Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Mkuu tatizo pia siyo kuwa gharama ni kubwa kama za private tu.

"Private unawaelewa wao wamejenga zao kama anavyosema Bashe."

Tatizo hapa ni kwa nini ni bei hizo zilizopo.

1. Nani anayepanga bei hIzi na kwa vigezo gani?
2. Je ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Iko kama lengo ni kuhakikisha tunakuwa mafukara kweli kweli.
Hebu tupe hizo bei za private vs Umma. Acha bla bla ku justify andiko lako.
 
Hebu tupe hizo bei za private vs Umma. Acha bla bla ku justify andiko lako.
Mkuu huku tulishatoka ila kwa faida yako niseme tunatambua tofauti ya hospitali za umma na binafsi.

Zingatia:

1. Hospitali za umma investment 100% ni umma.
2. Hospitali za umma hupewa bajeti tokea Kwa umma.
3. Mishahara hospitali za umma hulipwa na serikali.

Sasa hospitali private investment yote 100% ni private na hawapati lolote tokea serikalini.

Bado unataka kulinganisha bei zao kwa umma na hospitali za umma kwa umma?
 
Mkuu huku tulishatoka ila kwa faida yako niseme tunatambua tofauti ya hospitali za umma na binafsi.

Zingatia:

1. Hospitali za umma investment 100% ni umma.
2. Hospitali za umma hupewa bajeti tokea Kwa umma.
3. Mishahara hospitali za umma hulipwa na serikali.

Sasa hospitali investment 100% ni private na hawapati lolote tokea serikalini.

Bado unataka kulinganisha Bei zao kwa umma?
Haya yote yatachambuliwa baada ya taarifa ya tafiti. Kujua wapi tulipo na kwa nini tuko katika hali hii. Je ni halali au tunapigwa na huko duniani pia pakoje? Je tunastahili kuwa wapi?
 
Hili blanket la kusema tu kuhusu bodi haitoshi maana tunaolipa ni sisi iwe moja Kwa moja au kupitia bima.

Ipo hatari kubwa ya kuwa tunapigwa.

Tupewe wazi wazi vigezo hivi maana majengo ni ya umma na wafanyakazi ni wa umma pia.
Ni kweli majengo ni ya umma nasijui kama walipa kodi ya majengo na na bill za umeme na maji

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Mjadara mzuri huu.

Tips.
1.Wananchi/clients wanahitaji mchanganuo wa huduma na gharama zake.
2.Kuna concept kwa wananchi kuwa hospital na vituo vya Afya vya umma vinaendeshwa na Govt 100%..... kwa hili inabidi watu waelewe kuwa si kweli kuwa Govt inagharimia 100% cost za uendeshaji ... kuna percentage imeachwa kwa mtumiaji kuchangia. Na jukumu la kupanga bei limekaimishwa kwa bodi za uendeshaji wa vituo/hospital so wao ndio wanapanga bei ya hudumu ambazo mgonjwa atachajiwa ili ku-compliment kiasi kilichotolewa na serikali ili kukamilisha mzunguko mzima wa matibabu... hapa utakutana na pesa ya kufungua file, kitanda n. k

3.kuna baadhi ya gharama za uendeshaji zinategemea mapato ya kituo/hospital chenyewe eg. umeme, maji, posho za overtime na extra duty, on call allowances , Ulinzi, Usafi ...hapa si ajabu kituo cha kawaida kabisa kinahitaji 60M ku-cover hizo cost, so watu waelewe tanesco na mamlaka za maji zinatoza pesa as usual.

4.kuhusu itemization.. hili liko kwenye miongozo/maandishi kama wao wanavyopenda kusema .. BUT nani ana muda wa kuanza kumfafanulia clients item moja moja ...so huduma zimekuwa fixed kwenye mfumo wa package ... na kila package na bei yake(boards za uendeshaji ndo wazee wa shoo hizi).

