DP World Dar es salaam ianze uendeshaji katika Bandari ya Dar es salaam mwezi April 2024, tumepata mafanikio yafuatayo, kwa mujibu wa mkataba kampuni ya DP World ambayo kwetu Tanzania inakuwa DP World Dar es salaam inapaswa kuwekeza USD mil 250 (Tsh.bilioni 675) katika kipindi cha miaka mitano, sasa katika kipindi cha miezi mitano tu tayari kampuni hii imeshawekeza Tsh. bilioni 214.425 na hii ni sawa na 31% ya uwekezaji tuliotarajia katika kipindi cha miaka mitano”

“Maana yake huko nyuma kulikuwa na maneno tumeweka Wasanii sijui nini watakuja sasa hapa kwa lugha ya Kikinga we mean business na tutasimamia mkataba huu kuhakiksha maslahi ya Watanzania yanalindwa”

“Ukarabati wa mitambo iliyokuwa ya TPA imefanyika na usimikaji wa mifumo ya TEHAMA ya uendeshaji wa Bandari umefanyika, sasa manufaa mengine ambayo wakati ule tuliyaimba sana tukaitwa Wasanii na mambo mengine mengi, wastani wa muda wa meli kusubiri wakati ule meli zetu zilikuwa zinasubiri siku 46 nyingine hadi siku 70 lakini sasa hivi meli zinasubiri kwa siku 7 maana yake tunapunguza gharama ambazo Serikali kupitia TPA imekuwa ikiwalipa wenye meli kutokana na meli zao kusubiri muda mrefu kushusha mizigo, na hiyo ni wastani lakini zipo meli hazisubiri kabisa, meli za makasha hakuna kusubiri zikija zinashusha zinaondoka”

“Tunaendesha bandari kwa faida, tulikuwa tunaendesha bandari kwa hasara, katika kipindi cha miezi mitano tangu DP World waanze kazi Serikali imefanikiwa kukusanya Tsh. bilioni 325.3 ikiwa ni mapato yanayotokana na shughuli za mikataba iliyoingia kati ya TPA na DP World, haya ni maeneo ambayo tulipotoshwa sana tumeanza kupata faida”
#MillardAyoUPDATES

View attachment 3180294

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Binafsi naona hiyo milions 600+ iliyokuwa imewekwa ni ndogo sanaa kulingana na mapato yanayopatikana pale. Walau mkataba ungesema Bil 2000 kidg ingekaa vzr. Lakini si mbaya madam tumejifunza, next time serikali yetu itaset mikataba mizuri
 
Kwani wewe ni kipofu mpaka huoni ziliko kwenda? Kwamba huoni barabara zikiendelea kujengwa?huoni shule za msingi kwa sekondari zikiendelea kujengwa?huoni mishahara ya watumishi wa umma ikiendelea kuwahi kutoka? Huoni ajira kwa vijana zikiendelea kutolewa? Huoni huduma za afya zikiendelea kuboreshwa? Huoni namna madawa ,vifaa tiba na wataalamu wa afya wakiendelea kujaa katika vituo vya afya mpaka hospitali za kanda mpaka Taifa? Huoni namna serikali inavyotoa ruzuku katika kilimo? Huoni serikali namna inavyonunua mazao ya wakulima kwa bei nzuri na yenye kuleta tabasamu kwa wakulima?
Aya bhana! Kwahiyo hizo hela ni za watanzania au hela za samia?? Team Mapambio bhana
 
Back
Top Bottom