Ghafla CCM wanampenda Lissu. Yeye ataingia mtegoni?

Njoo ujifunze unafiki ili usiendelee kuandika upuuzi wa namna hii.
 
Maoni binafsi yanayogusa taasisi unayoiongoza hayawezi kuwa maoni binafsi.

Ukisikia Rais anasema kwa maoni yake binafsi Waziri Mkuu atekelezi kazi yake ipasavyo. Maoni hayo binafsi utayatenganishaje na nafasi yake ya uraisi anayoishikilia?
Ndani ya CHADEMA kuna shida kubwa. Na shida haiwezi kuisha kwa kukaa kimya. Kwa kifupi yule fisadi mkubwa, Abdul alipewa fedha na mama yake kwenda kuwapa viongozi wengi wa CHADEMA. Kuna waliochukuwa ila Lissu alikataa. Amejaribu kurekebisha mambo kwenye vikao vya ndani lakini nusu wambadilishie kibao. Pia tatizo jingine lipo kwa Mbowe kukaa muda mrefu kwenye madaraka. Amepata hangover inayoendana na kiongozi anapokaa kwenye madaraka kwa muda mrefu.
 
Nimekusoma sehemu tu, na nikaona pengine utakuwa unamhukumu Lissu bila sababu.
Lisuu amekwisha jipambanua kuwa hana "mfugaji"; iwe ndani ya chama au nje ya chama.
Ukifanya madudu asiyo kubaliana nayo, haijalishi wewe upo wapi, ndani ya CHADEMA au nje ya chama, atakupa chai yako.
Hivi huko kwenye maswala ya "mazungumzo ya Maridhiano", ambalo ndilo swala kuu linaloonekana kuamsha hisia za wengi; Mwenyekiti alikuwa kila mara akiweka wazi ndani ya chama kilicho kuwa kikiendelea huko kwenye mazungumzo?
Sasa wahenga wanasemaga:: "The rooster has come home"!

Usitegemee hata siku moja kumwona Lissu akishirikiana na uovu ulioko CCM. Tafuta sababu nyingine.

Hiyo NCCR unayo itolea mfano kusambaratishwa; hapa usimtwishe Lissu kuwa mhusika wa kazi hiyo. Wahusika ni hao unao onekana kuwakingia kifua katika andiko lako.
 
Na matokeo ya pesa hiyo sasa yanazidi kujifunua zaidi huko huko CHADEMA. Watu wanaandika waraka kumjibu Lissu kana kwamba waraka wenyewe umetokea kwa viongozi wa CCM! Si maajabu hayo!

Halafu mtu anashindwa kuona tatizo linatoka wapi, badala ya kutazama kwenye tatizo, sasa anaangusha zigo kusiko kuwa na tatizo.
Bure kabisa.
 
Kwa mtazamo huo huo, vipi kama ni mpango wa CHADEMA kuwavuruga CCM kupitia Lissu? maana kama anaisema Chadema na huku yuko kwenye vikao lakini na viongozi wenzake wamekaa kimya kuna nini hapo?
 
Kwa sasa Mbowe hana credibility
 
CHADEMA ya kabla ya 2015 ilikuwa na clear vision and agenda. Ilikuwa na vichwa vyenye mawazo fresh ambayo wengi wetu tuliwaona kama idols hadi ikafikia kijana akisema ni CCM alionekana kama amezeeka kifikra
Unasubiri nini mkuu, jinsi ulivyo jieleza inaonekana ACT-Wazalendo ndiyo nyumbani. Sasa hizi 'Activism' zinazo kuchosha sijui ni za nini tena, wakati mbadala tayari upo!
 
