Kila mtu unaejuana nae akifariki at some point utamkumbuka.Akifariki ipo siku utamkumbuka, utalia Sana na kujuta pindi utakapo soma. huu Uzi wako
Wewe ni mshamba?Jamani nikwamba ilikuaje hadi kuwaza ujinga huu?kua mmuwekee sumu mzazi kisa anawasumbua?Mungu aturehemu maana unaweza zaa ukijua umepata wakukutunza siku nguvu zimekuishia kumbe anawaza kukupa sumu hivi mnajua ilivyokazi kulea mimba hadi kitoto kilivyokidogo kijitambue?
Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
Hata akibaki hana tena faida.kifo kilivyo cha ajabu waweza kuta mkavuta nyie yeye akabaki
Ni baba yako, kwanini kutuhusisha sisi? Inategemeana na mlivyoishi.Kuna kipindi pia aliumwaaa.... tukafikia hatua tukasema bora tu arudishe number maana sasa inakuwa changamoto kwetu. Akaja akapona. Shida ikawa pale pale. Hakuna afadhali akiwa mzima shida akiugua shida. Ni msumbufu sana.
Sasa this time anaumwa tena. mwezi wa 3 huu amelala tumehamisha hosp zote. Tunagharamia ukimwangalia age yake nayo imeenda sana. 90 plus. Anataka aendelee kuishi kufanya nini hapa duniani? Sasa tunatumia pesa ambazo zingesaidia wajukuu wake kumtibu mgonjwa mbaye kwa kweli ameshakula chumvi ya kutosha hapa duniani. Mwisho wa siku tunamuona tu kama chuma ulete. Maana kila pesa zetu zinaenda kwenye matibabu yake. Meno yake yameshatoka, anaishi kwa shida. Anaanikwa tu juani kama mjusi ila bado anataka aendelee kuishi. Unajiuliza aishi kufanya nini hapa duniani? Mbona alishamaliza kila kitu?
Sasa inafikia kipindi tunasema bora tu akapumzike nasi tupumzike kidogo maana atatufilisi kwa kweli. Mimi nimeshauza gari moja, nimechukua mkopo, nimekuwa sasa nina madeni ile mbaya. Kwa mabro wengine nao.. ishakuwa shida. Maana tulishampeleka mpaka India kipindi fulani. Wakatwambia kwa huu umri asifanyiwe hayo matibabu maana kinga zake nazo zimekosa nguvu. So alilazwa tu akipewa madawa miezi mitatu. Gharama kubwa ilikuja kwetu. Akarudi amekuwa tia maji tia maji kama gari la mkaa trip moja shamba nyingine gereji.
Ila bado mbishi sana, bado anataka atibiwe na kupelekwa hosp za gharama, sasa mzee si atatuacha watoto wake tumefilisika halafu ndo afe? Hapo tutakuwa tumefanya nini? Nahitaji ushauri wenu kwa kweli hili jambo limenifika hatua nimechoka sana. Sipendi unafiki... hii hali ni ngumu sana maana sasa hata ukiona simu toka kwa ndugu unashindwa kupokea maana huchelewi kuambiwa sasa tuchangie kila mtu atoe 700,000 kuna vipimo na matibabu flani tena yanatakiwa.
Ndio hatokufa?Mkazanieni chakula bora.
Ajabu nini hapo?Nawewe utakuja kuwa hivyo,tena wewe ndio utasumbua kweli kweli..
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Sikiliza wewe pimbi!Ww mbwa hapo umeongea kisomi gani.???? We unaona mazuri hayo uliyo andika kuhusu mzazi.???? Hivi ww huyo ni baba yako kweli unaongea maneno ya kifedhuli kiasi hiki.mshenzi mkubwa wewe.sasa baba yako akishakufa ndio utapata nafuu unadhani.?? Kwann usiwe na subra ?? Uzee ni kitu kisichokwepeka
Unamsahau mzazi wako? Mshamba ni wewe basiKila mtu unaejuana nae akifariki at some point utamkumbuka.
Lakin itafika wakati unamsahau na maisha yanaendelea kama kawa.
Acha ushamba!