5.Kuhusu Gharama kuwa juu ... inabidi tufanye comperative ... unasema gharama iko juu ukilinganisha na wapi? kwa ukanda wetu sisi ndio tunatoa huduma cheap sana.... kama refference point ni uchumi wa watumiaji (mimi nikiwemo) hapo huwezi kuturidhisha wotee.

WHO IS RESPONSIBLE.

again .. mwananchi eg mwanzilishi wa maada anatakiwa aihoji mamlaka(mhimili uliojichimbia zaidi) kuhusu gharama hizi na itemazation.

CRAZY OPINION FROM MY COLLEGUE.
Turudi sera ya nyuma kidogo ... huduma za Afya na Elimu ziachiwe Govt tuuu na ziwe buree ... private sector abakie huko kwingine ... hii haitatuhitaji BIMA wala mbwembwe nyiingi .. kwanza wahudumu hawatakuwa na choices za kukimbia kimbia mara yuko kituoni kwake muda kidogo yuko private ... hakutakuwa na upotevu wa bidhaa za Afya .. hata akiiba cormodity atapeleka wapi?


Kongole mleta mada .. but kuwa flexible wa Tz hatuko serious hivyo .. tunasubir Afe tukachange msibani at the time hatukuweza kuchangia gharama ya Tiba.

Mkuu nikiri sikuwa nimeiona nondo hii ya nguvu kwa hakika umemaliza kila kitu.

Nitakurudia kifungu kwa kifungu ila nisiache kukutaarifu kimsingi ninakubaliana nawe kama 100%.

"Mhimili uliojichimbia zaidi unayo majibu yetu. Inabidi tuyapate."
 
Imekuwa si nadra kusikia ankara za mamilioni ya pesa kwa ajili ya tiba kwenye hospitali za umma.

Nani anayepanga bei hizi na kwa vigezo gani?

Je, ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Au ni yale ya Bashe na wakulima na bei zao za vyakula?

Kwamba kama bei ni kubwa basi kila mtu akaanzishe hospitali yake?

Kama taifa tunakoelekea yaweza kuwa siyo kwema sana.
Umemkumbuka mwalimu jkn na matibabu ya aftatu
 
Nakubaliana nawe, lakini crazy opinion ya serikali kufany kila kitu wakati kuna wilaya hapa mjini 75% ya vituo vya afya ni binafsi. Tutahitaji muda na maandalizi.

Mkuu nadhani umeiona nondo ya bwana SMC TZ. Na huo ndiyo ulio ukweli kamili.

Sikuwa nimeiona mada yake mapema, nitamrejea kifungu kwa kifungu na kumshirikisha kwenye hadidu za rejea kama ilivyo kwenye post #375.

Ninaamini tuko kwenye njia sahihi.

Mhimili uliojichimbia zaidi uko na majibu yetu.

Kumjua mwenye majibu ni mwanzo wa ufumbuzi.
 
Mjadara mzuri huu.

Tips.
1.Wananchi/clients wanahitaji mchanganuo wa huduma na gharama zake.
2.Kuna concept kwa wananchi kuwa hospital na vituo vya Afya vya umma vinaendeshwa na Govt 100%..... kwa hili inabidi watu waelewe kuwa si kweli kuwa Govt inagharimia 100% cost za uendeshaji ... kuna percentage imeachwa kwa mtumiaji kuchangia. Na jukumu la kupanga bei limekaimishwa kwa bodi za uendeshaji wa vituo/hospital so wao ndio wanapanga bei ya hudumu ambazo mgonjwa atachajiwa ili ku-compliment kiasi kilichotolewa na serikali ili kukamilisha mzunguko mzima wa matibabu... hapa utakutana na pesa ya kufungua file, kitanda n. k

3.kuna baadhi ya gharama za uendeshaji zinategemea mapato ya kituo/hospital chenyewe eg. umeme, maji, posho za overtime na extra duty, on call allowances , Ulinzi, Usafi ...hapa si ajabu kituo cha kawaida kabisa kinahitaji 60M ku-cover hizo cost, so watu waelewe tanesco na mamlaka za maji zinatoza pesa as usual.