Kwenye vikao kuna mambo ambayo watu wanakubaliana kutokubaliana kwahiyo kila mtu anabaki na maamuzi yake lakini mambo yanaendelea, kwa sasa kuna uozo unao endelea ndani ya CDM, ambao wasipo angalia watakisambaratisha Chama kuondoka mtu kama Msigwa pamoja na njaa zake lakini kuna vitu kweli aliona haviko sawa na siyo yeye tu atakaye toka wapo wengine watatoka, swala la kutoka siyo hoja hoja ni sababu mtu inayo mfanya atako. Hivi vyama vya siasa kwa sasa vimegeuka kuwa malaika wa Shetani kwa hiyo watu wanaamua waende kwa Shetani mwenyewe, kuna vishetani vidogo vidogo ambavyo hivyo vinajipambanua kabisa kuwa wao na marafiki wa Shetani lakini kuna vyama vingine waio wanajifanya malaika wanuru kumbe nao ni mabaradhuli tu kama mabaradhuli wengine mimi nishauri watu angalau kuungana na shetani mwenyewe ujue upo kwa Shetani kuliko kuzani upo kwa malaika wa nuru kumbe uko kwa malaika wa Shetani. Covid19 wanaushirikiano mzuri tu na Mbowe na mimi wala sina ubaya na hilo, ubaya wangu kwa hilo ni kukataa kuliweka wazi kuwa hao ni wanachama wao hali.CDM na ACT ndiyo vyama vikuu vya upinzani ila niwaambie watu wazi, viongozi wa vyama hivyo si wakuwaamini sana hasa yanapokuja mapambano ya kweli, Jiulize kama Mbowre Anaweza kwenda kumchangisha Mwenyekiti wa CCM Milioni 150,na akapewa unazani anashindwa kwenda kumwambia hata shifa zake binafsi. Hivi vyama vya upinzani vinafanyiwa mabaya yote haya kwasababu viongozi wake tayari wameshawekwa mifukoni kwahiyo wanajulikana kuwa hawezi kuchukua maamuzi magumu yoyote kwakuwa wako kwenye Payrolls zao. Nini chakufanya ni kila mtu kuwa na Akili zake. ACT ndipo kwenye Maagent wengi ila CDM nako kunajengeka maagent. Haya mambo yanadidimiza Taifa kuwa na Taifa la vikaragosi. Kwa sasa vedha nyingi zinaelekezwa kwenye uharibu zaidi kuliko kuleta maendeleo.
 
Ukomavu wa chama unaonekana katika kukubali tofauti za mtazamo katika wanachama wake. Hili linaonyeshwa na CDM ambapo watu kama Lissu wako wazi kuwa hawakukubaliana na baadhi ya maamuzi ya chama chao na chama hakiwanyamazishi. Na hapo baadae wakionekana kuwa walikuwa sahihi, chama kinakiri kuwa kilikosea. Hii ni strength sio weakness.

Upande wa pili kimekuwa chama cha Mwenyekiti wake na wachache mno ndio wanadiriki kuonyesha wazi kuwa wanatofautiana na uelekeo wa chama.

Lissu hakichimbi chama maana anasema waziwazi. Anasema anayosema kwa ajili ya afya ya chama chake. Pamoja na juhudi za kuwatenganisha, imani yake kwa Mwenyekiti wake iko pale pale. Ukosoaji wa chama chake hadharani ni ishara ya imani yake kuwa hakitatetereka kutokana na msingi imara kilichokuwa nacho.

Amandla...
 
Kuna watu wanachanganya vitu binafsi na mambo ya siasa. Mbowe hakumchangisha Samia peke yake, aliwachangisha pia wakina Halima na Esther. Kwa mfano, ikiwa Samia atakuwa na harusi ya mjukuu wake sitashangaa kumuona Mbowe akihudhuria kama ataalikwa.
Kwenye mambo ya siasa Mbowe ni ruthless kama Lissu. Hakuna asiyejua kuwa anampenda sana Halima lakini alimfukuza kwenye chama hadharani.

Msigwa alipotofautiana na wakina Lissu kwenye suala la Ngorongoro hakutimuliwa pamoja na kuwa alikuwa anazungumzia tofauti hizo hadharani. Ila walipopata ushahidi kuwa amekuwa compromised wakamchinjia baharini.

Amandla...
 
Ilijua tena?....hii iliyopo ni ipi?
 
Unasubiri nini mkuu, jinsi ulivyo jieleza inaonekana ACT-Wazalendo ndiyo nyumbani. Sasa hizi 'Activism' zinazo kuchosha sijui ni za nini tena, wakati mbadala tayari upo!
Ndio tatizo la watu mlioshikilia siasa kama dini. Mnapenda sana kushambulia watu kuliko hoja. Usinipe tags na dhana zisizo sangu. Deal na nilichokiongea tu
 
We Jamaa bhana! Hongera sana una argue very critically basing on facts yaani kifupi una akili sana,na nmekuelewa sana..ngoja ninywe supu yangu kwanza inapoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…