Wewe pambana na Hali yako bana ..sisi haituhusu hiyo ..uza kila kitu haituhusu, muue mzee wako haituhusu ..Yani kwa ufupi wewe pambana na Hali yako ..kila mtu ana Hali yake anapambana nayo.Mkuu.. wewe huujui uislamu kuliko mimi. Ungenyamaza tu ili usije leta mjadala wa kidini hapa. Mimi toka babu yangu alikuwa sheikh, mufti na alhaj.
Wewe maamuma tu unataka jifanya unaifahamu dini na mistari ya kukariri kuliko watu wenye uelewa wa dini? Acha huo upuuzi hapa tunaongea kisomi siyo kimaamuma.
Wewe ukishakuwa humble mbona inatosha. Maisha ya unafiki si mazuri hata kidogo.Kuwa tu humble na upokee nasaha ulizopewa na Akhi kule. Hata kama ni kweli umetoka katika familia ya Masheikh, unaweza kuwa mjinga vile vile. Unaweza kuwa ulisoma sana mpaka huko Lamu alipotoka Sheikh al-Habib Swaleh bin 'Alawy Jamalul-Layl lakini ukarudi mjinga au ukawa hukupata baraka ya Ilmu uliyoipata au ikawa sehemu kubwa mno ya Ilmu hukuipata pia. Unaweza kweli ukawa umesoma (tena kwa usahihi kabisa) lakini ukapinda hivyo kusoma kwako ikawa hakujakusaidia chochote, na watu wakaipuuza Ilmu yako. Unamjua Wasil ibn 'Ataa? Alikuwa Mwanafunzi wa Imaam Hassan al-Basry (Rahimahullah). Wasil aliachana na Imaam Hassan al-Basry akaenda kwa wanafalsafa huko wakamvuruga mwisho akajitenga na Imaam al-Basry, na ndio akaanzisha Madh-hab ya Mu'utazilah. Alijitenga na Imaam al-Basry licha ya kuwa Imaam Hassan al-Basry alikuwa ni katika Taabi'i wakubwa sana. Kinachoangaliwa ni umesimama sawa? Sasa unafanya au unasema jambo ambalo halipo katika dini, kisha ukiambiwa kwa kurekebishwa, unajitetea kwa kusema wewe ni mjukuu wa Mufti na umesoma mpaka Mombasa na Lamu. Haqq haipimwi kwa hivyo Chizi Maarifa.
Mtabiri wa Nyota Mzee Yahya Hassan Juma kwenda kwa Baba yako kuzungumza "habari za dini ya kiislamu" sio hoja pia.
Hata mimi pia akina Mtabiri Mzee Yahya Hassan ni katika wazee wangu, na baadhi ya Wazee wangu walikuwa ni Masheikh Maarufu tu wa Kisufi (Allah awasamehe makosa yao na Awarehemu). Ila bado kuna wengi katika familia zetu hawafahamu dini. Mimi mwenyewe ni miongoni mwa wasiojua dini hasa ndio naanza kusoma. Mwanzo nami nilijiona najua dini ila nimekuja kugundua sijui kitu, ndio kwanza naanza.
Be humble. Allah atuongoze sisi na wewe pia katika njia iliyonyooka.
Yangu ni hayo tu.
Ni baba yangu kwa nini wewe umejibu? For the same ground ungeachana nalo hili.Ni baba yako, kwanini kutuhusisha sisi? Inategemeana na mlivyoishi.
Daah ila wee jamaa kwa hiyo ikitokea ndugu yako kawa kiwete na sio productive tena unaona bora afe?? kweli mzazi wako ni wakumlipa haya maneno au kujikuta shujaa nyuma ya keyboardWewe ni mshamba?
Solution simple ni kumtelekeza mzee hospital ajifie taratibu.
Maana miaka 90+ huyo sio productive tena. Hata akipona hakai more than 10 years anakufa.
kwani kumkatia bima ilishindikana nini????Ni baba yangu kwa nini wewe umejibu? For the same ground ungeachana nalo hili.
Ilishindikana.kwani kumkatia bima ilishindikana nini????
Daaa poleni kama walikataaaa... ila wale bima hawaktaagi helaIlishindikana.