Ghafla CCM wanampenda Lissu. Yeye ataingia mtegoni?

Ghafla CCM wanampenda Lissu. Yeye ataingia mtegoni?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Tundu Lissu ni mwanasheria makini na mwanaharakati maarufu wa haki za binadamu. Lakini natilia shaka kama yeye ni mwanasiasa mahiri na pia sijui kama yeye pia anajua nafasi yake aliyopo kisiasa.

Wengi wetu tunajua kuwa tangu mwaka 2005 CHADEMA kwa mara ya kwanza kusimamisha mgombea uraisi, CCM imekuwa inatamani sana CHADEMA igeuke kuwa NCCR ya zama hizi.

Harakati za CCM kuisambaratisha CHADEMA zilikuwa zinafanyika toka nje ya CHADEMA kwa umma dhidi ya CHADEMA.

Lakini tangu baada ya uchaguzi wa mwaka 2020, CCM inaonekana imepata usaidizi usiotarajiwa toka kwa Tundu Lissu.

Lissu inawezekana amejipa daraja la kuirekebisha CHADEMA kutokea nje, badala ya ndani ambako yeye ni mjumbe wa vikao vya chama.

Lissu anakikosoa chama chake kutokea nje kiasi kwamba inazusha maswali mengi sana kumhusu Lissu na kujitambua kwake kisiasa.

Makamu Mwenyekiti wa chama inawezekanaje ukawa si sehemu ya maamuzi ya vikao ambavyo wewe ulishiriki na kufanya mijadala iliyofikia maamuzi husika?

Kama maamuzi ya vikao yalikuwa na makosa, kwa nini yeye aamini kuwa si sehemu ya makosa hayo ya vikao?

Bahati mbaya Lissu kila anachosema sasa kinapokewa kwa chereko kubwa sana toka CCM.

Sasa hivi makada maarufu wa CCM ndiyo wamekuwa ni wasambazaji wakubwa wa kila wanachoona kama ni kiashiria cha mfarakano ndani ya CHADEMA kutokana na maneno yasemwayo na Lissu.

Hawa wana CCM ambao walisema waziwazi kuwa walitamani Lissu angekufa kwenye lile shambilio la Dodoma leo ghafla wamekuwa ni waunga mkono mitizamo ya Lissu?

Lissu mwenyewe anaelewa kinachoendelea?
 
Msitafute mtu wa kumtupia lawama, CHADEMA ilijiua yenyewe 2015 kwa kuondoa ule utakatifu, credibility na ajenda yake dhidi ya ufisadi. Baada ya hapo vilivyofuata ni kelele zilizokosa direction kiasi cha kudandia matukio kama commentators.

CHADEMA jivueni gamba kama mnaweza, muda mnao
 
Ccm ni chama mfu. Hakitaki kusikia mawazo yenye kuamsha hisia za watu. Lisu anakiumiza kichwa kweli chama cha MANGURUWE (ccm)
Anajua anategwa Ili apotezwe? Kajifunza chochote toka kwa Ibrahim Lipumba wa CUF au Zitto Kabwe wa CHADEMA aliyetoka akiaminishwa na CCM kuwa anayo nguvu ya kuanzisha chama cha "kuibomoa" CHADEMA?
 
Msitafute mtu wa kumtupia lawama, CHADEMA ilijiua yenyewe 2015 kwa kuondoa ule utakatifu, credibility na ajenda yake dhidi ya ufisadi.
Yaani kwa maelezo yako haya unaashiria kuwa CCM ni chafu ila CHADEMA imekosa "credibility" ya kuikosoa CCM kwa kuwa tu ilimsimamisha Edward Lowasa kugombea urais mwaka 2020.

Kwa mtazamo huo wewe unaweza kuvumilia ufisadi unaofanywa na CCM, ila huwezi kuamini imepita miaka 9 tangu Lowassa agombee urais ivo hiyo unayosema "credibility" ya kuikosoa CCM imerudi CHADEMA.

Kama CCM ndiyo inayofanya ufisadi, lawama unazielekezaje CHADEMA?
 
Upinzani sio chama wala mtu !!! Upinzani ni ideology miyoyoni mwa watu.
Ideology bila action ni sawa na kupanda mbegu pasipo kujali misimu ya mvua na jua. Mwisho wa siku hutoweza kujua lini itazaa matunda

Nadhani CHADEMA inahitaji strategist wazuri kama bado wanafikiria kurudi katika ubora wao maana ni wazi watu waliopo behind the scene hawajaweza kutetemesha nchi. Wajisuke na kujipanga upya tu na sio kusubiri watu wakosee ili wawalaumu maana ni sawa na kujichimbia kaburi zaidi
 
Tofautisha maoni binafsi ya Lissu na maamuzi ya Makamo Mwenyekiti wa CHADEMA ndani ya vikao.

Mbowe ameshwaambia makada " tu umiliane".
Maoni binafsi yanayogusa taasisi unayoiongoza hayawezi kuwa maoni binafsi.

Ukisikia Rais anasema kwa maoni yake binafsi Waziri Mkuu atekelezi kazi yake ipasavyo. Maoni hayo binafsi utayatenganishaje na nafasi yake ya uraisi anayoishikilia?
 
Maoni binafsi yanayogusa taasisi unayoiongoza hayawezi kuwa maoni binafsi.