4.kuhusu itemization.. hili liko kwenye miongozo/maandishi kama wao wanavyopenda kusema .. BUT nani ana muda wa kuanza kumfafanulia clients item moja moja ...so huduma zimekuwa fixed kwenye mfumo wa package ... na kila package na bei yake(boards za uendeshaji ndo wazee wa shoo hizi).

5.Kuhusu Gharama kuwa juu ... inabidi tufanye comperative ... unasema gharama iko juu ukilinganisha na wapi? kwa ukanda wetu sisi ndio tunatoa huduma cheap sana.... kama refference point ni uchumi wa watumiaji (mimi nikiwemo) hapo huwezi kuturidhisha wotee.

WHO IS RESPONSIBLE.

again .. mwananchi eg mwanzilishi wa maada anatakiwa aihoji mamlaka(mhimili uliojichimbia zaidi) kuhusu gharama hizi na itemazation.

CRAZY OPINION FROM MY COLLEGUE.
Turudi sera ya nyuma kidogo ... huduma za Afya na Elimu ziachiwe Govt tuuu na ziwe buree ... private sector abakie huko kwingine ... hii haitatuhitaji BIMA wala mbwembwe nyiingi .. kwanza wahudumu hawatakuwa na choices za kukimbia kimbia mara yuko kituoni kwake muda kidogo yuko private ... hakutakuwa na upotevu wa bidhaa za Afya .. hata akiiba cormodity atapeleka wapi?


Kongole mleta mada .. but kuwa flexible wa Tz hatuko serious hivyo .. tunasubir Afe tukachange msibani at the time hatukuweza kuchangia gharama ya Tiba.

Bila shaka mjadala kuwa mzuri una maana hoja ni ya msingi na so Kwa maslahi binafsi.

Kama ulivyomalizia inafahamika kuwa watanzania huwa hawako serious na mambo ya msingi. Kabla ya jambo mtu kumkuta, ubinafsi uliopitiliza ndiyo kwao.

Jambo jingine la kutambua ni uvivu wao wa kuchambua mambo na utayari wao kuhoji mambo

Pamoja na yote niweke hapa wazi kuwa hakuna kurudi nyuma na neno flexibility litazingatiwa.

Yafuatayo ni maoni zaidi kuhusiana na bandiko lako, kifungu kwa kifungu kwa mlolongo ule ule kama ulivyokuja nao:

Tips:

1. Wananchi/clients wanahitaji mchanganuo wa huduma na gharama zake.
2. Concept iliyopo ni kuwa inawezekana bajeti ya serikali kuziendesha hospitali hizi haitoshi. Kwa kiasi gani haijulikani. Hapa ni muhimu kukafanyika audit ya kuaminika ili ijulikane bayana.

Kwa hili inajulikana kuwa bajeti kutoka serikalini inaweza kuwa haigharimii 100%. Gharama za uendeshaji ziko je?

"Audit ya kuaminika itatoa jibu hapa."

... Kwamba kuna percentage imeachwa kwa mtumiaji kuchangia. Hili lina ukakasi.

"Kiasi gani kimeachwa na kwa kigezo?" Hilo litakuwa swali #1 niliache pending kwanza.

Kwamba kuna % imeachwa na jukumu la kupanga bei limekaimishwa kwa bodi za uendeshaji wa vituo/hospital so wao ndio wanapanga bei ya hudumu ambazo mgonjwa atachajiwa ili ku-compliment kiasi kilichotolewa na serikali ili kukamilisha mzunguko mzima wa matibabu... hapa utakutana na pesa ya kufungua file, kitanda n. k.
-------
Niseme kuwa hapo unasomeka kigezo kikiwa swali #1 pending limejibiwa.

