Gharama ya kuweka sakafu ya zege/rough floor

Kazi ya ujenzi hakikisha huruhusu fundi ajisimamie hata kama atakupiga maneno matamu kiasi gani.

Mpe wife wako akusimamie kazi itafanikiwa vizuri.
Dah mkuu yani ni changamoto tu
No wife
Nipo na dogo nae ni shule
So tegemeo langu linakua fundi

Nikisema nisubiri hadi likizo hela haikai cause ya kudunduliza
Now nme stop kwanza
 
Hapo mnapigwa tafuta fundi mwingine

Huyo anaweza kuwa dalali na sio fundi akipata kazi anatafuta mafundi na kuelewana nao gharama kisha anaondoka na chake
 
Kodi mashine ya zege kisha unaweza walipa mafundi Day
mashine kutwa lak na ishirini, operator30, usafiri wa kwenda site na kuirudisha.?.ongea na fundi upate punguza la wastani or utapata fundi atakaelipua kaz yako..ongeza usimamiz mzuri.bt fundi anakupa huduma kama mjasiriamali asichukuliwe kama mwiz..mbali ya ukubwa nyumba pia unyoofu wa kuta zako pia waweza kua kigezo cha bei ya plasta.kama kuta zilipinda kaz inakua kubwa thats why fundi anajua itakula muda mwingi wa kazi..pokea ushaur bt fanya tathmin ya kina
 
Bei gani unafanya na wewe
Jumlisha na na huo urembo
Makadirio ya Plasta nje na ndani ni 1.5 M

Bei za Urembo ni hizi na kwa sasa nipo Iringa


IRINGAAAAAA.....Mikonoooo juu!!! [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ladies and Gentleman

Kijana wenu nipo IRINGA MJINI kwa kazi maalumu...

Nicheki kwa offer zetu zinaendelea...Mdau Wa IRINGA NA MAENEO YA JIRANI

Dirisha Tsh 40,000

Kona Tsh 30,000

Nguzo Tsh 40,000

Mlango Tsh 35,000

Dining (Arch) 100,000

Arch ya nje Tsh 25000

Skating nzima Tsh 200,000

Tuna punguzo kubwa kwenye skiming na rangi

Nipigie kwa namba 0789005562

Au njoo wasap kwa link hii [emoji116][emoji116][emoji116]

Https//Wa.me//255789005562

Punguzo kubwa kwenye skimming ....Mikoani tunafika
 
Kutegemeana na eneo. Mfano mimi Dar nyumba ya 16 kwa 14 Rough floor labour chaji nililipa 300. Na Plaster nje na ndani 1.5M. Kwa ndani tu 900k ongea na fundi akupunguzie bei uchumi wenyewe huu sio
Rough floor ilikuwa na nchi ngpi
 
UKUbwa wa chumba ukiwa ngapi Kwa ngapi
 
Mafundi wa bunju wako na bei za ajabu sana
 
Ila wakuu kupitia jamvi hli yaani mmenisaidi sana maana kuna fundi alishanipiga kwenye msingi na kunyanyua boma "4mil", sasa iv alitaka kunipiga pesa mingi kwenye rough
Ameniambia kupiga rough nyumba ya vyumba 3 sebule ,Dinning, jiko na stoo 1mil
Lakini kupitia jamvi hili nimepata fundi wa laki 3 na ni fundi mzuri yule wa milion nimempiga chini , nashangaa leo ananifata anaomba hata kazi ya kusimamia nikamwambia ntasimamia mwenyewe.
Nawashukuru sana wakuu .

Nilichojifunza kuna mafundi wengi wazuri lakini hawana Majina "hawajajulikana" tuwatumie hawa tena hawana tamaa wala wizi.
 
Kwa ndan tu laki 9 hapana ghali 1m ndan na nje sawa
 
Nimepiga plasta ndani tu, vyumba viwili, jiko, vyoo viwili, sebule na dining. Pia akapiga na rafu chini. Bei ilikua 800,000/- jumla Kwa vyote plasta na rafu. Kwako haitakiwi kuzidi 1.2mil total.

Fundi aitwa Ayubu Marwa, Facebook anapatikana Kwa jina hilo hilo. Contact yake 0716478927
 
Kumbe Mimi nilibiwa kipindi najenga rough flouur fundi alinifanyia Kwa laki8 Haya mamho
 
Nimemuona jamaaa yuko vizuri kazi zake.
 
Kumbe Mimi nilibiwa kipindi najenga rough flouur fundi alinifanyia Kwa laki8 Haya mamho

[emoji28]


Yaan rough chin umepigwa sanaa lak 3 mana uwa ni kazi ya siku moja tu iyo
 
Sa
Mnapigwa kwa sababu yakutaka kufanya vitu local. Mkuu ujenzi una taratibuu zake na protocol ukifwata hizo taratibu hata kwa ujenzi mdogo unapunguza hasara nyingi sana.

Moja ya stage muhimu sana katika ujenzi nikupata Boq ya kazi yako. Mtafute mtaalamu akutengenezee Boq itakusaidia mambo yafuatayo.
1. Utapata makadirio ya material zinazohitajika
2. Utapata makadirio ya price range ya kazi husika kutokana na square meters ya nyumba yako.

Huu muongozo ukiwa nao wewe unamwita fundi unamwambia sema bei yako huku ww kichwani una figure ya range ya bei stahiki zinazotakiwa ( hapa ni rahisi kumbana na uka bageini vizur)

Na uzur kutengenezewa Boq standard kwa nyumba kama yako haizidi laki mpk laki na nusu

Ila ukisema u mtegemee fundi ukimbana angle moja anakukamata angle nyingine ukisema umwambie utamlipa day atafanya makadirio kazi ichukue siku nyingi na bado akupige kwny material ila ukiwa na Boq ww unatembea na muongozo wako.
Mfano kama plaster imeandikwa wastani ya mifuko inayohitajika ni 20 unaleta material kutokana na kazi na stage aliyofika itakusaidia sana kumonitor upotevu wa material. Asilimia kubwa watu wanapata loss katika ujenzi kwa ajili ya kutaka short kati na kukwepa wataalamu
 
Mimi wameniambia mifuko 20,
Yawezekana ni sahihi.

Nitachokifanya ni kutoondoka saiti mpaka wamalize mifuko yote.
Kama kweli ulitumia mifuko 20 ya simenti kwa eneo la 14 X 12.5m X 2" basi ndo maana mimi uwa sipati kazi za watu binafsi kirahisi na kimsingi uwa sihangaiki kuzitafuta ntapambana na hizi hiz za serikali. Nyumba zetu zinachoka mapema sana sbb ratio hiyo ni dhaifu sana kwangu kwa uchache ningekugonga mifuko 36. Mnajua kwamba mfuko 1 wa cement unaweza kujenga mpaka tofali zaidi ya 90 wkt std ni 50? Ushauri wangu kwa wote tafuta hela kidogo 30 au 50 muone mtaalam ukiwa na maswali yako akupe mwanga mfano
1. Ratio ya zege nyumba ya kawaida ipoje?
2. Ratio ya plaster, floor etc etc.
Upande wa labor charge inategemeana sana fundi ni wa eneo gani, uzoefu + ubora na speed kwny kazi. Kuna mafundi nawalipa 20 wengi 35 per day na wametofautiana mbaya kwa kila kitu. Saidia fundi 12 per day ilikua 15 nikashusha baada ya kuanza mizinguo kazin.
 
Plasta Laki 6 hiyo ya Flow sawa Lak 5
 
Punguza ujuaji usio maana ktk maisha...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…