Ukisikia Rais anasema kwa maoni yake binafsi Waziri Mkuu atekelezi kazi yake ipasavyo. Maoni hayo binafsi utayatenganishaje na nafasi yake ya uraisi anayoishikilia?

..kuna exaggeration na misinterpretation inafanyika ili kuonyesha kuna mgogoro Chadema.

..mtu asipojiongeza kwa kwenda kwenye chanzo cha uhakika cha habari anaweza kuyumbishwa na propaganda za Ccm.
 
Yaani kwa maelezo yako haya unaashiria kuwa CCM ni chafu ila CHADEMA imekosa "credibility" ya kuikosoa CCM kwa kuwa tu ilimsimamisha Edward Lowasa kugombea mwaka 2020.

Kwa mtazamo huo wewe unaweza kuvumilia ufisadi unaofanywa na CCM, ila huwezi kuamini imepita miaka 9 tangu Lowassa agombee urais ivo hiyo unayosema "credibility" ya kuikosoa CCM imerudi CHADEMA.

Kama CCM ndiyo inayofanya ufisadi, lawama unazielekezaje CHADEMA?
Na hii ndio sababu CHADEMA inazidi kuisha kwa sababu ipo obsessed na CCM kama shabiki badala ya mkubwa mwenzie. Inasubiria CCM au watumishi wa serikali wakosee ili watoe tamko kana kwamba bila hivyo hawana relevance. Hii ni mbaya sana

CHADEMA ya kabla ya 2015 ilikuwa na clear vision and agenda. Ilikuwa na vichwa vyenye mawazo fresh ambayo wengi wetu tuliwaona kama idols hadi ikafikia kijana akisema ni CCM alionekana kama amezeeka kifikra

Kwa hiyo kuiweka CCM na CHADEMA kwenye sentensi moja ya uchafu tayari inaonesha jinsi CHADEMA imefubaa.

By the way mkuu mimi naongea kama mtizedi tu, kufuatilia na kuzichambua siasa nishaacha muda sana kuepuka sonona. Ila jua tu CHADEMA mnahitaji vichwa haswaa na sura mpya za kufufua chama na sio hizi zinazotegemea activism. Tunahitaji LEADERS
 
CCM mtasubiri sana kwa Lissu, hawezi kujiunga na kumdi la wabakaji wa demokrasia kamwe.

Leo alikuwa Singida kumzika mwanachama wake aliyeuawa kwa kupigwa risasi na askari. Tafuta clip yake sikiliza kwa makini
 
CCM watasubiri sana kwa Lissu, hawezi kujiunga na kundi la wabakaji wa demokrasia kamwe.

Leo alikuwa Singida kumzika mwanachama wake aliyeuawa kwa kuoigwa risasi na askari. Tafuta clip yake sikiliza kwa makini
 
Nchi inatetemeshwaje? Yaani nini kifanyike ili Nchi itetemeshwe?

Anzeni kwa kuleta sura mpya ambazo ni za viongozi wenye intellect, credibility and class. Zalisheni watu kama Zitto Kabwe wa mwanzo ambao watakuja na solutions na sio complaints au activism kama sasa. Lazma wawe na sura ya uongozi zaidi kuliko activism

Kingine rudini kwenye mioyo ya watanzania wa hali ya chini kwa kusolve matatizo yao. Kama vijana wa vyuo wanaanzisha taasisi za kusaidia maskini, itakuwa taasisi kama CHADEMA ?..

Hivyo onekaneni kwa watu na sio kusubiri mpate madaraka ndio mfanye kitu. Prove your worth

Tafuteni pia strategists wa kukisuka chama vizuri ili kuja na mkakati na vision madhubuti . Wawashauri na mengineyo pia
 
Ukisikia CCM imempenda Lissu ujue ni mwanzo wa mwisho wa siasa za Bwana Lissu.
CCM hawezi kumhitaji Lissu,sana sana wanataka Chadema ipasuke vipande vipande ikiwa bado Lissu ni kiongozi wa chama kama Makamu Mwenyekiti.
CCM hupanga mashambulizi kwa muda mrefu,walipoona hanunuliwi,nadhani walipanga mfumo mzito haitajiki kwenye vyama vikubwa.
Wanajua Lissu wa moto ameishaanza kupoa kwa kasi atapasuka tu.
 
Ukisikia CCM imempenda Lissu ujue ni mwanzo wa mwisho wa siasa za Bwana Lissu.
CCM hawezi kumhitaji Lissu,sana sana wanataka Chadema ipasuke vipande vipande ikiwa bado Lissu ni kiongozi wa chama kama Makamu Mwenyekiti.
CCM hupanga mashambulizi kwa muda mrefu,walipoona hanunuliwi,nadhani walipanga mfumo mzito haitajiki kwenye vyama vikubwa.
Wanajua Lissu wa moto ameishaanza kupoa kwa kasi atapasuka tu.

..Ccm hata ushindi wao wa kishindo hawajasherehekea wamejielekeza kupotosha kauli za Tundu Lissu.

..Lissu kumpiga Mama za chombo sasa Ccm kwasababu hawana majibu wanakimbilia kupotosha kauli zake.

. Kilichotokea kwenye serikali za mitaa ni aibu kwa Mama, na baya zaidi aliyeharibu ni mwanae / mkwe wake.
 
Back
Top Bottom