3. Kwamba kuna baadhi ya gharama za uendeshaji zinategemea mapato ya kituo/hospital chenyewe eg. umeme, maji, posho za overtime na extra duty, on call allowances , Ulinzi, Usafi ...hapa si ajabu kituo cha kawaida kabisa kinahitaji 60M ku-cover hizo cost, so watu waelewe tanesco na mamlaka za maji zinatoza pesa as usual.
------
Haya hayana tatizo kutegemea na majibu ya swali #1 lililo pending.

4. Kuhusu itemization, haina tatizo kuwa iko miongozo/maandishi kama wao wanavyopenda kusema .. kwamba nani ana muda wa kuanza kumfafanulia clients item moja moja ...kwamba huduma zimekuwa fixed kwenye mfumo wa package ... na kila package na bei yake(boards za uendeshaji ndo wazee wa shoo hizi).
--------

Hili Kwa setup iliyopo inafahamika ambako ndiko tunakoita kuuziana mbuzi kwenye gunia.

Tunamjua mwenye lake jambo. Hapa siyo hospitali (kwa maana ya madaktari au wahudumu).

Ni kweli kuwa wao wanatumia tu hizi packages zenye bei zote za huduma programed ndani.

Mwenye package ndiye mwenye majibu na huyo ndiye anayemhitajika awafafwnulie wadau wake zaidi ya bei za huduma. Yaani kwenye gharama, item kwa item kwa kila huduma.

Kwa vile bila shaka ni Kwa maslahi yake kuonyesha kuwa tuko fair, bila shaka atakuwa forthcoming kutoa ushirikiano wenye kujua alizifikia je bei hIzi zinazolalamikiwa.

(boards za uendeshaji ndo wazee wa shoo hizi).

Bila shaka hapo una maana hao ndiyo wenye hizo packages.

5. Kuhusu Gharama kuwa juu hili ni kuhusiana na uchumi wa watumiaji. Kwamba ni chini kuliko wa ukanda huu? Hilo sisi halituhusu kwa sababu kodi, tozo, uchumi, mipango, sera nk za nchi hizi tofauti.

"Wasiwasi wetu ni kuwa bei zinazotozwa ni kubwa mno kwa watu au mfuko wowote wa bima kutokufilisika."

Kwamba kama reference point ni uchumi wa watumiaji hapo hatuwezi kuwaridhisha wote? Hapana. Kujua gharama halisi kwa uwazi zitamridhisha kila mtu.

Izingatiwe hakunaombwi msaada, bali kinachogomba ni dalili za kukosekana kwa haki bin haki.

Zaidi sana kuwekwa mipango jumuishi yenye kuwaridhisha wote ni jambo linalowezekana. Hii ninaitunza kama swali #2 pending.


WHO IS RESPONSIBLE.

Ni wajibu wa wananchi kuihoji mamlaka(mhimili uliojichimbia zaidi) kuhusu gharama hizi na itemization.

Zingatia post #375 kwenye Uzi huu ina hadidu za rejea ya nini kifuate.

Mawazo, maoni au mapendekezo yoyote kuyaboresha yaliyomo kwenye post #375 litakuwa jambo jema.

Ni muhimu tukawa wageni rasmu Kwa Mh. Waziri Ummy Mwalimu kuziona ni mbivu au mbichi, na kulikoni.

CRAZY OPINION FROM YOUR COLLEGUE.

Turudi sera ya nyuma kidogo ... huduma za Afya na Elimu ziachiwe Govt tuuu na ziwe buree ... private sector abakie huko kwingine ... hii haitatuhitaji BIMA wala mbwembwe nyiingi .. kwanza wahudumu hawatakuwa na choices za kukimbia kimbia mara yuko kituoni kwake muda kidogo yuko private ... hakutakuwa na upotevu wa bidhaa za Afya .. hata akiiba cormodity atapeleka wapi?

Hili ni muafaka kama maswali yale pending mawili pale juu yatakuwa yamejibiwa, kwa mfano:

1. Kwa nini Kuna percentage imeachwa kwenye gharama za uendeshaji na serikali?

Kwamba serikali itoe 100% ya gharama za uendeshaji. Ambapo kupitia bima, tozo au kodi ihakikishe hospitali zinapata mahitaji yake 100%.

2. Serikali inaweza kulenga certain percentage e.g. 90% ya population kuona kuwa inaridhika. Halafu ikawa na maalum kwa wanaobakia.

Pamoja na yote tuko kwenye njia sahihi, kwamba yote yajengwe katika msingi wa bei zilizo halali.

Kila bei ya huduma kwenye hospitali ya umma ni lazima ijulikane item kwa item.

"Asiibiwe mtu moja kwa moja au mtu kupitia bima."

Nisiache kushukuru kwa kufuatilia na kutambua kuwa kuna hoja ya msingi yenye kuhitaji majibu kutoka kwa wahusika.

Haifurahishi kusikia aana wapendwa marehemu wanashikiliwa kwa kushindwa kulipa gharama zaa matibabu za matibabu zisizo mchanganuo.

Haifurahishi kusikia watu wameshindwa kulipa, watu au mifuko ya bima imefilisika. Kisa na mkasa ikiwa ni kukosekana kwa uwazi katika bei hIzi.

Yote ni mapambano.

Aluta Continua.
 
Tuweke kumbukumbu sawa sawa:

"Tunachohitaji ni break down gharama moja moja kwenye hospitali za umma."

Kwa maana nyingine:

"Kujua gharama za consumables kwa kila huduma kuhalalisha bei anayotozwa mgonjwa kwa huduma husika."

Tunajua kuwa serikali imewekeza vilivyo kwenye hospitali hIzi na pia hulipa mishahara ya wafanyakazi na hutoa bajeti Kila mwaka kwa ajili ya dawa, stationeries, magari nk.

Tunajua pia kuwa pesa wanazolipa wateja huishia serikalini.

Wasiwasi wetu ni kuwa bei zinazotozwa ni kubwa mno kwa watu au mfuko wowote wa bima kutokufilisika.

Ni nia yetu kuona mifuko hii haitumiki vibaya na wajanja wachache.

Kufanyika kwa "independent audit" kujua kama kuna upungufu wa bajeti, kwa kiasi gani na namna gani ufidiwe, bila shaka itakuwa ni njia sahihi zaidi ya kupata haki kwa wote.

Ifahamike kuwa haupo uhalali wa kuibebesha mizigo isiyostahili mifuko ya bima za afya au awaye yote anayelipia gharama hIzi.
Kama kuna nakisi ya bajeti kwenye hiyo wizara, kama zilivyo wizara nyingi, naona serikali ingetakiwa kuwa na vipaumbele, ijue kipi cha muhimu zaidi, hivyo kitangulie.

Wakifanya hivyo, naamini hiki kilio cha gharama kubwa za huduma ya afya kitaondoka kabisa.
 
Kama kuna nakisi ya bajeti kwenye hiyo wizara, kama zilivyo wizara nyingi, naona serikali ingetakiwa kuwa na vipaumbele, ijue kipi cha muhimu zaidi, hivyo kitangulie.

Wakifanya hivyo, naamini hiki kilio cha gharama kubwa za huduma ya afya kitaondoka kabisa.

Mkuu hapa kuna matatizo ya msingi. Suala hili halina tofauti na tozo za Mwigulu. Ni mambo yale yale ya kina Zungu au kina Bashe.

Kinachotakiwa ni pesa bila kujali zinatoka wapi. Mtego kamili upo mahospitalini. Huku kwingine cha mtoto:

"Watakuja tu kwa maana watapenda wapendwa wao kuishi."

Hawachelewi kuweka bei kuwa ni vyote mlivyo navyo ndugu na jamaa ikibidi na marafiki kama mnataka mpendwa wenu aishi.

Karata wanaicheza vyema. Kwa mfano bila dialysis mtu anaweza asidumu kwa zaidi ya juma moja kutegemea na matatizo ya figo aliyo nayo. Labda bila operation mtu atakufa ndani ya siku kadhaa nk.

Kwamba mpendwa atakufa ndani ya week, mbona mtauza vyote hata kama hakuna litakalobadilika? Kwamba hata akawaacha mkiwa fukara zaidi?

"Pana mwamba kanena ukitaka kuujua umaskini wako uguza."

Si ajabu ndani ya mchezo kusikia hiki au kile hakiko kwenye bima yako.

Tusiposimama hapa na mapema hawa jamaa watatumaliza siyo wema!

FolQpVRaEAEb4UX.jpeg


Hospitali ni za umma na zinapata mgawo kwenye bajeti za umma. Zinawatoza umma laki kahaa plus kwa MRI, CT scan nk zisizokuwa na consumables, Kwa uhalali upi?

Bei zote zisizoakisi gharama za uzalishaji ni kwa manufaa ya nani? Maduka mengi ya dawa ni ya vigogo serikalini na wa mahospitalini humo humo.

Mawodi, ICU hadi mortuary kumegeuka kuwa guest houses au 5 Star hotel. Yaani marehemu analipia malazi yake mortuary kwa siku.

Zingatia gharama hizi ni za malazi pekee. Malipo kwa huduma zingine zozote, hayo bado.

Bila kuliangalia hili kwa mapana yake huwezi kujua kuwa, kumbe bima ya afya ni bomba tu la kupitishia unyonyaji wao kutufikia kisiri siri wote popote tulipo.

Bei zilizowekwa kwa huduma ni bei hewa, Si halali na haijali mlipaji ni nani. Kwa hakika atafilisika tu iwe ni mtu, bima, au hata angekuwa Bill Gates.

Watatosheka na nini wakoloni wetu weusi hawa?

Kwa hakika wana roho ngumu sana. Ngumu kuliko maelezo.

"Hawa ndiyo wale wazalendo wanaopeleka pesa zetu China!"

Mtu unaelewa sasa zile siri za serikali zinazotakiwa kulindwa Kwa gharama yoyote. Mwananchi gani ataridhia utopolo huu?

Tunahitaji mwanzo mwingine. Hawa hawatufai. Kwa hakika si kwa mwendo huu.

Kulikoni?

"Usoni kama watu."
 
Mwenzio keshanielewa tayari wewe hapa unarudia yaleyale, nendeni mkafanye review ya hizo bei ziendane na dhana ya cost sharing.
Hoja zenu ni takataka kabisa.

Bei nnasema ziko juu, lakini hamtoi mapendekezo zintakuwa kuwaje.

Mfano, vituo vyote vya Afya na Zahanati gharama zake zinapangwa na baraza la madiwani (council meeting) ambalo ni wawakilishi wa wananchi hao hao.

Vile vile, vituo vyote vina kamati za Afya msingi ambao hao kamati Zina signary na maamuzi, hizi kamati ni wananchi wa maeneo hayo hayo kilipo Kituo.

Sasa unaposema mfanye review, unamaanisha kina Nani wafanye???

Mnabweka sana utafikiri madaktari na Manesi ndio wanakaa wanapanga hizo gharama za matibabu.
 
Hoja zenu ni takataka kabisa.

Bei nnasema ziko juu, lakini hamtoi mapendekezo zintakuwa kuwaje, huo ni upumbavu.

Mfano, vituo vyote vya Afya na Zahanati gharama zake zinapangwa na baraza la madiwani (council meeting) ambalo ni wawakilishi wa wananchi hao hao.

Vile vile, vituo vyote vina kamati za Afya msingi ambao hao kamati Zina signary na maamuzi, hizi kamati ni wananchi wa maeneo hayo hayo kilipo Kituo.

Sasa unaposema mfanye review, unamaanisha kina Nani wafanye???

Mnabweka sana utafikiri madaktari na Manesi ndio wanakaa wanapanga hizo gharama za matibabu.
Mkuu yaonesha umeguswa vilivyo.
Siyo kwa makasiriko haya!

Matusi ya nini kama kweli una hoja?

Bei ni kubwa kwa misingi hii hapa:

"Wasiwasi wetu ni kuwa bei zinazotozwa ni kubwa mno kwa watu au mfuko wowote wa bima kutokufilisika."

Mfano gharama ya MRI kwanini kuwa zaidi ya 350,00/- wakati kimsingi hakuna consumables zozote tuseme zinakuwa zimetumika?

Anayebweka bweka haitakuwa ni wewe ndugu?

Tunasema utaratibu huu wa bei kwa kuchukua "a fraction of a replica" kutokea "private hospitals" siyo sahihi. Hii haijalishi aliyeridhia hayo ni nani.

Zingatia:

1. Tunaolipa ni sisi na mifuko hii ni yetu, hatutaki tufilisike!

2. Tumepewa bei za huduma. Haturidhiki nazo. Tunahitaji kujua kipengele kwa kipengele ndani ya huduma hizo, kujua gharama halisi ili nasi kama wateja tujiridhishe na bei za huduma.

3. Mchango wa umma kwenye hospitali za umma.

Matatu haya kwa nini kukukera wewe hivyo?

Hatuna tatizo na wahudumu wa afya. Tunajua wao ni wahanga tu kama sisi, ila (bila shaka) ninyi kwenye ule mhimili uliojichimbia zaidi matatizo yetu hayahuwasu.

Tangu lini mwenye shibe akawajua wenye njaa?
 
Imekuwa si nadra kusikia ankara za mamilioni ya pesa kwa ajili ya tiba kwenye hospitali za umma.

Nani anayepanga bei hizi na kwa vigezo gani?

Je, ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Au ni yale ya Bashe na wakulima na bei zao za vyakula?

Kwamba kama bei ni kubwa basi kila mtu akaanzishe hospitali yake?

Kama taifa tunakoelekea yaweza kuwa siyo kwema sana.
Ishu ya hospital na kilimo tofauti.
 
Ishu ya hospital na kilimo tofauti.

Tulidhani anakoelekea Bashe price regulation haihusu biashara zote binafsi. Ndiyo maana tuna hoji kwa hospitali za umma si hospitali binafsi.

Tunasubiri pia kusikia hakuna regulation kwenye nauli za mabasi, vituo vya mafuta au mitandao ya simu, kwani hizo ni mali binafsi kwa mujibu wa waziri Bashe.
 
Mkuu yaonesha umeguswa vilivyo. Siyo kwa makasiriko haya!

Matusi ya nini kama kweli una hoja?

Bei ni kubwa kwa misingi hii hapa:

"Wasiwasi wetu ni kuwa bei zinazotozwa ni kubwa mno kwa watu au mfuko wowote wa bima kutokufilisika."

Mfano gharama ya MRI kwanini kuwa zaidi ya 350,00/- wakati kimsingi hakuna consumables zozote tuseme zinakuwa zimetumika?

Anayebweka bweka haitakuwa ni wewe ndugu?

Tunasema utaratibu huu wa bei kwa kuchukua "a fraction of a replica" kutokea "private hospitals" siyo sahihi. Hii haijalishi aliyeridhia hayo ni nani.

Zingatia:

1. Tunaolipa ni sisi na mifuko hii ni yetu, hatutaki tufilisike!

2. Tumepewa bei za huduma. Haturidhiki nazo. Tunahitaji kujua kipengele kwa kipengele ndani ya huduma hizo, kujua gharama halisi ili nasi kama wateja tujiridhishe na bei za huduma.

3. Mchango wa umma kwenye hospitali za umma.

Matatu haya kwa nini kukukera wewe hivyo?

Hatuna tatizo na wahudumu wa afya. Tunajua wao ni wahanga tu kama sisi, ila (bila shaka) ninyi kwenye ule mhimili uliojichimbia zaidi matatizo yetu hayahuwasu.

Tangu lini mwenye shibe akawajua wenye njaa?
Hawa watukanaji ni wa kuripoti tu wapigwe ban, huna haja ya kuhangaika na punguani.....
 
Back
Top Bottom